Yale tunayoyawaza na kuyatafakari kwenye fikra zetu yana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu. Ikiwa tunataka kufanikiwa basi ni lazima tufikiri na kutafakari juu ya kufanikiwa.
“Tunakuwa kile tunachofikiri”
Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani, ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu vitakavyotuhamasisha.
Karibu nikufahamishe nukuu 50 (quotes) ambazo zitakuhamasisha katika maswala mbalimbali unayoyafanya maishani mwako.
“Chochote ambacho akili ya binadamu inaweza kuumba na kufikiri, inaweza kukikamilisha pia.”
“Njia ya kuanza ni kuacha kuzungumza na kuanza kutenda.”
“Usiruhusu jana itawale sana leo.”
“Kama unafanyia kazi kitu kinachokusisimua na unachokijali kweli, hauhitaji kusukumwa. Maono yako yatakusukuma.”
“Kufahamu haitoshi, ni lazima tuweke kwenye matendo, Kutamani haitoshi, ni lazima tufanye.”
“Tunatengeneza hofu tunapokaa bila kufanya kitu. Tunaishinda hofu kwa matendo.”
“Ikiwa unafikiri unaweza au huwezi, uko sahihi.”
“Mtu mwenye kujiamini ndani yake, anapata kujiamini kwa wengine.”
“Fanya kile unachoweza kwa vyote ulivyonavyo, popote ulipo.”
“Akili ni kila kitu. Unavyofikiri ndivyo unavyokuwa.”
“Muda mzuri wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita. Lakini muda mwingine mzuri wa pili ni sasa.”
“Muda wako ni mdogo, usiupoteze kuishi maisha ya mtu mwingine.”
“Kushinda siyo kila kitu, lakini kutaka kushinda ni kila kitu.”
“Huwezi kuvuka bahari kama huna ujasiri wa kuacha kuona ufukwe.”
“Kisasi kizuri ni mafanikio makubwa.”
“Kuna njia moja tu ya kuepuka kukosolewa: usifanye kitu, usiseme kitu na usiwe chochote.”
“Anzia ulipo. Tumia kile ulichonacho. Fanya kile unachokiweza.”
“Anguka mara saba simama mara ya nane.”
“Mlango mmoja wa furaha ukifungwa, mwingine unafunguliwa, lakini mara nyingi tunautazama sana ule uliofungwa na kushindwa kuona ule uliofunguliwa kwa ajili yetu.”
“Kila kitu kina uzuri wake, lakini siyo kila mtu anaweza kuuona.”
“Changamoto zinafanya maisha yavutie na kuzishinda ni kufanya maisha kuwa na maana.”
“Kama unataka kujiinua mwenyewe juu, mwinue mwingine juu kwanza.”
“Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”
“Kila siku ninajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko nilivyo fanya jana.”
“Mtu ambaye hajawahi kufanya kosa hajawahi kujaribu kitu chochote.”
“Mtu anayesema hawezi kufanya hatakiwi kumwingilia mtu anayesema ninaweza kufanya.”
“Haujachelewa kuwa ambaye ungeweza kuwa.”
“Unakuwa kile unachoamini.”
“Jenga ndoto zako wewe mwenyewe, la sivyo mtu mwingine atakuajiri kujenga zake.”
“Ota ndoto kubwa na dhubutu kushindwa”
“Badili kufikiri kwako na utakuwa umebadili ulimwengu.”
“Andika kitu chenye manufaa kusomwa au fanya kitu chenye manufaa kuandikwa.”
“Njia pekee ya kufanya kazi nzuri ni kupenda kile unachokifanya.”
“Ikiwa unaweza kuliota, unaweza kulifanikisha.”
“Ndoto zetu zote zinaweza kutokea ikiwa tuna ujasiri wa kuzifuata.”
“Usilie juu ya kile ambacho huna; tumia vizuri kile ulichonacho.”
“Mambo mazuri huja kwa watu wanaosubiri, lakini mambo bora huja kwa wale wanaoondoka na kwenda kuayachukua.”
“Fursa hazitatokea, unatakiwa kuziunda.”
“Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio, bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”
“Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio, akili ndogo huzungumzia watu.”
“Ikiwa hauthamini muda wako, hata wengine hawatauthamini. Acha kupoteza muda na vipaji vyako sasa – anza kuvifanyia kazi”
“Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”
“Usiinue sauti yako, boresha hoja yako.”
“Ninaamini kwamba ujasiri pekee mtu yeyote anaouhitaji ni ujasiri wa kufuata ndoto zako mwenyewe.”
“Fursa zina aibu, zinakusubiri uzikimbilie.”
“Ubunifu unatofautisha kati ya kiongozi na mfuasi.”
“Hofu ni mojawapo ya adui mkubwa kwa mafanikio.”
“Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.”
“Hatua ya mwanzo ya mafanikio yoyote ni matamanio.”
“Baadaye inamilikiwa na wale wote wanaoamini kwenye uzuri wa ndoto zao.”
Naamini umehamasika na kufurahia nukuu hizi za hamasa. Ni wazi kuwa kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu – tunavyowaza ndivyo tunavyokuwa.
Je una swali, maoni au nukuu nyingine ambayo ungependa tuiweke hapa? Karibu utushirikishe kwa kutuandikia kupitia sehemu ya maoni hapo chini.
Usisahau pia kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook pamoja na kuwashirikisha wengine makala hii.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Nimaoni yanayojengakutazauhamasishowamaisha
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mambo mbona kimya Sana
Nimezipenda sana hizi nukuu! Zinahimiza na kutia moyo.
Nimezidi kujifunza siku kwa siku na kuwafunza wengine
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Hello, samahani Mimi kwa majina naitwa Salehe gae Salum Mwangalamo. Ni muandishi mchanga wa nukuu, naombeni msaada wenu ili nitimize ndoto zangu za kuwa muandishi wa nukuu zangu mwenyewe..
Jufenze zaidi kwanza kwa waliofanikiwa; kisha anza kuandika za kwako. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
good
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
naomba kuunganishwa kwenye group la whtsapp kamalipo
Sawa; tutakufahamisha na kukuunga. Asante na karibu Fahamuhili.com
Mnyama unayempenda zaidi huzibeba sifa zako.
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Nimepata funzo kwenye hizi nukuu nimejikuta navaa ujasiri mkubwa sana naimani ndoto zangu bado zinawezekana
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Amizing quote
Mungu akubariki kwa kutukumbusha
Wanadamu ni wepesi Sana wa kusahau, ni kutokana na changamoto za maisha ya mazoea.
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Nukuu nzuri Asante sana nazidi kujifunza
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Shida ya macho ilipata kwa sababu ya kusoma makasha usiku kucha kwa kutumia koroboi. Safari ya ufanisi si rahisi, ina miba mirefu njia yake. Inahitaji uvumilivu na kujitolea.
Pole sana kwa changamoto hiyo. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com