Sifa 10 Zitakazokufanya Kuwa Kiongozi Bora - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Sifa 10 Zitakazokufanya Kuwa Kiongozi Bora

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Je kiongozi bora ni yule mwenye wafuasi wengi au miaka mingi katika uongozi? La hasha, kiongozi bora hujengwa kwa sifa anuwai.

Ni rahisi kufikiri kuwa kiongozi bora hutokea kwa bahati tu au hakuna haja ya kujifunza jinsi ya kuwa kiongozi bora. Wewe kama mtu anayehitaji kusimamia na kuratibu shughuli mbalimbali ni lazima ufahamu sifa zinazomfanya mtu kuwa kiongozi bora ili uwe na mafaniko.

“Kama matendo yako yanawahamasisha wengine kupata ndoto zaidi, kujifunza zaidi, kufanya na kuwa zaidi, wewe ni kiongozi.”

John Quincy Adams

Katika makala hii utaweza kufahamu sifa 10 zitakazokufanya kuwa kiongozi bora.

1. Uwazi

Uwazi ni sifa muhimu inayomfanya mtu kuwa kiongozi bora. Kiongozi bora ni lazima awe wazi katika utendaji kazi wake.

Uwapo kiongozi kuna siri za kazi lakini namna ya utendaji kazi hautakiwi uwe siri au usioeleweka kwa wale unaowaongoza. Kiongozi bora anatakiwa kuwa na mpangilio mzuri na unaoeleweka wa utendaji kazi wake.

2. Maono

“Kiongozi ni yule anayejua njia, anakwenda njia hiyo na anaonyesha njia.”

John C. Maxwell

Maono ni picha inayojengeka katika fikira ya matokeo ya jambo ambalo linapangwa kutekelezwa.

Kama wewe ni kiongozi asiyeweza kuona picha ya baadaye ya kampuni au taasisi hutawea kuiongoza kampuni kufikia mafaniko na malengo yake. Jitahidi kujifunza kuwa na maono katika jambo lolote unalolifanya ili lifanikiwe.

3. Uadilifu

Ili uwe kiongozi bora huna budi kuwa mwadilifu. Heshimu kazi, tunza muda, tunza fedha pia tumia nafasi yako kwa njia amabyo si ya kibadhirifu.

Ni rahisi mtu kushawishika kutumia ofisi au nafasi ya kiuongozi kwa maslahi binafsi jambo ambalo linamfanya kupoteza sifa yake ya kiongozo bora.

4. Ujasiri

Huwezi kuwa kiongozi bora kama hutakuwa na ujasiri katika maswala mbalimbali. Unahitaji ujasiri kufanya maamuzi mbalimbali katika eneo au taasisi unayoiongoza kama vile kufanya uwekezaji mpya, kubadili mfumo wa utendaji kampuni au taasisi n.k.

Lazima kiongozi aoneshe ujasiri kwa watawaliwa au wafanyakazi wengine katika maamuzi yake anayoyafanya kila siku.

5. Subira

Kuna mambo yanayohitaji subira katika maisha. Kiongozi asiye bora hutaka kila kitu kitimie kwa siku moja. Kuwa kiongozi mkomavu ni kuwa subira na uvumilivu.

Wakati mweingine kampuni au taasisi yako inaweza kuwa inapita kwenye kipindi kigumu; usipokuwa kiongozi mwenye subira unaweza kufanya maamuzi ambayo yataathiri kampuni daima.

6. Mbunifu

“Ubunifu unatofautisha kati ya kiongozi na mfuasi.”

Steve Jobs

Kufankiwa kwa kampuni au taasisi kunahitaji ubunifu wa hali ya juu kila mara. Hivyo basi ili uweze kuwa kiongozi bora jitahidi kuwa mbunifu.

Buni mbinu, mawazo na miradi mbalimbali ambayo itawezesha kampuni au taasisi kukua na kufikia malengo yake.

Epuka kutegemea mawazo ya zamani hata kama bado yanailetea kampuni faida kwani mambo yanaweza kubadilika wakati wowote.

7. Uwajibikaji

“Uongozi ni kuwa mtumishi kwanza.”

Allen West

Ukitaka kuwa kiongozi bora huwezi kujitenga na uwajibikaji. Lazima uwajibike kutimiza majukumu yako yote.

Utawezaje kuwaongoza na kuwahimiza wengine kutimiza majukumu yao kama wewe mwenyewe huwezi kutimiza majukumu yako? Nasisitiza tena kwa kusema wajibika katika nafasi yako na wale unaowaongoza watawajibika katika nafasi zao.

8. Kujituma

Kujituma ni jambo muhimu sana kwa kiongozi bora. Kiongozi bora hahitaji sheria na usimamizi mkali ili atimize majukumu yake.

Hivyo basi, ukitaka kuwa kiongozi bora ni lazima ujifunze kujituma bila kusukumwa na mtu. Fanya bidii uwapo kazini au katika nafasi yako yaa kiuongozi; hili litakujenga na kukufanya kuwa kiongozi bora.

9. Mawasiliano

Mawasiliano ni swala muhimu sana linalojenga utawala bora. Katika taasisi au kampuni isiyokuwa na mfumo mzuri wa mawasiliano lazima kutatokea migongano na misuguano isiyokuwa na sababu.

Ukiwa kiongozi hakikisha unakuwa na mfumo mzuri wa mawasiliano na watu wengine katika taasisi au kampuni unayoiongoza. Hakikisha pia unajenga mfano mzuri wa kutoa taarifa katika kampuni au taasisi iliyopo.

10. Nidhamu

Kuna mambo ambayo huwezi kufanya unapokuwa kiongozi hata kama wengine wanayafanya au unavutiwa nayo. Siku zote epuka tabia zisizo endana na kiongozi bora kama vile ulevi, umbeya, uvivu, anasa, starehe, kuongea hovyo n.k.

Onesha watu unaowaongoza kuwa wewe ni kiongozi mwenye uelewa uliokujengea nidhamu na kujitawala.

Hitimisho

Hapa nimekueleza sifa kumi zitakazo kuwezesha kuwa kiongozi bora. Ni wazi kuwa huwezi kuwa kiongozi atakayeleta mabadiliko katika taasisi au kampuni unayoiongoza kama hutojifuza kuwa kiongozi bora.

Je una maoni gani juu ya hoja zilizojadiliwa hapa pamoja na suala zima la kiongozi bora? Tafadhali tupe maoni yako hapa chini tafadhali. Pia usisahau kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.

3.9 34 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

78 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Abubakary Ahmed
Abubakary Ahmed
5 years ago

Hongera kiongozi

spajo
spajo
5 years ago

nmeipendaaa

samwel
samwel
5 years ago

well done

george
george
4 years ago

Napenda sifa hizi na ni nzuri na nilizitumia chache zikaniletea faida; ila asante kwa kusijua nyingine .

Elias David
Elias David
4 years ago

Nimefurahishwa na uchambuzi wenu

Scarface
Scarface
4 years ago

Yamegusa nyoyo za watu wengi na kila kiongozi angependa kufuata hizi kanuni.

Abeid Juma Abeid Heke
Abeid Juma Abeid Heke
4 years ago

Nime elewa Sana juu y’all sifa za Kuwa kiongozi bora. Hongera Sana kwa kuelimisha jamii

Zabron
Zabron
3 years ago

Kazi nzuri kiongozi.
Tuko pamoja

Christina
Christina
Reply to  Kornelio Maanga
3 years ago

Nimependa sana mafunzo haya,nikiwa nahitaji mwongozo,nakupataje?

Peter Michael
Peter Michael
3 years ago

Somo zuri sana

Emmanuel
Emmanuel
3 years ago

Nice explaination

Bundala thomas
Bundala thomas
3 years ago

Good

Bundala thomas
Bundala thomas
3 years ago

Nimeipanda sana iko powa

Petro
Petro
3 years ago

Ahsant kwa elimu

abdallah
abdallah
3 years ago

Kazi nzuri shukrani kiongozi

Datius pantaleo
Datius pantaleo
3 years ago

Asante sana hakika ukizifata hizo mafanikio yatakuwa mara mia

BULUKAY
BULUKAY
2 years ago

Nashukuru sana nimejifunza mengi ambayo nilikuwa siyajui kuhusu sifa za kiongozi.

Titus Korir kutoka Bomet
Titus Korir kutoka Bomet
2 years ago

Sifa hizi kwa ukweli. Imenijenga Sana nimeanza Sasa kutumia hizi sifa kumi Asante Sana.

Nathaniel
Nathaniel
2 years ago

NICE!

Frank Jacob maguha
Frank Jacob maguha
2 years ago

Hongera sana mkuu

Tito
Tito
2 years ago

Habari

haroun
haroun
2 years ago

hongera sana

Mwl na mwinjilisti MASEBO
Mwl na mwinjilisti MASEBO
1 year ago

Hakika nimetosheka na maelezo mazuri

Daniel Kitua
Daniel Kitua
1 year ago

Mafunzo haya ni muhimu sana na yameelezea kwa utafiti mkubwa

Juma mwita
Juma mwita
1 year ago

Fafanua vizuri sifa ya mawasiliano haijawa wazi

Tosha Andrew
Tosha Andrew
1 year ago

Hili darasa ni Zaid ya chuo kikuu,asante sana

Thomas malimi
Thomas malimi
1 year ago

Good

Thomas malimi
Thomas malimi
1 year ago

Nimejifunza kitu kikubwa san,naanza kulifanyia kazi nami kama kiongozi.

DERICK DEUS
DERICK DEUS
1 year ago

Nashukulu kwa mafunzo hayo

Boniphace Mathias
Boniphace Mathias
Reply to  Kornelio Maanga
1 year ago

Nimependa sana somo lako hili mkuu shukrani sana. vp nikihitaji kuwasiliana nawe zaidi nitakupataje mkuu.

Joshua George
Joshua George
1 year ago

I am a Ugandan who seeks knowledge about kiswahili any sites for helping me improve my overall knowledge of kiswahili please

Gerald Njimba
Gerald Njimba
1 year ago

Asantee nimejifunza. Naomba kuuliza kuna tofauti gani kati ya Kiongozi na Mwanasiasa ?

Patrick
Patrick
1 year ago

Nimekuelewa mkuu kumbe tuna kosea na hatujui. Asante kwa maalifa

Yusuph s. Masatu
Yusuph s. Masatu
1 year ago

Asantee sana kwa ushauri mzuri pia mawazo yenye nguvu kubwa zaidi

Mathew Friday
Mathew Friday
1 year ago

Perfect

Shoko mnarani
Shoko mnarani
1 year ago

Asante sana kwa mafunzo yenye Hekima ya uongozi🙏

Masudi
Masudi
1 year ago

Asante kwa Ushauli

Khaddy
Khaddy
1 year ago

Nimejifunza

James James
James James
11 months ago

Asante sana nmeelewa mengi sana

catherine
catherine
10 months ago

lovely teachings

Bugaba Arnold
Bugaba Arnold
10 months ago

Mimi ni mpya sana

Masatu
Masatu
9 months ago

Niwashukulu Kwa kuelezea kiufasaha.

Irakoze Jean Damour
Irakoze Jean Damour
8 months ago

Ni bora

78
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x