Maendeleo Binafsi Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Maendeleo Binafsi

Fahamu Tabia 10 za Watu Wenye Wivu Ili Uwaepuke

Fahamu Tabia 10 za Watu Wenye Wivu Ili Uwaepuke

Maendeleo Binafsi
Mara mtu apatapo mafanikio mambo mengi hutokea au hubadilika. Moja kati ya mambo ambayo hutokea ni mabadiliko kwa watu wanao mzunguka mtu huyo. Wengine humpenda, wengine humheshimu, wengine humchukia au hata kumwonea wivu. Wivu umekuwa ukitesa na kurudisha maendeleo ya watu nyuma hasa wale ambao ndio huwa na wivu huo mioyoni mwao. Kwa kuwa wivu hauwaathiri wale walio nao pekee, ni vyema nawe ukafahamu tabia za watu wenye wivu ili uwaepuke wasije wakakuathiri kwa kukurudisha nyuma katika hatua zako za maendeleo. 1. Hawastaajabishwi na mafanikio ya wengine Moja kati ya tabia kubwa ya watu wenye wivu ni kutostaajabishwa na mafanikio ya wengine. Wao hata wasikie jambo zuri au kubwa kiasi gani la mtu mwingine wao hujifanya kuliona kama la kawaida tu. Unaweza kusikia hata wakisem...
Mambo 6 Yatakayokufanya Ufikiri Kama Mshindi Ili Uboreshe Maisha Yako

Mambo 6 Yatakayokufanya Ufikiri Kama Mshindi Ili Uboreshe Maisha Yako

Maendeleo Binafsi
Kila jambo tunaloliona kwenye ulimwengu wa leo lilianza kwanza kwenye fikra. Mwanariadha hawezi kushinda kama hawezi kufikiri na kujiona kuwa mshindi akilini mwake kabla ya kuanza mbio; kadhalika mtu mwingine yeyote hawezi kufanikiwa ikiwa hatoona lile analotaka kulifanya au kulifanikisha akilini mwake kwanza. Ikiwa basi unapenda kuboresha maisha yako kwa kuishi kama mshindi, karibu nikushirikishe mambo 6 yatakayokufanya ufikiri kama mshindi. 1. Amini kuwa kila kitu kinawezekana Hakuna mtu yeyote anayeweza kuwa mshindi bila kuamini kwanza kuwa kila kitu kinawezekana. Ikiwa hauamini kuwa kila kitu kinawezekana, utawezaje kufanya mambo kwa bidii na kwa imani kuwa yatafanikiwa? Hebu fikiri juu ya watu waliofanya safari ya kwanza kwenda mwezini; ni wazi kuwa hakukuwa na safari ...
Nukuu (Quotes) 30 za Uongozi Zitakazokujenga Zaidi

Nukuu (Quotes) 30 za Uongozi Zitakazokujenga Zaidi

Maendeleo Binafsi
Uongozi ni dhamana; tena ni nafasi ya kipekee inayopaswa kutumiwa vyema. Tuna viongozi wengi katika jamii yetu lakini siyo wote ni viongozi bora. Baadhi hutumia uongozi kama silaha, chanzo cha kipato au hata kichaka cha kuficha maovu. Kwa hakika kila kiongozi anatakiwa kujitambua na kupata maarifa stahiki ya uongozi. Ikiwa unapenda kuongeza maarifa yako au unataka kufahamu zaidi kuhusu uongozi; basi karibu nikufahamishe nukuu 30 za uongozi. Soma pia: Sifa 10 Zitakazokufanya Kuwa Kiongozi Bora Je wewe ni kiongozi? Je umejifunza kitu kutokana na nukuu hizi za uongozi? Tafadhali andika maoni yako hapo chini kisha washirikishe wengine makala hii.
Vitu 10 Ambavyo Wanaume Waliokomaa Hawavifanyi

Vitu 10 Ambavyo Wanaume Waliokomaa Hawavifanyi

Maendeleo Binafsi
Je mwanaume aliyekomaa ni yupi? Je ni mwenye miaka zaidi ya 18? Kwa kawaida kuna makundi makuu mawili ya wanaume, wanaume wachanga na wanaume waliokomaa. Kama kulivyo na tofauti kubwa kati ya mtoto mchanga na mtu mzima au aliyekomaa ndivyo ilivyo pia kwa makundi haya mawili ya wanaume. Mwanaume aliyekomaa ni yule ambaye maamuzi na matendo yake yanahusisha busara, hekima pamoja na utafiti wa kutosha. Ikiwa unapenda kuwa au kumfahamu vyema mwanaume aliyekomaa basi karibu nikufahamishe vitu 10 ambavyo wanaume waliokomaa hawavifanyi. 1. Hawaruhusu hofu kuwazuia kufikia furaha na malengo yao Kwa hakika ni kweli kabisa hofu ni adui mkubwa wa mafanikio yetu. Wanaume waliokomaa wanafahamu madhara ya hofu maishani mwao hivyo hawaruhusu hofu hasa ile ya kushindwa iwatawale. Wanaum...
Faida 10 za Kusoma Nje ya Nchi

Faida 10 za Kusoma Nje ya Nchi

Maendeleo Binafsi
Watu wengi wamekuwa wakitamani kusoma nje ya nchi, labda ni kutokana na kupata safari nyingi za ndege au fedha za udhamini wa masomo. Kwa hakika kusoma nje ya nchi kuna manufaa makubwa sana zaidi ya kusafiri kwa ndege pamoja na kupata fedha za udhamini wa masomo. Ikiwa unataka kuongeza maarifa au unataka kusoma nje ya nchi, basi fahamu faida 10 za kusoma nje ya nchi. 1. Kuongeza uwezo wako wa lugha Kusoma kwenye nchi nyingine itakulazimu kujifunza lugha ya nchi husika ili uweze kuwasiliana na kuitumia kujifunza mambo mbalimbali. Kwa mfano watu wengi wanaosoma nchi za ulaya huongeza uwezo wao wa kuzungumza kiingereza zaidi. Hivyo kusoma nchi za kigeni kutakuwezesha kujifunza na kuongeza uwezo wako wa lugha za kigeni kama vile Kichina, Kifaransa, Kijapani, Kiingereza, Kijer...
Faida 6 za Kufundisha Watu Wengine Kile Unachokijua

Faida 6 za Kufundisha Watu Wengine Kile Unachokijua

Maendeleo Binafsi
Sio watu wengi wanaopenda au wanafahamu umuhimu wa kuwafundisha watu wengine kile wanachokifahamu. Wengi huona kuwa kufundisha watu wengine ni kazi duni ambayo haiwezi kuwanufaisha kwa njia yoyote ile. Ukweli ni kuwa kufundisha watu wengine ni swala lenye manufaa mengi ambayo watu wasiofanya hivyo wanayakosa. Ikiwa unapenda kuwa bora zaidi pamoja na kuongeza maarifa yako, basi karibu nikufahamishe faida 6 za kufundisha watu wengine. 1. Hukuongezea maarifa Kufundisha wengine ni njia bora ya kuongeza maarifa yako. Kwanza kabisa utahitajika kujiandaa kwa kusoma na kujifunza mambo mbalimbali ili uweze kufundisha vyema, hili litakuongezea kiwango kikubwa cha maarifa. Pili wakati wa kufundisha utajifunza mambo mbalimbali kutoka kwa yule unayemfundisha au wale unaowafundisha kwani...
Sababu 10 za Kwa Nini Baadhi ya Watu Wanafahamu Mambo Mengi

Sababu 10 za Kwa Nini Baadhi ya Watu Wanafahamu Mambo Mengi

Maendeleo Binafsi
Kwa hakika kuna watu ukiwatazama au kuwasikiliza unaweza kufikiri wana akili ya ziada. Maamuzi na ujenzi wao wa hoja ni wa hali ya juu sana. Watu hawa wanajua mambo kwa undani na kwa usahihi. Ukiwauliza hiki au kile watakujibu bila wasiwasi tena hata na ziada yake. Naamini sote tunatamani kuwa kama watu hawa. Je ni sababu gani zinawafanya watu hawa kufahamu mambo mengi? Karibu nikushirikishe sababu 10 zinazowafanya baadhi ya watu kufahamu mambo mengi zaidi kuliko wengine. 1. Wanasoma sana Kusoma ni chanzo kimoja kikuu cha maarifa. Watu wanaojua mambo mengi husoma vitabu na makala nyingi kadri wawezavyo. Hawasomi tu vitabu au makala, bali wanasoma vile ambavyo vina ubora na maarifa stahiki. Kwa njia hii wanafahamu mambo mengi na kuwafanya kutoa hoja zenye ushahidi na ufaf...
Nukuu (Quotes) 25 za Malengo Zitakazokuhamasisha

Nukuu (Quotes) 25 za Malengo Zitakazokuhamasisha

Maendeleo Binafsi
Malengo ni muhimu sana kwenye maisha ili yatuongoze kufikia mafanikio yetu au kuwa yule ambaye tunapaswa kuwa. Kwa hakika, ikiwa huna malengo ni wakati wa kujiwekea malengo sasa; na ikiwa unayo basi ni wakati wa kutathimini kama unayaelekea. Kwa kutambua umuhimu wa malengo maishani, karibu nikushirikishe nukuu (quotes) 25 za malengo ambazo zitakuhamasisha kufikia malengo yako. Naamini umefurahia nukuu hizi pamoja na kuhamasika kuendelea kupigania malengo yako. Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako Tafadhali andika maoni yako hapo chini kisha washirikishe wengine makala hii. Unaweza kutufuatilia kwa barua pepe au kwa kulike ukurasa wetu wa Facebook i...
Faida 15 za Kusoma Vitabu Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 15 za Kusoma Vitabu Unazotakiwa Kuzifahamu

Maendeleo Binafsi
Ni watu wachache sana ndiyo wanaopenda na wanafahamu umuhimu wa kusoma vitabu. Watu wengi hasa waafrika hawapendi kusoma vitabu ikiwa hakuna kinachowalazimisha kufanya hivyo kama vile mtihani, kazi, n.k. Kwa hakika kuna maarifa mengi yaliyofichwa kwenye vitabu; hii ndiyo sababu watu wengi waliofanikiwa husoma au hata kuandika vitabu. Ikiwa unataka kupata maarifa na kuboresha maisha yako kwa njia ya kusoma vitabu, basi fahamu faida 15 za kusoma vitabu. 1. Hukuongezea marifa mapya Lengo kubwa linalowafanya waandishi wa vitabu kuandika vitabu ni kuweka maarifa yao kwenye maandishi. Hivyo kwa kusoma vitabu unapata maarifa mbalimbali yaliyowekwa kwenye kitabu husika. Hivi leo kuna vitabu vinavyohusu takriban kila kitu; kwa hiyo maarifa yoyote unayoyahitaji unaweza kuyapata kwenye...
Tabia 10 za Watu Waliojipanga

Tabia 10 za Watu Waliojipanga

Maendeleo Binafsi
Kuna watu ukitazama utendaji wao wa kazi au maisha yao yanavutia. Ukitazama jinsi wanavyotekeleza mambo yao unaweza kufikiri kuna mfumo fulani unawaendesha au kuwaongoza kwa siri. Mara nyingi watu hawa huwa na mfuatano au mpangilio mzuri na unaoeleweka wa kazi au maamuzi yao. Kwa kifupi watu hawa hufanikiwa sana na ndiyo huitwa watu waliojipanga. Inawezekana nawe unahitaji kufahamu sifa za watu waliojipanga ili ujifunze jambo. Basi karibu nikushirikishe tabia 10 za watu waliojipanga. 1. Wanaandika kila kitu Kuandika vitu ni njia mojawapo ya kutekeleza mambo kwa mpangilio. Watu waliojipanga huandika mambo yote wanayotakiwa kufanya ili wasiyasahau na wanyafanye kwa wakati. Watu waliojipanga hukagua pale walipoandika mara kwa mara ili kuona wamekamilisha lipi na lipi bado hawaj...