Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu - Fahamu Hili
Friday, April 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Kahawa

Kahawa ni kinywaji maarufu na kinachopendwa sana na watu wengi. Kahawa pia imekuwa ni zao mashuhuri la kibiashara duniani kwa muda mrefu.

Kwa hakika umaarufu na kupendwa kwa kinywaji cha kahawa unatokana na manufaa kadhaa yanayopatikana ndani ya kinywaji hiki.

Ikiwa unapenda kunywa kahawa au unapenda kuongeza maarifa yako, basi fahamu faida 10 za kunywa kahawa.

1. Huchangamsha mwili

Kahawa huwafanya watu wasijisikie kuchoka na huwaongezea kiwango cha nguvu za mwili. Caffeine inayopatikana kwenye kahawa huuchangamsha ubongo na kuufanya mwili kuwa katika hali nzuri.

Hii ndiyo sababu watu wengi wenye kazi nyingi hupenda kunywa kahawa wakati wa kazi au baada ya kazi zao.

2. Huyeyusha mafuta mwilini

Tafiti mbalimbali zinaeleza kuwa kahawa huchangia katika kuyeyusha mafuta mwilini na kupelekea kupunguza uzito wa mwili.

Utafiti mmoja uliofanyika ulibaini kuwa kahawa iliweza kusaidia kupunguza mafuta kwa watu wanene kwa asilimia 10 na kwa asilimia 29 kwa watu wembamba.

3. Kahawa ina virutubisho muhimu

Kahawa ni kinywaji chenye virutubisho muhimu kwa ajili ya afya za miili yetu.

Inaelezwa kuwa kikombe kimoja cha kahawa kina virutubisho vifuatavyo:

  • Riboflavin (Vitamini B2): 11%.
  • Asidi ya Pantothenic (Vitamini B5): 6%.
  • Manganese na Potasiamu: 3%.
  • Magnesiamu na Niacin (B3): 2%.

Hivyo kunywa vikombe 2-3 kwa siku kutaongeza kiwango cha virutubisho hivi.

4. Hukabili aina ya pili ya kisukari

Kisukari ni ugonjwa ambao mwili hushindwa kutawala kiwango cha sukari mwilini. Inakadiriwa kuwa ugonjwa huu unawatesa zaidi ya watu milioni 300 duniani kote.

Hata hivyo, inasadikiwa kuwa watumiaji wa kahawa wana hatari ndogo ya kupata aina ya pili ya kisukari (type 2 diabetes).

5. Huzuia maradhi ya kupoteza kumbukumbu

Maradhi ya kupoteza kumbukumbu huwakabili watu wengi hasa wenye umri wa kuanzia miaka 65.

Kwa sasa hakuna tiba ya maradhi haya lakini yanaweza kuzuiwa au kupunguzwa kwa lishe bora pamoja na mazoezi.

Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa watu wanaokunywa kahawa hupunguza kama siyo kukabili athari za maradhi haya kwa asilimia 65.

6. Hulinda afya ya ini

Ini ni kiungo muhimu sana kwenye mwili wa binadamu. Hata hivyo maradhi kama vile uvimbe kwenye ini (hepatitis) pamoja na tatizo la seli za ini kugeuka makovu (cirrhosis), huathiri afya ya ini kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande mwingine tafiti zinaeleza kuwa kahawa hupunguza uwezo wa seli za ini kuwa makovu (cirrhosis) kwa asilimia 80.

Soma pia: Madhara 12 ya Pombe Kiafya

7. Huondoa msongo wa mawazo

Msongo wa mawazo ni tatizo baya la kiakili na kisaikolojia ambalo linaweza kuathiri maisha kwa kiasi kikubwa hata kusababisha kifo.

Inaelezwa kuwa watu wanaokunywa angalau vikombe vinne vya kahawa kila siku hupunguza msongo wa mawazo kwa kiasi kikubwa.

8. Hukabili baadhi ya saratani

Saratani ni maradhi yanayoua watu wengi sana duniani ambayo husababishwa na kukua kwa seli zisizo za kawaida ndani ya mwili wa binadamu.

Kahawa husaidia kupunguza kutokea kwa saratani ya ini na ile ya utumbo kwa asilimia 40.

9. Hukabili maradhi ya moyo na kiharusi

Watafiti mbalimbali wa afya wanaeleza kuwa kahawa haisababishi maradhi ya moyo pia huzuia kwa asilimia 20 uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa kiharusi (stroke).

10. Hukufanya uishi muda mrefu

Kama ulivyotangulia kusoma katika hoja zilizotangulia kuwa kahawa huzuia maradhi mbalimbali. Hivyo huwafanya watu wanaokunywa kahawa kuishi muda mrefu zaidi kwa kuwaepushia kufa mapema.

Watafiti wanaeleza kuwa hatari ya kifo hupungua kwa silimia 20 kwa wanaume na asilimia 26 kwa wanawake wanaokunywa kahawa.

Soma pia: Sababu 6 za Kwanini Mara Nyingi Wanawake Huishi Zaidi ya Wanaume

Hitimisho

Naamini baada ya kusoma makala hii hutokunywa tena kahawa kwa mazoea au kupuuza unywaji wa kahawa kwani una manufaa kemkem.

Sanjari na hayo ni muhimu kukumbuka kuwa kila kitu chenye uzuri kina ubaya wake, hivyo ni muhimu kuwa na kiasi katika mambo yote ikiwemo unywaji wa kahawa.

Soma pia: Njia 12 za Kuondoa Sumu Mwilini

Je wewe huwa unakunywa kahawa? Je unanufaika vipi? Tafadhali tuandikie maoni yako kisha washirikishe wengine makala hii.

4.1 20 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

20 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
mwajabu
mwajabu
4 years ago

ina faida nyingi hasa katika kujenga mwili

Kornelio Maanga
Reply to  mwajabu
4 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Ndanginga Zablon Ndaki
Ndanginga Zablon Ndaki
4 years ago

Asante kwa somo zuri

Kornelio Maanga
Reply to  Ndanginga Zablon Ndaki
4 years ago

Tunashukuru sana kwa kuwa msomaji wetu; pia tunashukuru kwa maoni yako ya thamani; tunakutakia kila la heri katika kutimiza malengo yako…karibu sana Fahamuhili.

allyjafari
allyjafari
Reply to  Kornelio Maanga
4 years ago

mimi bila kunywa kahawa nakuwa mchovu sana nasinzia hovyo hovyo ukweli kahawa ni mkombozi wangu kimawazo kiakili

Kornelio Maanga
Reply to  allyjafari
3 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

santieli john
santieli john
Reply to  Kornelio Maanga
4 years ago

Asante jmn nlikuwa sijui

Kornelio Maanga
Reply to  santieli john
3 years ago

Asante sana; karibu sana Fahamuhili.com

Henry msinga
Henry msinga
3 years ago

Aisee kahawa n nzur Sana. Inaondoa usingiz

Kornelio Maanga
Reply to  Henry msinga
3 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Christopher mtiso
Christopher mtiso
2 years ago

Asante kwa somo !
Swali.
Nini madhara ya utumiaji kahawa kupitiliza?

Kornelio Maanga
Reply to  Christopher mtiso
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Tutajitahidi kuandaa makala juu ya hilo. Karibu sana Fahamuhili.com

Rob
Rob
Reply to  Kornelio Maanga
1 year ago

Nimefurah sana.Taratiiiiibu naanzisha utaratibu wa kunywa kahawa.

Kornelio Maanga
Reply to  Rob
1 year ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com

Batholomeo Shija
Batholomeo Shija
2 years ago

Hongeraihho

julius shayo
julius shayo
1 year ago

tunashuku kwa kujua faida za kunya kahawa nimejifunza vitu vingi vya unyaji wa kawaha

Kornelio Maanga
Reply to  julius shayo
8 months ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Hilaria
Hilaria
1 year ago

jmn naomben msaada m kahawa naipebda sana lakin nikinywa ndo napata usingiz nisipokunywa silala,ila nikinywatu naanza kusinzia nifanyeje wadau

Issack
Issack
1 year ago

Huwa nasikia kahawa inaadhiri moyo
Kivipi inawezA

BONIPHACE MARCO
BONIPHACE MARCO
1 year ago

Napenda Sana ujumbe huu

20
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x