
Sifa 17 za Kuzingatia Kwa Mtu Unayetaka Kuoa au Kuolewa Naye
Swala la mtu wa kuoa au kuolewa naye ni swala nyeti linalohitaji maamuzi yanayohusisha hekima, utulivu, kumwomba Mungu pamoja na uchunguzi wa kutosha. Maisha ya watu wengi yamekuwa na matatizo makubwa kutokana na kufanya makosa katika kuchagua mtu wa kuoa au kuolewa naye. Kwa hakika hakuna mtu au mwenzi mkamilifu, lakini kuna sifa za msingi ambazo kila mtu unayetarajia kuoa au kuolewa anapaswa kuzizingatia na kuzitilia maanani. Naamini unapenda kuoa au kuolewa na mtu sahihi. Karibu nikushirikishe sifa 17 za kuzingatia kwa mtu unayetaka kuoa au kuolewa naye.
1. Ana malengo na maono
Hakikisha mtu unayetaka kuoana naye ni mtu mwenye malengo katika maisha yake. Mtu mwenye malengo hujishughulisha kila mara kuhakikisha anaandaa baadaye yake. Mtu asiyekuwa na malengo huwaza matumiz...