Kipato Archives - Fahamu Hili
Tuesday, June 6Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Kipato

Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kucheza Michezo ya Kubahatisha

Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kucheza Michezo ya Kubahatisha

Kipato
Kutokana na hali ngumu ya kiuchumi au changamoto za maisha watu wengi hutekwa na mambo mbalimbali hasa yale yanayohusu kupata pesa za haraka. Nilipofanya utafiti mdogo nilibaini kuwa “njia za kupata pesa kwa haraka” pamoja na “njia za kupata utajiri kwa haraka” ni moja kati ya vitu vinavyotafutwa sana na watu kwenye mtandao. Hii inadhihirisha uhitaji mkubwa wa watu kutaka kupata pesa, tena kwa muda mfupi. Hivyo basi, hili limepelekea watu wengi kutekwa na michezo ya bahati nasibu wakifikiri kuwa inaweza kuwatoa katika matatizo au mahitaji yao ya kifedha. Haijalishi unacheza au huchezi michezo ya kubahatisha, karibu nikufahamishe sababu 7 za kwanini hutakiwi kucheza michezo ya kubahatisha. 1. Ni biashara Hakuna mtu atakayetoka China, India au Marekani ili aje Afrika kukugawia...
Faida 8 za Kuweka Akiba Unazopaswa Kuzifahamu

Faida 8 za Kuweka Akiba Unazopaswa Kuzifahamu

Kipato
Kuweka akiba ni kanuni mojawapo ya matumizi mazuri ya pesa. Hata hivyo kutokana na watu wengi kutokuwa na matumizi mazuri ya pesa, bado wengi wanashindwa kuweka akiba. Baadhi ya watu hufikiri kuwa ili uweze kuweka akiba ni lazima uwe na pesa nyingi, lakini ukweli ni kuwa kuweka akiba ni maamuzi tu na siyo kuwa na pesa nyingi. Ikiwa umekuwa ukipuuza suala la kuweka akiba na kuliona kuwa halina maana, basi fahamu faida 8 za kuweka akiba. 1. Uhuru wa kifedha Uhuru wa kifedha ni zaidi ya kuwa na pesa, uhuru wa kifedha ni kuwa mtu ambaye unatakiwa kuwa maishani na kuweza kufanya au kupata kile unachokihitaji maishani. Hata hivyo pesa ni muhimu sana kwenye swala la uhuru wa kifedha, ingawa pesa hizi zinatakiwa ziambatane na fikra sahihi. Kwa njia ya kujiwekea akiba utaweza kuji...
Mambo Matano Muhimu ya Kuzingatia Kabla ya Kuomba Mkopo

Mambo Matano Muhimu ya Kuzingatia Kabla ya Kuomba Mkopo

Kipato
Kutokana na kipato cha watu wengi kutokutosheleza mahitaji yao, hujikuta wakilazimika kukopa. Wapo waliofanikiwa sana kwenye mipango yao kutokana na mikopo, lakini wapo pia waliofilisika kutokana na mikopo. Kwa hakika swala la mikopo linahitaji umakini mkubwa pamoja na mipango na mikakati stahiki ili lisije likakuingiza kwenye madeni yasiyokwisha. Ikiwa una mpango wa kukopa, basi fahamu mambo matano muhimu ya kuzingatia kabla ya kuomba mkopo. 1. Bainisha uwezo wako wa kifedha Ili upate na utumie mkopo vyema, ni muhimu ufahamu uwezo wako wa kifedha. Ikiwa uwezo wako wa kifedha ni shilingi milioni moja, ukikopa mkopo wa bilioni 1 hutoweza kuupata wala kuurejesha. Hakikisha unatathimini kipato chako pamoja na uwezo wako wa kutumia pesa ili usije ukatumbukia kwenye madeni. So...
Mambo 6 Muhimu ya Kufanya Kabla ya Kustaafu

Mambo 6 Muhimu ya Kufanya Kabla ya Kustaafu

Kipato
Kustaafu ni msimu mpya ambao kila mwajiriwa anapaswa kuufahamu na kujiandaa kwa msimu huo vyema. Kumeshuhudiwa watu wakiishi maisha ya taabu na mahangaiko makubwa baada ya kustaafu. Hili linatokana na kutokujiandaa vyema kabla ya kustaafu. Kwa kufahamu umuhimu wa kujiandaa vyema kabla ya kustaafu; karibu ufahamu mambo 6 muhimu ya kufanya kabla ya kustaafu. 1. Jiandae kisaikolojia Kustaafu ni kipindi tofauti sana na kipindi ulichokuwa kwenye ajira. Kipindi hiki utakutana na mtindo mpya wamaisha tofauti na ule uliouzoea. Ni muhimu kujiandaa kisaikolojia kwa maswala kama vile kukaa bila kupata mshahara, ofisi, gari la kampuni au taasisi, nyumba ya taasisi au kampuni pamoja na manufaa mengine ya wafanyakazi. Andaa fikra zako kutambua kuwa wakati wa kufaidi mambo mbalimbali ku...
Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Benki

Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Benki

Kipato
Benki ni taasisi muhimu ambayo siyo rahisi mtu kukwepa kuitumia kwa njia moja au nyingine. Kuhifadhi au kusafirisha pesa kwa njia za zamani kumepitwa na wakati; sasa ni wakati wa kutumia mifumo salama na ya kisasa. Kwa kuwa benki ni taasisi muhimu, huna budi kuchukua hatua kadhaa ili kupata benki nzuri kwa ajili ya shughuli zako za kifedha. Ikiwa unataka kupata benki nzuri, basi fahamu mambo 10 unayopaswa kuzingatia wakati wa kuchagua benki kwa ajili ya matumizi yako. 1. Usalama wa pesa zako Kwa kawaida kila benki husimamiwa na benki kuu ya nchi ili kuhakikisha usalama wa fedha za wateja. Hata hivyo kuna baadhi ya benki huanzishwa na kuendeshwa kinyemela bila kuwa chini ya benki kuu. Ni muhimu kuhakikisha benki unayotaka kuitumia imesajiliwa na inajiendesha kwa kuzingatia sh...
Maswali 10 Muhimu ya Kujiuliza Kabla ya Kuacha Kazi

Maswali 10 Muhimu ya Kujiuliza Kabla ya Kuacha Kazi

Kipato
Wakati wengine wakitafuta kazi usiku na mchana, wengine wanatamani kuacha kazi mara moja. Kutokana na sababu mbalimbali, swala la kuacha kazi linawakabili watu wengi. Mazingira mabaya ya kazi, matatizo ya kifamilia au kiafya yamekuwa chanzo kikubwa cha watu kutamani au kutaka kuacha kazi. Swala la kuacha kazi ni swala nyeti ambalo linahitaji utulivu na maamuzi yenye kuhusisha utafiti na busara kubwa. Wengi huacha kazi kutokana na misukosuko midogo na kujikuta wakiingia kwenye matatizo makubwa zaidi. Ikiwa unataka kuacha kazi unayoifanya ili utafute nyingine au ujiajiri mwenyewe, basi jiulize maswali haya 10 kabla ya kumpungia mwajiri wako mkono. 1. Je unaacha kwa sababu sahihi? Inawezekana umekaripiwa na mwajiri wako kutokana na kosa ulilolifanya, swala hili limekukasirisha ...
Njia 10 za Kuepuka Madeni

Njia 10 za Kuepuka Madeni

Kipato, Tija
Hakuna mtu anayependa kuwa na madeni, lakini mara nyingi watu hujikuta katika madeni makubwa. Kwa kiasi kikubwa watu wengi huingia kwenye madeni kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha matumizi kuliko kipato. Madeni siyo kitu kizuri hasa ikiwa hayatalipwa kwa wakati. Swala la kuepuka madeni ni swala linalohitaji maamuzi sahihi ya kifikra pamoja na mikakati stahiki. Je unapenda kuepuka au kupunguza kiwango chako cha madeni? Karibu nikufahamishe njia 10 za kuepuka madeni. 1. Jiwekee bajeti binafsi Utawasikia watu wakikosoa bajeti ya serekali lakini hawana bajeti zao binafsi. Bajeti binafsi ni muhimu kwani hukuwezesha kupanga juu ya mapato na matumizi yako. Ili kuepuka madeni, ni muhimu kuweka bajeti binafsi ambayo itakuongoza juu ya matumizi yako ya pesa ili usije ukatumia kul...
Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Kipato, Tovuti na Blogu
Je unatafuta njia ya kujipatia pesa kwenye mtandao ambayo siyo ya utapeli? Blog ni njia moja wapo unayoweza kuitumia kujipatia fedha huku ukifanya kile ukipendacho. Katika makala hii nitakushirikisha njia 14 unazoweza kuzitumia kupata pesa kwa kutumia blog yako. Kumbuka! Hizi si njia za kupata pesa za mteremko haraka haraka kwa usiku mmoja. Kamwe usidanganywe na matangazo ya kuwa utafanywa kuwa tajiri mkubwa siku moja. Mambo hayaendi hivyo. Awali ya yote utahitaji kuwa na blog yako; pia utahitajika kuwekeza rasilimali ya muda au pesa kiasi fulani ili kuweza kuona matokeo kutokana na blog yako. 1. Kuwa wakala Unaweza kupata pesa kwenye blog yako kwa njia ya kuwa wakala wa wauzaji wa bidhaa au huduma mbalimbali. Mara mtu anunuapo kitu kwa kukifikia kupitia blog yako basi utapata ...
Njia 10 Zitakazokuwezesha Kutumia Pesa Vyema

Njia 10 Zitakazokuwezesha Kutumia Pesa Vyema

Kipato, Tija
Je, huwa unajisikia vibaya unapohitaji pesa kwa ajili ya matumizi yako lakini unajikuta mifuko yako ni mitupu? Haijalishi unapata pesa kiasi gani, swala la matumizi mazuri ya pesa ni jambo muhimu; hili litakuwezesha kuwa na kitu wakati wa uhitaji. Watu wengi wanapata pesa lakini si wote wanaoweza kuzitumia vyema. Wengi hujikuta wakizitumia kwenye mambo na mipango ambayo mwishoni haiwaletei tija katika maisha yao. Naamini ungependa kuwa na matumizi mazuri ya pesa; sasa fahamu njia 10 zitakazokuwezesha kutumia pesa vyema. 1. Weka bajeti Ni rahisi kusikia watu wakilalamikia bajeti za serekali na kuzikosoa lakini wao wenyewe hawana bajeti zao binafsi. Unawezaje kukosoa bajeti ya serekali wakati ya kwako mwenyewe imekushinda? Fikiri tofauti; tambua umuhimu na jinsi ya kujiwekea baje...
Tovuti 15 za Kufanya Kazi Kwenye Mtandao

Tovuti 15 za Kufanya Kazi Kwenye Mtandao

Kipato
Mara nyingi milango ya matumizi ya fedha ni mingi kuliko milango ya mapato. Hivyo ni vyema kufikiri namna ya kuongeza milango mingi zaidi ya kipato. Inawezekana wewe ni mwajiriwa, mjasiriamali, mwanafunzi au hujaajiriwa bado; ni vyema ukafahamu kuwa zipo kazi zinazopatikana kwenye mtandao ambazo zinaweza kukuzalishia kipato kizuri. Hakuna sababu ya kukaa na maarifa au ujuzi ulionao ambao ungeweza kuutoa na ukajipatia kipato. Kufanya kazi kwa njia ya mtandao ni rahisi zaidi na kunakupa uhuru mkubwa wa mazingira ya kufanyia kazi. Fahamu kuwa unaweza kupata kazi nzuri zenye kipato kizuri katika tovuti 15 nilizoziorodhesha hapa. Soma Pia: Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao. 1. Upwork Upwork ni tovuti ambayo awali ilifahamika kama Odesk, k...