Njia 10 za Kuwa Mhariri Bora - Fahamu Hili
Friday, September 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Njia 10 za Kuwa Mhariri Bora

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Uhariri

Hakuna uandishi bora au andiko bora pasipo uhariri bora. Hivyo uandishi mzuri hauwezi kutengwa na uhariri bora. Ni dhahiri kuwa makala au andiko lililohaririwa vyema na kwa ustadi wa hali ya juu litakubalika na kupendwa na wasomaji wengi zaidi. Watu wengi wamekuwa wakitamani kuandika matini zilizohaririwa vyema lakini wamekuwa wakikwama juu ya ni njia gani wanaweza kuwa wahariri bora. Pengine umekuwa ukitamani kunufaika kupitia kazi ya uhariri lakini hujui ufanyeje ili uweze kuwa mhariri bora. Fuatana nami katika makala hii nikueleze njia 10 zitakazokufanya kuwa mhariri bora.

1. Jifunze sarufi ya lugha na kanuni za uandishi

Uhariri ni taaluma kama ilivyo kwa taaluma nyingine. Hivyo ili uwe mhariri bora basi huna budi kujifunza kanuni za sarufi ya lugha husika pamoja na kanuni za uandishi katika lugha. Hili litakuwezesha kufahamu mpangilio na matumizi ya maneno katika sentensi pamoja na utumizi wa alama mbalimbali za uandishi kama vile nukta, koma, kistari, mabano, nusu mkato n.k.

Mfano:

Kabla ya uhariri:

Juma na roza ni watoto wazuri wanapenda kusoma na kuchezaga pamoja

Baada ya uhariri:

Juma na Roza ni watoto wazuri, wanapenda kusoma na kuchezaga pamoja.

Katika mfano huu inaonyesha dhahiri nafasi ya sarufi ya lugha pamoja na alama za uandishi katika uhariri.

Soma pia: Mbinu 7 za Kuwa Mwandishi Bora.

2. Soma kwa sauti

Kuna tofauti kubwa kati ya kusoma kwa sauti na kusoma kimya. Unaposoma kwa sauti unaweza kubaini makosa ambayo macho yameshindwa kuyabaini. Jizoeze kusoma matini husika kwa sauti ili kuweza kubaini pia mtiririko wa mawazo na maneno usio sahihi. Unaweza kutumia mtu mwingine au programu za kopyuta kama vile Google Translate na Balabolka kufanya kazi hii. Utashangaa jinsi ambavyo utaweza kubaini makosa ambayo hukuweza kuyabaini kwa macho.

3. Acha andiko kwa muda

Unaposoma andiko au matini muda mrefu huifanya matini husika ikae kichwani; hivyo kukufanya kuwa vigumu kubaini dosari. Kadri unavyoacha matini au andiko kwa muda, ndivyo unavyotoa nafasi ya andiko kuwa jipya zaidi kwenye ubongo wako. Hivyo inashauriwa kuliacha andiko baada ya muda na kulihariri tena ili uweze kubaini makosa ambayo hukuyabaini awali.

4. Punguza zaidi kuliko kuongeza

Mara nyingi waandishi wana maneno mengi, lakini si yote yanafaa katika matini husika. Hivyo, mara uhariripo matini jizoeze kupunguza zaidi kuliko kuongeza ili kuhakikisha mawazo yanaeleweka kwa urahisi. Epuka maneno ya kuzunguka na kujaza nafasi.

Mfano.

Kabla ya uhariri:

Yule babu yangu mzee aliyekuja jana jioni ni babu yangu wa karibu sana kuliko babu zangu wengine wote.

Baada ya uhariri:

Babu aliyekuja jana jioni ni wa karibu kwangu kuliko wote.

Au

Babu aliyekuja jana jioni ni wa karibu kwangu kuliko babu zangu wote.

Ni dhahiri kuwa, mfano huu umekuonyesha maana halisi ya kuondoa zaidi kuliko kuongeza katika uhariri.

5. Jifunze kutoka kwa wahariri mashuhuri

Kama ilivyo kwa taaluma nyingine ambazo watu hujifunza kwa magwiji, basi ndivyo ilivyo pia katika uhariri. Tafuta wahariri mashuhuri unaowapenda kisha fuatilia mtindo na mbinu wanazozitumia katika kufanya kazi ya uhariri. Kwa kufanya hivi, utajifunza namna unavyoweza kukabili mazingira na changamoto mbalimbali za kiuhariri; hivyo kuwa mhariri bora zaidi.

6. Tambua matini(andiko) husika

Kila matini ina utofauti wake wa kimuundo na mtindo. Hivyo kuielewa matini ni hatua ya kwanza na muhimu ili kuweza kuihariri vyema. Kwa mfano mtindo na muundo wa matini za kidini ni tofauti kabisa na matini za burudani au za fasihi. Hivyo basi, kumbuka kutambua matini husika kutakuwezesha kuchagua njia na mtindo utakaotumika katika kuihariri.

7. Hariri matini mbalimbali

Uzoefu hutokana na mtu kukifanya kitu mara kwa mara ndani ya kipindi fulani cha muda. Hivyo kuhariri matini mbalimbali kutakupa uzoefu juu ya matini mbalimbali na kukufanya kuwa mhariri bora.

8. Kagua zaidi  ya mara moja

Binadamu hawezi kufanya kazi bila makosa. Hivyo ni muhimu ukajizoesha kurudia kukagua matini yako zaidi ya mara moja ili kuweza kubaini makosa uliyoyasahanu.

9. Mfahamu mwandishi

Ikiwa unahariri matini ya mtu mwingine, kumfahamu mwandishi ni hatua muhimu katika uhariri kwani kutakuwezesha kuhariri matini kwa urahisi zaidi. Usipomfahamu mwandishi ana msimamo na mtazamo gani pia anapendelea muundo upi unaweza ukafanya kazi ambayo haitakubaliwa na mwandishi. Ni vyema ukamuuliza mwandishi maswali pale ambapo umeona kuna jambo ambalo linakutatiza katika kazi yake.

10. Pokea maoni

Wahariri wengi wanapenda kusikilizwa zaidi kuliko kusikiliza. Ni vyema ukajifunza kupokea maoni kutoka kwa watu wengine kwani yatakuwezesha kuboresha zaidi shuguli yako ya uhariri. Kumbuka, wanaokupima pia ni watu wengine na siyo wewe mwenyewe. Hivyo kwa kusikiliza maoni ya watu wengine wakiwemo wasomaji na waandishi utaweza kuboresha utendaji kazi wako.

Hitimisho

Ni dhahiri kuwa uhariri ni taaluma rasimi na kamili. Hivyo inahitaji maarifa na maandalizi stahiki ili uweze kuimudu vyema. Hakikisha unajifunza mambo na kanuni mbalimbali zihusuzo uhariri, pia usisahau kufanya mazoezi ya kutosha ili uweze kujinoa zaidi.

Naamini sasa utaweza kuwa mhariri aliyebobea. Je una swali au maoni yoyote? Tafadhali tuandikie hapo chini kisha washirikishe wengine.

3 4 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

20 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
christopher siahi
christopher siahi
5 years ago

dhima ya uhariri ni ipi

Eston J.
Admin
Reply to  christopher siahi
5 years ago

Asante ndugu Christopher kwa swali lako; tafadhali tutajitahidi kukujilisha hivi karibuni; endelea kutufuatilia; asante.

Ayubu Mwahagamab
Ayubu Mwahagamab
4 years ago

Yes

Vincent Okwetso
Vincent Okwetso
4 years ago

Inapendeza sana

Augustino peter
Augustino peter
4 years ago

Katika taaluma ya uhariri ni mtu yeyote anaweza kuifanya au mbaka usomee? Nakama kusomea ni masomo yapi yanayokuongoza ili uweze kuhariri?

Majula
Majula
Reply to  Augustino peter
1 year ago

Uhariri ni taaluma inayosomewa darasani. Ili uimudu lazima uipende lugha ya Kiswahili na kuisoma katika viwango mbalimbali.

Jemimah Kemumah
Jemimah Kemumah
3 years ago

Kuna uhusiano upi kati ya mhariri na wafanyikazi wengine katika shirika la uchapishaji

Martha Kaingu
Martha Kaingu
2 years ago

Asante lakini sifa za mhariri n zipi na sheria kuhusu haki za kunakili ni gani?

ismailkorir
ismailkorir
Reply to  Martha Kaingu
7 months ago

sifa za mhariri bora/mzuri au mhariri duni rejelea swali lako n

kelvin
kelvin
1 year ago

tofauti kati ya uhariri na usarifu matini

swali la pili ni jadili madhara yanayoweza kutokana na uhariri mbaya katika vitabu vya shuleni na magazetini na katika habari za vyombo vya habari

Jumbe mohamedi
Jumbe mohamedi
8 months ago

Join

Jumbe mohamedi
Jumbe mohamedi
8 months ago

Sifa za mhariri bora

Nshoma shija
Nshoma shija
4 months ago

Kwa kutumia mifano eleza nafasi ya uhariri katika kuboresha usomekaji wa andiko

Martha abdul
Martha abdul
3 months ago

Zipi ni alama anazozitumia mhariri katika uhariri?

20
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x