Usafiri na Safari Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Usafiri na Safari

Faida 10 za Kusafiri Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 10 za Kusafiri Unazotakiwa Kuzifahamu

Usafiri na Safari
Najua umeshajiuliza faida za kusafiri? Ndiyo, kusafiri kuna faida nyingi unazopaswa kuzifahamu. Swala la kusafiri au kutembelea maeneo mbalimbali halijazoeleka sana kwetu waafrika kama ilivyo kwa wenzetu wazungu. Kusafiri siyo lazima kwenda nchi nyingine, bali hata safari za ndani ya nchi au za ndani ya eneo lako zina maana kubwa. Kwa hakika zipo sababu kuntu zinazowafanya wenzetu wa magharibi kusafiri kwenda sehemu mbalimbali duniani. Ikiwa basi unataka kufahamu faida za kusafiri ili uzifanyie kazi, basi karibu nikushirikishe faida 10 za kusafiri. 1. Kujifunza mambo mbalimbali Unaposafiri unajifunza mambo mbalimbali ambayo isingekuwa rahisi kujifunza mambo hayo ukiwa nyumbani. Unaposafiri utajifunza jografia, utamaduni au hata mtindo wa maisha wa watu wa eneo utakalotembelea. ...
Mambo 7 ya Kuzingatia Unapoendesha Gari Wakati wa Mvua au Ukungu

Mambo 7 ya Kuzingatia Unapoendesha Gari Wakati wa Mvua au Ukungu

Usafiri na Safari
Kama ambavyo nimekuwa nikieleza kwenye makala nyingine kuwa gari ni chombo kinachorahisisha usafiri lakini kinatakiwa kutumiwa kwa umakini na tahadhari kubwa. Umakini na tahadhari zaidi vinahitajika ikiwa utaamua kuendesha gari wakati hali ya hewa ikiwa siyo nzuri, yaani kuna maswala kama vile mvua au ukungu. Taarifa mbalimbali za usalama barabarani zinaeleza kuwa zipo ajali nyingi zinazogharimu maisha na mali za watu ambazo husababishwa na mvua au ukungu. Hivyo ikiwa unataka kuongeza maarifa pamoja na kulinda usalama wako, basi fahamu mambo ya kuzingatia unapoendesha gari wakati wa mvua  au ukungu. 1. Punguza mwendo Mwendo mkubwa ni hatari sana, lakini ni hatari zaidi mara hali ya hewa inapokuwa mbaya. Kumbuka kuwa wakati wa mvua au ukungu barabara huteleza na ni vigumu...
Mambo 8 Yanayosababisha Gari Kuwaka Moto na Jinsi ya Kuyaepuka

Mambo 8 Yanayosababisha Gari Kuwaka Moto na Jinsi ya Kuyaepuka

Usafiri na Safari
Gari ni kifaa au chombo kinachorahisisha usafiri, lakini kinapaswa kutumiwa kwa tahadhari kubwa. Ajali zinazotokana na magari kuwaka moto, mara kadhaa zimekuwa zikisababisha hasara kubwa au hata kugharimu maisha ya watu. Kwa hakika jambo hili si zuri, hivyo kila dereva au mtumiaji wa gari ni muhimu akachukua hatua za tahadhari mapema ili kukabili tatizo hili. Gari kuwaka moto kunaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, fuatilia makala hii kwa karibu ili ufahamu mambo 9 yanayosababisha gari kuwaka moto na jinsi ya kuyaepuka. 1. Kuvuja kwa mafuta Ikiwa gari litavuja mafuta  ni rahisi sana kuwaka moto. Kumbuka mafuta ya gari pamoja na mafuta lainishi (oil) ni rahisi sana kushika moto. Tafiti mbalimbali za ajali zimebaini kuwa kuvuja kwa mafuta ni chanzo kikubwa cha magari kuwaka...
Mambo 10 ya Kufanya Ili Kuepuka Ajali Unapoendesha Pikipiki

Mambo 10 ya Kufanya Ili Kuepuka Ajali Unapoendesha Pikipiki

Usafiri na Safari
Pikipiki au kwa jina maarufu bodaboda, zinatumiwa na watu wengi sana kwa usafiri. Licha ya pikipiki kutumiwa kama usafiri, wengine huzitumia kama chanzo cha kipato chao cha kila siku. Hata hivyo kila mmoja amewahi kusikia au kushudia juu ya changamoto kubwa ya ajali inayokabili usafiri wa pikipiki au bodaboda. Wengine wamepata majeraha, kupoteza maisha, kupoteza mali au hata kupata ulemavu wa kudumu. Pasipo shaka sasa ni wakati wa kutazama ni nini hasa chanzo cha ongezeko kubwa la ajali za pikipiki ili kikabiliwe. Ikiwa unaendesha pikipiki au unataka kuongeza maarifa yako, basi fahamu mambo 10 ya kufanya ili kuepuka ajali unapoendesha pikipiki au bodaboda. 1. Pata elimu sahihi ya kuendesha pikipiki Pikipiki ni chombo cha kitaalamu kinachohitaji maarifa sahihi ya kukitumia. A...
Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla na Wakati wa Kuendesha Gari Umbali Mrefu

Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla na Wakati wa Kuendesha Gari Umbali Mrefu

Usafiri na Safari
Kuendesha gari ni suala linalohitaji umakini na utulivu mkubwa, hasa pale unapoendesha gari umbali mrefu. Mara kwa mara kumeshuhudiwa ajali mbalimbali ambazo kimsingi zinatokana na madereva kutokuzingatia kanuni muhimu katika utumiaji wa vyombo vya usafiri. Ili kuhakikisha usalama wako pamoja na watumiaji wengine wa barabara, yapo mambo kadhaa unayopaswa kuyazingatia kabla na wakati wa kuendesha gari umbali mrefu. 1. Kagua na andaa gari Kabla ya safari yoyote gari linahitaji kukaguliwa na kuandaliwa, hasa kabla ya safari ndefu. Kuna mambo kadhaa unayohitaji kuyakagua kwenye gari lako: Kagua hali na ubora wa magurudumu. Hakikisha magurudumu yamejaa vizuri na hayajazeeka. Kagua mafuta lainishi (oil). Hakikisha gari yako ina mafuta lainishi ya kutosha tena ya ubora unaotakiwa...
Mambo 10 ya Kuepuka Unapokuwa Kwenye Nchi ya Kigeni

Mambo 10 ya Kuepuka Unapokuwa Kwenye Nchi ya Kigeni

Usafiri na Safari
Kila mahali pana taratibu na mambo yake. Mtindo wa maisha ulioouzoea kwenye nchi yako ya nyumbani, unaweza usikubalike kwenye nchi ya kigeni. Inawezekana umepanga kutembelea nchi ya kigeni hivi karibuni, au tayari uko kwenye nchi ya kigeni. Karibu nikufahamishe mambo 10 ambayo kama utayaepuka utaweza kukaa kwenye nchi ya kigeni bila tatizo. 1. Kukiuka utamaduni wa nchi husika Kila nchi ina tamaduni na taratibu zake. Kuna nchi haziruhusu kuvaa mavazi fulani au kufanya matendo fulani. Ni vyema ukahakikisha mambo unayoyafanya hayakiuki tamaduni za nchi husika. Kwa mfano nchi nyingi za Kiarabu haziruhusu kubusu au kukumbatiana hadharani baina ya mwanamke na mwanaume. Ukikamatwa ukifanya kosa hili, unaweza kuchukuliwa hatua kali. Soma pia: Maeneo 10 Ambayo ni Marufuku Kubusu au K...
Faida 5 za Kuvaa Kofia Ngumu (Helmet)

Faida 5 za Kuvaa Kofia Ngumu (Helmet)

Usafiri na Safari
Usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda, umeenea sana hivi leo. Karibu kila mtu ameshatumia au anatumia usafiri huu. Hata hivyo kumekuwepo na changamoto kubwa ya ajali zitokanazo na pikipiki. Kutokana na tatizo hili, mara nyingi tumekuwa tukisikia vyombo mbalimbali hasa vile vya usalama barabarani, vikisisitiza juu ya kuvaa kofia ngumu (helmet). Je kuna manufaa gani yaliyoko kwenye swala hili? Ni ukweli usiopingika kuwa kuna manufaa makubwa sana kwenye swala la kuvaa kofia ngumu. Karibu nikushirikishe faida 5 za kuvaa kofia ngumu. 1. Unatii sheria Kabla ya kuzungumzia faida binafsi anazozipata mtu anayevaa kofia ngumu; kwanza anapata faida ya kutii sheria. Hii ina maana kuwa ataepuka adhabu ya tozo au kifungo. Sheria zimewekwa ili zifuatwe, hivyo kutokufuata au kutii sheri...
Mambo 17 ya Kuzingatia Kabla ya Kusafiri Kwenda Nchi Nyingine

Mambo 17 ya Kuzingatia Kabla ya Kusafiri Kwenda Nchi Nyingine

Usafiri na Safari
Safari ni jambo linalohitaji maandalizi, hasa safari ya kwenda nchi nyingine. Watu wengi hujikuta wakiingia kwenye matatizo mbalimbali kutokana na kutokufahamu mambo ya kuzingatia kabla ya safari. Ikiwa umeshasafiri, au ni mara yako ya kwanza kusafiri kwenda nchi nyingine, basi karibu nikushirikishe mambo 17 ya kuzingatia kabla ya kusafiri kwenda nchi nyingine. 1. Hakiki muda wa mwisho wa pasi yako ya kusafiria Kama una pasi ya kusafiria, hakikisha muda wake wa matumizi haujakaribia kwisha. Hakikisha pia kurasa zilizo wazi hazijakaribia kwisha. Kumbuka kuwa baadhi ya nchi haziruhusu watu kuingia au kutoka kwa kutumia pasi za kusafiria zilizobakiza muda wa miezi 6 kuisha muda wake. 2. Fahamu nyaraka zinazohitajika Kila nchi ina taratibu na sheria zake. Hivyo hakikisha nyaraka ...
Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Tija, Usafiri na Safari
Ni wazi kuwa gari linahitaji mafuta ili kusafiri toka sehemu moja hadi nyingine. Lakini swali ni je, unaweza kutawala kiwango cha mafuta kinachotumika? Ndiyo, unawea kutawana kiwango cha mafuta na kupunguza garama za matumizi ya mafuta zisizokuwa na ulazima. Kama unapenda kuokoa kiasi cha mafuta yanayopotea bila sababu ya msingi katika gari lako, basi tumia njia hizi 8 zifuatazo. 1. Kabili upepo Unapoendesha gari upepo hukinzana na gari; hivyo kadri gari linavyokinzana zaidi na upepo ndiyo pia unavyotumia mafuta mengi zaidi. Hivyo basi, usipende kuweka mizigo juu ya gari kwa nje (carrier) au kufungua vioo kwani kutasabisha ukinzani zaidi kati ya gari na upepo. Kwa kukabili upepo vyema utapunguza ukinzani na kuokoa mafuta ambayo yangetumika kukabili ukinzani huo wa upepo. 2. Pu...
Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Usafiri na Safari
Je wajua kuwa kuna viwanja vya ndege vinavyopokea ndege zaidi ya 400 kwa siku lakini bado vinamudu kufanya kazi kwa ubora na ufanisi wa juu? AirHelp.com hivi karibuni imetoa orodha ya viwanja bora vya ndege duniani kwa kutegemea vigezo vitatu ambavyo ni: kufanya kazi kwa kuzingatia muda, ubora wa huduma na kuridhika kwa wasafiri. Fuatana nami katika makala hii ili kuona orodha ya viwanja bora zaidi vya ndege duniani. 1. Uwanja wa ndege wa Changi Singapore Uwanja wa ndege wa Changi unakadiriwa kuwa takriban ndege 450 huruka katika uwanja huu kila siku, na kuufanya kuwa uwanja wa ndege wa sita wenye shughuli nyingi Asia na wa 17 duniani. Pamoja na hayo inasemekana kuwa ni aslilimia 12 pekee ya ndege hizo huchelewa kwa zaidi ya dakika 15 - na hili huufanya uwanja huu kuwa bora kabisa...