Blog - Page 18 of 20 - Fahamu Hili
Friday, April 26Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Blog

Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Teknolojia
Kuna taarifa nyingi tunazoweka kwenye mtandao; lakini je, sasa ni wakati wa kuweka mipaka juu ya ni lipi la kuweka na kutoweka kwenye mitandao? Ndiyo; huu ni wakati sahihi. Hivyo basi, tambua vitu 11 ambavyo haupaswi kuviweka kwenye mitandao ya kijamii. 1. Tarehe kamili ya kuzaliwa Wakati mwingine unaweza kuvutiwa na namna marafiki zako wanavyoweka taarifa za kuzaliwa kwenye mtandao, au hata misisitizo ya mitandao ya kijamii kama vile Facebook juu ya kukamilisha akaunti yako kwa kuweka tarehe ya kuzaliwa. Kuweka tarehe halisi au kamili ya kuzaliwa kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kutoa mwanya kwa wahalifu kupata taarifa zako muhimu na hata kufungua au kuingilia akaunti zako zinazotumia tarehe yako ya kuzaliwa. Mambo ya kufanya: Ficha au ondoa tarehe yako halisi ya kuzal...
Hatua 7 za Maumivu Zisizoepukika Kabla ya Kufanikiwa

Hatua 7 za Maumivu Zisizoepukika Kabla ya Kufanikiwa

Hamasa
Mafanikio ni safari ndefu. Katika safari ya mafanikio kuna mengi, milima na mabonde yasiyotabirika. Wengi huanza safari ya mafanikio wakiwa na malengo makubwa, lakini wanasahau kuwa kufanikiwa ni kupambana na changamoto bila kukata tamaa huku ukiyatazama malengo na maono yako. Kama unalenga kufanikiwa katika maisha yako ni vyema ukazifahamu hatua hizi saba za maumivu zisizoepukika katika safari hiyo. 1. Utahisi maumivu Kila mtu aliyefanikiwa amepitia kwenye safari yenye maumivu; ikumbukwe kuwa kupita njia yenye changamoto ndiko hutuelekeza kwenye mafanikio. Jifunze kutumia changamoto na maumivu kuwa kama hamasa ya kufanya juhudi zaidi kufikia mafanikio. Hakuna haja ya kulalamika na kukata tamaa bali anzia ulipo kwenda mbele ili kukamilisha malengo yako. 2. Kutamani kukata tamaa m...
Njia 13 za Kupata Usingizi Mzuri/Kulala Vizuri

Njia 13 za Kupata Usingizi Mzuri/Kulala Vizuri

Mtindo wa Maisha
Usingizi wa uhakika ni jambo jema sana kwa ajili ya afya ya mwili wako. Lakini kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, pamoja na kujengeka kwa jamii yenye mfumo wa maisha wenye shughuli nyingi, watu wengi hawapati usingizi mzuri. Namkumbuka rafiki yangu mmoja alipata kazi nyingi sana kwenye mtandao. Hivyo ikamlazimu azifanye zote kwa muda mfupi bila kulala wala kula ipasavyo. Matokeo yake ameugua kwa miezi minne sasa na bado afya yake haijaimarika kama awali. Hili linatupa umuhimu wa kuchunguza ni nini hasa manufaa ya kulala au usingizi mzuri? Huimarisha na kuboresha ukuaji wa mwili. Hujenga na kuimarisha kinga mwili. Hukuweka katika hali nzuri (mood). Hukuongezea kumbukumbu. Hurefusha maisha. Huboresha tendo la ndoa. Huondoa msongo wa mawazo. Ha...
Dondoo 5 za Kuishi Ndoto Zako

Dondoo 5 za Kuishi Ndoto Zako

Maendeleo Binafsi, Tija
Kila mmoja ana ndoto zake katika maisha yake. Wengine wana ndoto kubwa za kubadilisha ulimwengu huu, huku wengine wakiwa na ndoto za kuishi maisha ya kupata mahitaji yao ya msingi tu. Wote hawa wanahitaji kuzitimiza ndoto zao; lakini kuna vikwazo na mambo mbalimbali ambayo huwazuia watu wasiishi ndoto zao na kuishia kulamu na kulalamika hasa uzeeni. Fuatana nami katika makala hii nikueleze dondoo tano za msingi zitakazokuwezesha kuishi ndoto zako. 1. Tambua kinachokuvuruga Maisha yetu ya kila siku yamejaa vitu na shunguli mbalimbali lakini si zote huturuhusu kuishi katika ndoto zetu. Inawezekana unapenda kitu au tabia fulani kiasi kwamba imetawala au imekuwa ya kwanza kwenye maisha yako. Nitajuaje kitu au tabia imetawala/imekuwa ya kwanza katika maisha? Jibu ni rahisi, kile una...
Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Usafiri na Safari
Je wajua kuwa kuna viwanja vya ndege vinavyopokea ndege zaidi ya 400 kwa siku lakini bado vinamudu kufanya kazi kwa ubora na ufanisi wa juu? AirHelp.com hivi karibuni imetoa orodha ya viwanja bora vya ndege duniani kwa kutegemea vigezo vitatu ambavyo ni: kufanya kazi kwa kuzingatia muda, ubora wa huduma na kuridhika kwa wasafiri. Fuatana nami katika makala hii ili kuona orodha ya viwanja bora zaidi vya ndege duniani. 1. Uwanja wa ndege wa Changi Singapore Uwanja wa ndege wa Changi unakadiriwa kuwa takriban ndege 450 huruka katika uwanja huu kila siku, na kuufanya kuwa uwanja wa ndege wa sita wenye shughuli nyingi Asia na wa 17 duniani. Pamoja na hayo inasemekana kuwa ni aslilimia 12 pekee ya ndege hizo huchelewa kwa zaidi ya dakika 15 - na hili huufanya uwanja huu kuwa bora kabisa...
Hatimaye Ghana Yarusha Satelaiti Yake ya Kwanza Kwenda Anga za Juu

Hatimaye Ghana Yarusha Satelaiti Yake ya Kwanza Kwenda Anga za Juu

Habari, Teknolojia
Satelaiti ijulikanayo kama GhanaSat-1, ambayo iliundwa na wanafunzi kutoka katika Chuo Kikuu cha All Nations cha Koforidua, ilirushwa kwenda kwenye mzingo wa dunia kutoka kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu. Shange na vifijo vya watu takriban 400 wakiwemo wanafunzi na waandisi walikokuwa wakishuhudia tukio hili zilisikika katika mji wa kusini mwa Ghana. Mji huo ndipo lilipofanyika zoezi hilo la urushaji wa satelaiti hiyo. Mawasiliano na chombo hicho yalianza kupokelewa muda mfupi baada ya chombo hicho kurushwa. Maradi huo uligharimu dola za kimarekani 50,000 ulifadhiliwa na shirika la Japan Aerospace Exploration Agency (JAXA). Satelaiti hiyo itatumika katika mambo mabalimbali kama vile kufwatilia ukanda wa pwani wa Ghana, kuchora ramani na kuijengea nchi hiyo uwezo kati...
Faida 10 za Kunywa Maziwa Usizozifahamu

Faida 10 za Kunywa Maziwa Usizozifahamu

Mtindo wa Maisha
Maziwa hufanya mambo mengi mazuri kwa ajili ya afya yako. Wataalamu wa afya na wauzaji wa maziwa wamekuwa wakieleza faida kadha wa kadha za kunywa maziwa. Je umewahi kujiuliza hasa ni faida gani hizo zitokanazo na unywaji wa maziwa? Ni wakati wako sasa wa kujiuliza kwa kina juu ya faida zitokanazo na unywaji wa maziwa. Fuatana nami katika makala hii nikueleze faida 10 zitokanazo na unywaji wa maziwa. 1. Hujenga na kulainisha ngozi Je unamfahamu Cleopatra? Cleopatra alikuwa ni malikia wa Misri anaesadikiwa kuwa mzuri sana. Inaaminikia uzuri wa Cleopatra ulitokana na tabia yake ya kuogea maziwa mara kwa mara. Hivyo basi, ni wazi kuwa, vitamini na virutubisho vilivyoko katika maziwa ni muhimu kwa ajili ya ngozi bora. Ni vyema kunywa angalau bilauri moja ya maziwa kila siku. 2. Hu...
Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Kipato, Tovuti na Blogu
Kila mtu anahitaji kupata pesa ili kumudu mahitaji yake ya kila siku kama vile kununua chakula, nguo, kulipia matibabu, usafiri, ujenzi wa nyumba, n.k. Swali hapa ni kwa njia gani zitapatikana hizo pesa; kwani mara nyingi watu wanajikuta mishahara au kipato chao cha awali hakitoshi. Hivyo basi watu wanatafuta njia mbalimbali za kuwawezesha kuongeza kipato chao. Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamepelekea kukua kwa ajira na biashara katika mtandao; takwimu zinaonyesha kuwa kuna watu wengi wanaoomba na kufanya kazi katika matandao. Fuatana nami katika makala hii ili ufahamu mambo matano ya kuzingatia kabla ya kulenga kupata fedha kupitia kazi za kwenye mtandao. 1. Tovuti za matapeli Hivi leo ni rahisi kuona tovuti zinazojinadi kuwawezesha watu kupa kipato kwa urahisi ndani ...
China Kujenga “Mji Msitu” Ambao Utakuwa na Mamilioni ya Mimea na Miti 40,000

China Kujenga “Mji Msitu” Ambao Utakuwa na Mamilioni ya Mimea na Miti 40,000

Teknolojia
China kujenga “mji msitu” ambao utakuwa na mamilioni ya mimea na miti 40,000. Kazi hii inatarajiwa kutekelezwa kwenye Mji Msitu wa Liuzhou ulioko katika milima ya kusini mwa Guangxi kabla ya 2020. Mji huu uliobuniwa na msanifu majengo Stefano Boeri unatekelezwa sasa, ambapo nyumba, ofisi, shule na hosipitali zitafunikwa kabisa na miti na mimea mingine. Mjii huu unatarajiwa kuchukua eneo la hekta 175, na utakapokamilika utaweza kuchukua watu takriban 30,000. Mji huo utakapokamilika utatumia usafiri wa treni ya umeme kutoka Liuzhou. Mji huo pia utatumia nishaji ya joto ardhi (geothemal) kwa matumizi ya ndani nyumba pamoja na umeme jua (solar). Wanaamini kuwa kupanda miti zaidi kutanyonya tani 10,000 za hewa ukaa (C02) na tani 75 za hewa chafuzi nyingine, wakati huo ikizalisha ta...
Kilimo cha Kisasa: Kilimo bila Jua, Udongo wala Maji Mengi

Kilimo cha Kisasa: Kilimo bila Jua, Udongo wala Maji Mengi

Teknolojia
Kwa kawaida kilimo kinahitaji maji, urdhi ya kutosha, jua n.k. Lakini hali ni tofauti kwa kampuni ya AeroFarms ambayo imekuja na mawazo tofauti ya kulima mazao mbalimbali bila kutumia udongo, jua wala maji mengi. Kilimo chao hufanyika ndani ya nyumba tena kwenye ghala la zamani; hii ina maana kuwa kilimo hiki kinaweza kufanyika popote bila kuathiriwa na hali ya hewa. Wazo hili lilianzishwa na Ed Harwood, ambaye ni profesa kwenye Chuo cha kilimo cha Cornel aliyetaka kupanda vitu bila kutumia vitu vinavyokuza vitu. Kilimo bila ardhi au udongo AeroFarms wametengeneza vitu kama rafu au shelfu ambavo zina vitambaa maalumu ambavyo mbegu husiwia juu yake badala ya udongo. Mizizi ya mmea husika hujishikiza katika kitambaa hicho kuelekea chini kujipatia virutubisho na maji. Rafu/...