Uwekezaji Archives - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Uwekezaji

Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Biashara na Uchumi
Hakuna mtu anayeanzisha biashara akitegemea ife, lakini wakati mwingine hili hutokea. Utafiti umebaini kuwa biashara na kampuni nyingi hufa ndani ya kipindi cha miaka miwili hadi mitano tangu kuanzishwa kwake. Kufa kwa biashara siyo jambo zuri, ni wazi kuwa kila mtu nayefanya biashara atatamani kufanya juu chini ili ainusuru biashara yake isife. Zipo sababu mbalimbali zinazosababisha biashara mbalimbali kufa. Fahamu sababu 13 zinazosababisha biashara nyingi kufa pamoja na jinsi ya kuziepuka. 1. Mipango duni Ili ufanikiwe katika biashara unahitaji mpango mzuri wa biashara. Biashara nyingi zinazoanzishwa Afrika hazina mipango madhubuti ya kibiashara inayoonyesha maswala kama vile muundo wa utawala, mtaji, mikakati au mipango ya mauzo, n.k Biashara nyingi pia hukosa lengo; jambo a...
Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka

Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka

Ujasiriamali
Kuanza biashara kutoka kiwango cha sifuri siyo kazi rahisi. Kama mjasiriamali utakutana na changamoto nyingi. Hili haliwezi kuwa tatizo ikiwa uko tayari kujifunza kutokana na makosa na kufahamu njia za kuyaepuka huko mbeleni. Hivi ndivyo wajasiriamali wengi wanavyojifunza na kukua. Unapokuwa kwenye biashara ni lazima ufahamu makosa ambayo yanaweza kuathiri biashara au uwekezaji wako; ili ujitahidi kuyaepuka ama kuyapunguza kadri iwezekanavyo. Ni dhahiri kuwa wajasiriamali wengi wamekwama kutokana na kupuuzia au kutofahamu makosa haya 15 ambayo hata wewe unatakiwa kuyafahamu na kuyaepuka. 1.Kujifanya unafahamu kila kitu Usijifanye unajua kila kitu, hasa kama ndiyo umeingia kwenye ulimwengu wa kibiashara. Kwanini? Kwa sababu kuendesha biashara ni kujifunza na kupata uzoefu. Jitahidi ku...
Nembo/Logo za Kibiashara Zilizobeba Maana Usizozijua

Nembo/Logo za Kibiashara Zilizobeba Maana Usizozijua

Biashara na Uchumi
Kama unavyojua nembo au logo ya kibiashara ina nafasi kubwa katika utambulisho wa kampuni. Nembo iliyobuniwa vizuri inaweza kuwafanya watu wengi kutambua huduma au bidhaa unayotoa. Hii ndiyo sababu logo nyingi hupitia usanifu na maboresho mbalimbali ili kuhakikisha zinawakilisha kampuni au biashara vyema. Hata hivyo, zipo logo zilizofanikiwa kufanya vizuri  wakati nyingine hazijafanikiwa. Kwa zile zilizofanikiwa unaweza kushangaa ni kwa namna gani wabunifu wake wameweza kuficha maana fulani muhimu kuhusu kampuni husika. Fahamuhili kwa kutambua umuhimu wa utambulisho katika biashara au kampuni, tumekuletea orodha hii ya nembo zaidi ya 10 pamoja na maana zilizojificha ndani yake. Tunaamini makala hii itakupa mwangaza muhimu pale utakapokuwa unatengeneza logo yako. Soma pia: Mamb...
Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Watu wengi wamekuwa wakitamani kuanza biashara lakini wanafikiri namna ya kuanza kwani mtaji wao ni mdogo sana. Ni ukweli usiopingika kuwa idadi kubwa ya watu walioshindwa kuanzisha biashara wakishindwa katika eno hili la kuanza biashara na mtaji mdogo. Usiogope; kuwa na mtaji mdogo au kutokuwa nao kabisa sio mwisho wako wa kutimiza malengo yako. Zipo mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukuwezesha kufanya biashara hata kama utakuwa na mtaji mdogo. Tafadhali fuatilia hoja jadiliwa hapo chini kwa ufafanuzi zaidi. 1. Kuwa mbunifu Moja kati ya mambo ambayo yatakusaidia sana kwenye kuanza biashara kwa mtaji mdogo ni ubunifu. Kwa njia ya ubunifu utaweza kushinda biashara na bidhaa zilizoko sokoni kwa urahisi zaidi. Unaweza kufanya haya yafuatayo: Chagua wazo la biashara unalolipenda na ku...