Afya Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Afya

Athari 8 Kiafya za Dawa za Kuulia Wadudu — Viwatilifu

Athari 8 Kiafya za Dawa za Kuulia Wadudu — Viwatilifu

Afya
Dawa za kuulia wadudu maarufu kama viwatilifu zimetengenezwa kwa lengo la kuangamiza wadudu wanaoharibu mazao au wanaomdhuru binadamu. Hata hivyo kutokana na sababu kuwa lengo la dawa hizi ni kuangamiza, huathiri pia viumbe hai vingine akiwemo binadamu. Takwimu kutoka shirika la afya duniani WHO zinabainisha kuwa kuna zaidi ya vifo 220,000 vitokanavyo na athari za sumu zilizoko kwenye dawa za kuulia wadudu—viwatilifu. Ikiwa unataka kuweka afya yako salama, basi karibu nikushirikishe athari 8 kiafya za dawa za kuulia wadudu — viwatilifu. 1. Husababisha saratani Watafiti mbalimbali wa maradhi ya saratani wanaeleza kuwa dawa za kuulia wadudu zinachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha seli za saratani mara zinapoingia kwenye mwili wa binadamu. Hatari hii hutokea zaidi pale amb...
Sababu 6 za Kwanini Mara Nyingi Wanawake Huishi Zaidi ya Wanaume

Sababu 6 za Kwanini Mara Nyingi Wanawake Huishi Zaidi ya Wanaume

Afya
  Mara nyingi tumeshuhudia katika familia nyingi mwanaume akitangulia kufa kabla ya mwanamke. Simaanishi kuwa wanaume wote wanakufa mapema, lakini mara nyingi wanawake huishi zaidi kuliko wanaume. Swala hili limepelekea kuibua shauku ya kufanya utafiti zaidi juu ya sababu za wanaume wengi kufa mapema kuliko wanawake. Kwa kuwa lengo la Fahamuhili.com ni kukupa maarifa, basi karibu ufahamu kwanini mara nyingi wanawake huishi miaka mingi zaidi ya wanaume. 1. Wanawake hujali afya zao zaidi Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya zilibaini kuwa wanawake hujali afya zao zaidi. Tafiti hizo zinaeleza kuwa wanawake wengi wanapojihisi kuumwa huenda hosipitalini ili kupata ushauri wa kitaalamu. Hali ni tofauti kwa wanaume, kwani wao huvumilia maumizu au hata kutumia...
Sababu 10 za Kwa nini Unatakiwa Kuacha Kuvuta Sigara

Sababu 10 za Kwa nini Unatakiwa Kuacha Kuvuta Sigara

Afya
Kuna baadhi ya tabia kuzianza ni rahisi sana, lakini kuziacha kunakuwa ni kugumu. Watu wengi hasa vijana, hushawishiwa na marafiki kuingia kwenye tabia kama vile unywaji wa pombe, uvutaji sigara au kutumia madawa ya kulevya bila kufahamu madhara yake. Hakika kuna madhara mengi sana yatokanayo na uvutaji wa sigara kiafya, kiakili, kijamii na kiuchumi. Ikiwa basi unataka kufahamu sababu za kwanini unatakiwa kuacha kuvuta sigara, basi karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe sababu 10 za kuacha kuvuta sigara. 1. Unaokoa pesa Moja kati ya mambo yanayowapotezea watu pesa ni tabia kama vile uvutaji wa sigara. Kwa kuacha kuvuta sigara utaweza kuokoa pesa ambazo huwa unazitumia kwa ajili ya kununua sigara, na kuzitumia kufanya mambo mengine yenye manufaa kwako. Soma pia: Njia 10 Zitakaz...
Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Afya
Hakuna mtu anayependa kupata majeraha au kuchelewa kupona majeraha. Kwa kuwa uhai na uzima wetu haupo mikononi mwetu, ni vyema tukafahamu kuwa kuna wakati tunaweza kuumia. Kwa kutambua hili karibu nikufahamishe mambo matano unayoweza kuyafanya ili kuharakisha kupona majeraha. 1. Kula vizuri Lishe bora ni muhimu wakati wote, lakini ni muhimu zaidi mara unapokuwa na majeraha. Ili uweze kupona majeraha mapema unahitaji ule matunda na vyakula vyenye protini, vitamini C, B12 pamoja na madini ya chuma kwa wingi. Vyakula na matunda hayo ni kama vile machungwa, mapapai, mayai, maziwa, samaki, maharage, n.k. Kwa kula vyakula hivi mwili utaweza kutibu majeraha kwa haraka zaidi. 2. Pumzika vya kutosha Kupumzika ni njia ya kuupa mwili nafasi ya kujijenga na kujitibu wakati wa majeraha. K...
Madhara 6 ya Kutumia Dawa Bila Ushauri wa Kitaalamu

Madhara 6 ya Kutumia Dawa Bila Ushauri wa Kitaalamu

Afya
Mara nyingi watu wanaugua maradhi mbalimbali, lakini wengi wao hawapendi kwenda hospitali kufanya vipimo au kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari. Kutokana na uwepo wa maduka ya dawa baridi, watu wengi wanapojisikia kuwa wagonjwa, hununua dawa kwenye maduka hayo na kuanza kuzitumia. Ni ukweli usiopingika kuwa dawa zimetengenezwa ili kutibu maradhi fulani ambayo yatabainika kwa mgonjwa baada ya uchunguzi wa kitaalamu. Hivyo matumizi ya dawa bila kufanya uchunguzi wa kitaalamu yanaweza kuwa na madhara makubwa kwenye afya yako. Fahamu madhara 6 ya kutumia dawa bila ushauri au uchunguzi wa kitaalamu. 1. Huongeza sumu mwilini Dawa zimetengenezwa kwa kutumia kemikali mbalimbali ambazo kimsingi ni sumu zinazoua vimelea vya magonjwa. Hivyo kutumia dawa bila vipimo kunaku...
Athari 5 za Kutumia Vyombo vya Chakula vya Plastiki

Athari 5 za Kutumia Vyombo vya Chakula vya Plastiki

Afya
Plastiki ina nafasi kubwa kwenye jamii ya leo; hutumika kwenye magari, vyombo vya nyumbani, vifaa vya watoto vya kuchezea, simu, kompyuta n.k. Kwa hakika siyo rahisi mtu kumaliza siku nzima bila kutumia kifaa chochote cha plastiki. Pamoja na nafasi hii kubwa ya matumizi ya plastiki, plastiki imekuwa na athari mbalimbali kwenye afya ya binadamu pamoja na mazingira. Karibu nikufahamishe madhara au athari 5 zitokanazo na matumizi ya vifaa au vyombo vya chakula vilivyotengenezwa kwa plastiki. 1. Sumu zilizoko kwenye plastiki zinaweza kukufanya uugue Tafiti mbalimbali zimebainisha kuwa sumu zilizoko kwenye vifaa vya plastiki zinaweza kusababisha maradhi kama vile saratani, maradhi ya kupoteza kumbukumbu, maradhi ya moyo pamoja na kupoteza uwezo wa kuona. Wataalamu mbalimbali wali...
Rangi 11 za Mkojo na Maana Zake Kwenye Mwili wako

Rangi 11 za Mkojo na Maana Zake Kwenye Mwili wako

Afya
Ni watu wachache sana ndiyo hupenda kuchunguza rangi za mikojo yao. Lakini kiuhalisia rangi hizi zinaeleza mambo mengi kuhusu afya yako; Ikiwa hunywi maji ya kutosha au una maradhi fulani, basi utafahamu kupitia rangi hizi. Hapa chini kuna mchoro-taarifa (infographic) unaoonyesha kinachomaanishwa na rangi 11 za mkojo na nini unachotakiwa ufanye. Naamini sasa umepata maarifa; pia naamini sasa hutopuuzia tena kuchunguza mkojo wako. Je una swali au maoni yoyote? Tafadhali tuandikie hapo chini kisha washirikishe wengine makala hii. Usisahau pia kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.
Njia 12 za Kuondoa Sumu Mwilini

Njia 12 za Kuondoa Sumu Mwilini

Afya
Asilimia kubwa ya maradhi yanayowasumbua watu hivi leo yanatokana na sumu zilizopo katika miili yao. Inawezekana umewahi kusikia mambo mengi kuhusu sumu kwenye mwili, lakini hufahamu chazo halisi cha sumu hizi. Mabadiliko ya mazingira na mtindo wa maisha hupelekea kutengenezeka na kuingia kwa sumu nyingi ndani ya mwili wa binadamu. Sumu hizi hutokana na vyakula, vinywaji na hata mazingira tunayoishi. Sumu hizi huweza kuleta madhara makubwa mwilini kama vile kushindwa kufanya kazi kwa viungo vya mwili na hata aina mbalimbali za saratani. Ni vyema ukafahamu njia bora za kuondoa sumu mwilini mwako ambazo unaweza kuzifanya wewe mwenyewe bila gharama za ziada. 1. Kula vyakula vya asili Hivi leo watu hufikiri kula vyakula vya asili ni kupitwa na wakati. Wengi husifu vyakula vya vi...
Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Afya
Siyo siri kuwa pombe husababisha matatizo makuwa ya kiafya, yakiwemo magonjwa ya moyo, ini pamoja na majeraha yatokanayo na ajali zitokanazo na ulevi. Ni dhahiri kuwa vinywaji halisi vilivyotengenezwa kwa matunda bila kilevi ni bora zaidi kwa afya yako kuliko vile vyenye kilevi. Licha ya kuwepo kwa kampeni kadha wa kadha zinazopinga matumizi ya pombe, bado watu wengi wameendelea kushikilia kinywaji hiki bila kufahamu athari zake kwenye afya zao. Fuatilia hapa chini athari 12 za pombe kiafya. 1. Matatizo ya moyo Unywaji mkubwa wa pombe husababisha  matatizo mbalimbali ya moyo kama vile cardiomyopathy, ambapo mishipa ya moyo hudhoofika na kushindwa kusukuma damu. Jambo hili huweza kusababisha damu kuganda na kusababisha kiharusi (stroke). Pombe huchangia sana katika kudhoofisha mish...
Utafiti: Karatasi Zinazobandikwa Ukutani Zinaweza Kusababisha Ugonjwa

Utafiti: Karatasi Zinazobandikwa Ukutani Zinaweza Kusababisha Ugonjwa

Afya, Habari
Utafiti umebaini kuwa sumu zinazozalishwa na kuvu(fangus) zinazojizalisha kwenye karatasi za ukutani katika nyumba zetu zinaweza kuharibu hewa na kuiingia mwilini kwa urahisi, na kusababisha "maradhi ya jengo;". Maradhi ya jengo hutumiwa kuelezea hali ambayo wakazi wa jengo wanajihisi madhara makubwa ya afya ambayo yanaonekana kuwa yanahusishwa moja kwa moja na wakati waliotumia katika jengo fulani. "Tulionyesha kwamba sumu ya mycotoxins inaweza kuhamishwa kutoka vifaa vya vilivyo ukutani kwa hewa, katika ya hali ambayo inaweza kukutana na binadamu katika majengo," alisema Jean-Denis Bailly, Profesa katika Shule ya Veterinary School ya Toulouse nchini Ufaransa. "Kwa hiyo, mycotoxins inaweza kuvutwa na binadamu na inapaswa kuchunguzwa kama vigezo vya kupima ubora wa hewa ya nda...