Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu.
Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu.
Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu 7 zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu.
1. Chagua wazo bora
Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya:
- Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema.
- Chagua mada ambayo inahitajiwa na wasomaji.
- Chagua mada ambayo haikiuki sheria au maadili ya eneo unalolenga.
- Chagua mada ambayo inaziba pengo lililoachwa na vitabu vingine.
2. Pangilia kabla ya kuandika
Mpangilio ni jambo muhimu sana katika uandishi wa vitabu. Hakikisha unapangilia mtiririko wa mawazo pamoja na muundo mzima wa kitabu chako kabla ya kuanza kuandika. Hakikisha unabainisha sura zitakazokuwepo kwenye kitabu chako pamoja na kitakachozungumziwa katika sura hizo.
Ikiwa unashindwa kupanga mawazo pamoja na kubainisha sehemu kuu za kitabu chako, basi kuna haja ya kutafakari upya wazo ulilolichagua.
3. Zingatia kanuni za uandishi
Uandishi ni taaluma kamili; hivyo ni muhimu kuzingatia kanuni bora za uandishi kama vile matumizi bora ya lugha, mpangilio wa hoja au mawazo pamoja na matumizi ya alama za uandishi. Ikiwa wewe siyo mtaalamu mzuri wa lugha; unaweza kutafuta mtaalamu wa lugha anayeweza kukusaidia kuboresha kazi yako.
Soma pia: Mbinu 7 za Kuwa Mwandishi Bora.
4. Zingatia mazingira bora ya uandishi
Siyo kila mazingira yanafaa kwa ajili ya kufanya kazi ya uandishi; ni lazima uhakikishe unatafuta mazingira ambayo ni tulivu na yasiyokuwa na muingiliano. Katika swala la kuandaa mazingira unaweza kufanya haya yafuatayo:
- Tafuta eneo lililotulia lisilo na usumbufu wowote.
- Tenga muda ambao uko vizuri kiafya na kiakili. Mara nyingi muda wa asubuhi ni bora zaidi kufanya kazi hii kwani mwili na akili vinakuwa viko vizuri.
- Ondoa vitu vinavyoweza kukuvuruga kama vile mitandao ya kijamiii, televisheni, simu, watu wasiohusika, n.k.
Kwa kufanya hivi utaweza kupata utulivu wa kutosha na kuweza kuondoa vitu ambavyo vinaweza kuingilia shughuli yako ya uandishi.
5. Tafuta kazi inayoshabihiana
Mara nyingi kila kitu duniani kina kitu kingine kinachoshabihiana nacho. Tafuta kitabu ambacho kinakaribiana na kile unachotaka kuandika; kwa kufanya hivi utaweza kukitumia kama mwongozo wako.
Tazama jinsi ambavyo mwandishi wa kitabu husika amepanga mawazo au hoja katika kitabu chake; tazama pia lugha na mbinu nyingine za kiuandishi alizozitumia kukamilisha kazi yake.
6. Tambua hadhira
Aina za uandishi hutofautiana baina ya aina moja ya hadhira na nyingine. Uandishi wa vitabu vya watoto ni tofauti na uandishi wa vitabu vya vijana au wazee. Hivyo ni muhimu ukabaini ni kundi gani na lenye sifa gani unalolilenga katika kitabu chako. Ifahamu vyema hadhira yako, fahamu inapendelea nini ili uweze kuilenga vyema.
7. Zingatia uhariri
Hakuna uandishi bora pasipo uhariri bora. Ni muhimu sana ukazingatia uhariri kwani utakuwezesha kufanya kazi bora ambayo itaonekana imefanywa kitaalamu. Hakikisha unapata muda wa kutosha wa kuhariri hoja, mawazo, mpangilio pamoja na lugha katika kitabu chako.
Ikiwa huna uwezo au muda wa kuhariri kitabu chako basi unaweza kutafuta mhariri akakusaidia kuhariri kitabu chako.
Soma pia: Njia 10 za Kuwa Mhariri Bora.
Hitimisho
Uandishi wa vitabu ni taaluma pana ambayo inahitaji uzoefu wa muda mrefu ili kuimudu vyema. Lakini kama utafanya maamuzi ya dhati ya kuzingatia mbinu hizi za uandishi wa vitabu, ni wazi kuwa utaweza kumudu swala la uandishi wa vitabu ndani ya muda mfupi. Usisubiri, anza kuandika leo, ndipo utakapozidi kukomaa kadri siku zinavyosogea.
“Safari ya maelfu ya maili huanza na hatua moja.”
Je bado una shida kwenye swala la uandishi wa vitabu? Tafadhali tuandikie maoni na maswali yako hapo chini. Usisahau kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook pamoja na kuwashirikisha wengine makala hii.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Habari,Mimi nimefiwa na mama angu lakini mama angu amefanya vitu vizuri vingi lakini ninataka niandike kitabu kinachomhusu mama angu hivyo basi naombeni ushauri kwenu
Habari Ndugu Marco;
Kwanza pole kwa kufiwa na mama yako mpendwa; pili hongera kwa kuamua kumuenzi mama kwa njia ya kumwandikia kitabu. Unaweza kuandika kitabu chenye kumwelezea moja kwa moja au kinachohusisha mbinu za kifasihi kwa kiasi fulani lakini kikimwelezea. Nitajitahidi kuandaa maelezo zaidi kisha nitakujulisha. Asante.
habari, mimi nimepitia misukosuko mingi sana katika maisha yangu sasa nimeamua kuandika kitabu chenye kueleza maisha yangu. ningependa unisaidie au unishauri chochote kuhusu uandishi wa vitabu. ahsante
Nashukuru sana kwa kutembelea blog yetu ya Fahamuhili; tunashukuru pia kwa maoni yako mazuri. Pole kwa uliyopitia; pili hongera kwa kuandika kitabu; Unaweza kunitumia nakala pepe ya kitabu chako nione jambo la kukushauri; asante.
Habari mimi naomba namba zako unisaindie kuandika kitabu namba zangu 0656633474
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mawasiliano:
Email: fahamuhili[at]gmail.com
Simu: 0758 444 771
Asante kwa kanunu hizi, Mimi Naitwa David sijawahi andika kitabu lakini natamani kuanza kuandika tatizo langu mawazo yanakuja na kupotea.
Habari David; Jifunze kuandika kila wazo linalokuja akilini mwako ili lisipotee; mawazo ni sawa na mali yasipotunzwa yanapotea. Jizoeze kutembea na daftari dogo au shajara (Diary) ili upatapo wazo ulitunze; unaweza pia kuandika kwenye notebook ya simu janja. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Naomba kuuliza umuhimu wa CV katika uandishi wa vitabu, Mana mara nyingi ukiangalia vitabu vingi nyuma yake utaona picha na wasifu wa mwandishi, je hiyo Ina umuhimu gani? Je watu wa elimu ya kawaida tuu waweza kuwa waandishi?
Wasifu binafsi unamsaidia msomaji kumfahamu mwandishi; mtu yoyote anaweza kuwa mwandishi ilimradi tu amezingatia kanuni za uandishi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mr.Kornel naomba msaada juu ya Hilo, pia nashukuru kea makala hii
Karibu nikusaidie ndugu; umekwama wapi?
Uandishi ni stadi maalum inayohitaji maandalizi ya kutosha na umakini.jadili
naishi zanzibar upande wa unguja nimefurah juu ya kupata muongozo ama mbinu zakuwa muandishi bora niko na ndoto zakuwa mtunzi bora sikumoja asanteni sitasita kuwatafuta mpaka pale nitakapo fanikiwa
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; usiache kupigania ndoto yako hiyo; karibu sana Fahamuhili.com
Mungu akubariki sana, na akuinue!!
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Kwa jina naitwa mariam kalinga , ninamengi ya kuelezea ila nataman unitafute kwenye watssup namba 0762695852, nataman kuandika maisha ya MTU fulan ninayemfaha.. Sasa kunavtu ambavyo vinanishinda..
Karibu tuwasiliane kwa fahamuhili@gmail.com
Natamani sana kutunga kitabu juu ya maisha yangu tangu kuzaliwa kwangu maisha yangu yana funzo kubwa sana kwa watu kidunia na kiroho lkn nashindwa nianzeje sina huo utaalamu
Tutaandaa makala yenye muongozo wa kuandika kitabu hivi karibuni. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nimependa makala yako ya mbinu 7 za uandishi wa vitabu, imeniongezea kitu mana nami nataka kuwa mwandishi wa vitabu, asante sana.Ila nimeona kwenye wasifu wako kuwa unajishughulisha na TEHAMA. Je, nikihitaji kujifunza kutengeneza APP za simu janja naweza pata msaada?.
Tunashukuru sana kwa kuwa msomaji wetu; pia tunashukuru kwa maoni yako ya thamani; tunakutakia kila la heri katika kutimiza malengo yako…kwa sasa hatutoi mafunzo ya utengenezaji wa App lakini tukianza kufanya hivyo tutakujulisha…karibu sana Fahamuhili.
Napenda kuandika kitabu ambacho kinausu MAISHA YA MWANADAMU ndo wazo langu ila napenda unishauri kuwa wazo langu lipo vizuri au niweke jina lengine la kitabu ila ndani maudhui yake yawe ya kuusu maisha ya mwanadamu. Naomba ushauri wako na mbinu zote saba nimezielewa vizuri kabisa. Ahsante.
Tunashukuru sana kwa kuwa msomaji wetu; pia tunashukuru kwa maoni yako ya thamani; tunakutakia kila la heri katika kutimiza malengo yako…karibu sana Fahamuhili.
Habari
Nimeandika hadith mbalimbal katka madaftari yangu, je nifanyeje ili kuchapisha kitoke kitabu.
Tutajitahidi kuandaa mwongozo wa jinsi ya kuanza kuandika kitabu. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Je katka taluma hii ya uhariri nahitajika kusoma sana lugha ya kiswahili?
Ikiwa unataka kuhariri matini za lugha ya Kiswahili, huna budi kujifunza lugha hiyo. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mtu anaeingia katika taluma hii ya uhariri ndio kwanza ajifunza atachukuwa mda gani kuhari vitabu?
Kadri unavyofanya mazoezi ya kutosha pamoja na kujiuongezea maarifa stahiki ya uhariri ndivyo utakavyoimarika kwa muda mfupi. Asante sana; karibu sana Fahamuhili.com
Hello nina story na ninataka kuandika inahusu maisha tu yaani nataka niandike kuhusu mamaangu alivyotelekezwa na babaangu na alivyoteseka kunilea akiwa mwenyewe
Tutajitahidi kuandaa mwongozo wa jinsi ya kuanza kuandika kitabu. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Ila sijui namna ya kuanza na kuipanga
Tutajitahidi kuandaa mwongozo wa jinsi ya kuanza kuandika kitabu. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
nina kitabu ninacho andika japo kws sasa nimesimama kidogo ila nikimaliza itabidi nikuone
ahsante kwa mbinu hizo
Hongera sana kwa uandishi huo; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mawasiliano:
Email: fahamuhili[at]gmail.com
Simu: 0758 444 771
Mimi ni kijana wa miaka kumi na saba na napenda kuandika vitabu lakini mpaka sasa nimeandika vitabu viwili ambavyo havijaisha na hilo ni kutokana na mawazo mapya yanayokuja kila siku na pia sina wa kuniongoza vizuri…. je naweza kusaidika
Tafadhali tumia mbinu tajwa hapo juu; usisubiri pia muongozo anza kuandika ukikwama ndiyo utafute msaada. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Habari mimi ni mwanachuo nahitaji kuandika kitabu kinacho weza kutoa muongozo katika maisha ya wanachuo hivyo naomba ushauri.
Tafadhali tumia mbinu tajwa hapo juu ukikwama tueleze ulipokwama tukushauri. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Asante kwa maelezo,nimetambuwa ni mini haswa kinahitajika na mini nitabadilisha
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Namshkuru Kwa kazi nzuri ya kutuelimisha juu ya uandishi
Binafsi sijapata taaluma yoyote juu ya uandishi lakini ni Suala ambalo nalipenda na kuna maandalizi nayafanya Kwa ajili ya uandishi Wa kitabu.
Hivyo Niko karibu ili kupata msaada wenu Kwa kuyasoma Makala yenu.
Asante sana kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Nimependa maelekezo mazuri uliyoyatoa. mm ni mwandishi ambaye nipo naandika kitabu hata muda huu. Nimefurahi kuona kwamba Kuna watu wengi wanapenda uandishi
Tupo wengi sana; endelea kuandika tunahitaji kusoma zaidi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Safi sana
Nataka kuandika kitabu kinacho nihusu mimi kwenye mahusiano naona kupitia kitabu vhangu kuna kitu watu wengine watajifunza
Kila la kheri katika hilo; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Habari ndugu
Naitwa joseph elias nina tamani kuandika kitabu changu cha riwaya ambayo nimeshaikianza kuliandika lkn najaribu kujitahidi ila na shindwa kutokana na kutokujua vizr mbn za uandishi naombeni msaada namba zangu za watspp ni 0626738025