Teknolojia Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Teknolojia

Athari au Madhara 10 ya Intaneti Unayopaswa Kuyafahamu

Athari au Madhara 10 ya Intaneti Unayopaswa Kuyafahamu

Teknolojia
Katika dunia hii ya leo ni vigumu kuishi bila kutumia intaneti kwa namna moja au nyingine. Watu hutumia intaneti kuwasiliana, kupata taarifa na habari au hata  kujipatia kipato. Kuwepo kwa intaneti kumerahisisha maisha ya mwanadamu kwa kiasi kikubwa na kufanya utendaji kazi wake uwe bora zaidi. Pamoja na intaneti kuwa na manufaa kadha wa kadha, intaneti ina athari mbalimbali. Hivyo basi fahamu madhara 10 ya intaneti. 1. Taarifa za uongo Kila mtu anaweza kuweka taarifa kwenye mtandao wa intaneti, hivyo ni rahisi kukumbana na taarifa zisizo za kweli. Swala hili limepelekea baadhi ya nchi na mashirika mbalimbali kujaribu kukabili taarifa mbalimbali zinazopatikana kwenye mtandao ili kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na taarifa hizo. Ni vyema kuhakikisha tovuti au blog ...
Balabolka: Programu Inayobadili Maandishi au Vitabu Kuwa Sauti

Balabolka: Programu Inayobadili Maandishi au Vitabu Kuwa Sauti

Teknolojia
Kwa kuwa vitabu ni kisima kikubwa cha maarifa, kila mara teknolojia inakuja na mbinu mbalimbali zitakazotuwezesha kuvuna maarifa haya. Ikiwa unapenda kusoma vitabu au una nia ya kusoma vitabu, basi fahamu programu ya Balabolka itakayokuwezesha kusoma maandishi au vitabu kwa sauti au kuvibadili kuwa sauti ili uvisikilize badala ya kuvisoma. Hivyo kwa kutumia programu hii unaweza kusoma vitabu pepe kwa urahisi kabisa na mahali popote bila kizuizi. Badala ya kusikiliza mziki siku nzima sasa unaweza kusikiliza vitabu. Sifa za programu ya Balabolka Ni programu ya BURE Inaweza kusoma vitabu vya lugha mbalimbali kama vile Kiingereza, Kiarabu, Kijerumani, Kifaransa, Kichina, n.k. Inaweza kubadili kitabu kuwa faili la sauti kama vile WAV, MP3, MP4, OGG au WMA Inaweza kusoma...
Kikombe cha Kisasa Kinachozuia Vitu Kumwagika

Kikombe cha Kisasa Kinachozuia Vitu Kumwagika

Teknolojia
Lengo kubwa la teknolojia ni kurahisisha maisha pamoja na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi. Kila siku kumekuwa kukibuniwa teknolojia mbalimbali hasa kwa lengo la kutatua matatizo mbalimbali yanayomkabili mwanadamu. Inawezekana umewahi kupoteza nyaraka zako muhimu au hata kuharibu vifaa vyako vya thamani kama vile simu au kompyuta kutokana na kumwagikiwa vimiminika kama vile maji, kahawa au chai. Teknolojia kutoka MightyMug inakuja na kikombe maalumu ambacho huzuia kinywaji kilichoko ndani yake kumwagika. Inawezekana una mtoto mkorofi au unafanya kazi kwenye eneo lenye mitikisiko mingi; sasa kwa kutumia kikombe kutoka MightyMug utaepusha vitu vyako vya thamani kumwagikiwa vimiminika. Sifa  za kikombe cha MightyMug Kikombe cha MightyMug kina uwezo wa kujishikiza kw...
Application/Programu 10 Muhimu za Kuwa Nazo Kwenye Simu (2017)

Application/Programu 10 Muhimu za Kuwa Nazo Kwenye Simu (2017)

Teknolojia
Ni wazi kuwa sasa kuna ongezeko kubwa sana la matumizi ya simu za mkononi hasa simu za kisasa (smartphone). Ni ukweli usiopingika kuwa yapo matumizi mengi ya simu za mkononi pamoja na programu zake (applications) ambayo bado hayajafahamika vyema kwa watumiaji wake. Fuatilia makala hi ufahamu programu 10 muhimu kuwa nazo kwenye simu yako ili uwe mwenye tija zaidi. 1. Google Drive Google drive ni zaidi ya hazina ya mafaili. Google Drive inakuwezesha kutengeneza ofisi yako ndogo yenye uwezo mzuri wa kuunda, kupanga, kuhariri na hata kusambaza mafaili mbalimbali kadri upendavyo. 2. Android Device Manager Ukizingatia kwamba simu ni muhimu sana kwenye maisha yetu, tunahitaji kitu cha kutusaidia ikiwa jambo litakwenda vibaya. Android Device Manager itakuwezesha kufanya mambo kama vile ...
Fahamu Njia 6 za Kulinda Akaunti Zako za Mitandao ya Kijamii

Fahamu Njia 6 za Kulinda Akaunti Zako za Mitandao ya Kijamii

Teknolojia, Tija
Mitandao ya kijamii ni kitu muhimu sana kwenye maisha binafsi na shughuli za kiuchumi kama vile biashara. Kutokana na umuhimu huu, kuna haja ya kuhakikisha akaunti zako za mitandao ya kijamii zinakuwa salama. Je ulishawahi kufikiri nini kitatokea ikiwa mtu mbaya atapata nafasi ya kuingia kwenye akaunti zako? Ni wazi kuwa mambo kama haya hapa chini yanaweza kutokea: Kuiba wafuasi wako utakaokuwa umewakusanya muda mrefu. Kutapeli watu mbalimbali wanaokufahamu katika mitandao ya kijamii kwa kutumia akaunti yako. Kuchafua taswira yako; kumbuka mtu mbaya anaweza kuweka maudhui mabaya yatakayoshusha hadhi yako. Kuiba ama kutumia vibaya taarifa zako binafsi zilizoko kwenye akaunti yako. Ni wazi kuwa ipo sababu ya kuhakikisha akaunti zako za mitandao ya kijamii zinakuwa sal...
Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Maarifa, Teknolojia
Hakika ulimwengu huu una  mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu. Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua. Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web) Deep web ni nini? Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane. ...
Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Maarifa, Teknolojia
Hivi leo kuna mambo mengi kuhusu intaneti, lakini hapa nitakuonyesha baadhi ya mambo ambayo naamini yatakuvutia na kukushangaza. Historia ya intaneti inaanzia miaka ya 1950 ikienda sambamba na maendeleo ya kompyuta. Ni wazi kuwa, ulimwengu wa intaneti wa leo ulianzwa na mwanasayansi wa kompyuta wa Uingereza Tim Berners-Lee. Kuundwa kwa intaneti yake ya kwanza, moja kwa moja kulibadili ulimwengu, vyombo vya habari, mahusiano, burudani na mambo mengine mengi. Tunapotazama intaneti leo, ni wazi kuwa tunaona mambo mengi ambayo intaneti imepitia tokea kuanzishwa kwake hadi hivi leo. Karibu ufuatilie makala hii ili ufahamu mambo 18 ya kushangaza kuhusu intaneti usiyoyajua. 1. Tovuti ya kwanza bado ipo Tovuti ya kwanza kutengenezwa bado ipo na inafanya kazi hadi leo. Jambo pekee ni ku...
Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Teknolojia
Kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari mawasiliano (TEHAMA), mfumo wa biashara pia umebadilika. Hivi leo ni rahisi kutuma na kupokea pesa, kuuza au hata kununua bidhaa kwa njia ya mtandao. Watu wengi hupenda kufanya manunuzi na mauzo ya bidhaa kwenye mtandao kutokana na urahisi wa upatikanaji wa bidhaa na huduma kupitia mtandao. Pamoja na nafasi hii kubwa ya mtandao katika maswala yanayohusu fedha, zipo changamoto mbalimbali zinazoandamana na miamala na manunuzi ya kwenye mtandao. Fahamu jinsi unavyoweza kujilinda unapofanya miamala au manunuzi mbalimbali kupitia mtandao. 1. Tumia kinga-virusi (antivirus) bora Mtandao wa intanet ni chanzo kikubwa cha virusi na wadukuzi. Hivyo ni vyema ukatumia programu madhubuti kwa ajili ya kukukinga na virusi na wadukuzi mara unapofanya manu...
Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Teknolojia
Katika ulimwengu wa leo nywila au password si jambo geni. Mara kadhaa umeona au kutumia password katika vitu na maendeo kadhaa kama vile benki, simu, kompyuta n.k. Jambo la kushangaza ni jinsi watu wanavyotumia nywila bila kujali umuhimu wake katika eneo husika. Mtazamo wa ujumla juu ya nywila (password) Nywila ni ufunguo wa kufungua na kufunga sehemu husika; hivyo aliye nao ndiye atakayeweza kufungua na kufunga. Nywila ngumu = usalama zaidi; nywila rahisi = uslama kidogo. Mhalifu anaweza kutumia nywila kufanya uhalifu. Hivyo basi ni muhimu kufahamu namna ya kutengeneza nywila imara na salama kwa ajili ya kifaa au akaunti yako. Fuatilia makala hii ili uweze kujifunza mambo kadhaa ya kufanya ili kutengeneza nywila imara. 1. Epuka namba na maneno rahisi Wengi wetu hatu...
Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Teknolojia
Shughuli nyingi pamoja na kubadilika kwa mtindo wa maisha kumewafanya madereva wengi kusinzia wakati wanaendesha magari. Kusinzia wakati wa kuendesha gari kunaweza kusababisha madhara makubwa. Inashauriwa kuwa unapojisikia kuchoka ni vyema ukapumzika. Panasonic wanaamini kuwa wana utatuzi: kwa kutumia akili bandia (Artificial inteligence) wanaweza kumfanya dereva awe macho wakati wote. Kwa mujibu wa Panasonic kuna aina tano za kusinzia: kutosinzia, kusinzia kidogo, kusinzia halisi, kusinzia sana na kusinzia kulikopitiliza. Kampuni hii ya Kijapani imegundua mfumo wa kwenye magari unaoweza kutambua kusinzia kwa dereva na kupambana nako kabla ya kutokea. Mfumo huu humfwatilia dereva kwa kutumia kamera na vihisi (sensors). Mfumo huu unaweza kutambua mambo kama vile kupepesa macho,...