Malengo ni muhimu sana kwenye maisha ili yatuongoze kufikia mafanikio yetu au kuwa yule ambaye tunapaswa kuwa. Kwa hakika, ikiwa huna malengo ni wakati wa kujiwekea malengo sasa; na ikiwa unayo basi ni wakati wa kutathimini kama unayaelekea.
Kwa kutambua umuhimu wa malengo maishani, karibu nikushirikishe nukuu (quotes) 25 za malengo ambazo zitakuhamasisha kufikia malengo yako.
“Kuweka malengo ni hatua ya kwanza ya kugeuza yasiyoonekana yaoonekane.”
“Weka malengo makubwa, usiache mpaka uyafikie.”
“Nidhamu ni daraja kati ya malengo na ukamilishaji.”
“Fikiri malengo madogo na utarajie mafanikio madogo. Fikiri malengo makubwa na upate mafanikio makubwa.”
“Njia pekee ya kupata msukumo wa kuendelea mbele ni kuwa na malengo makubwa kila wakati.”
“Watu wenye malengo hufanikiwa kwa sababu wanajua ni wapi wanakokwenda.”
“Pitia malengo yako mara mbili kwa siku ili kujikita kwenye kuyafanikisha.”
“Kinachonifanya niendelee mbele ni malengo.”
“Malengo huamua unaelekea kuwa nani.”
“Kuweka malengo na kuendelea nayo mbele kunasisimua.”
“Unahitaji malengo ya juu. Kisha uyaimarishe kwa maadili mazuri ya kazi.”
“Malengo hukusaidia kuelekeza nguvu yako kwenye matendo.”
“Malengo hayaji kirahisi. Hakuna mtu anayekupa malengo.”
“Kazi yangu ni kushinda malengo.”
“Hamasa moyoni mwangu ni kufanya kazi kuelekea malengo na ndoto zangu.”
“Unapaswa kuwa mtu unayeweka malengo yako wewe mwenyewe, na kujaribu kufikia malengo hayo.”
“Kila siku nafanya ndoto zangu kuwa malengo.”
“Unaweza ukafanya chochote kama utaweka malengo. Unahitajika tu kujisukuma wewe mwenyewe.”
“Ninafurahia kufanya kazi kwa bidii; ninapenda kuweka malengo na kuyafikia.”
“Mungu aliniumba niwaburudishe watu kwa malengo yangu.”
“Kuweka malengo na kuyafanikisha malengo hayo — hiki ndicho tu ninachofanya.”
“Malengo hukufanya ufanye zaidi kwa ajili yako na wengine pia.”
“Sijawahi kuacha kutazama malengo yangu. Sijawahi kuacha kufikiri kuwa ninaweza kufika juu.”
“Bila malengo ningekuwa nimekufa. Nahitaji kitu kinachonifanya niendelee mbele.”
“Kama unataka kuishi maisha ya furaha, yashikize na malengo na wala si watu au vitu.”
Naamini umefurahia nukuu hizi pamoja na kuhamasika kuendelea kupigania malengo yako.
Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako
Tafadhali andika maoni yako hapo chini kisha washirikishe wengine makala hii. Unaweza kutufuatilia kwa barua pepe au kwa kulike ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.