Biashara na Uchumi Archives - Page 2 of 2 - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Biashara na Uchumi

Mambo 5 ya Kuzingatia Kabla ya Kuchagua Wazo la Biashara

Mambo 5 ya Kuzingatia Kabla ya Kuchagua Wazo la Biashara

Biashara na Uchumi
Kuchagua wazo la biashara ni hatua ngumu na muhimu sana. Watu wengi hawafanikiwi kwenye biashara zao kwa kuwa wanakosea katika hatua hii. Uchaguzi sahihi wa wazo la biashara ni msingi muhimu katika kufikia malengo ya biashara yako. Ikiwa unataka kuanza biashara, basi karibu nikushirikishe mambo 5 ambayo unapaswa kuyazingatia kabla ya kuchagua wazo la biashara. 1. Chagua wazo unalolipenda Kanuni mojawapo ya kufanikiwa katika kile unachokifanya ni kwa kupenda kile unachokifanya. Unapochagua wazo unalolipenda ni wazi kuwa utalifanya kwa moyo na kwa ufanisi mkubwa hata kama utakutana na changamoto. Hivyo, usichague wazo kwa sababu fulani amelichagua au linampa faida kubwa mtu mwingine; kwako linaweza kuwa gumu na lenye hasara kubwa. 2. Chagua wazo unalolifahamu na kulimu...
Makosa 10 ya Kuepuka Unapotengeneza Logo au Nembo

Makosa 10 ya Kuepuka Unapotengeneza Logo au Nembo

Biashara na Uchumi
Nembo au logo ni jiwe la msingi la bidhaa na kampuni yako. Utambulisho wa biashara, kampuni yako au bidhaa unaonyeshwa kupitia nembo yako, ambayo ni pamoja na jina la kampuni yako. Hivyo, nembo ni moja kati ya mambo makuu ambayo yanafanya biashara yako kukumbukwa na kutambulika. Kwa kutambua umuhimu huu, kampuni na watu mbalimbali wamekuwa wakiwekeza fedha nyingi ili kupata nembo bora. Pamoja na kuwekeza pesa nyingi, bado kampuni na watu wengi hawapati nembo bora. Kwa mfano kampuni ya Pepsi iliwekeza dola milioni 1 lakini wakaishia kupata nembo iliyokumbana na ukosoaji mkubwa. Ni wazi kuwa kuna mambo unayotakiwa kuyazingatia kabla ya kuamua kulipia au kutengeneza nembo yako. Fahamu makosa 10 ambayo kama utayaepuka wakati wa kutengeneza au kuchagua nembo, basi utaweza kuwa na n...
Makosa 8 ya Kuepuka Unapofanya Biashara Kwenye Mtandao

Makosa 8 ya Kuepuka Unapofanya Biashara Kwenye Mtandao

Biashara na Uchumi
Kufanya biashara kwenye mtandao ni jambo lenye faida na changamoto zake. Unaweza ukawa na bidhaa nzuri sana, lakini ukumbuke kuwa kila siku kunaanzishwa tovuti za kuuza bidhaa mtandaoni. Haijalishi kuwa wewe ni muuzaji wa bidhaa wa siku nyingi au wa karibuni, ni wazi kuwa utakutana na changamoto kadha wa kadha. Sasa utafanyaje? Hakuna jibu rahisi, bali ni wazi kuwa makosa unayofanya wakati wa kuendesha biashara kwenye mtandao, ndiyo yanayokugharimu wewe na mapato yako. Yafuatayo ni makosa 8 ambayo unatakiwa kufanya juu chini ili kuhakikisha unayaepuka unapofanya biashara kwenye mtandao. 1. Kukosa kitengo cha huduma kwa wateja Ni rahisi mtu kukaa dukani kwake siku nzima ili kuwahudumia wateja; lakini unaona hakuna umuhimu wa kukaa karibu na wateja wake wa kwenye mtandao. Kumbuka ha...
Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Biashara na Uchumi
Hakuna mtu anayeanzisha biashara akitegemea ife, lakini wakati mwingine hili hutokea. Utafiti umebaini kuwa biashara na kampuni nyingi hufa ndani ya kipindi cha miaka miwili hadi mitano tangu kuanzishwa kwake. Kufa kwa biashara siyo jambo zuri, ni wazi kuwa kila mtu nayefanya biashara atatamani kufanya juu chini ili ainusuru biashara yake isife. Zipo sababu mbalimbali zinazosababisha biashara mbalimbali kufa. Fahamu sababu 13 zinazosababisha biashara nyingi kufa pamoja na jinsi ya kuziepuka. 1. Mipango duni Ili ufanikiwe katika biashara unahitaji mpango mzuri wa biashara. Biashara nyingi zinazoanzishwa Afrika hazina mipango madhubuti ya kibiashara inayoonyesha maswala kama vile muundo wa utawala, mtaji, mikakati au mipango ya mauzo, n.k Biashara nyingi pia hukosa lengo; jambo a...
Nembo/Logo za Kibiashara Zilizobeba Maana Usizozijua

Nembo/Logo za Kibiashara Zilizobeba Maana Usizozijua

Biashara na Uchumi
Kama unavyojua nembo au logo ya kibiashara ina nafasi kubwa katika utambulisho wa kampuni. Nembo iliyobuniwa vizuri inaweza kuwafanya watu wengi kutambua huduma au bidhaa unayotoa. Hii ndiyo sababu logo nyingi hupitia usanifu na maboresho mbalimbali ili kuhakikisha zinawakilisha kampuni au biashara vyema. Hata hivyo, zipo logo zilizofanikiwa kufanya vizuri  wakati nyingine hazijafanikiwa. Kwa zile zilizofanikiwa unaweza kushangaa ni kwa namna gani wabunifu wake wameweza kuficha maana fulani muhimu kuhusu kampuni husika. Fahamuhili kwa kutambua umuhimu wa utambulisho katika biashara au kampuni, tumekuletea orodha hii ya nembo zaidi ya 10 pamoja na maana zilizojificha ndani yake. Tunaamini makala hii itakupa mwangaza muhimu pale utakapokuwa unatengeneza logo yako. Soma pia: Mamb...
Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Hivi leo wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika kuwahi na kufanyia kazi fursa mbalimbali. Fursa hizo ni pamoja na uwekezaji katika biashara ndogo na za kati. Ni dhahiri kuwa mama ndiye nayeumia zaidi pale familia inapokuwa na uchumi mbaya. Mama hapendi kuona watoto wanakosa mahitaji yao ya msingi kama vile chakula, mavazi, elimu, matibabu n.k. Hivyo suala la kuboresha kipato cha familia limewafanya wanawake wengi kutafuta njia mbalimbali za kujipatia kipato ikiwemo njia ya kufanya biashara. Hata hivyo pamoja na jitihada hizi zinazofanywa na wanawake, bado biashara zao ngingi hufa kutokana na sababu kadha wa kadha. Fuatana nami katika makala hii ufahamu mambo matano yanayosababisha biashara nyingi za wanawake kufa. 1. Kukosa maarifa na elimu ya biashara Kitu chochote au kazi y...
Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kuchagua Jina la Biashara

Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Kuchagua Jina la Biashara

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Uteuzi wa jina la biashara ni hatua muhimu kama ilivyo kwa jiwe la pembeni katika nyumba. Watu wengi wamekuwa hawatilii maanani mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kuchagua jina la biashara au kampuni. Nimekuwa nikishuhudia makapuni mengi yakitumia majina ya ajabu ajabu yasiyoendana na biashara zao. Kwa sehemu kubwa kufanikiwa na kujulikana kwa biashara yako kunategemea jina la biashara yako. Fuatana nami katika makala hii ambayo nitakueleza mambo kadhaa ya kuzingatia kabla ya kuchagua jina la biashara. 1. Uhusiano wa jina na bidhaa au huduma Je unafahamu kwamba jina la biashara linatakiwa liakisi huduma au biashara unayoifanya? Ni jambo jema kutumia jina linaloakisi kile unachokifanya. Kwa mfano jina kama vile “Samelctro” lifaa kwa kampuni ya vifaa vya kielektroniki, “Pamba L...
Mambo 7 ya Kufanya Kabla ya Kuanzisha Kampuni au Biashara

Mambo 7 ya Kufanya Kabla ya Kuanzisha Kampuni au Biashara

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Inawezekana una wazo zuri sana la biashara na unatamani kulitekeleza haraka kadri iwezekananavyo. Pengine umeajiriwa katika taasisi au ofisi fulani na unashauku kubwa ya kuacha kazi ili uweze kuanzisha kampuni au biashara yako. Kabla hujafanya maamuzi yoyote ni vyema ukae chini na utafakari mambo kadhaa ambayo yatakuwa na manufaa makubwa kwako. Katika makala hii nitakueleza mambo 7 muhimu ambayo utahitajika kuyafanya kabla ya kuanza biashara yako. 1. Chagua wazo la biashara vyema Katika eneo ambalo watu wengi hukosea wakati wanapoanzisha kampuni au biashara ni uchaguzi wa wazo la kibiashara. Unapochagua wazo baya au usilolimudu, ni wazi kuwa hutoweza kulitekeleza na kupata faida. Hakikisha wazo unalolichagua unalimudu vyema pia linatekelezeka. Epuka kuchagua wazo pana sana au...
Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Watu wengi wamekuwa wakitamani kuanza biashara lakini wanafikiri namna ya kuanza kwani mtaji wao ni mdogo sana. Ni ukweli usiopingika kuwa idadi kubwa ya watu walioshindwa kuanzisha biashara wakishindwa katika eno hili la kuanza biashara na mtaji mdogo. Usiogope; kuwa na mtaji mdogo au kutokuwa nao kabisa sio mwisho wako wa kutimiza malengo yako. Zipo mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukuwezesha kufanya biashara hata kama utakuwa na mtaji mdogo. Tafadhali fuatilia hoja jadiliwa hapo chini kwa ufafanuzi zaidi. 1. Kuwa mbunifu Moja kati ya mambo ambayo yatakusaidia sana kwenye kuanza biashara kwa mtaji mdogo ni ubunifu. Kwa njia ya ubunifu utaweza kushinda biashara na bidhaa zilizoko sokoni kwa urahisi zaidi. Unaweza kufanya haya yafuatayo: Chagua wazo la biashara unalolipenda na ku...