Mahusiano na Familia Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Mahusiano na Familia

Vitu 10 Ambavyo Kila Mzazi au Mlezi Anatakiwa Kumfundisha Mtoto Wake

Vitu 10 Ambavyo Kila Mzazi au Mlezi Anatakiwa Kumfundisha Mtoto Wake

Mahusiano na Familia
Mzazi au mlezi ndiye mwalimu namba moja wa mtoto wake. Kwa kiasi kikubwa sana mtoto hujifunza na kuiga vitu au mambo mbalimbali kutoka kwa wazazi au walezi wake. Hivyo ni muhimu sana mzazi kuhakikisha anamfundisha mtoto wake mambo muhimu anayopaswa kujifunza ili akue katika malezi bora na awe na baadaye (future) njema. Kwa kutambua umuhimu wa mzazi au mlezi kumfundisha mtoto wake mambo kadhaa muhimu; karibu ufahamu vitu au mambo 10 ambayo kila mzazi au mlezi anatakiwa kumfundisha mtoto wake. 1. Matumizi mazuri ya muda Matumizi ya muda ni swala muhimu kwa kila mtu, tena ni msingi wa mafanikio kwa kila mtu. Hivyo mzazi au mlezi anapaswa kumfundisha mtoto wake matumizi ya muda tangu akiwa mtoto ili akue akiwa na tabia hiyo. Mzazi au mlezi anapaswa kumfundisha mtoto wake maswala...
Vitu 10 Ambavyo Wazazi Wawajibikaji Wanavifanya

Vitu 10 Ambavyo Wazazi Wawajibikaji Wanavifanya

Mahusiano na Familia
Malezi ni swala linalohusisha pande kuu tatu, yaani wazazi, mtoto na jamii. Hivyo wazazi wanapaswa kuwajibika kusimamia nafasi yao ya malezi ya watoto ili watoto wao wakue kwenye misingi bora ya maadili. Hili linatupa makundi mawili ya wazazi, yaani wale wanaowajibika na wale wasiowajibika katika familia na malezi. Ikiwa wewe ni mzazi au unatarajia kuwa mzazi, basi fahamu vitu 10 ambavyo wazazi wawajibikaji wanavifanya katika malezi ya familia zao. 1. Wanafanya kwa matendo kuliko maneno Wazazi wawajibikaji wanafanya kwa matendo kuliko maneno, yaani wao kama wanawaagiza watoto wafanye kazi kwa bidii, nao utawakuta kila wakati wanafanya kazi kwabidii. Ikiwa wanawahamasisha watoto wao kumcha Mungu au kuwa na maadili mema kwenye jamii, basi nao utawakuta wakiwa mstari wa mbele kuya...
Maneno 20 Ambayo Hutakiwi Kumwambia Mtoto Wako

Maneno 20 Ambayo Hutakiwi Kumwambia Mtoto Wako

Mahusiano na Familia
Mara kadhaa wazazi wamekuwa wakiwaambia watoto wao maneno mbalimbali wakati wakiwa na furaha au hasira. Ipo nguvu kubwa kwenye maneno ya kutamkiwa ambayo wazazi wengi hawaifahamu. Kwa hakika maneno yanaweza kujenga au kubomoa maisha ya mtoto kwa kiasi kikubwa. Hivyo fahamu maneno 20 ambayo hutakiwi kumwambia mtoto wako. 1. Wewe ni mtoto mbaya Wazazi wengi wanapokasirishwa na mtoto humwambia wewe ni mtoto mbaya, hili humfanya mtoto ajione hafai. Hivyo ni vyema kuepuka kumwambia mtoto neno hili badala yake mweleze kosa lake na athari zake ili aliepuke. 2. Kwanini usiwe kama dada au kaka yako? Kauli hii humfanya mtoto ajione dhaifu kwa sababu unamlinganisha na wengine. Kauli hii pia humjengea chuki na wivu kwa wale unaowataja kwake kuwa ni bora. Hili husababisha watoto kuchukian...
Mambo Yanayosababisha Baadhi ya Watoto Wasifanye Vizuri Kwenye Masomo

Mambo Yanayosababisha Baadhi ya Watoto Wasifanye Vizuri Kwenye Masomo

Mahusiano na Familia
Mara kadhaa imeshuhudiwa baadhi ya watoto wakishindwa kufanya vizuri kwenye masomo. Jambo hili siyo zuri kwani linaathiri maisha ya watoto wenyewe pamoja na wazazi au walezi. Wakati mwingine swala hili limekuwa kubwa kiasi cha kuwafanya baadhi ya watoto kupata shida hata kufanya mambo madogo kama vile kusoma na kuandika. Hata hivyo kila jambo linalotokea duniani hutokea kwa sababu. Hivyo ukiwa wewe umeguswa na swala la baadhi ya watoto kutokufanya vizuri shuleni, basi karibu nikushirikishe mambo yanayosababisha baadhi ya watoto wasifanye vizuri kwenye masomo. 1. Matatizo ya kisaikolojia Watoto wanaweza kukabiliwa na matatizo mbalimbali ya kisaikolojia ambayo huathiri uwezo wao wa kujifunza shuleni. Baadhi ya watoto huzaliwa na matatizo haya huku mengine hutokana na matendo k...
Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kutafuta Mpenzi Kwenye Mtandao wa Intaneti

Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kutafuta Mpenzi Kwenye Mtandao wa Intaneti

Mahusiano na Familia
Maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia hasa katika sekta ya mawasiliano yamebadili mambo mengi. Hili ni tofauti na hapo awali ambapo watu walitegemea njia duni za mawasiliano kama vile posta. Kutokana na maendeleo haya katika teknolojia ya mawasiliano, suala la mahusiano pia limebadilika kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanaweza kutafuta wapenzi kwenye mtandao wa intaneti bila kizuizi chochote. Kwa hakika bila shaka kila jambo lina uzuri na ubaya  wake; hivyo suala la kutafuta wapenzi kwenye mtandao linatakiwa kutazamwa kwa jicho la pili. Ikiwa umejiunga au unataka kujiunga na mitandao ya kutafuta wapenzi, basi fahamu sababu 7 za kwanini hutakiwi kutafuta mpenzi kwenye mtandao wa intaneti. 1. Watu wanaigiza uhalisia Katika eneo ambalo watu wanaigiza uhalisia wa maisha kw...
Vitu 10 Vinavyoharibu Maadili ya Watoto

Vitu 10 Vinavyoharibu Maadili ya Watoto

Mahusiano na Familia
Kwa miaka ya hivi karibuni kumeshuhudiwa kuporomoka kwa maadili ya watoto kwa kiwango kikubwa. Hili limepelekea kuibuka kwa maswali mengi juu ya ni nini hasa chanzo cha tatizo hili. Hivi leo watoto wengi hawaheshimu wazazi wala waliowazidi umri, wanatumia pombe na madawa, wanaiba, wana kiburi, wavivu, n.k. Kwa hakika vipo vitu vinavyochangia katika kuporomoka kwa maadili ya watoto. Karibu nikushirikishe vitu 10 vinavyoharibu maadili ya watoto. 1. Wazazi kuwa mfano mbaya Wazazi wa karne hii wengi wanawalaumu watoto kuwa wana maadili mabaya, lakini chanzo cha tatizo hili ni wao wenyewe. Wazazi wamekuwa wakilewa, kutukanana, kupigana au hata kufanya mambo mengine machafu kama vile uzinzi mbele ya watoto. Kwa hakika tabia hizi zinapofanywa mbele ya watoto nao huziiga na kuzifany...
Mambo 10 ya Kuzingatia Unapomtafutia Mtoto Shule

Mambo 10 ya Kuzingatia Unapomtafutia Mtoto Shule

Mahusiano na Familia
Hivi leo kuna shule nyingi, lakini siyo shule zote ni bora au zinafaa kwa ajili ya mtoto wako. Hii ni kutokana na shule nyingi kuanzishwa na kuendeshwa kwa misingi ya kibiashara kuliko huduma. Swala la kuhakikisha mtoto wako anapata elimu bora ni swala la msingi. Hii ni kutokana na nafasi na umuhimu wa elimu kwa maisha ya sasa na ya baadaye ya mtoto. Ikiwa unataka kupata shule nzuri kwa ajili ya mtoto wako, karibu nikufahamishe mambo 10 ya kuzingatia unapomtafutia au kumchagulia mtoto wako shule. 1. Kiwango cha ufaulu Hakuna mzazi au mlezi ambaye anapenda mtoto wake asifanikiwe kwenye masomo. Kufanikiwa kwa mtoto kwa kiasi kikubwa kunategemea kiwango cha ufaulu cha shule. Ni wazi kuwa shule inayofaulisha vyema itakuwa inafundisha vyema pia. Hivyo kagua kwanza matokeo ya miti...
Sifa 17 za Kuzingatia Kwa Mtu Unayetaka Kuoa au Kuolewa Naye

Sifa 17 za Kuzingatia Kwa Mtu Unayetaka Kuoa au Kuolewa Naye

Mahusiano na Familia
Swala la mtu wa kuoa au kuolewa naye ni swala nyeti linalohitaji maamuzi yanayohusisha hekima, utulivu, kumwomba Mungu pamoja na uchunguzi wa kutosha. Maisha ya watu wengi yamekuwa na matatizo makubwa kutokana na kufanya makosa katika kuchagua mtu wa kuoa au kuolewa naye. Kwa hakika hakuna mtu au mwenzi mkamilifu, lakini kuna sifa za msingi ambazo kila mtu unayetarajia kuoa au kuolewa anapaswa kuzizingatia na kuzitilia maanani. Naamini unapenda kuoa au kuolewa na mtu sahihi. Karibu nikushirikishe sifa 17 za kuzingatia kwa mtu unayetaka kuoa au kuolewa naye. 1. Ana malengo na maono Hakikisha mtu unayetaka kuoana naye ni mtu mwenye malengo katika maisha yake. Mtu mwenye malengo hujishughulisha kila mara kuhakikisha anaandaa baadaye yake. Mtu asiyekuwa na malengo huwaza matumiz...
Makosa 15 ya Kuepuka Katika Malezi ya Watoto

Makosa 15 ya Kuepuka Katika Malezi ya Watoto

Mahusiano na Familia
Swala la malezi ya watoto ni swala nyeti, pana, gumu, na lenye changamoto nyingi; hivyo linahitaji umakini mkubwa na maarifa stahiki. Kutokana na umuhimu huu basi, ni wazi kuwa changamoto au matatizo mengi ya kimalezi yanayotokea kwenye maisha ya watoto yanatokana na makosa yanayofanywa na wazazi katika malezi. Pamoja na kwamba hakuna kanuni ya malezi, lakini yapo makosa ambayo wazazi wanapaswa kuyaepuka katika swala la malezi ili kuhakikisha watoto wao wanakuwa katika maadili na misingi sahihi. Karibu nikufahamishe makosa 15 ambayo kila mzazi au mlezi anatakiwa kuyaepuka katika malezi ya kilasiku ya watoto. 1. Kumfurahisha mtoto Kumfurahisha mtoto ni muhimu kufanywa na kila mzazi au mlezi, lakini ni lazima kuwe na kiasi. Wazazi wengi wamekuwa wakifanya kosa la kutaka kuwafa...