Tija Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tija

Mbinu 7 za Kukurahisishia Kusoma Vitabu Unapokuwa na Shughuli Nyingi

Mbinu 7 za Kukurahisishia Kusoma Vitabu Unapokuwa na Shughuli Nyingi

Tija
Kama nilivyoeleza kwenye makala mbalimbali kuwa kusoma vitabu kuna manufaa mengi sana ambayo kila mtu mwenye maono anapaswa kuyapata. Vitabu hubeba maarifa kemkem ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kukusaidia kubadili maisha yako. Soma pia: Faida 15 za Kusoma Vitabu Unazotakiwa Kuzifahamu Hata hivyo bado watu wengi wanashindwa kusoma vitabu jinsi ipasavyo. Ikiwa unapenda kusoma vitabu lakini una shughuli nyingi, basi karibu nikushirikishe mbinu kadhaa zitakazo kuwezesha kusoma vitabu kwa urahisi. 1. Tumia simu yako Karibu kila mtu leo ana simu ya kisasa ya mkononi (smartphone), hata hivyo bado watu wengi hawafahamu nguvu au matumizi adhimu yanayopatikana kwenye simu hizo. Ni ukweli usiopingika kuwa ulimwengu wa kutumia simu kama kifaa cha kupiga na kupokea simu pamoj...
Madhara 6 ya Kutazama Televisheni (TV) Unayopaswa Kuyafahamu

Madhara 6 ya Kutazama Televisheni (TV) Unayopaswa Kuyafahamu

Tija
Miaka ya nyuma televisheni ilikuwa ni kitu adimu sana. Lakini hivi leo takriban kila familia au mtu ana televisheni nyumbani kwake; inaweza kuwa sebuleni, chumbani au hata kwenye simu yake ya kisasa. Hata wale wasiokuwa na televisheni nyumbani kwao bado wanapata nafasi ya kutazama televisheni kwenye migahawa, mabasi au hata kwenye ofisi za kampuni au taasisi mbalimbali. Televisheni imekuwa ni kifaa muhimu kwa ajili ya habari na burudani; hata hivyo televisheni inaweza kuwa na madhara kadha wa kadha kwako ikiwa haitotawaliwa vyema. Basi karibu ufahamu madhara ya kutazama televisheni (TV) 1. Hupoteza muda Unapokaa na kuangalia televisheni ni wazi kuwa unatumia muda mwingi na wa muhimu sana. Hii ni kutokana na sababu kuwa watu wengi hutazama televisheni kwa muda mrefu au hata siku...
Mambo ya Kuzingatia Ili Kuchagua Kichwa Kizuri cha Kitabu

Mambo ya Kuzingatia Ili Kuchagua Kichwa Kizuri cha Kitabu

Tija
Swala la uandishi wa vitabu ni swala linalohitaji kuzingatia hatua kadhaa muhimu. Moja kati ya hatua hizi ni uchaguzi wa wazo au kichwa cha kitabu. Haijalishi ni kitabu cha kifasihi au kisicho cha kifasihi, utahitajika kuchagua kichwa kizuri au bora cha kitabu chako. Ikiwa wewe ni mwandishi au unajiandaa kuwa mwandishi wa vitabu, basi fahamu mambo ya kuzingatia ili kuchagua kichwa kizuri cha kitabu. 1. Fanya utafiti Utafiti ni msingi mkuu wa kupata kichwa kizuri cha kitabu. Ni muhimu kufanya utafiti katika vitabu au makala nyingine mbalimbali zinazohusiana na kile unachotaka kukiandikia. Unaweza kuzingatia haya wakati wa utafiti: Fanya utafiti kwenye vitabu vilivyochapishwa pamoja na vile vilivyoko kwenye mtandao wa intaneti ili kubaini kama kichwa unachokitaka kimeshatumi...
Faida 8 za Kufanya Kazi Kwa Bidii Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 8 za Kufanya Kazi Kwa Bidii Unazotakiwa Kuzifahamu

Tija
Kuna fikra potofu zimejengeka miongoni mwa watu wakidhani kuwa kufanya kazi kwa bidii ni utumwa. Hii ni kutokana na dunia ya sasa kujaa watu wasiopenda kazi na wavivu. Kwa hakika kufanya kazi kwa bidii kuna manufaa mengi sana ambayo watu wengi hawayajui. Huu ni wakati wa kubadili mtazamo wako juu ya kufanya kazi kwa bidii kwa kufahamu faida 8 za kufanya kazi kwa bidii. 1. Utaweza kutumia muda vyema Huwezi kutumia muda vyema kama hutofanya kazi kwa bidii. Ukiwa na bidii katika kufanya kazi, unaweza kufanya kazi za siku nzima ndani ya saa moja au kazi za siku mbili ndani ya siku moja. Hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa bila kutumia muda vyema; muda ni mali, hivyo yakupasa uutumie vyema kwa kufanya kazi kwa bidii. Soma pia: Kanuni 9 za Kufanikiwa katika Matumizi ya Muda 2. Kufiki...
Faida 7 za Kuwa na Ratiba Binafsi

Faida 7 za Kuwa na Ratiba Binafsi

Tija
Ratiba siyo muhimu tu kwa ajili ya taasisi fulani pekee; ni muhimu pia kwa mtu binafsi. Watu wengi hushindwa kutumia muda wao vyema kutokana na kutokuwa na ratiba nzuri inayoeleweka. Kuweka ratiba kutakuwezesha kupangilia kazi na mipango yako kwa namna ambayo utaweza kuitekeleza vyema. Ikiwa unataka kuwa mwenye tija na ufanisi zaidi, basi fahamu faida 7 za kuwa na ratiba binafsi. 1. Kutumia muda vyema Moja kati ya manufaa makubwa ya kuwa na ratiba ni kuweza kutumia muda vyema. Unapokuwa na ratiba ni vigumu kupata muda ambao haujapangiwa jukumu au kazi kwenye ratiba. Unapokuwa na ratiba muda wako wote utatumika vizuri tena kwa shughuli yenye tija iliyopangwa. Hivyo ni vyema kuhakikisha unajiwekea ratiba na unaifuata ipasavyo. Soma pia: Kanuni 9 za Kufanikiwa katika Matumiz...
Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kuhifadhi Nyaraka Muhimu Salama

Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kuhifadhi Nyaraka Muhimu Salama

Tija
Katika maisha yetu ya kila siku hatuwezi kuepuka kuwa na nyaraka mbalimbali. Baadhi ya nyaraka ni za muhimu sana kwetu kiasi cha kutoweza kuzipata tena iwapo zitaharibika au kupotea. Ni ukweli usiopingika kuwa nyaraka kama vile vyeti ya taaluma, bima, hati za kusafiria, leseni, wosia, vyeti vya ndoa, talaka, mikataba, hati za nyumba na viwanja ni baadhi ya nyaraka zinazotakiwa kutunzwa sana. Kutokana na watu wengi kutofahamu umuhimu wa nyaraka mbalimbali au kutokuzihifadhi vyema, wengi wamejikuta kwenye matatizo makubwa baada ya nyaraka zao muhimu kuharibika au kupotea. Ikiwa basi unataka kuweka nyaraka zako salama, karibu nikushirikishe mambo 7 ya kuzingatia ili kuhifadhi nyaraka muhimu salama. 1. Tumia kabati au sanduku maalumu ya kuhifadhi nyaraka Zipo kabati na masan...
Vitu 20 Usivyotakiwa Kusema Wakati wa Usaili wa Kazi (Job Interview)

Vitu 20 Usivyotakiwa Kusema Wakati wa Usaili wa Kazi (Job Interview)

Tija
Inawezekana una maarifa stahiki pamoja na uzoefu unaohitajika kwenye kazi fulani, lakini ukakosa kazi hiyo kutokana na vitu ulivyosema au kufanya wakati wa usaili wa kazi. Ni muhimu kufahamu kuwa lengo la usahili wa kazi siyo kukufahamu wewe au kufahamu matakwa yako, bali ni kutathimini kama unafaa kwenye kazi au kampuni husika. Hivyo ni muhimu kuhakikisha yale yote unayoyasema na kuyafanya kwenye usaili, yanaonyesha kufaa kwako kwenye kazi husika. Ikiwa unatafuta kazi au umeitwa kwenye usaili wa kazi, basi fahamu vitu 20 ambavyo hutakiwi kuvisema au kuvifanya wakati wa usaili wa kazi (Job Interview). Sipendi kazi yangu ya sasa au ya awali. (Kwa hiyo utachukia na hii unayoomba?) Mwajiri wangu wa awali ni mbaya. Kwa kusema hivi utaonekana utamchukia na huyu wa sasa. ...
Vitu Vinne Vinavyokufanya Usikamilishe Kazi Zako

Vitu Vinne Vinavyokufanya Usikamilishe Kazi Zako

Tija
Hakuna mtu anayependa kushindwa kukamilisha kazi au kitu alichokianza. Hata hivyo mara nyingi kutokukamilisha kazi hutokea kwa watu wengi. Ni ukweli usiopingika kuwa zipo sababu kadha wa kadha zinazosababisha tatizo hili. Karibu nikufahamishe vitu vinne vinavyokufanya usikamilishe kazi zako. 1. Usingizi Kuna usemi usemao “usingizi ni mlango wa umaskini”; kwa hakika kulala kupita kiasi ni jambo ambalo litakupotezea muda mwingi pamoja na ufanisi. Unapolala sana unakosa muda wa kutosha kutimiza majukumu yako. Pia kulala muda mrefu hukufanya uamke ukiwa umechoka na kukufanya ukose ari na motisha wa kufanya kazi. Soma pia: Njia 10 za Kuamka Mapema Asubuhi. 2. Intaneti na simu Maendeleo yana manufaa yake na hasara zake. Kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, watu wengi...
Njia 10 za Kuepuka Madeni

Njia 10 za Kuepuka Madeni

Kipato, Tija
Hakuna mtu anayependa kuwa na madeni, lakini mara nyingi watu hujikuta katika madeni makubwa. Kwa kiasi kikubwa watu wengi huingia kwenye madeni kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha matumizi kuliko kipato. Madeni siyo kitu kizuri hasa ikiwa hayatalipwa kwa wakati. Swala la kuepuka madeni ni swala linalohitaji maamuzi sahihi ya kifikra pamoja na mikakati stahiki. Je unapenda kuepuka au kupunguza kiwango chako cha madeni? Karibu nikufahamishe njia 10 za kuepuka madeni. 1. Jiwekee bajeti binafsi Utawasikia watu wakikosoa bajeti ya serekali lakini hawana bajeti zao binafsi. Bajeti binafsi ni muhimu kwani hukuwezesha kupanga juu ya mapato na matumizi yako. Ili kuepuka madeni, ni muhimu kuweka bajeti binafsi ambayo itakuongoza juu ya matumizi yako ya pesa ili usije ukatumia kul...
Njia 10 za Kukufanya Kuwa na Furaha

Njia 10 za Kukufanya Kuwa na Furaha

Tija
Kutokana na changamoto za kimazingira, kiuchumi na kijamii, watu wengi wamejikuta wakikosa furaha. Ni wazi kuwa kukosa furaha kuna madhara makubwa kwenye afya ya mwili, akili na hata katika utendaji wako wa kazi. Watu wengi hutamani kuwa na furaha lakini bado hawapati furaha; wengi hudhani kuwa na vitu kama vile pesa ndiyo chanzo cha furaha, lakini mambo hayawi kama walivyotarajia pindi wapatapo vitu hivyo. Je unahitaji kuwa na furaha ili uboreshe afya na ufanisi wa utendaji kazi wako? Karibu nikushirikishe njia 10 za kukufanya kuwa na furaha. 1. Samehe Watu wengi hukosa furaha kutokana na kubeba uchungu na maumivu yaliyotokana na watu waliowakosea. Ikiwa unataka kuwa na furaha ni muhimu kumsamehe aliyekukosea hata kama hajaomba msamaha. Kumsamehe aliyekukosea kuna manufaa k...