Maarifa Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Maarifa

Madaraja 15 Makubwa au Marefu Zaidi Duniani

Madaraja 15 Makubwa au Marefu Zaidi Duniani

Maarifa
Kwa siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa maendeleo makubwa katika shughuli mbalimbali za binadamu. Sekta ya ujenzi na usafiri ni moja kati ya sekta ambazo binadamu amepiga hatua kubwa. Kila siku kumekuwa kukibuniwa na kufanyika maboresho mbalimbali katika miundombinu ya usafirishaji. Kumeshuhudiwa ujenzi wa barabara za kisasa, reli, viwanja vya ndege au hata kubuniwa kwa baadhi ya aina mpya za usafiri. Kutokana na hili, yapo madaraja mbalimbali yaliyojengwa sehemu mbalimbali duniani ili kuboresha usafiri wa barabara na reli. Karibu uongeze maarifa yako kwa kufahamu madaraja 15 makubwa au marefu zaidi duniani kwa sasa. 1. Daraja la Danyang–Kunshan Daraja la Danyang–Kunshan ndilo daraja refu kuliko yote duniani, lina urefu wa kilometa 164.8. Daraja hili linapatikana huko China kat...
Yafahamu Majengo 10 Marefu Zaidi Duniani

Yafahamu Majengo 10 Marefu Zaidi Duniani

Maarifa
Dunia imeendelea kushuhudia uhaba mkubwa wa rasilimali mbalimbali kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu. Moja ya rasilimali ambazo zimekua adimu sana duniani kwa wakati huu ni ardhi, uhaba wa ardhi umefanya wahandisi kote duniani kuumiza vichwa vyao kufikiri namna ambavyo ardhi iliyopo itatumika vyema na kwa manufaa zaidi kwa wengi. Pamoja na sababu nyingine lukuki, ufinyu wa ardhi umechangia kwa kiasi kikubwa kujengwa kwa majengo marefu na ya kushangaza katika maeneo mbalimbali duniani. Yafuatayo ni majengo kumi marefu zaidi duniani maarufu kama sky scrapers kwa lugha ya kimombo. 10. International Commerce Centre Jengo hili linashika nafasi ya kumi kwa majengo marefu zaidi duniani. Lina urefu wa mita 484 pamoja na ghorofa 108; lilijengwa mwaka 2010. 09. Shanghai worl...
Maeneo 10 Ambayo ni Marufuku Kubusu au Kukumbatiana Hadharani

Maeneo 10 Ambayo ni Marufuku Kubusu au Kukumbatiana Hadharani

Maarifa
Wakati kwenye maeneo mengine kubusu au kukumbatiana kati ya mwanamke na mwanaume ni jambo la kawaida, kwenye maeneo mengine ni kosa kubwa. Baadhi ya nchi za kimagharibi zimewapa raia wake uhuru kiasi cha kuweza hata kufanya matendo ya faragha hadharani. Lakini baadi ya nchi, hasa zile zenye misingi imara ya kidini, zimepiga marufuku kuonyesha hisia za kimapenzi hadharani. Kwa kuwa lengo letu ni kukupa maarifa, basi fahamu maeneo 10 ambayo ni marufuku kubusu au kukumbatiana baina ya mwanamke na mwanaume hadharani. 1. Qatar Qatar ni nchi yenye utamaduni wa Kiislamu ambayo hairuhusu mtu kubusu au kukumbatiana hadharani. Hata hivyo matendo haya baina ya wanafamilia au marafiki wa jinsia moja (wasio mashoga) siyo jambo baya. 2. India Kwa mujibu wa sheria za India, mtu atak...
Virusi 10 vya Kompyuta Hatari Zaidi Kuwahi Kutokea

Virusi 10 vya Kompyuta Hatari Zaidi Kuwahi Kutokea

Maarifa
Virusi vya kompyuta ni tatizo la muda mrefu ambalo limeathiri watu wengi kwa namna moja au nyingine. Inawezekana wewe ni mmojawapo kati ya wale waliowahi kuathiriwa na virusi vya kompyuta; inawezekana pia hujawahi kuathiriwa au hata kusikia swala hili kabisa. Katika muda ambao Mungu amenijalia kutumia kompyuta (2002 - hadi sasa), nimeshuhudia mengi na kukabiliana na mengi kuhusu virusi vya kompyuta. Nimewahi kuona watu wakilia kwa kupoteza taarifa muhimu, wengine wakitoa fedha nyingi kutengeneza kompyuta zao zilizoathirika. Mimi mwenyewe nimewahi kuathiriwa mara kadhaa na virusi hivi. Hivyo basi, hebu leo tutazame virusi 10 vya kompyuta vilivyowahi kutokea ambavyo ni hatari zaidi. 1. Code Red Kirusi cha Code Red kiliibuka mnamo mwaka 2001 na kubainiwa na wafanyakazi wawi...
Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu

Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu

Maarifa
Hofu ni hisia ambazo zinatulinda na vitisho vinavyotuzunguka. Kila mtu ana hofu, lakini viwango na aina ya hofu hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Wapo watu ambao huhofu juu ya vitu na mambo mbalimbali hadi kushindwa kuendelea na majukumu au maisha yao ya kawaida. Ikiwa unapenda kufahamu aina za hofu (phobia) ili pia uchunguze kama una aina hizo basi fuatilia makala hii nikufahamishe aina 70 za hofu. Pogonophobia – Pogonophobia ni hofu ya kuogopa ndevu au kukaa karibu na mtu mwenye ndevu. Hofu hii huwapata zaidi wanawake. Astraphobia – Hofu hii pia inajulikana kama astrapophobia, brontophobia, keraunophobia, au tonitrophobia; hii ni hofu ya kuogopa radi. Photophobia – Hii ni hofu ya kuogopa mwanga; mara nyingi husababishwa na matatizo ya kiafya ya macho. So...
Fahamu Vitu Vilivyotengenezwa Upya (recycled) na Kuzalisha Vitu Vingine vya Kuvutia

Fahamu Vitu Vilivyotengenezwa Upya (recycled) na Kuzalisha Vitu Vingine vya Kuvutia

Maarifa
Hivi leo wabunifu mbalimbali wametokea duniani. Wabunifu wengine wamejikita kwenye kutumia ubunifu wao kukabiliana na changamoto mbalimbali hasa za uharibifu wa mazingira. Wapo watu na wabunifu mbalimbali walioona umuhimu wakutengeneza (recycle) tena vitu mbalimbali ambavyo matumizi yake yamekwisha, ili vifae tena kwa matumizi mengine. Mara nyingi tumeshuhudia magurudumu, chupa, mapipa, na hata vifaa vya mitambo mbalimbali vikitupwa hovyo baada ya kumalizika kwa matumizi yake. Lakini sasa ungana nami nikushirikishe vitu kadhaa vilivyotengenezwa upya (recycled) na kuzalisha vitu vya kuvutia na vyenye tija kubwa. 1. Mapipa ya kemikali na mafuta 2. Matairi yaliyozeeka 3. Injini ya gari na sehemu nyingine za gari 4. Sehemu za baisikeli 5. Chupa za plastiki Picha hizi...
Mambo 20 ya Kukushangaza Kuhusu Dhahabu

Mambo 20 ya Kukushangaza Kuhusu Dhahabu

Maarifa
Dhahabu ni moja kati ya madini ya thamani duniani. Dhahabu huchimbwa katika sehemu mbalimbali duniani na kisha kutumiwa kutengeneza vitu mbalimbali kama vile fedha, medali, vito vya thamani n.k Nchi nyingi zimejizolea utajiri mkubwa kutokana na madini haya; pamoja na utajiri huu pia nchi nyingi zimesababishiwa uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na uchimbaji wa dhahabu. Naamini umewahi kusikia mengi kuhusu dhahabu, lakini sasa fuatilia makala hii nikufahamishe mambo 20 yakushangaza kuhusu dhahabu. Katika tani moja ya simu za mkononi unaweza kupata dhahabu nyingi zaidi kuliko ambayo ungeipata kutoka kwenye gwangala la dhahabu (gold ore). Ikiwa utafanikiwa kukusanya dhahabu yote iliyoko baharini, basi kila mtu duniani anaweza kupata dhahabu takriban kilo 4. Inakadiriwa k...
Mambo 20 Usiyoyajua Kuhusu Jengo Refu Zaidi Duniani la Burj Khalifa

Mambo 20 Usiyoyajua Kuhusu Jengo Refu Zaidi Duniani la Burj Khalifa

Maarifa
Je unalifahamu jengo la Burj Khalifa lililoko Dubai? Burj Khalifa ni jengo refu zaidi duniani linalodhihirisha uwezo mkubwa wa wahandisi majengo wa karne ya 21. Unapozungumzia urefu wake au kutazama muundo wake, kwa hakika jengo hili litakushangaza; jengo hili liligharimu takriban dola bilioni 1.5 za Kimarekani kulijenga. Pamoja na kuwa ni jengo refu zaidi duniani, jengo hili limevunja rekodi nyingine kadha wa kadha zilizokuwa zimewekwa na majengo mengine. Naamini unapenda kulifahamu zaidi ili kuongeza maarifa yako. Karibu ufuatilie makala hii ili nikujulishe mambo 20 usiyoyajua kuhusu jengo hili la Burj Khalifa. Burj Khalifa ni jengo refu zaidi lililotengenezwa na binadamu duniani, lina urefu wa futi 2,723 au mita 829.8 kutoka kwenye kilele chake hadi ardhini. Hivyo kulifanya ...
Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Maarifa
Kila siku binadamu anafanya shughuli mbalimbali katika kuandaa au kutengeneza mazingira bora kwa ajili yake kuishi. Kazi hii zinahusisha ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji, makazi, viwanda, ofisi n.k. Hata hivyo, shughuli hizi za binadamu hupelekea uharibifu mkubwa wa mazingira ya asili ikiwemo misitu, mito, milima, wanyama, maziwa, hewa n.k Wapo watu waliolitambua hili na kuamua kufanya kazi zao kwa kuzingatia kulinda na kuheshimu mazingira ya asili. Karibu utazame picha kadha wa kadha zinazonyesha kazi hizo. 1. Nyumba ya duara iliyojengewa kwenye mti huko Tokyo, Japan 2. Mgahawa wa kahawa huko Shanghai, China 3. Mti katikati ya nyumba huko Almaty, Kazakhstan 4. Mti kwenye hoteli huko Izmir Uturuki 5. Nyumba ya makazi huko West Virginia 6. Nyumba iliyojengwa katik...
Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Maarifa, Teknolojia
Hakika ulimwengu huu una  mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu. Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua. Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web) Deep web ni nini? Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane. ...