Hamasa Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Hamasa

Faida 7 za Kuwa na Uvumilivu Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 7 za Kuwa na Uvumilivu Unazotakiwa Kuzifahamu

Hamasa
Maisha yana milima na mabonde, kipindi cha raha na shida. Katika kipindi cha shida au wakati mtu anapokutana na changamoto swala la uvumilivu linahitajika sana, tena sana. Kukosa uvumilivu kumewafanya wengi kushindwa kufanya maamuzi sahihi na kujikuta wakitumbukia kwenye shida zaidi. Haijalishi unapitia magumu mengi kiasi gani, kuvumilia ni lazima. Ikiwa unataka kujifunza faida au umuhimu wa uvumilivu, basi fahamu faida 7 za uvumilivu katika maisha yako. 1. Hukuwezesha kufanya maamuzi sahihi Ndani ya uvumilivu kuna subira, ikumbukwe kuwa wahenga walisema subira yavuta heri. Hii ina maana kuwa kufanya maamuzi mara ukutanapo na changamoto kunaweza kukusababishia kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Kwa mfano hebu fikiri mtu ameachwa na mchumba wake ghafla naye mara moja anataka kupa...
Mambo 6 Unayoweza Kujifunza Kutoka Kwa Mashabiki wa Mpira wa Miguu

Mambo 6 Unayoweza Kujifunza Kutoka Kwa Mashabiki wa Mpira wa Miguu

Hamasa
Mchezo wa mpira wa miguu ulianza takriban kati ya karne ya 2 na ya 3 KB huko China. Mchezo huu umejizolea umaarufu mkubwa na kuwa chanzo cha kipato kwa watu wengi. Mpira wa miguu ni mchezo unaopendwa na watu wengi duniani, inakadiriwa kuwa mchezo huu una mamilioni ya mashabiki kote duniani. Kumeshuhudiwa mashabiki wa mpira wa miguu wakijitoa kwa dhati kushabikia timu zao; jambo hili limewagharimu pesa, muda au hata uhai wao. Kwa mtu yoyote mwenye shauku ya kupata maarifa, anaweza kujifunza kitu kutoka kwa mashabiki wa mpira wa miguu; Ikiwa unapenda maarifa, basi karibu nikufahamishe mambo 6 unayoweza kujifunza kutoka kwa mashabiki wa mpira wa miguu. 1. Mapenzi ya dhati Huwezi ukakosa swala la mapenzi ya dhati kwa timu pamoja na mchezo wenyewe kwa shabiki yeyote yule wa mpira...
Mambo 12 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Bill Gates

Mambo 12 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Bill Gates

Hamasa
Kwa mujibu wa Forbes 2017, Bill Gates ndiye mtu tajiri zaidi duniani akiwa na utajiri unaokadiriwa kuwa dola za Marekani bilioni 86. Bill Gates ndiye mwanzilishi na mmiliki wa kampuni ya Microsoft. Microsoft ni kampuni iliyotengeneza programu endeshi (operating system) maarufu na mashuhuri sana duniani ya Window. Kampuni hii pia inazalisha bidhaa nyingine kama vile vifaa vya michezo ya kielektroniki, pogramu mbalimbali pamoja na vifaa vingine vya kiteknolojia. Kwa hakika Bill Gates ni mtu aliyefanikiwa sana ambaye kila mtu anayetaka kufanikiwa anaweza kujifunza mambo kadhaa kutoka kwake. Kwa kutambua umuhimu wa kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa, karibu nikushirikishe mambo 12 unayoweza kujifunza kutoka kwa Bill Gates. 1. Anza mapema kadri iwezekanavyo Bill Gates alianza kuj...
Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha

Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha

Hamasa
Kila mtu ana maana yake ya mafanikio. Ni wazi kuwa mafanikio ni kuweza kukabiliana na changamoto au kushindwa bila kukata tamaa au kuacha. Mara nyingi huwa napenda kusoma nukuu (Quotes) mbalimbali kwani huwa zinanipa hamasa kubwa ya kuzidi kufanyia kazi ndoto zangu. Naamini hata wewe unaweza kuhamasika na kupata ari zaidi kwa kusoma nukuu hizi 30 za mafanikio. Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazo Kuhamasisha Maishani Mwako. Naamini umehamasika na kupata shauku zaidi ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako ili ufanikiwe. Kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu. Naamini umebaini wazi kuwa maana ya mafanikio ni pana; pia mafanikio siyo kutokukabiliana na cha...
Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako

Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako

Hamasa
Yale tunayoyawaza na kuyatafakari kwenye fikra zetu yana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu. Ikiwa tunataka kufanikiwa basi ni lazima tufikiri na kutafakari juu ya kufanikiwa. Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani, ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu vitakavyotuhamasisha. Karibu nikufahamishe nukuu 50 (quotes) ambazo zitakuhamasisha katika maswala mbalimbali unayoyafanya maishani mwako. Naamini umehamasika na kufurahia nukuu hizi za hamasa. Ni wazi kuwa kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu - tunavyowaza ndivyo ...
Mpiga Ngoma Maarufu wa Mtaani Anayetengeneza Midundo kwa Kutumia Ndoo

Mpiga Ngoma Maarufu wa Mtaani Anayetengeneza Midundo kwa Kutumia Ndoo

Hamasa
Nani anahitaji ngoma wakati anaweza kutumia ndoo kutengeneza sauti na midundo ya pekee? Mpiga ngoma wa mtaani kule Australia aitwaye Gordo, ambaye awali alisoma nchini Japan, anafahamu kuwa inawezekana kutengeneza muziki kutoka kwenye kila kitu bila tatizo lolote. Akiwa mwenye nguvu, nia na shauku, Gordo anaonekana akitumia ndoo, vijiti vya kupigia ngoma na miguu yake kutengeneza midundo mizuri ya ngoma. Ikiwa hana shughuli na wasanii wengine, mwaliko kwenye tukio au sherehe basi utamkuta Gordo akiwa kwenye mitaa ya Sydney akidhihirisha kipaji chake katika jamii. Watu wengi huvutiwa na kipaji chake na hata kumzawadia pesa na vitu vingine; naamini hata wewe utakapotazama video zake hapa chini, hakika atakuvutia na kukuhamasisha sana. Karibu! https://www.youtube.com/watch?v=s...
Mambo 20 Yakushukuru Kwa Ajili Yake Kwenye Maisha

Mambo 20 Yakushukuru Kwa Ajili Yake Kwenye Maisha

Hamasa
Wakati mwingine tunatazama tu mambo ambayo hatuna kwenye maisha, kuliko yale tuliyo nayo. Mara nyingi huwa hatutambui umuhimu wa kitu hadi pale tunapokikosa. Niwazi kuwa wapo watu wanaotafuta vile tunavyoviona ni vidogo lakini hawavipati. Ni muhimu kutenga muda wa kukumbuka yale mambo yote ambayo tunapaswa kushukuru kwa ajili yake. Kama una chochote kati ya hivi basi yakupasa kushukuru. Afya njema Mara nyingi hatutambui kuwa na afya njema pekee ni jambo muhimu na kubwa sana. Kuna wengi wanaotamani kuwa na afya kama ya kwako lakini hawana; hivyo yakupasa kushukuru kwa afya njema. Pesa ulizonazo Unaweza kufikiri kiasi cha pesa ulizonazo ni kidogo sana hivyo hauhitaji kushukuru. Kuna mahali pengine wewe ni tajiri mkubwa sana. Wapo wasiokuwa na pesa wala chochote kile wanachow...
Mambo 10 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Lionel Messi

Mambo 10 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Lionel Messi

Hamasa
Lionel Messi alizaliwa tarehe 24 Juni 1987 huko Rosario, Jimbo la Santa Fe huko Argentina. Akiwa na miaka mitano Messi alianza kucheza mpira wa miguu kwenye klabu ya Grandol iliyokuwa ikifundishwa na baba yake. Wakati Messi akiwa mdogo, alibainika kuwa na tatizo au maradhi ya kuwa na upungufu wa seli za ukuaji. Akiwa na umri wa miaka 13 alihamia Uhispania na kujiunga na klabu ya Barcelona ambayo ilikubali kugharamia matibabu yake. Pamoja na changamoto alizokuwa nazo Messi amefanikiwa kupata mafanikio makubwa sana. Messi anachukuliwa kama mchezaji bora zaidi duniani na mmoja kati ya wachezaji bora waliowahi kuwepo. Messi ni mchezaji pekee aliyeshinda tuzo ya FIFA ya Ballon d'Or  mara tano, zikiwemo nne mfulilizo. Pia ni mchezaji pekee aliyeshinda tuzo ya kiatu cha dhahabu (European Gol...
Kitu Muhimu Mark Zuckerberg Alichokijenga Harvard

Kitu Muhimu Mark Zuckerberg Alichokijenga Harvard

Hamasa
Mark Zuckerberg akiwa chuoni Harvard Ukimuuliza Mark Zuckerberg juu ya alichokikamilisha alipokuwa akisoma chuoni Harvard jibu lake linaweza kukushangaza. Unaweza kufikiri ni Facemash ambayo baadaye ilikuja kuwa Facebook lakini siyo. "Priscilla ni mtu muhimu zaidi katika maisha yangu, na jambo muhimu zaidi nililojenga wakati wangu hapa." Zuckerberg alisema hayo kuhusu mke wake wakati wa hotuba ya ufunguzi wa mahafali huko kwenye chuo cha Harvard mwaka huu. Mkurugenzi huyu mkuu wa Facebook mwenye miaka 33 alitumia kiasi kikubwa cha muda wake wakati wa hotuba hiyo akionyesha jinsi alivyokutana na Priscilla Chan, daktari wa watoto ambaye hatimaye walifunga ndoa mwaka 2012. Mark Zuckerberg na mke wake Priscilla Chan Zuckerberg alikutana na Chan kwenye sherehe na akampenda. Chan ...
Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Hamasa
Kwa mijibu wa jarida la Forbes linaeleza kuwa Reginald Mengi ni miongoni mwa watu maarufu katika tasnia ya habari kupitia kampuni yake ya IPP; ambayo ni moja kati ya kampuni kubwa za habari Afrika. Kampuni yake ya IPP ina magazeti 11 na vituo kadhaa vya televisheni pamoja na vyanzo mabalimbali vya kwenye mtandao. Mengi pia anamiliki kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers, ambayo ni kampuni pekee inayozalisha vinywaji vya jamii ya Coca-Cola kwa kanda ya kaskazini mwa Tanzania. Pia anazalisha maji ya Kilimanjaro yaliyojizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania. Mengi anajihusisha pia na uchimbaji wa madini kupitia kampuni yake ya IPP Resources yenye kampuni tanzu kadhaa. Reginald Mengi pia mekuwa akitoa misaada mbalimbali kusaidia makundi ya watoto, vijana, wanawake, wazee, ...