Eston J., Author at Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Eston J.

Eston ni mtafiti na mwandishi wa makala mbalimbali zinazohusu tija, maendeleo binafsi pamoja na afya bora. Analenga kuwahamasisha wengine pamoja na kuubadili ulimwengu kwa kupitia maarifa stahiki.
Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 10 za Kunywa Kahawa Unazotakiwa Kuzifahamu

Mtindo wa Maisha
Kahawa ni kinywaji maarufu na kinachopendwa sana na watu wengi. Kahawa pia imekuwa ni zao mashuhuri la kibiashara duniani kwa muda mrefu. Kwa hakika umaarufu na kupendwa kwa kinywaji cha kahawa unatokana na manufaa kadhaa yanayopatikana ndani ya kinywaji hiki. Ikiwa unapenda kunywa kahawa au unapenda kuongeza maarifa yako, basi fahamu faida 10 za kunywa kahawa. 1. Huchangamsha mwili Kahawa huwafanya watu wasijisikie kuchoka na huwaongezea kiwango cha nguvu za mwili. Caffeine inayopatikana kwenye kahawa huuchangamsha ubongo na kuufanya mwili kuwa katika hali nzuri. Hii ndiyo sababu watu wengi wenye kazi nyingi hupenda kunywa kahawa wakati wa kazi au baada ya kazi zao. 2. Huyeyusha mafuta mwilini Tafiti mbalimbali zinaeleza kuwa kahawa huchangia katika kuyeyusha mafuta mwili...
Athari 8 Kiafya za Dawa za Kuulia Wadudu — Viwatilifu

Athari 8 Kiafya za Dawa za Kuulia Wadudu — Viwatilifu

Afya
Dawa za kuulia wadudu maarufu kama viwatilifu zimetengenezwa kwa lengo la kuangamiza wadudu wanaoharibu mazao au wanaomdhuru binadamu. Hata hivyo kutokana na sababu kuwa lengo la dawa hizi ni kuangamiza, huathiri pia viumbe hai vingine akiwemo binadamu. Takwimu kutoka shirika la afya duniani WHO zinabainisha kuwa kuna zaidi ya vifo 220,000 vitokanavyo na athari za sumu zilizoko kwenye dawa za kuulia wadudu—viwatilifu. Ikiwa unataka kuweka afya yako salama, basi karibu nikushirikishe athari 8 kiafya za dawa za kuulia wadudu — viwatilifu. 1. Husababisha saratani Watafiti mbalimbali wa maradhi ya saratani wanaeleza kuwa dawa za kuulia wadudu zinachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha seli za saratani mara zinapoingia kwenye mwili wa binadamu. Hatari hii hutokea zaidi pale amb...
Faida 19 za Kula Maharage Kiafya

Faida 19 za Kula Maharage Kiafya

Mtindo wa Maisha
Maharage ni chakula ambacho watu wengi hukichukulia kama chakula cha hadhi ya chini kisichokuwa na manufaa kiafya. Watu wengi huchukulia vyakula kama vile nyama na samaki kuwa ni vya kitajiri wakati maharage yakichukuliwa kuwa ni chakula cha kimaskini. Huu ni upotoshaji, kwani maharage yana faida nyingi sana mwilini ambazo watu wasiokula maharage wanazikosa. Kwa kuwa lengo letu ni kukupa maarifa, basi karibu ufuatilie makala hii ili uweze kufahamu faida 19 za kula maharage. 1. Hupunguza lehemu (cholesterol) Moja kati ya vyakula vinavyopunguza lehemu mwilini ni maharage. Nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye maharage hujishikiza na lehemu ziwapo tumboni na kuzuia lehemu zaidi kufyonzwa mwilini. 2. Huzuia saratani Maharage ni chakula chenye madini ya manganese pamoja na vitamini K a...
Fahamu Faida 10 za Kuota Jua Kiafya

Fahamu Faida 10 za Kuota Jua Kiafya

Mtindo wa Maisha
Kuna mambo ambayo huwa tunayachukulia ya kawaida na wala hatuko tayari kufahamu umuhimu wake. Jua ni kitu mojawapo ambacho huwa tunakiona kila siku, lakini ni mara chache tumelichunguza. Kwa hakika kuna umuhimu mkubwa wa jua kwa mimea na viumbe vingine akiwemo binadamu. Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya, zimebaini kuwa kuna manufaa makubwa ya kuota jua angalau kwa kiasi fulani kila siku. Kwa kuwa najua unapenda afya bora, basi fahamu faida 10 za kuota jua kiafya. 1. Kuua bakteria Jua linaweza kutumiwa kuua bakteria mbalimbali katika majeraha na ngozi. Tiba hii iligunduliwa na mshindi wa tuzo ya Nobel Niels Finsen. Tiba hii ilitumiwa kuponya vidonda vya wanajeshi wa Kijerumani baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia. 2. Huondoa msongo wa mawazo Inakadiriwa mtu a...
Sababu 10 za Kwa nini Unatakiwa Kuacha Kuvuta Sigara

Sababu 10 za Kwa nini Unatakiwa Kuacha Kuvuta Sigara

Afya
Kuna baadhi ya tabia kuzianza ni rahisi sana, lakini kuziacha kunakuwa ni kugumu. Watu wengi hasa vijana, hushawishiwa na marafiki kuingia kwenye tabia kama vile unywaji wa pombe, uvutaji sigara au kutumia madawa ya kulevya bila kufahamu madhara yake. Hakika kuna madhara mengi sana yatokanayo na uvutaji wa sigara kiafya, kiakili, kijamii na kiuchumi. Ikiwa basi unataka kufahamu sababu za kwanini unatakiwa kuacha kuvuta sigara, basi karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe sababu 10 za kuacha kuvuta sigara. 1. Unaokoa pesa Moja kati ya mambo yanayowapotezea watu pesa ni tabia kama vile uvutaji wa sigara. Kwa kuacha kuvuta sigara utaweza kuokoa pesa ambazo huwa unazitumia kwa ajili ya kununua sigara, na kuzitumia kufanya mambo mengine yenye manufaa kwako. Soma pia: Njia 10 Zitakaz...
Vitu 20 Usivyotakiwa Kusema Wakati wa Usaili wa Kazi (Job Interview)

Vitu 20 Usivyotakiwa Kusema Wakati wa Usaili wa Kazi (Job Interview)

Tija
Inawezekana una maarifa stahiki pamoja na uzoefu unaohitajika kwenye kazi fulani, lakini ukakosa kazi hiyo kutokana na vitu ulivyosema au kufanya wakati wa usaili wa kazi. Ni muhimu kufahamu kuwa lengo la usahili wa kazi siyo kukufahamu wewe au kufahamu matakwa yako, bali ni kutathimini kama unafaa kwenye kazi au kampuni husika. Hivyo ni muhimu kuhakikisha yale yote unayoyasema na kuyafanya kwenye usaili, yanaonyesha kufaa kwako kwenye kazi husika. Ikiwa unatafuta kazi au umeitwa kwenye usaili wa kazi, basi fahamu vitu 20 ambavyo hutakiwi kuvisema au kuvifanya wakati wa usaili wa kazi (Job Interview). Sipendi kazi yangu ya sasa au ya awali. (Kwa hiyo utachukia na hii unayoomba?) Mwajiri wangu wa awali ni mbaya. Kwa kusema hivi utaonekana utamchukia na huyu wa sasa. ...
Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Afya
Hakuna mtu anayependa kupata majeraha au kuchelewa kupona majeraha. Kwa kuwa uhai na uzima wetu haupo mikononi mwetu, ni vyema tukafahamu kuwa kuna wakati tunaweza kuumia. Kwa kutambua hili karibu nikufahamishe mambo matano unayoweza kuyafanya ili kuharakisha kupona majeraha. 1. Kula vizuri Lishe bora ni muhimu wakati wote, lakini ni muhimu zaidi mara unapokuwa na majeraha. Ili uweze kupona majeraha mapema unahitaji ule matunda na vyakula vyenye protini, vitamini C, B12 pamoja na madini ya chuma kwa wingi. Vyakula na matunda hayo ni kama vile machungwa, mapapai, mayai, maziwa, samaki, maharage, n.k. Kwa kula vyakula hivi mwili utaweza kutibu majeraha kwa haraka zaidi. 2. Pumzika vya kutosha Kupumzika ni njia ya kuupa mwili nafasi ya kujijenga na kujitibu wakati wa majeraha. K...
Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Mtindo wa Maisha
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo. Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii. Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida 25 za kutembea kwa miguu. Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu. Huimarisha mifupa. Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi. Husaidia kupunguza uzito. Huzuia saratani ya utumbo mpana. Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua. Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance). Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya...
Madhara 6 ya Kutumia Dawa Bila Ushauri wa Kitaalamu

Madhara 6 ya Kutumia Dawa Bila Ushauri wa Kitaalamu

Afya
Mara nyingi watu wanaugua maradhi mbalimbali, lakini wengi wao hawapendi kwenda hospitali kufanya vipimo au kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari. Kutokana na uwepo wa maduka ya dawa baridi, watu wengi wanapojisikia kuwa wagonjwa, hununua dawa kwenye maduka hayo na kuanza kuzitumia. Ni ukweli usiopingika kuwa dawa zimetengenezwa ili kutibu maradhi fulani ambayo yatabainika kwa mgonjwa baada ya uchunguzi wa kitaalamu. Hivyo matumizi ya dawa bila kufanya uchunguzi wa kitaalamu yanaweza kuwa na madhara makubwa kwenye afya yako. Fahamu madhara 6 ya kutumia dawa bila ushauri au uchunguzi wa kitaalamu. 1. Huongeza sumu mwilini Dawa zimetengenezwa kwa kutumia kemikali mbalimbali ambazo kimsingi ni sumu zinazoua vimelea vya magonjwa. Hivyo kutumia dawa bila vipimo kunaku...
Faida 15 za Kula Tunda la Embe

Faida 15 za Kula Tunda la Embe

Mtindo wa Maisha
Embe ni tunda linalofahamika na kupendwa na watu wengi. Watu hula tunda hili moja kwa moja au kulitumia kutengeneza sharubati (juice). Kwa hakika ikiwa haupendi au haufahamu umuhimu wa tunda hili katika afya yako ni wakati wa kujifunza kitu sasa. Je unajua matunda ni muhimu kwa ajili ya afya yako? Karibu nikushirikishe faida 15 za kula tunda la embe. 1. Huboresha metaboli Embe ni tunda lenye nyuzinyuzi kwa kiasi kikubwa. Nyuzinuzi zinahitajika sana katika kufanya mchakato wa metaboli (mwili kutumia vrutubisho kujipa nguvu) kwenda vizuri. 2.Huboresha afya ya macho Kula embe kutakunufaisha kwa kulinda macho yako dhidi ya kudhoofu kwa misuli ya macho. Embe ni chanzo kizuri cha vitamini A ambayo ni muhimu kwa ajili ya macho. Soma pia: Aina 9 za Vyakula Vitakavyoboresha Uwezo W...