Tovuti na Blogu Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tovuti na Blogu

Mambo 10 ya Kuzingatia Unapochagua Anwani ya Mtandao (Domain)

Mambo 10 ya Kuzingatia Unapochagua Anwani ya Mtandao (Domain)

Tovuti na Blogu
Anwani mtandao ni muhimu sana kwa ajili ya utambulisho wa tovuti au blog ya kile unachokifanya. Inawezekana unamajina mengi ambayo unataka uyatumie kama anwani ya mtandao ya tovuti au blog yako; lakini ni muhimu kufahamu kuwa ukifanya makosa kwenye kuchagua anwani ya mtandao utaathirika kwa kiasi kikubwa. Madhara ya kukosea kuchagua anwani ya mtandao (domain) Kutokutambulisha vyema kile unachokifanya Kukosa nafasi kwenye injini pekuzi Kupoteza wasomaji au watembleaji Kuingia kwenye migogoro ya kisheria ikiwa utatumia anzwani inayofanana na za wengine. Ikiwa unataka kufungua website au blog kwa ajili yako binafsi au bishara yako, basi fahamu mambo 10 ya kuzingatia unapochagua anwani ya mtandao (domain). 1. Upekee Hakikisha unapochagua domain ni ya kipekee sana na i...
Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kulinda Tovuti Yako Dhidi ya Wadukuzi

Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kulinda Tovuti Yako Dhidi ya Wadukuzi

Tovuti na Blogu
Kutengeneza tovuti ni jambo moja na kuilinda ni jambo la pili. Kutokana na kukua kwa sayansi na teknolojia, kumepelekea kukua na kushamiri kwa uhalifu kwa njia ya mtandao. Visa kadha wa kadha vimeripotiwa vikieleza juu ya udukuzi uliofanyika kwenye makampuni mbalimbali na kusababisha hasara kubwa. Kwa mfano kampuni ya Sony ilidukuliwa mnamo mwaka 2014 na kupata hasara ya takriban dola milioni 15 za Marekani. Ni muhimu kulinda tovuti au blog yako dhidi ya wadukuzi ili kuepusha hasara na uharibifu unaoweza kutokea. Ikiwa unataka kulinda tovuti yako, basi fahamu mambo 7 ya kufanya ili kulinda tovuti yako dhidi ya wadukuzi. 1. Hakikisha unazingatia usasishaji (updating) Ikiwa unatumia programu yoyote katika website yako, hakikisha unaisasisha kwa wakati. Programu kama vile Wordp...
Sababu 11 za Kwa nini Utumie WordPres Kwenye Blog Yako

Sababu 11 za Kwa nini Utumie WordPres Kwenye Blog Yako

Tovuti na Blogu
Mara unapotaka kutengeneza blog au tovuti, swali gumu linalokuja kichwani mwako ni njia, teknolojia, mfumo au programu ipi utakayoitumia kutengenezea tovuti au blog yako. Kwa hakika kuna teknolojia mbalimbali zinazoweza kutumiwa kutengeneza blog na tovuti, WordPress kama Content Management System ni mojawapo. WordPress ni programu ya bure (open source software) inayotumika kutengenezea tovuti na blogs ambayo unaweza kuisambaza, kuitumia au hata kuibadilisha bila kizuizi chochote. Unaweza kupakua WordPress na kuihost wewe mwenyewe au kwenye huduma yoyote nzuri ya kuhost website Karibu ufuatilie makala hii nikufahamishe sababu 11 za msingi za kwanini utumie WordPress kwenye blog au tovuti yako. 1. WordPress inatumiwa na zaidi ya asilimia 25 ya tovuti Zaidi ya asilimia 25 za to...
Mambo 9 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Web Host

Mambo 9 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Web Host

Tovuti na Blogu
Kuna mahali ambapo kila tovuti au blog hutunzwa, mahali hapo ndipo hufahamika kama web host. Web host bora ni muhimu sana kwa ajili ya tovuti au blog yako. Watu wengi wamekuwa wakifanya makosa wakati wa kuchagua web host kutokana na uelewa mdogo juu ya umuhimu wa web host bora pamoja na njia za kubaini web host bora. Madhara ya web host duni ni: Kasi ndogo ya tovuti yako au blog. Athari ya kudukuliwa kutokana na miundombinu duni ya usalama. Kukosa huduma bora na muhimu. Kutokupatikana kwa tovuti yako kila wakati. Ikiwa unataka kuchagua web host bora kwa ajili ya tovuti au blog yako, basi fahamu mambo 9 muhimu ya kuzingatia wakati wa kuchagua web host. 1. Bainisha mahitaji yako Kabla ya kuchagua web host ni muhimu ubainishe mahitaji yako kwanza. Je tovuti au blo...
Mambo 9 ya Kuzingatia Wakati Wa Kuchagua Kampuni ya Matangazo Kwenye Blog

Mambo 9 ya Kuzingatia Wakati Wa Kuchagua Kampuni ya Matangazo Kwenye Blog

Tovuti na Blogu
Kuweka matangazo kwenye blog ni njia mojawapo ya kupata pesa kupitia blog ambayo inafahamika kwa watu wengi. Kuna baadhi ya blog au tovuti ambazo zimefanikiwa kutengeneza pesa nyingi sana wakati nyingine zikiwa hazipati pesa za maana au hazipati kabisa kupitia njia hii ya matangazo. Kwa hakika watu wengi huchagua njia ya kuweka matangazo ya kampuni mbalimbali kwenye blog zao ili kujipatia kipato kutokana na kutokufahamu njia nyingine za kupata pesa au kutokana na kuona blog nyingine zikitumia njia hiyo. Ikiwa basi wewe ni mmojawapo wa watu wanaotaka kutumia njia ya kuweka matangazo kwenye blog ili kupata pesa, basi fahamu mambo 9 ya kuzingatia wakati wa kuchagua kampuni ya matangazo kwenye blog au tovuti yako. 1. Wakati sahihi Kuna wakati sahihi wa kujiunga na kampuni ya matang...
Madhara 8 ya Kunakili Machapisho kutoka Kwenye Blog au Tovuti Nyingine

Madhara 8 ya Kunakili Machapisho kutoka Kwenye Blog au Tovuti Nyingine

Tovuti na Blogu
Uandishi ni kazi ngumu na inayochosha, uandishi unahitaji kutafiti, muda, maarifa sahihi na hata rasilimali fedha. Kutokana na sababu hizi wamiliki wengi wa blog au tovuti hujikuta wakinakili maudhui kutoka kwenye blog au tovuti nyingine. Swala la kunakili maudhui kutoka kwenye blog au tovuti nyingine limekuwa likisababishwa pia na kukosa lengo, uvivu, kukosa ubunifu pamoja na kutokujua madhara ya kunakili. Ikiwa wewe ni blogger au mmiliki wa tovuti, basi karibu nikushirikishe madhara 8 yatokanayo na kunakili machapisho (post) kutoka kwenye blog au tovuti nyingine. 1. Hukufanya uonekane duni Unaponakili machapisho kutoka kwenye tovuti au blog nyingine, moja kwa moja unawaambia wasomaji wako kuwa huna cha kuwaambia kama usipomnakili mtu mwingine. Hivyo wasomaji wako watak...
Sababu 6 za Kwanini Hutakiwi kununua Followers na Likes

Sababu 6 za Kwanini Hutakiwi kununua Followers na Likes

Tovuti na Blogu
Nitatumia maneno haya kwenye makala hii: Followers - Wafuatiliaji Likes - Penda au Poa Post - Chapisho Comment - Maoni Kumbuka! Nitatumia pia ukurasa wetu wa Facebook kwa mifano ili uelewe kwa uhalisia zaidi. Inawezekana umeanzisha ukurasa wa Facebook au Twitter, na unashauku kubwa ya kuuendeleza. Lakini tatizo ni kuwa unauona ni dhaifu kutokana na kukosa likes au followers. Mara moja wazo linalokuja kwenye akili yako ni kutafuta njia za kuongeza likes na followers, ama kwa kununua au kwa njia nyingine. Unapofikiri hivyo jiulize maswali haya: Maana ya likes na followers kwenye ukurasa wangu ni nini? Je lengo langu ni nini? Je likes na followers vitanisaidia kufikia lengo? Je followers au likes za kununuliwa zinatokana na nini? Je kurasa au watu ...
Makosa 25 ya Kuepuka Unapotengeneza Tovuti (website) au Blog

Makosa 25 ya Kuepuka Unapotengeneza Tovuti (website) au Blog

Tovuti na Blogu
Kuna tovuti na blog nyingi zinazotengenezwa kila siku, lakini siyo zote zinakidhi viwango vya ubora. Hili linasababishwa na tovuti nyingi kutengenezwa bila kuzingatia kanuni muhimu za utengenezaji wa tovuti au blog. Zipo athari nyingi za kutengeneza tovuti zenye ubora mdogo kama vile kupoteza wasomaji au watembeleaji pamoja na kupata nafasi ndogo kwenye injini pekuzi. Ni muhimu ukafahamu kuwa  tovuti (website) au blog ni sura yako au ya biashara yako kwenye ulimwengu. Hivyo ikiwa hutozingatia utengenezaji bora wa tovuti au blog yako, basi utaharibu picha yako au ya biashara yako. Ikiwa unataka kutengeneza tovuti (website) au blog bora, basi fahamu makosa 25 yakuepuka wakati wa kutengeneza tovuti au blog. 1. Muundo mbaya wa tovuti au blog Kosa la muundo mbaya wa tovuti hufany...
Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Kipato, Tovuti na Blogu
Je unatafuta njia ya kujipatia pesa kwenye mtandao ambayo siyo ya utapeli? Blog ni njia moja wapo unayoweza kuitumia kujipatia fedha huku ukifanya kile ukipendacho. Katika makala hii nitakushirikisha njia 14 unazoweza kuzitumia kupata pesa kwa kutumia blog yako. Kumbuka! Hizi si njia za kupata pesa za mteremko haraka haraka kwa usiku mmoja. Kamwe usidanganywe na matangazo ya kuwa utafanywa kuwa tajiri mkubwa siku moja. Mambo hayaendi hivyo. Awali ya yote utahitaji kuwa na blog yako; pia utahitajika kuwekeza rasilimali ya muda au pesa kiasi fulani ili kuweza kuona matokeo kutokana na blog yako. 1. Kuwa wakala Unaweza kupata pesa kwenye blog yako kwa njia ya kuwa wakala wa wauzaji wa bidhaa au huduma mbalimbali. Mara mtu anunuapo kitu kwa kukifikia kupitia blog yako basi utapata ...
Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Kipato, Tovuti na Blogu
Kila mtu anahitaji kupata pesa ili kumudu mahitaji yake ya kila siku kama vile kununua chakula, nguo, kulipia matibabu, usafiri, ujenzi wa nyumba, n.k. Swali hapa ni kwa njia gani zitapatikana hizo pesa; kwani mara nyingi watu wanajikuta mishahara au kipato chao cha awali hakitoshi. Hivyo basi watu wanatafuta njia mbalimbali za kuwawezesha kuongeza kipato chao. Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamepelekea kukua kwa ajira na biashara katika mtandao; takwimu zinaonyesha kuwa kuna watu wengi wanaoomba na kufanya kazi katika matandao. Fuatana nami katika makala hii ili ufahamu mambo matano ya kuzingatia kabla ya kulenga kupata fedha kupitia kazi za kwenye mtandao. 1. Tovuti za matapeli Hivi leo ni rahisi kuona tovuti zinazojinadi kuwawezesha watu kupa kipato kwa urahisi ndani ...