Biashara na Uchumi Archives - Fahamu Hili
Tuesday, March 19Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Biashara na Uchumi

Mambo 10 ya Kuzingatia ili Kutoa Huduma Nzuri kwa Wateja

Mambo 10 ya Kuzingatia ili Kutoa Huduma Nzuri kwa Wateja

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Changamoto ya huduma duni kwa wateja imekuwa kubwa sana kwenye biashara nyingi za kiafrika. Watoa huduma wengi hawajui na hawataki  kufahamu umuhimu wa kutoa huduma nzuri kwa wateja. Kwenye biashara na huduma nyingi mteja huchukuliwa kama kitu kisicho na nafasi wala umuhimu wowote. Lakini ukweli ni kuwa mteja ni msingi muhimu sana katika kufanikiwa kwa huduma au biashara yoyote ile. Kumbuka biashara yoyote isiyozingatia kutoa huduma nzuri kwa wateja wake itapoteza wateja na hatimaye itakufa. Kwa kutambua umuhimu wa kutoa huduma nzuri kwa wateja karibu nikushirikishe mambo 10 ambayo unapaswa kuyazingatia ili kutoa huduma nzuri. 1. Elewa hitaji la mteja Kamwe huwezi kumhudumia mteja vizuri bila kufahamu hitaji lake. Mara mteja anapofika katika biashara yako hakikisha unafa...
Mbinu 7 za Kulinda Biashara Yako Dhidi ya Athari za Corona (COVID 19)

Mbinu 7 za Kulinda Biashara Yako Dhidi ya Athari za Corona (COVID 19)

Biashara na Uchumi
Ni wazi kuwa dunia nzima inapitia msimu mpya baada ya kuibuka kwa ugonjwa wa homa ya mapafu wa Corona ulioibuka mnamo mwaka 2019 (COVID 19). Pasipo shaka sekta na taasisi mbalimbali zimeshuhudia mabadiliko makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa hayakutegemewa wala hazikujiandaa kwa mabadiliko hayo. Moja ya sekta iliyoathiriwa na inaendelea kuathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko yaliyoletwa na Corona ni biashara; biashara nyingi zimeporomoka, nyingine zimekufa na wakati nyingine zikijikuta katika wakati mgumu wa kujiendesha kwa utamaduni wake uliozoeleka. Karibu nikushirikishe mbinu 7 ambazo ikiwa utazitekeleza kikamilifu basi kwa kiasi kikubwa utaweza kukabili athari zitokanazo na ugonjwa wa Corona  (COVID 19) kwenye biashara. 1. Punguza matumizi yasiyo ya lazima Kutoka...
Athari 5 za Kukopesha Pesa na Bidhaa kwa Wateja

Athari 5 za Kukopesha Pesa na Bidhaa kwa Wateja

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Katika jaamii zetu za kiafrika suala la mikopo ya bidhaa au fedha kutoka kwenye biashara kwenda kwa wateja limezoeleka sana. Ingawa jambo hili linaweza kuwa na manufaa kwa upande fulani, hata hivyo kutokana na kukosekana kwa uaminifu miongoni mwa watu wengi jambo hili limekuwa na athari nyingi kuliko faida. Inawezekana umekuwa ukiwakopesha wateja wako wa maana sana, au umekuwa ukitumia mikopo kama njia ya kuuza huduma au bidhaa zako, lakini karibu nikushirikishe athari tano za mikopo hiyo. 1. Kumpoteza mteja Kuna usemi usemao kumkopesha mteja ni kumfukuza. Nimesikia mara kadhaa wafanyabiashara wakisema tangu ni mkopeshe haji tena dukani kwangu, au tangu nimkopeshe anapita mbali tu. Mara nyingi mteja akishakopeshwa pesa au bidhaa haji tena kwenye biashara husika ili kukwepa ku...
Mambo 8 ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Eneo la Kufanyia Biashara

Mambo 8 ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Eneo la Kufanyia Biashara

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Je ni maeneo gani sahihi ya kufungua biashara ili uweze kupata wateja, kukuza biashara na kutengeneza faida. Je, kila eneo linafaa kwa biashara? Hivyo basi, ili tuweze kujibu maswali haya vyema, hatuna budi kuangalia mambo 8 muhimu ya kuzingatia wakati wakuchagua eneo la kufanyia biashara ili ipate soko na kukua kila wakati. 1. Ushindani Ushindani ni jambo muhimu sana linaloweza kufanya eneo la biashara kuwa zuri au baya. Hebu fikiri mtu mchanga kabisa anaanzisha biashara mahali ambapo tayari kuna wafanyabiashara wengine wakubwa wenye uzoefu, mtaji, vitendeakazi au hata mtandao mzuri wa washirika. Bila shaka, itakuwa vigumu sana kwa mtu huyo kukua kibiashara. Ni lazima mtu apime na achague eneo amabalo lina ushindani ambao anaweza kuumudu na kukua. 2. Uhusiano kati ya biashar...
Zifahamu Aina 9 za Wateja ili Ukuze Biashara Yako

Zifahamu Aina 9 za Wateja ili Ukuze Biashara Yako

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Mteja ni nani? Mteja ni mtu yeyote anayenunua bidhaa au huduma inayotolewa na biashara fulani. Mteja ni mtu muhimu sana katika biashara yoyote. Lengo la kuanzisha biashara ni kupata wateja watakaonunua bidhaa au  huduma yako. Biashara yoyote isipopata wateja bora na wa uhakika, ni wazi kuwa haiwezi kufanikiwa; itakufa tu. Soma pia: Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa Kutokana na kukosa uelewa, wafanyabiashara wengi hawawafahamu wateja vyema, hivyo kutokuwamudu vyema; jambo ambalo huwakwamisha kufikia malengo yao. Ikiwa wewe ni mfanya biashara tayari au unataka kuanza kufanya biashara, karibu nikushirikishe aina 9 za wateja unazoweza kuzitumia kukuza biashara yako. 1. Wateja wapya Hawa ni wateja ambao huja kwenye biashara yako kwa mara ya kwanza, mnaweza kuwa m...
Mambo 10 ya Kujifunza Kama Mjasiriamali Kutokana na Anguko la Nokia

Mambo 10 ya Kujifunza Kama Mjasiriamali Kutokana na Anguko la Nokia

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Kama wewe uliwahi kidogo kwenye ulimwengu wa simu za mkononi, utakuwa umetumia au hata kusikia juu ya uimara, umaarufu na ubora wa simu za Nokia. Mnamo mwaka 1998 Nokia ilikuwa ndiyo kampuni bora ya kutengeneza na kuuza simu za mkononi duniani kote. Faida ya kampuni ya Nokia ilikwea kutoka dola za kimarekani bilioni 1 mwaka 1995 hadi dola bilioni 4 mwaka 1999; huku simu yake ya Nokia 1100 ikiwa ndiyo simu iliyowahi kuuzwa zaidi duniani. Nokia 1100 (Chanzo cha Picha: marketplace.citify.ca) Pamoja na mafanikio haya Nokia iliyoyapata, kwa kipindi kisichozidi miaka sita kuanzia mwaka 2007, hisa za Nokia ziliporomoka kwa asilimia 90.Kwa kutambua nafasi Nokia iliyokuwa nayo ikilinganishwa na anguko kubwa lililoipata, ni wazi kuwa kuna mengi ya kujifunza kama mjasiriamali au kiongoz...
Mambo Matano ya Kuzingatia Kabla ya Kuajiri Mtu Kupitia Mtandao wa Intaneti

Mambo Matano ya Kuzingatia Kabla ya Kuajiri Mtu Kupitia Mtandao wa Intaneti

Biashara na Uchumi
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili maisha ya mwanadamu kwa kiasi kikubwa. Sekta ya ajira nayo imepokea mabadiliko mengi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hivi leo ni rahisi mtu kuishi Afrika akafanya kazi Marekani au mtu akaishi India akaajiriwa Tanzania. Haya yote ni kutokana na teknolojia kuwezesha watu kuajiri au kuajiriwa kwa kupitia njia ya mtandao wa intaneti. Kwa kutambua kuwa kuajiri kwa njia ya mtandao ni njia nzuri ya kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni pamoja na kupata mtu mwenye sifa stahiki kwa kazi husika, basi fahamu mambo matano ya kuzingatia kabla ya kuajiri mtu kupitia mtandao. 1. Maarifa sahihi Kuna wafanyakazi wengi kwenye mtandao wa intaneti, lakini siyo wote ni bora au wana maarifa stahiki. Ni muhimu sana kufanya utafiti wa ...
Njia 12 za Kupunguza Gharama za Uendeshaji wa Kampuni

Njia 12 za Kupunguza Gharama za Uendeshaji wa Kampuni

Biashara na Uchumi
Mbinu mojawapo ya kuongeza faida katika kampuni au biashara yako ni kwa kupunguza matumizi ya kampuni yako. Suala la kupunguza matumizi ya pesa ni muhimu zaidi hasa pale ambapo kampuni inakuwa inakabiliwa na changamoto za kifedha. Kwa hakika kupunguza matumizi ya uendeshaji wa kampuni ni jambo linalowezekana ikiwa mikakati na hatua stahiki zitachukuliwa. Ikiwa unapenda kufahamu jinsi ya kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni, basi fahamu njia 12 unazoweza kuzitumia kufanikisha lengo hili. 1. Tathimini upya matumizi Kuna matumizi mbalimbali kwenye kila kampuni lakini siyo yote ni ya muhimu. Matumizi mengine ni ya lazima lakini yamepewa kipaumbele kuliko umuhimu wake. Kwa kupunguza matumizi ya vitu kama vile simu, umeme, maji, mafuta au hata intaneti, kutaokoa kiasi kikubw...
Njia 9 za Kutangaza Biashara Yako Bila Pesa

Njia 9 za Kutangaza Biashara Yako Bila Pesa

Biashara na Uchumi
Matangazo ni swala muhimu kwa kila biashara. Tatizo linatokea pale ambapo biashara inashindwa kumudu gharama za matangazo, hasa matangazo ya gharama kubwa. Naamini wewe kama mjasiriamali unafahamu kuwa kuna wakati bajeti ya biashara inakuwa imebana. Hivyo swala la kujitangaza linakuwa na changamoto. Fuatilia makala hii kwa karibu ili nikufahamishe njia 9 unazoweza kuzitumia kutangaza biashara yako bure au kwa gharama nafuu sana. 1. Tumia tovuti Tovuti au blog ni njia rahisi na ya gharama nafuu ya kujitangaza. Ikiwa una blog au tovuti ambayo inaidadi nzuri ya watembeleaji, unaweza kuweka tangazo la biashara yako hapo na likaonekana kwa watu wengi zaidi. 2. Tumia mitandao ya kijamii Kama ilivyo wenye njia ya blog, vivyo hivyo unaweza kutumia mitandao ya kijamii kama vile Facebo...
Mbinu 10  za Kuongeza au Kuvutia Wateja Kwenye Biashara

Mbinu 10 za Kuongeza au Kuvutia Wateja Kwenye Biashara

Biashara na Uchumi
Haijalishi huduma au bidhaa yako ni kubwa kiasi gani, biashara yako haitazalisha pesa kama wateja hawatakuwa tayari kununua bidhaa au huduma yako. Hakuna wateja, hakuna biashara. Tatizo la kukosa wateja hukabili sana biashara ndogo, na hata kusababisha biashara hizo kufa. Siyo kwamba wateja hawapendi kununua bidhaa za biashara hizi, bali tatizo kubwa ni mbinu duni za kujitangaza na masoko. Katika makala hii nitakueleza mbinu 10 rahisi na za gharama nafuu ambazo unaweza kuzitekeleza na ukaongeza au kuvutia wateja zaidi kwenye biashara yako. 1. Lugha nzuri Katika mambo yanayowapotezea wafanyabiashara wengi wateja ni lugha mbaya kwa wateja. Hakuna mteja anayependa kupokelewa au kujibiwa vibaya. Hakikisha unazungumza na wateja wako kwa namna bora ambayo wataona unawajali, unawathamini na ...