Ujasiriamali Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Ujasiriamali

Mambo 10 ya Kuzingatia ili Kutoa Huduma Nzuri kwa Wateja

Mambo 10 ya Kuzingatia ili Kutoa Huduma Nzuri kwa Wateja

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Changamoto ya huduma duni kwa wateja imekuwa kubwa sana kwenye biashara nyingi za kiafrika. Watoa huduma wengi hawajui na hawataki  kufahamu umuhimu wa kutoa huduma nzuri kwa wateja. Kwenye biashara na huduma nyingi mteja huchukuliwa kama kitu kisicho na nafasi wala umuhimu wowote. Lakini ukweli ni kuwa mteja ni msingi muhimu sana katika kufanikiwa kwa huduma au biashara yoyote ile. Kumbuka biashara yoyote isiyozingatia kutoa huduma nzuri kwa wateja wake itapoteza wateja na hatimaye itakufa. Kwa kutambua umuhimu wa kutoa huduma nzuri kwa wateja karibu nikushirikishe mambo 10 ambayo unapaswa kuyazingatia ili kutoa huduma nzuri. 1. Elewa hitaji la mteja Kamwe huwezi kumhudumia mteja vizuri bila kufahamu hitaji lake. Mara mteja anapofika katika biashara yako hakikisha unafa...
Athari 5 za Kukopesha Pesa na Bidhaa kwa Wateja

Athari 5 za Kukopesha Pesa na Bidhaa kwa Wateja

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Katika jaamii zetu za kiafrika suala la mikopo ya bidhaa au fedha kutoka kwenye biashara kwenda kwa wateja limezoeleka sana. Ingawa jambo hili linaweza kuwa na manufaa kwa upande fulani, hata hivyo kutokana na kukosekana kwa uaminifu miongoni mwa watu wengi jambo hili limekuwa na athari nyingi kuliko faida. Inawezekana umekuwa ukiwakopesha wateja wako wa maana sana, au umekuwa ukitumia mikopo kama njia ya kuuza huduma au bidhaa zako, lakini karibu nikushirikishe athari tano za mikopo hiyo. 1. Kumpoteza mteja Kuna usemi usemao kumkopesha mteja ni kumfukuza. Nimesikia mara kadhaa wafanyabiashara wakisema tangu ni mkopeshe haji tena dukani kwangu, au tangu nimkopeshe anapita mbali tu. Mara nyingi mteja akishakopeshwa pesa au bidhaa haji tena kwenye biashara husika ili kukwepa ku...
Mambo 8 ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Eneo la Kufanyia Biashara

Mambo 8 ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Eneo la Kufanyia Biashara

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Je ni maeneo gani sahihi ya kufungua biashara ili uweze kupata wateja, kukuza biashara na kutengeneza faida. Je, kila eneo linafaa kwa biashara? Hivyo basi, ili tuweze kujibu maswali haya vyema, hatuna budi kuangalia mambo 8 muhimu ya kuzingatia wakati wakuchagua eneo la kufanyia biashara ili ipate soko na kukua kila wakati. 1. Ushindani Ushindani ni jambo muhimu sana linaloweza kufanya eneo la biashara kuwa zuri au baya. Hebu fikiri mtu mchanga kabisa anaanzisha biashara mahali ambapo tayari kuna wafanyabiashara wengine wakubwa wenye uzoefu, mtaji, vitendeakazi au hata mtandao mzuri wa washirika. Bila shaka, itakuwa vigumu sana kwa mtu huyo kukua kibiashara. Ni lazima mtu apime na achague eneo amabalo lina ushindani ambao anaweza kuumudu na kukua. 2. Uhusiano kati ya biashar...
Zifahamu Aina 9 za Wateja ili Ukuze Biashara Yako

Zifahamu Aina 9 za Wateja ili Ukuze Biashara Yako

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Mteja ni nani? Mteja ni mtu yeyote anayenunua bidhaa au huduma inayotolewa na biashara fulani. Mteja ni mtu muhimu sana katika biashara yoyote. Lengo la kuanzisha biashara ni kupata wateja watakaonunua bidhaa au  huduma yako. Biashara yoyote isipopata wateja bora na wa uhakika, ni wazi kuwa haiwezi kufanikiwa; itakufa tu. Soma pia: Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa Kutokana na kukosa uelewa, wafanyabiashara wengi hawawafahamu wateja vyema, hivyo kutokuwamudu vyema; jambo ambalo huwakwamisha kufikia malengo yao. Ikiwa wewe ni mfanya biashara tayari au unataka kuanza kufanya biashara, karibu nikushirikishe aina 9 za wateja unazoweza kuzitumia kukuza biashara yako. 1. Wateja wapya Hawa ni wateja ambao huja kwenye biashara yako kwa mara ya kwanza, mnaweza kuwa m...
Fahamu Njia 8 Unazoweza Kuzitumia ili Kupata Mtaji

Fahamu Njia 8 Unazoweza Kuzitumia ili Kupata Mtaji

Ujasiriamali
Nifanyeje nipate mtaji? Nina wazo zuri lakini sina mtaji? Haya ni maswali ambayo nimekuwa nikiulizwa sana na wasomaji wa Fahamuhili.com, pamoja na watu wengi ninaokutana nao kwenye maisha ya kila siku. Kutokana na sababu hii, nimeona ni vyema niandae makala ambayo itajibu maswali ya wasomaji wangu pamoja na wale wote wenye maswali kama haya. Ingawa mtaji siyo kigezo pekee cha kufanikiwa kwenye biashara au mradi unaoufanya, mtaji unabaki kuwa kiungo muhimu sana katika kutekeleza wazo fulani au mradi kwa ufanisi. Kwa kuwa watu wengi huanzisha miradi au biashara kwa lengo la kupata pesa, huwa vigumu sana kuwa na pesa za kutosha kuanza utekelezaji wa wazo hilo. Karibu ufuatilie makala hii kwa karibu nikushirikishe njia 8 unazoweza kuzitumia ili kupata mtaji wa kutekeleza wazo la...
Mambo 10 ya Kujifunza Kama Mjasiriamali Kutokana na Anguko la Nokia

Mambo 10 ya Kujifunza Kama Mjasiriamali Kutokana na Anguko la Nokia

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Kama wewe uliwahi kidogo kwenye ulimwengu wa simu za mkononi, utakuwa umetumia au hata kusikia juu ya uimara, umaarufu na ubora wa simu za Nokia. Mnamo mwaka 1998 Nokia ilikuwa ndiyo kampuni bora ya kutengeneza na kuuza simu za mkononi duniani kote. Faida ya kampuni ya Nokia ilikwea kutoka dola za kimarekani bilioni 1 mwaka 1995 hadi dola bilioni 4 mwaka 1999; huku simu yake ya Nokia 1100 ikiwa ndiyo simu iliyowahi kuuzwa zaidi duniani. Nokia 1100 (Chanzo cha Picha: marketplace.citify.ca) Pamoja na mafanikio haya Nokia iliyoyapata, kwa kipindi kisichozidi miaka sita kuanzia mwaka 2007, hisa za Nokia ziliporomoka kwa asilimia 90.Kwa kutambua nafasi Nokia iliyokuwa nayo ikilinganishwa na anguko kubwa lililoipata, ni wazi kuwa kuna mengi ya kujifunza kama mjasiriamali au kiongoz...
Sifa 10 Ambazo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuwa Nazo

Sifa 10 Ambazo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuwa Nazo

Ujasiriamali
Kwa hakika ujasiriamali ni chaguo muhimu sana kwenye karne hii ya sasa ili kujipatia kipato. Hivi leo kuna wajasiriamali wengi waliofanikiwa na wengine hawajafanikiwa. Kwa hakika wajasiriamali waliofanikiwa wanafahamu na wanaziishi sifa za wajasiriamali bora. Ni wazi kuwa huwezi kuwa mjasiriamali bora wakati una sifa za mwajiriwa. Ili kuwa mjasiriamali ni lazima kuzifahamu na kuziishi sifa za mjasiriamali. Karibu nikufahamishe sifa 10 za mjasiriamali. 1. Mwenye malengo Malengo ni mwongozo wa kukuwezesha kufanikisha jambo lolote. Kuwa na malengo ni sifa muhimu ambayo kila mjasiriamali anapaswa kuwa nayo. Je umeamua kuwa mjasiriamali kwenye nini? Kwa ajili ya nini? Malengo yatakuongoza ufanye nini, wapi lini na kwa ajili ya nini. Bila malengo utafanya mambo bila mwongozo wowot...
Tofauti 10 Kati ya Mwajiriwa na Mjasiriamali

Tofauti 10 Kati ya Mwajiriwa na Mjasiriamali

Ujasiriamali
Kwa hakika kuna tofauti kubwa kati ya mwajiriwa na mjasriamali; tofauti hii inahusisha tabia, fikra, maamuzi au hata matendo. Kuna baadhi ya watu ni wajasiriamali kwa mwonekano lakini kitabia ni waajiriwa; wapo pia wengine ni waajiriwa kimwonekano lakini ni wajasiriamali kitabia. Ikiwa basi unataka kuwa mjasiriamali, ni muhimu ufahamu tofauti 10 za msingi zilizopo kati ya mwajiriwa na mjasiriamali. 1. Mwajiriwa hupumzika kwenye likizo lakini mjasiriamali hutumia likizo kufanya kazi zaidi Kwa kawaida waajiriwa hufurahia muda wa likizo kwa sababu ndipo hupata muda wa kupumzika. Hali ni tofauti kwa mjasiriamali kwani hana likizo, na ikiwa ni mjasiriamali aliyeajiriwa, basi atatumia likizo yake kuendeleza mradi au biashara yake. 2. Mwajiriwa hulenga kupanda cheo lakini mjasiriamal...
Changamoto 12 za Ujasiriamali na Jinsi ya Kuzikabili

Changamoto 12 za Ujasiriamali na Jinsi ya Kuzikabili

Ujasiriamali
Kila jambo lina changamoto zake, ujasiriamali nao unachangamoto zake nyingi. Ni wazi kuwa wajasiriamali wakubwa na wadogo, wote hukutana na changamoto; tofauti yao ni chanzo cha changamoto hizo na njia wanazozitumia kuzikabili. Wajasiriamali wadogo ndiyo wamekuwa wakikabiliwa zaidi na changamoto hizo na hata kupelekea kupoteza biashara au miradi yao. Inawezekana wewe ni mmoja wapo wa wajasiriamali wanaokabiliana na changamoto. Karibu nikushirikishe changamoto 12 za ujasiriamali na jinsi ya kuzikabili. 1. Mtaji Kila biashara inahitaji mtaji ili iweze kujiendesha na kujipanua. Wajasiriamali wengi wanashindwa kuanzisha biashara au kupanua biashara zao kutokana na kukosa mtaji. Suluhisho: Kumbuka! Siyo lazima upate mtaji wote unaouhitaji, unaweza kuanza na mtaji kidogo sana n...
Kanuni 15 za Ujasiriamali Ambazo ni Lazima Uzifahamu

Kanuni 15 za Ujasiriamali Ambazo ni Lazima Uzifahamu

Ujasiriamali
Ikizingatiwa kuwa upatikanaji wa ajira umekuwa wa shida sana, watu wengi hujikuta wakiwa na chaguo la kuwa wajasiriamali pekee kwenye maisha yao. Wengi hutamani au hata kujiingiza kwenye ujasiriamali, lakini siyo wote wanaofanikiwa kutokana na kutokufahamu kanuni muhimu za ujasiriamali. Ni wazi kuwa ili uanzishe kitu chochote chenye mafanikio, ni lazima ufahamu kanuni za kukifanya kitu hicho jinsi ipasavyo. Ikiwa wewe ni mjasiriamali, au unataka kuwa mjasiriamali, basi fuatilia makala hii ili nikufahamishe kanuni 15 za ujasiriamali. 1. Kuwa mtatuzi wa matatizo Ujasiriamali ni zaidi ya kupata pesa, ni lazima kwanza utatue changamoto ya mtu ndipo utaweza kupata pesa kutoka kwa mtu husika. Ni muhimu ukafahamu kanuni hii kama mjasiriamali kwani hutojikita kutafuta pesa bali utajiki...