Ikizingatiwa kuwa upatikanaji wa ajira umekuwa wa shida sana, watu wengi hujikuta wakiwa na chaguo la kuwa wajasiriamali pekee kwenye maisha yao.
Wengi hutamani au hata kujiingiza kwenye ujasiriamali, lakini siyo wote wanaofanikiwa kutokana na kutokufahamu kanuni muhimu za ujasiriamali. Ni wazi kuwa ili uanzishe kitu chochote chenye mafanikio, ni lazima ufahamu kanuni za kukifanya kitu hicho jinsi ipasavyo.
Ikiwa wewe ni mjasiriamali, au unataka kuwa mjasiriamali, basi fuatilia makala hii ili nikufahamishe kanuni 15 za ujasiriamali.
1. Kuwa mtatuzi wa matatizo
Ujasiriamali ni zaidi ya kupata pesa, ni lazima kwanza utatue changamoto ya mtu ndipo utaweza kupata pesa kutoka kwa mtu husika. Ni muhimu ukafahamu kanuni hii kama mjasiriamali kwani hutojikita kutafuta pesa bali utajikita kutatua matatizo ya watu.
Kwa mfano kama kuna tatizo la upatikanaji wa mboga katika mji au eneo unalokaa, ikiwa wewe utaleta mboga katika eneo hilo ni wazi kuwa watu watakupa pesa ili uwape mboga. Hivyo ni muhimu kila mara ukatafuta changamoto ukaitatua, nawe bila shaka utapata pesa za uhakika.
“Pesa ni matokeo ya kutatua shida ya mtu”
2. Kuwa na maono
Hakuna ujasiriamali bila maono. Kuwa mjasiriamali bila maono ni sawa na kuendesha gari isiyokuwa na usukani. Maono katika ujasiriamali yatakuwezesha kukuongoza ufanye nini na kwa muda gani. Ni lazima ujiulize kuwa unataka kuwa nani, lini na unataka kufanya nini baadaye? Jonathan Swift alisema maono ni sanaa ya kuona kile ambacho wengine hawaoni. Ni lazima uwe na lengo na ufanye bidii kulifikia.
“Wajasiriamali waliofanikiwa ni wale walioweza kubadili maono yao kuwa uhalisia”
3. Chagua washirika au timu sahihi
Wakati mwingine utahitaji kufanya kazi na watu au mtu fulani. Ni muhimu kuwa makini wakati wa kuchagua washirika au timu ya kufanya nayo kazi ili kuhakikisha maono yako hayakwamishwi. Kamwe usichukue mtu tu kwa kigezo kuwa ni rafiki au ndugu yako, bali chukua mtu ambaye unaamini anaweza kufanya kitu chenye tija kwa ajili ya kufanikisha malengo yako kama mjasiriamali.
Soma pia: Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka.
4. Toa huduma au bidhaa yenye tija
Hivi leo sokoni kuna bidhaa na huduma nyingi ambazo ni za aina moja, lakini siyo zote zinafanya vizuri. Hii ni kutokana na baadhi ya bidhaa au huduma kutozingatia kuwa na tija kwa wateja wake. Ikiwa unatengeneza bidhaa au huduma fulani hakikisha itakuwa na manufaa makubwa na ya uhakika kwa wateja wako.
Kwa mfano nimewahi kuona vitafunwa vilivyoandaliwa katika mazingira duni na kuwa na dosari mbalimbali kama vile marashi, vipande vya nywele, mchanga n.k. Ni wazi kuwa bidhaa za namna hii zitakosa wateja kutokana na kuwa na ubora duni.
Kila mara kumbuka kuwa ushindani ni mkubwa, hivyo jitahidi kuongeza tija na ubora wa huduma na bidhaa zako.
5. Fahamu na jali wateja
Ikiwa wewe ni mjasiriamali, basi futa mawazo kuwa wateja wanakuhitaji wewe. Fahamu kuwa wewe kama mjasiriamali, ndiye unaye wahitaji wateja ili ukuze biashara au huduma yako. Hakikisha mambo haya kuhusu wateja:
- Fahamu wanataka nini.
- Sikiliza maoni na ushauri wao.
- Hakikisha unakamilisha mahitaji yao.
- Tumia lugha nzuri na rafiki kwa wateja.
- Mfanye mteja aone unamthamini.
- Mfanye mteja aone kuwa umetanguliza huduma kabla ya pesa.
Naamini kwa kufanya hivi utaweza kujijengea msingi mzuri wa wateja kwa ajili ya huduma au bidhaa zako kila siku.
6. Tumia pesa vyema
Changamoto ya matumizi mabaya ya pesa inawakabili watu wengi kuanzia kwenye matumizi yao binafsi ya pesa. Watu wengi wanapata pesa lakini zinaisha bila ya kufahamu wamezitumiaje au wamefanya kipi chenye tija.
Soma pia: Njia 10 Zitakazokuwezesha Kutumia Pesa Vyema.
Ni wazi kuwa matumizi mazuri ya pesa ni kanuni muhimu sana kwa mjasiriamali, kwani kwa njia hii utaweza kukuza biashara yako kila siku. Jifunze kufahamu hii ni pesa kwa ajili ya nini, na uitumie kwa mambo ya msingi pekee. Epuka tabia za kibadhirifu na anasa. Ikiwa biashara au uwekezaji wako ni mkubwa, basi unaweza kumwajiri mtu aliye na taaluma ya utunzaji na usimamizi wa pesa.
Unaweza pia kujifunza wewe mwenyewe jinsi ya kutunza na kutumia pesa vyema; unaweza pia kutumia programu za bure za kompyuta kama vile Wave app kutunza mahesabu yako.
7. Jifunze kusema hapana
“Hapana” ni jibu dogo lakini lenye manufaa makubwa. Ikiwa wewe ni mjasiriamali ni muhimu kuzingatia kanuni hii ya kusema hapana kwani itakutenga na mambo au mipango isiyokuwa na ulazima.
Kuna watu, mipango, vitu au hata tabia ambazo zinaweza kukuathiri vibaya sana kwenye ujasiriamali wako. Hivyo kusema hapana kutakuepusha kwa kiasi kikubwa na mambo haya.
Soma pia: Tabia 10 zitakazobadili maisha yako.
8. Usipuuze nafasi ya teknolojia
Tunaishi kwenye ulimwengu wa sayansi na teknolojia, hivyo wewe kama mjasiriamali huwezi kujitenga nao. Kwa kupitia teknolojia kama vile simu na mtandao wa intaneti, unaweza kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza mauzo ya huduma au bidhaa zako.
Hakikisha wewe kama mjasiriamali unakuwa karibu na wateja wako ili kutatua shida na mahitaji yao; pia hakikisha unajifunza mbinu bora za kufanya biashara kupitia mtandao.
Soma pia: Makosa 8 ya Kuepuka Unapofanya Biashara Kwenye Mtandao.
9. Fahamu soko
Kanuni mojawapo ya kuongeza mauzo yako kama mjasiriamali ni kulifahamu soko vyema. Hakikisha huduma au bidhaa unayoitoa inakidhi mahitaji na inafika kwenye soko stahiki.
Kwa mfano ikiwa wewe ni mzalishaji wa mayai, lakini eneo ulilopo soko ni duni, basi tafuta eneo jingine ambalo soko la bidhaa hii ni nzuri. Ikiwa wewe huwezi kwenda, unaweza kutafuta mtu kwenye eneo lenye soko zuri akakuuzia bidhaa yako na ukampa gawio fulani.
Kwa kufanya hivi utaweza kulenga soko na kujiongezea faida zaidi wewe kama mjasiriamali.
10. Ongeza maarifa
Kwanza nikupongeze kwa kusoma makala hii, ni wajasiriamali wachache sana ndiyo hupenda kusoma makala na vitabu mbalimbali ili kuongeza maarifa. Ni muhimu sana kila mara ukajizoesha kujiongezea maarifa, hasa ya ujasiriamali pamoja na kile unachokifanya; hili liitakuwezesha kuwa na tija na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Unaweza kusoma vitabu, majarida na tovuti mbalimbali (kama fahamuhili.com) ili kuongeza maarifa yako.
11. Jifunze kutokana na makosa
Moja ya kanuni inayozingatiwa na wajasiriamali waliofanikiwa ni kujifunza kutokana na makosa. Makosa ni shule nzuri sana kwa kila mtu hasa wajasiriamali. Ikiwa uliwekeza ukapata hasara, basi jifunze nini hasa kilikuwa chanzo cha hasara ili mbeleni uweze kukiepuka. Usikubali kukwamishwa na makosa, bali yawe ni hamasa kwako ya kuendelea mbele zaidi.
“Uzoefu ni kufanya makosa na kujifunza kutokana na makosa hayo”
12. Jifunze kwa waliofanikiwa
Watu wengi wameshindwa kufanikiwa kwenye maisha yao kwa sababu wanajifunza kwa walioshindwa. Walioshindwa wana maneno mengi, hasa ya kukatisha tamaa kama vile hili haliwezekani, hili linahitaji pesa nyingi sana, mimi lilinishinda, linachosha, lina faida ndogo, kuna wengi wanaolifanya, fulani alishindwa n.k.
Wewe kama mjasiriamali, epuka watu hawa na ujifunze kwa waliofanikiwa, fahamu walitatua vipi changamoto walizokabiliana nazo pamoja na mipango waliyoitumia hadi wakafika hapo walipo.
13. Tumia muda vizuri
Hakuna mtu mwenye zaidi ya saa 24 duniani; lakini mwingine muda unamtosha wakati mwingine analalamika muda haumtoshi. Ni wazi kuwa mpangilio au matumizi mabaya ya muda ndiyo husababisha changamoto hii. Wewe kama mjasiriamali ni muhimu ukaondoa mambo yasiyokuwa na ulazima kwenye ratiba yako. Tambua ni kitu gani ni cha muhimu zaidi na ukifanye kwa wakati.
Soma: Kanuni 9 za Kufanikiwa katika Matumizi ya Muda.
14. Weka vipaumbele
Wewe kama mjasiriamali, ni muhimu kuzingatia kanuni hii ya kujiwekea vipaumbele; vipaumbele vitakuwezesha kubaini ni kipi kianze na ni kipi kifuate kutokana na umuhimu wake.
Kwa mfano ikiwa kuna wateja walipata shida kupata huduma au bidhaa yako, maliza kwanza swala hili kabla ya kuendelea kuweka jitihada za kuuza bidhaa mpya. Kwa kufanya hivi utaweza kufanya mambo kutokana na umuhimu wake, jambo ambalo litakuwezesha kukua.
15. Usikate tamaa
Ni wazi kuwa katika safari ya ujasiriamali utakutana na changamoto mbalimbali. Jambo la msingi ni kukumbuka kanuni hii kuwa usikate tamaa. Tumia changamoto kama chachu ya kukuhamasisha kufanya bidii zaidi na usirudi nyuma.
Changamoto zipo leo na kesho lakini keshokutwa hazitakuwepo tena; jambo unalotakiwa kufanya ni kutazama lengo lako na kufanya bidii kila kukikucha kuzikabili changamoto husika ili ufikie lengo lako.
“Siri ya mafanikio yetu ni kutokukata tamaa”
Soma pia: Hatua 7 za Maumivu Zisizoepukika Kabla ya Kufanikiwa.
Hitimisho
Naamini umefahamu kuwa kuna kanuni muhimu ambazo wewe kama mjasiriamali unatakiwa kuzizingatia ili uweze kufanikiwa. Ni wazi kuwa bidii, mipango mizuri na kutokukata tamaa kutakuwezesha kufikia lengo lako la kufanikiwa kama mjasiriamali.
Je una swali, maoni au changamoto ambayo ungependa kutushirikisha? Tafadhali tuandikie maoni yako hapo chini nasi tutafurahi kukuhudumia. Pia unaweza kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook pamoja na kuwashirikisha wengine makala hii.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Ni vitu gan vya kuzingatia kabla hujaanza ujasiriamali
Asante kwa swali lako; kabla hujawa mjasiriamali kuna mambo mengi ya kuzingatia; tafadhali fahamu haya machache wakati nikiandaa makala kuhisiana na swala hili.
1. Lengo lako ni nini?
2. Mahitaji ya mtaji na upatikanaji wake
3. Una nini cha tofauti na kile kilichoko sokoni?
4. Utashirikiana na nani au utafanya kazi na nani?
5. Je una maarifa satahiki yanayohitajika?
Asante.
samahani naitwa ima naomba mnijuze kuhusu ujasiriamali
Karibu usome makala za ujasiriamali hapa: https://www.fahamuhili.com/category/ujasiriamali/
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
ahsante sana kwa mafunzo haya ni dalasa tosha, mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha TUMAINI MAKUMIRA ARUSHA. ninalenga kuanzisha kituo cha kufundisha kuanzia ngazi ya sekondari hadi advance..naomba ushauri nifanye nn kufanikisha lengo langu
Nashukuru sana kwa kutembelea blog yetu ya Fahamuhili; tunashukuru pia kwa maoni yako mazuri.
Kwanza hongera kwa wazo zuri la kuanzisha kituo cha kufundisha wanafunzi.Nakushauri uanze kidogo kadri uwezavyo; anza na wanafunzi wachache walioko jirani na wewe; unaweza kuanza kuwafundishia hata nyumbani au mahali pengine karibu na unapoishi ili kuokoa gharama. Zighatia ubora ili ujenge jina na soko likutambue kwa haraka ili uweze kukuza mradi wako huo. Nakutakia kila la heri katika hilo. Karibu.
je ujasiliamali unahitaji kuwa na elimu stage gani?
Maarifa sahihi tu ya ujasiriamali ndugu na si kiwango cha elimu; hata hivyo, ukiwa na kiwango fulani cha elimu ukiweza kukibadili kuwa maarifa na ukakitumia kwenye ujasiriamali kitakusaidia sana. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Elimu nzur sana
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
KAMA KAWA
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nafurah Sana kusoma nakala hii pia imenifunza
Ila mimi ninatatizo la kutokujua lipu nkfanye na kwawakati gani naomba msaada
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; tafadhali soma makala yetu ya kanuni za matumizi ya muda; karibu sana Fahamuhili.com
Jinsi gan nawez kupata mtaji
Hongera kwa kusoma makala zetu pia ninashukuru kwa swali lako la thamani; tafadhali nimejibu swali lako katika makala inayopatikana hapa: (https://www.fahamuhili.com/njia-unazoweza-kuzitumia-ili-kupata-mtaji/) asante na karibu sana Fahamuhili.com
Nawezaje kupata mtaji
Hongera kwa kusoma makala zetu pia ninashukuru kwa swali lako la thamani; tafadhali nimejibu swali lako katika makala inayopatikana hapa: (https://www.fahamuhili.com/njia-unazoweza-kuzitumia-ili-kupata-mtaji/) asante na karibu sana Fahamuhili.com
Nimefurahi Sana na nimejifunza vitu vikubwa viwili, MUDA, KUJIFUNZA KWA ALIYE FANIKIWA
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Kwanza nakushukru sana Bwn K. Maanga kwa kuchukua mda wako tuwapa watanzania elimu ya ujasiliamali.
Sasa ndg yangu kuna changamoto ya mtaji. Mtu unaweza kuwa nawazo la kuwekeza mradi flani lkn changamoto ikawa mtaji.
Sasa kwa mtu mwenye upungufu wa mtaji anaweza kutumia njia zipi kufikia malengo yake.
Hongera kwa kusoma makala zetu pia ninashukuru kwa swali lako la thamani; tafadhali nimejibu swali lako katika makala inayopatikana hapa: (https://www.fahamuhili.com/njia-unazoweza-kuzitumia-ili-kupata-mtaji/) asante na karibu sana Fahamuhili.com
Aya asante ssns
Asante Karibu sana.
Nmemalza kdato cha nne mwak jan nmefaul kwango cha div.3 bht mby au nzur xjachaguliw kuendlea na masom unanixhaur nfanyaje
Habari ndugu Joseph; usikate tamaa wala usipoteze muda wako kwa kushindwa kuendelea mbele kimasomo; jifunze fani mpya hasa inayohusu ujasiriamali na uiweke kwenye matendo. Jitahidi kufanya kile unachokipenda. Asante.
Yes
Asante sana kwa maoni yako; karibu sana Fahamuhili.com
Habari ya leo nashukuru kwa elimu nzuri sana kwa wanajamii nzima kwa kupoteza muda wako kutuelimisha tunashkuru kwa hilo…..
Jambo langu ni dogo lakini kubwa sana kwa upande wangu nimeanzisha biashara dogo ya ubunifu na kiasi chake nimejitahidi kuweka bidhaa yangu kwenye ubora mzuri kiasi chake na baadhi ya watumishi nilio washirikisha kunishauri wamenishauri vzr pia….Ila swali nalo liomba kushauri ni namna ya kupata masoko soko la bidhaa yangu bado ni duni sasa nashindwa kuelewa ni mkoa niliopo ndo tatizo la kuto kukua kwa biashara yangu au la naomba ushauri wako nifanye nini kufanya bz yangu iwe kubwa
Habari ndugu Isihaka; ingependeza kama ungenifahamisha ni biashara gani na uko mkoa gani ili nione jambo la kukushauri. Asante.
Weka mpangilio mzuri wa muda na uendeshaji ndugu; unaweza pia kupima ni wapi kuna manufaa zaidi ili utoe muda huko zaidi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
About self development
Tutazidi kuandika kuhusu maendeleo binafsi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Naitwa AJUAZY PHENSON
Nifate njia zipi I’ll kuzikabili changamoto zinazotokana na mabadiliko ya hewa na ulimwengu kwa ujumla .
Mfano nilikuwa mkulima wa mazao ya chakula 🌽 🌽 ila kutokana na janga la CORONA kilimo hiki kimekufa kutokana na kwamba niliwekeza mtaji mkubwa kwenye kilimo lakini mwisho masoko yalikosekana..
He nifanye nin kujikinga na athari kama hizi??# @ajuzy@
Tafadhali soma (https://www.fahamuhili.com/mbinu-za-kulinda-biashara-yako-dhidi-ya-athari-za-corona-covid-19/) utapata mwanga. Asante na karibu sana Fahamuhili.com
Nakubali kujiunga
Karibu sana ujiunge nasi: Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Kwanza nikupongeze kwa makala Yako,Naitwa Godfrey Niko mwanza naitaji kuanzisha Biashara ya viungo karibu
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; nakutakia kila la heri katika mpango wako. Karibu sana Fahamuhili.com
Samahan ingawa nimechelewa kuisoma , Napenda sana ujasiriamali lakin tatizo lang ni nakuwa na malengo mengi kichwani ndan ya mwaka mmoja,alafu nakuja kujikuta mwaka umeisha kila lengo nimeairisha
Pole kwa changamoto hiyo; jitahidi ubainishe lengo moja na ulifanyie kazi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Nataka kujua kanuni za biashara ndogondogo
Karibu usome: https://www.fahamuhili.com/kanuni-za-ujasiriamali/ Asante na karibu Fahamuhili.com