Kila mtu ana maana yake ya mafanikio. Ni wazi kuwa mafanikio ni kuweza kukabiliana na changamoto au kushindwa bila kukata tamaa au kuacha.
Mara nyingi huwa napenda kusoma nukuu (Quotes) mbalimbali kwani huwa zinanipa hamasa kubwa ya kuzidi kufanyia kazi ndoto zangu.
Naamini hata wewe unaweza kuhamasika na kupata ari zaidi kwa kusoma nukuu hizi 30 za mafanikio.
“Ni bora kushindwa kwenye kitu halisi kuliko kufanikiwa kwenye kitu cha kuiga.”
“Njia ya kufanikiwa na barabara ya kushindwa ni sawa kabisa.”
“Mafanikio huja kwa wale ambao wanafanya bidii kubwa kuyatafuta.”
“Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio. Bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”
“Acha kukimbilia pesa bali anza kukimbilia shauku yako.”
“Mafanikio ni kupita kutoka aina moja ya kushindwa hadi nyingine bila kukata tamaa.”
“Fanya kitu kimoja kila siku kinachokutisha.”
“Ukitazama kwa karibu, mafanikio ya usiku mmoja huchukua muda mrefu.”
“Hakuna siri ya mafanikio, ni matokeo ya maandalizi, kufanya kazi kwa bidii, na kujifunza kutokana na kushindwa.”
“Inaonekana mafanikio yameungwa na matendo. Watu waliofanikiwa wanaendelea mbele. Wanafanya makosa lakini hawaachi.”
“Kama unataka kufanya kitu, utatafuta njia. Kama hutafanya hivyo, utatafuta kisingizio.”
“Siwezi kukupa kanuni ya mafanikio, lakini ninaweza kukupa kanuni ya kushindwa – nayo ni: Jaribu kumridhisha kila mtu.”
“Mafanikio siyo ufunguo wa furaha. Furaha ni ufunguo wa mafanikio. Kama unapenda unachokifanya, utafanikiwa.”
“Mafanikio siyo vitu ulivyokamilisha kwenye maisha yako, bali ni nini ulichowahamasisha wengine kufanya.”
“Baadhi ya watu wengine wanaota mafanikio wakati wengine wanaamka na kufanya kazi.”
“Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”
“Ili kufanikiwa ni lazima tuamini kuwa tunaweza.”
“Kushindwa kwingi kwenye maisha ni watu wanaoshindwa kufahamu jinsi walivyo karibu na mafanikio wanapokata tamaa.”
“Mafanikio ni kupata unachotaka, furaha ni kutaka unachopata.”
“Eneo baya la mafanikio ni kujaribu kutafuta mtu ambaye ana furaha kwa ajili yako.”
“Usipoteze muda kupiga ukuta, ukitumaini kuubadili kuwa mlango.”
“Nimefanikiwa leo kwa sababu nilikuwa na rafiki aliyeniamini na sina moyo wa kumwangusha.”
“Yote unayohitaji kwenye maisha yako ni ujinga na ujasiri; kisha mafanikio ni hakika.”
“Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”
“Changamoto kubwa baada ya kufanikiwa ni kunyamaza kuhusu mafanikio hayo.”
“Mafanikio hayahusishi kutokufanya kosa bali kutokurudia kosa hilo mara ya pili.”
“Mafanikio ni pale ambapo maandalizi na fikra vinakutana.”
“Kila mara kujiamini na bidii kutakupa mafanikio.”
“Mafanikio siyo mwalimu mzuri, kushindwa hukufanya kuwa mnyenyekevu.”
“Kabla ya kitu kingine chochote, maandalizi ni ufunguo wa kufanikiwa.”
Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazo Kuhamasisha Maishani Mwako.
Naamini umehamasika na kupata shauku zaidi ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako ili ufanikiwe. Kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu.
Naamini umebaini wazi kuwa maana ya mafanikio ni pana; pia mafanikio siyo kutokukabiliana na changamoto bali ni kuzikabili.
Je una maoni au maswali? Je umehamasika au kujifunza kitu? Tafadhali tuandikie maoni yako hapo chini. Usisahau kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi. Karibu pia uwashirikishe wengine makala ya nukuu hizi.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.