Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako - Fahamu Hili
Tuesday, October 3Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Hamasa

Yale tunayoyawaza na kuyatafakari kwenye fikra zetu yana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu. Ikiwa tunataka kufanikiwa basi ni lazima tufikiri na kutafakari juu ya kufanikiwa.

“Tunakuwa kile tunachofikiri”

Earl Nightingale

Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani, ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu vitakavyotuhamasisha.

Karibu nikufahamishe nukuu 50 (quotes) ambazo zitakuhamasisha katika maswala mbalimbali unayoyafanya maishani mwako.

  1. “Chochote ambacho akili ya binadamu inaweza kuumba na kufikiri, inaweza kukikamilisha pia.”

    Napoleon Hill
  2. “Njia ya kuanza ni kuacha kuzungumza na kuanza kutenda.”

    Walt Disney
  3. “Usiruhusu jana itawale sana leo.”

    Will Rogers
  4. “Kama unafanyia kazi kitu kinachokusisimua na unachokijali kweli, hauhitaji kusukumwa. Maono yako yatakusukuma.”

    Steve Jobs
  5. “Kufahamu haitoshi, ni lazima tuweke kwenye matendo, Kutamani haitoshi, ni lazima tufanye.”

    Johann Wolfgang
  6. “Tunatengeneza hofu tunapokaa bila kufanya kitu. Tunaishinda hofu kwa matendo.”

    Dr. Henry Link
  7. “Ikiwa unafikiri unaweza au huwezi, uko sahihi.”

    Henry Ford
  8. “Mtu mwenye kujiamini ndani yake, anapata kujiamini kwa wengine.”

    Hasidic Proverb
  9. “Fanya kile unachoweza kwa vyote ulivyonavyo, popote ulipo.”

    Theodore Roosevelt
  10. “Akili ni kila kitu. Unavyofikiri ndivyo unavyokuwa.”

    Buddha
  11. “Muda mzuri wa kupanda mti ni miaka 20 iliyopita. Lakini muda mwingine mzuri wa pili ni sasa.”

    Chinese Proverb
  12. “Muda wako ni mdogo, usiupoteze kuishi maisha ya mtu mwingine.”

    Steven Jobs
  13. “Kushinda siyo kila kitu, lakini kutaka kushinda ni kila kitu.”

    Vince Lombardi
  14. “Huwezi kuvuka bahari kama huna ujasiri wa kuacha kuona ufukwe.”

    Christopher Columbus
  15. “Kisasi kizuri ni mafanikio makubwa.”

    Frank Sinatra
  16. “Kuna njia moja tu ya kuepuka kukosolewa: usifanye kitu, usiseme kitu na usiwe chochote.”

    Aristotle
  17. “Anzia ulipo. Tumia kile ulichonacho. Fanya kile unachokiweza.”

    Arthur Ashe
  18. “Anguka mara saba simama mara ya nane.”

    Japanese Proverb
  19. “Mlango mmoja wa furaha ukifungwa, mwingine unafunguliwa, lakini mara nyingi tunautazama sana ule uliofungwa na kushindwa kuona ule uliofunguliwa kwa ajili yetu.”

    Helen Keller
  20. “Kila kitu kina uzuri wake, lakini siyo kila mtu anaweza kuuona.”

    Confucius
  21. “Changamoto zinafanya maisha yavutie na kuzishinda ni kufanya maisha kuwa na maana.”

    Joshua J. Marine
  22. “Kama unataka kujiinua mwenyewe juu, mwinue mwingine juu kwanza.”

    Booker T. Washington
  23. “Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”

    Bill Cosby
  24. “Kila siku ninajitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko nilivyo fanya jana.”

    Reginald Mengi
  25. “Mtu ambaye hajawahi kufanya kosa hajawahi kujaribu kitu chochote.”

    Albert Einstein
  26. “Mtu anayesema hawezi kufanya hatakiwi kumwingilia mtu anayesema ninaweza kufanya.”

    Chinese Proverb
  27. “Haujachelewa kuwa ambaye ungeweza kuwa.”

    George Eliot
  28. “Unakuwa kile unachoamini.”

    Oprah Winfrey
  29. “Jenga ndoto zako wewe mwenyewe, la sivyo mtu mwingine atakuajiri kujenga zake.”

    Farrah Gray
  30. “Ota ndoto kubwa na dhubutu kushindwa”

    Norman Vaughan
  31. “Badili kufikiri kwako na utakuwa umebadili ulimwengu.”

    Norman Vincent Peale
  32. “Andika kitu chenye manufaa kusomwa au fanya kitu chenye manufaa kuandikwa.”

    Benjamin Franklin
  33. “Njia pekee ya kufanya kazi nzuri ni kupenda kile unachokifanya.”

    Steve Jobs
  34. “Ikiwa unaweza kuliota, unaweza kulifanikisha.”

    Zig Ziglar
  35. “Ndoto zetu zote zinaweza kutokea ikiwa tuna ujasiri wa kuzifuata.”

    Wale Disney
  36. “Usilie juu ya kile ambacho huna; tumia vizuri kile ulichonacho.”

    Reginald Mengi
  37. “Mambo mazuri huja kwa watu wanaosubiri, lakini mambo bora huja kwa wale wanaoondoka na kwenda kuayachukua.”

    Hajulikani
  38. “Fursa hazitatokea, unatakiwa kuziunda.”

    Chris Grosser
  39. “Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio, bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”

    Albert Einstein
  40. “Akili kubwa hujadili mawazo, akili ya wastani hujadili matukio, akili ndogo huzungumzia watu.”

    Eleanor Roosevelt
  41. “Ikiwa hauthamini muda wako, hata wengine hawatauthamini. Acha kupoteza muda na vipaji vyako sasa – anza kuvifanyia kazi”

    Kim Garst
  42. “Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”

    David Brinkley
  43. “Usiinue sauti yako, boresha hoja yako.”

    Hajulikani
  44. “Ninaamini kwamba ujasiri pekee mtu yeyote anaouhitaji ni ujasiri wa kufuata ndoto zako mwenyewe.”

    Orarah Winfrey
  45. “Fursa zina aibu, zinakusubiri uzikimbilie.”

    Reginald Mengi
  46. “Ubunifu unatofautisha kati ya kiongozi na mfuasi.”

    Steve Jobs
  47. “Hofu ni mojawapo ya adui mkubwa kwa mafanikio.”

    Reginald Mengi
  48. “Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.”

    Less Brown
  49. “Hatua ya mwanzo ya mafanikio yoyote ni matamanio.”

    Napoleon Hill
  50. “Baadaye inamilikiwa na wale wote wanaoamini kwenye uzuri wa ndoto zao.”

    Eleanor Roosevelt

Naamini umehamasika na kufurahia nukuu hizi za hamasa. Ni wazi kuwa kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu – tunavyowaza ndivyo tunavyokuwa.

Je una swali, maoni au nukuu nyingine ambayo ungependa tuiweke hapa? Karibu utushirikishe kwa kutuandikia kupitia sehemu ya maoni hapo chini.

Usisahau pia kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook pamoja na kuwashirikisha wengine makala hii.

4.3 10 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

21 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Abeid shehoza
Abeid shehoza
3 years ago

Nimaoni yanayojengakutazauhamasishowamaisha

Peter Michael
Peter Michael
3 years ago

Mambo mbona kimya Sana

Eliud Timothy
Eliud Timothy
3 years ago

Nimezipenda sana hizi nukuu! Zinahimiza na kutia moyo.
Nimezidi kujifunza siku kwa siku na kuwafunza wengine

Salehegae
Salehegae
2 years ago

Hello, samahani Mimi kwa majina naitwa Salehe gae Salum Mwangalamo. Ni muandishi mchanga wa nukuu, naombeni msaada wenu ili nitimize ndoto zangu za kuwa muandishi wa nukuu zangu mwenyewe..

rashiku
rashiku
2 years ago

good

said suleiman said
said suleiman said
1 year ago

naomba kuunganishwa kwenye group la whtsapp kamalipo

Renatus Kaizirege Remigius
Renatus Kaizirege Remigius
1 year ago

Mnyama unayempenda zaidi huzibeba sifa zako.

Saimon joseph
Saimon joseph
1 year ago

Nimepata funzo kwenye hizi nukuu nimejikuta navaa ujasiri mkubwa sana naimani ndoto zangu bado zinawezekana

Makaranga s makaranga
Makaranga s makaranga
1 year ago

Amizing quote
Mungu akubariki kwa kutukumbusha
Wanadamu ni wepesi Sana wa kusahau, ni kutokana na changamoto za maisha ya mazoea.

Mary
Mary
1 year ago

Nukuu nzuri Asante sana nazidi kujifunza

Nickson M Hamisi
Nickson M Hamisi
9 months ago

Shida ya macho ilipata kwa sababu ya kusoma makasha usiku kucha kwa kutumia koroboi. Safari ya ufanisi si rahisi, ina miba mirefu njia yake. Inahitaji uvumilivu na kujitolea.

21
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x