Watu wengi wamekuwa wakitamani kuanza biashara lakini wanafikiri namna ya kuanza kwani mtaji wao ni mdogo sana.
Usiogope; kuwa na mtaji mdogo au kutokuwa nao kabisa sio mwisho wako wa kutimiza malengo yako.
“Usilie juu ya kile ambacho huna; tumia vizuri kile ulichonacho.”
Zipo mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukuwezesha kufanya biashara hata kama utakuwa na mtaji mdogo. Tafadhali fuatilia hoja jadiliwa hapo chini kwa ufafanuzi zaidi.
1. Kuwa mbunifu
Moja kati ya mambo ambayo yatakusaidia sana kwenye kuanza biashara kwa mtaji mdogo ni ubunifu. Kwa njia ya ubunifu utaweza kushinda biashara na bidhaa zilizoko sokoni kwa urahisi zaidi. Unaweza kufanya haya yafuatayo:
- Chagua wazo la biashara unalolipenda na kuliweza vyema. Hili litakusaidia kukabili changamoto vyema.
- Angalia tatizo au uhitaji uliopo sasa na uutatue kwa bidhaa au huduma yako.
- Panga bei vizuri; unaweza kuweka bei ambayo ni tofauti kidogo na bidhaa au huduma ambazo tayari ziko sokoni ili uwavutie wateja.
Kwa kufanya mambo yaliyoelezwa hapa juu utaweza kukuza biashara na mtaji wako kwa muda mfupi zaidi.
2. Anza na unachokijua
Unapokuwa na mtaji mdogo huhitaji kuhusisha mambo mengi mageni au yanayotegemea sana watu wengine kwa kuwa huna pesa za kuyagaramia.
Kwa mfano kama unaanzisha biashara ya ushonaji basi anza kutengeneza mavazi yale unayoyaweza kwa kutumia vifaa ulivyonavyo; kwa njia hii utajenga mtaji wako kisha baadaye utaweza kuajiri wengine watakao kuwezesha kutengeneza aina nyingine zaidi.
Unapofanya kile unachokijua gharama huwa haziwi kubwa sana kwani ni kitu unachokimudu mwenyewe.
Soma pia: Mambo 7 ya Kufanya Kabla ya Kuanzisha Kampuni au Biashara.
3. Waambie watu unachokifanya
Waambie watu unachokifanya kwani hili litakuwezesha kupata wateja na kufahamika. Watu wakijua unachokifanya watatamani kukifahamu zaidi; hili litakuwezesha kupata wateja na kuongeza mtaji wako.
Usiogope kueleza kuwa unafanya biashara ya mboga, chakula, duka dogo la bidhaa n.k. Kwani hujui unaemweleza atakuwa nani kwenye biashara yako.
Ukiwa na marafiki kwenye mitandao ya kijamii waeleze pia juu ya kile unachokifanya.
4. Epuka gharama zisizokuwa za lazima
Kwakuwa bado una mtaji mdogo jitahidi kuepuka garama zisizo za lazima kama vile ofisi ya kifahari, matangazo ya gharama kubwa n.k.
Kuwa na matumizi mazuri ya fedha hasa kwa mambo ya msingi tu. Watu wengi wameshindwa kwenye biashara kwa sababu wameanza biashara kwa mbwembwe za matumizi badala ya huduma bora zenye ubunifu.
5. Fanya kazi kwa bidii
Kamwe huwezi kuona mafanikio kama hutofanya bidii. Kumbuka wewe ni mjasiriamali anayeanza hivyo ni lazima ufanye bidii ili soko litambue kuwa upo pia unaweza.
Tumia muda vizuri, pia hakikisha unatoa huduma yenye ubora wa hali ya juu kwa bei ambayo wateja wataweza kuimudu. Jitese kwa muda mfupi kwa kipindi cha kuweka msingi wa biashara yako kwani hata kipindi cha kupanda katika kilimo huwa ni cha taabu.
Soma pia: Tabia 10 Unazotakiwa Kijifunza Kutoka kwa Watu Waliofanikiwa.
6. Tumia rasilimali na fursa zilizopo
Njia nyingine itakayokuwezesha kuanza biashara ukiwa na mtaji mdogo ni kutumia fursa zilizopo. Kumbuka kuwa huwezi kutengeneza fursa kama huwezi kutumia fursa zilizopo.
Tumia fursa kama vile mitandao ya kijamii ili kujitangaza. Pia unaweza kutumia udhaifu uliopo katika biashara nyingine za watangulizi wako kama fursa kwani unaweza ukarekebisha udhaifu huo kupitia biashara yako.
Zipo pia fursa za mikopo yenye masharti nafuu ambayo itakuwezesha kuongeza mtaji wako. Kumbuka unahitaji kutumia mkopo kwa makini kwani utahitajika kuurudisha pamoja na riba tena kwa wakati.
7. Jali wateja
Kujali wateja katika biashara ni jambo muhimu sana kama unataka kuona matokeo chanya. Siku zote ninapenda kusema “wateja hufugwa”. Wateja hufugwaje? Hufugwa kwa huduma nzuri.
Waheshimu wateja wako pia hakikisha unatimiza na kumaliza haja zao katika ubora wa hali ya juu. Kumbuka siku zote mteja huja kwanza kabla ya pesa; hivyo usitangulize pesa kabla ya huduma nzuri kwa mteja.
Ukilifanyia kazi hili utaweza kukuza biashara na mtaji wako kwa muda mfupi.
Soma pia: Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka.
Hitimisho
Zilizojadiliwa hapa ni mbinu saba zitakazokuwezesha kuanza biashara na mtaji mdogo. Usiogope unaweza hata kama una kiasi kidogo sana cha fedha.
Thubutu, nza, fanya bidii, weka nidhamu, mtangulize Mungu na hakika utaona mafanikio chanya katika biashara yako.
“Anzia ulipo.Tumia ulicho nacho. Fanya unachoweza.”
Bado umekwama katika eneo la kuwa na mtaji mdogo? Tafadhali tupe maoni yako; pia karibu uwashirikishe wengine makala hii. Usisahau pia kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Nashukuru kwa elimu nzuri, ila kuna mambo ningependa kuuliza kutoka kwako kama hutojali
Namba yangu 0759428***
Nashukuru sana kwa maoni yako; Karibu; Hakuna shida ndugu unaweza kuuliza tu swali lako bila wasiwasi wowote. Kama utapenda kutumia simu unaweza kutumia 0785138819 au barua pepe ya korneliomaanga[at]gmail.com
Nataka kuwa wakala
Wakala wa kitu gani ndugu?
Hey kaka
Habari Mr. Paul, karibu Fahamuhili.com
Uliza
Karibu uulize ndugu;
Kwanza niwashukuru watoa mawazo mazuri hapo hujuu kwan wamenifungua akili vzr.mm nina tatizo la kukata tamaa mapema je nifanyaje? naombeni msaada wenu
Habari ndugu Michael; Tunashukuru kwa kusoma makala ya blog yetu pamoja na maoni yako. Ni faraja kwetu kuwa makala hii imekuwa ya manufaa kwako. Ikiwa unakabiliwa na tatizo la kukata tamaa fanya yafuatayo. 1. Ondoa mawazo hasi. Kukata tamaa kwanza kunaanzia kwenye fikra zako. Epuka mawazo kuwa hautafanikiwa, au umekosea au lingine ulishindwa au wengine walishindwa. Ona kushinda akilini mwako kwanza; ndipo utakapoona kushinda na kufanikiwa maishani mwako. 2. Jiwekee malengo na uyaandike na kuyatazama kila mara. Unapokata tama tazama malengo yako ili yakupe hamasa zaidi ya kusonga mbele ili uyafikie. (soma pia faida za kuwa na malengo). 3. Ainisha… Read more »
Asanteni kwa ushauli wenu
Tunashukuru sana kwa maoni yako; karibu.
Chamuhimu ni kujua nini unapenda kufanya napia sio pesa ndio ufanye biashara ila mawazo kwanza.
Ni kweli kabisa; tunashukuru sana kwa maoni yako na karibu sana Fahamuhili.com
Its okay and fantastic
Tunashukuru sana; karibu sana Fahamuhili.com
hakika nimejifunza vitu vizuri hapa
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mada nimeielewa nilikua nashindwa jinsi ya kuanza sasa nimepata mwanga ninamtaji wa kiasi cha laki najifikilia cha kufanya bado xijapata jibu naomben mawazo nifanye mini?
Hongera kwa kusoma makala zetu pia ninashukuru kwa swali lako la thamani; tafadhali nimejibu swali lako katika makala inayopatikana hapa: (https://www.fahamuhili.com/njia-unazoweza-kuzitumia-ili-kupata-mtaji/) asante na karibu sana Fahamuhili.com
ndg nashukukru kwa somo lako zuri najua nitayafanyia kazi
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Elimu yako iko vizuri.Je,ukiwa na 50000 Unaweza kuanza mtaji?
Inatosha kabisa kuwa mtaji; inategema tu unataka kufanya nini; jifunze kuanza kidogo ili ujifunze huku ukikua. Asante.
Asante sana kwa ushauri mzuri kuhusu ujasiriamali.
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Asante KWA ushauli mm namtaji wa30000 nitafanyaje
Karibu: https://www.fahamuhili.com/jinsi-ya-kuanza-biashara-na-mtaji-mdogo/. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nashukur Sana kwa elimu hii nataka kuwa mfanya biashara was nguo nitaifanya sehemu gani?
Unaweza kufanya sehemu ile ambayo unaona uko huru kifika na kufanya biashara ipasavyo; pia fanya biashara kwenye eneo ambalo umelifanyia utafiti wa kina na kujihakikishia kuwa malengo yako yatatimia. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nashukur Sana kwa elimu hii nataka kuwa mfanya biashara was nguo nitaifanya sehemu gani hiyo maana naona sehemu zote Kuna ushindani Sana na mm Sina mtaji was kutosha kumudu huo ushindani
Hongera sana kwa kuthubutu kuwa mjasirimali biashara; jitahidi kuwa mbunifu pia usikate tamaa. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nashukuru kwa somo zurii sana nimefurah saana kupata elimu hii pia Nina maswali machache nahitaji kuuliza
Karibu Fahamuhili.com tukujibu.
Naweza kuwa wakala wa M-pesa kwa mtaji wa 100,000?
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mawasiliano:
Email: fahamuhili[at]gmail.com
Simu: 0758 444 771
Nataka kufanya biashara ya uwakala mpesa,tigo pesa unanishauri Nini?
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mawasiliano:
Email: fahamuhili[at]gmail.com
Simu: 0758 444 771
Nimefarijika sana na elimu unayotoa MUNGU azidi kukupa nguvu ili uzidi kutuelimisha..
Napendekeza ungeazisha na group la whatsap ili tuwe karib nawe zaid😊
Tutafanyia kazi maoni yako; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mmh asante Ila nahitaji kujua zaidi kabisa natumaini nitazidi kukufuatilia kwani
Hakika; Asante sana kwa maoni yako ya thamani kwetu; karibu sana Fahamuhili.com
Nimeshukuru
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Asanteni kwa ushauri wenu mim Ni mfanya bihashara ila hii bihashara tuna share watu wa will sasa mwenzangu mda mwingi anakuwa anahusika na mimi mda mwingine nakuwa kazini niliko ajiliwa ila inapotokea kama kuhusika kifedha uwa nahusika bila tatizo kama kuna pesa inaitajika ili kupiga hatua kibihashara kinacho nipa hofu Sasa Ni wakati wa kuibland bidhaa yetu yeye ndio anae jitambulisha zaidi ata kutoa mawasioiano anatoa contakti moja tu ambayo Ni yake mfano kwenye nembo ya bihashara , vipeperushi, ata business card yaan kiujumla hakuna kitu chochote kinachoonyesha kuwa na mim Ni muhusika je happy nini nifanye nahisi italeta shida… Read more »
Kama mlianza kwa pamoja zungumzeni ili muwe na baadaye njema ambayo haina kutokuelewa. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Thnks
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mm nimuajiliwa ninauwezo wa kupata mtaji mdogo lakn sjui nifanye biashala gan yaan hapo tu ndpo mm nakwama
Kika jamabo huanza kidogo; unaweza kufanya biashara yoyote unayoipenda na kuimudu kwa mtaji wako huo mdogo bila shida yoyote. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
What are business which does not involve any capital?
Hakuna; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Je, ni gani yakuweza kupata mikopo kuongezea mitaji midogo tuliyonayo?
Ndiyo unaweza kupitia;
1. Vikundi vidogo vya kuweka akiba na kukopa kama vile SACCOS na VICOBA
2. Taasisi za kifedha kama vile benki na Micro-finances
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Njemaa
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Ahsante saana kwa ushauri mzur
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mungu akubariki Mimi tayari ni mjasiriamali wa genge dogo la mahitaji madogomadogo ya nyumbani nashukuru Kwa Elimu nzuri
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Kiukweli, nimejifunza vingi na kupata ujasiri wa kile nachokwenda kukifanya..MUNGU ATUTANGULIE SOTE..BILA KURUDI NYUMA.
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com