Mtindo wa Maisha Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Mtindo wa Maisha

Madhara 8 ya Kusikiliza au Kutazama Mziki

Madhara 8 ya Kusikiliza au Kutazama Mziki

Mtindo wa Maisha
Kwa hakika kila jambo lenye uzuri au faida lina hasara zake. Nafahamu umekuwa ukisikia faida kede kede za kusikiliza mziki, lakini haujasikia kuwa kwa upande mwingine mziki unaweza kuwa na madhara kwako. Ikiwa wewe ni mpenzi wa muziki, ni vyema ukafahamu madhara ya kusikiliza au kutazama mziki ili uutawale mziki usikuathiri. 1. Huathiri afya ya masikio Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kumeibuka vifaa mbalimbali katika swala la utengenezaji, usambazaji na hata usikilizaji wa mziki. Kutokea kwa teknolojia ya vifaa vya kusikilizia mziki vijulikanavyo kama headphones au earphones kumesababisha watu wengi hasa vijana kusikiliza mziki karibu kila mahali na kila wakati. Taarifa mbalimbali za kitabibu zinaeleza kuwa vifaa hivi vimechangia sana kuharibu masikio au mfum...
Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu

Mtindo wa Maisha
Kahawa ni kinywaji maarufu na kinachopendwa sana na watu wengi. Kahawa pia imekuwa ni zao mashuhuri la kibiashara duniani kwa muda mrefu. Kwa hakika umaarufu na kupendwa kwa kinywaji cha kahawa unatokana na manufaa kadhaa yanayopatikana ndani ya kinywaji hiki. Ikiwa unapenda kunywa kahawa au unapenda kuongeza maarifa yako, basi fahamu faida 10 za kunywa kahawa. 1. Huchangamsha mwili Kahawa huwafanya watu wasijisikie kuchoka na huwaongezea kiwango cha nguvu za mwili. Caffeine inayopatikana kwenye kahawa huuchangamsha ubongo na kuufanya mwili kuwa katika hali nzuri. Hii ndiyo sababu watu wengi wenye kazi nyingi hupenda kunywa kahawa wakati wa kazi au baada ya kazi zao. 2. Huyeyusha mafuta mwilini Tafiti mbalimbali zinaeleza kuwa kahawa huchangia katika kuyeyusha mafuta mwili...
Faida 19 za Kula Maharage Kiafya

Faida 19 za Kula Maharage Kiafya

Mtindo wa Maisha
Maharage ni chakula ambacho watu wengi hukichukulia kama chakula cha hadhi ya chini kisichokuwa na manufaa kiafya. Watu wengi huchukulia vyakula kama vile nyama na samaki kuwa ni vya kitajiri wakati maharage yakichukuliwa kuwa ni chakula cha kimaskini. Huu ni upotoshaji, kwani maharage yana faida nyingi sana mwilini ambazo watu wasiokula maharage wanazikosa. Kwa kuwa lengo letu ni kukupa maarifa, basi karibu ufuatilie makala hii ili uweze kufahamu faida 19 za kula maharage. 1. Hupunguza lehemu (cholesterol) Moja kati ya vyakula vinavyopunguza lehemu mwilini ni maharage. Nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye maharage hujishikiza na lehemu ziwapo tumboni na kuzuia lehemu zaidi kufyonzwa mwilini. 2. Huzuia saratani Maharage ni chakula chenye madini ya manganese pamoja na vitamini K a...
Fahamu Faida 10 za Kuota Jua Kiafya

Fahamu Faida 10 za Kuota Jua Kiafya

Mtindo wa Maisha
Kuna mambo ambayo huwa tunayachukulia ya kawaida na wala hatuko tayari kufahamu umuhimu wake. Jua ni kitu mojawapo ambacho huwa tunakiona kila siku, lakini ni mara chache tumelichunguza. Kwa hakika kuna umuhimu mkubwa wa jua kwa mimea na viumbe vingine akiwemo binadamu. Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya, zimebaini kuwa kuna manufaa makubwa ya kuota jua angalau kwa kiasi fulani kila siku. Kwa kuwa najua unapenda afya bora, basi fahamu faida 10 za kuota jua kiafya. 1. Kuua bakteria Jua linaweza kutumiwa kuua bakteria mbalimbali katika majeraha na ngozi. Tiba hii iligunduliwa na mshindi wa tuzo ya Nobel Niels Finsen. Tiba hii ilitumiwa kuponya vidonda vya wanajeshi wa Kijerumani baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia. 2. Huondoa msongo wa mawazo Inakadiriwa mtu a...
Faida 15 za Kufunga Kula Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 15 za Kufunga Kula Unazotakiwa Kuzifahamu

Mtindo wa Maisha
Watu wengi wanafahamu kuwa kufunga kula ni swala linalohusiana na imani zaidi. Wengi hawafahamu kuwa kufunga kula kuna manufaa ya kiafya pia. Kufunga kula ni tendo lenye historia ndefu sana ambayo kimsingi chimbuko lake ni sababu za kiimani. Hata hivyo shuhuda na tafiti mbalimbali zimedhihirisha kuwa kuna manufaa mengine kemkem ya kufunga kula mbali na yale ya kiimani. Ikiwa basi unapenda kuongeza maarifa pamoja na kuboresha afya yako, fahamu faida 15 za kufunga kula. 1. Huboresha metaboli Metaboli ni mchakato ambao mwili hutumia virutubisho kutoka kwenye vyakula ili kujipa nguvu. Unapofunga kwanza unapumzisha mfumo wako wa umeng’enyaji, pili unaufanya mchakato wa metaboli kwenda vizuri kwani mwili utatumia vyema virutubisho vilivyoko mwilini tayari. 2. Huboresha mzunguko w...
Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Mtindo wa Maisha
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo. Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii. Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida 25 za kutembea kwa miguu. Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu. Huimarisha mifupa. Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi. Husaidia kupunguza uzito. Huzuia saratani ya utumbo mpana. Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua. Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance). Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya...
Faida 15 za Kula Tunda la Embe

Faida 15 za Kula Tunda la Embe

Mtindo wa Maisha
Embe ni tunda linalofahamika na kupendwa na watu wengi. Watu hula tunda hili moja kwa moja au kulitumia kutengeneza sharubati (juice). Kwa hakika ikiwa haupendi au haufahamu umuhimu wa tunda hili katika afya yako ni wakati wa kujifunza kitu sasa. Je unajua matunda ni muhimu kwa ajili ya afya yako? Karibu nikushirikishe faida 15 za kula tunda la embe. 1. Huboresha metaboli Embe ni tunda lenye nyuzinyuzi kwa kiasi kikubwa. Nyuzinuzi zinahitajika sana katika kufanya mchakato wa metaboli (mwili kutumia vrutubisho kujipa nguvu) kwenda vizuri. 2.Huboresha afya ya macho Kula embe kutakunufaisha kwa kulinda macho yako dhidi ya kudhoofu kwa misuli ya macho. Embe ni chanzo kizuri cha vitamini A ambayo ni muhimu kwa ajili ya macho. Soma pia: Aina 9 za Vyakula Vitakavyoboresha Uwezo W...
Faida 20 za Kula Parachichi

Faida 20 za Kula Parachichi

Mtindo wa Maisha
Parachichi ni aina ya kipekee ya tunda. Matunda mengi kwa asili ni wanga lakini parachichi limejaa mafuta yenye manufaa makubwa kiafya. Tafiti mbalimbali zilizofanyika zimebaini kuwa tunda la parachichi limesheheni manufaa makubwa katika afya ya mwanadamu. Ikiwa unapenda kuwa na afya bora kwa kula tunda la parachichi, basi karibu nikushirikishe faida 20 za kula tunda la parachichi. 1. Parachichi limejaa virutubisho mbalimbali Parachichi ni tunda la pekee ambalo limebeba virutubisho mbalimbali ambavyo ni muhimu kwa ajili ya miili yetu. Baadhi ya virutubisho vinavyopatikana kwenye parachichi ni: Kalori 240 (184 inatokana na mafuta) Miligramu 11 za sodiamu Gramu 13 za wanga Gramu 10 za nyuzinyuzi za lishe Gramu 1 tu ya sukari Vitamini K: asilimia 26 Vitamini...
Faida 10 za Kuogea Maji ya Baridi

Faida 10 za Kuogea Maji ya Baridi

Mtindo wa Maisha
Watu wengi hupenda kuogea maji ya moto, hii ni kutokana na kuogopa baridi au sababu za kimazoea tu. Ingawa mara nyingi umekuwa ukisisitiziwa kuwa maji moto yana manufaa mengi, lakini hata maji ya baridi nayo yana manufaa yake. Je uko tayari kuongeza maarifa au hata kubadili mtazamo wako? Karibu nikushirikishe faida 10 za kuogea maji ya baridi. 1. Huongeza utayari Maji ya baridi hukufanya uchangamke, hili ni tofauti na maji ya moto. Mara nyingi mtu anapoogea maji ya baridi hasa baada ya kuamka humfanya awe katika hali nzuri ya kuwa tayari kuendelea na majukumu yake. Kumbuka hata wakati wa kuogea maji baridi kasi ya upumuaji hubadilika na kukufanya kuongeza kiasi cha oksijeni kinachoingia mwilini. 2. Hulainisha ngozi na nywele Maji moto huchubua ngozi na nywele, hasa kwa kuondo...
Sababu 7 za Kwanini Kila Mwanaume Anatakiwa Kujua kupika

Sababu 7 za Kwanini Kila Mwanaume Anatakiwa Kujua kupika

Mtindo wa Maisha
Kutokana na asili ya utamaduni wa Kiafrika, bado kwa kiasi kikubwa swala la kupika linachukuliwa kama kazi ya mwanamke. Wanaume wengi hawafahamu kupika wala hawataki kujifunza kupika. Nimeshuhudia wengi wakiwa tayari kula hotelini au kula mikate pindi wakosapo watu wa kuwapikia chakula. Kwa hakika yapo mambo mengi mazuri ambayo mwanaume asiyejua kupika anayakosa. Karibu nikushirikishe sababu 7 za kwanini kila mwanaume anatakiwa kujua kupika; nami naamini baada ya makala hii utajifunza mengi na kuhamasika. 1. Kuweza kula unachokitaka Kwa njia ya kufahamu kupika unaweza kula chakula unachotaka ambacho isingekuwa rahisi kukipata hotelini au kupikiwa na mtu mwingine. Ikiwa pia kuna aina fulani ya upishi unaipenda, basi kwa njia ya kufahamu kupika utaweza kuifanya wewe mwenyewe. ...