Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Nukuu za mafanikio

Kila mtu ana maana yake ya mafanikio. Ni wazi kuwa mafanikio ni kuweza kukabiliana na changamoto au kushindwa bila kukata tamaa au kuacha.

Mara nyingi huwa napenda kusoma nukuu (Quotes) mbalimbali kwani huwa zinanipa hamasa kubwa ya kuzidi kufanyia kazi ndoto zangu.

Naamini hata wewe unaweza kuhamasika na kupata ari zaidi kwa kusoma nukuu hizi 30 za mafanikio.

  1. “Ni bora kushindwa kwenye kitu halisi kuliko kufanikiwa kwenye kitu cha kuiga.”

    Herman Melville
  2. “Njia ya kufanikiwa na barabara ya kushindwa ni sawa kabisa.”

    Colin R. Davis
  3. “Mafanikio huja kwa wale ambao wanafanya bidii kubwa kuyatafuta.”

    Henry David Thoreau
  4. “Usijaribu kuwa mtu wa mafanikio. Bali jaribu kuwa mtu wa thamani.”

    Albert Einstein
  5. “Acha kukimbilia pesa bali anza kukimbilia shauku yako.”

    Tony Hsieh
  6. “Mafanikio ni kupita kutoka aina moja ya kushindwa hadi nyingine bila kukata tamaa.”

    Winston Churchill
  7. “Fanya kitu kimoja kila siku kinachokutisha.”

    Hajulikani
  8. “Ukitazama kwa karibu, mafanikio ya usiku mmoja huchukua muda mrefu.”

    Steve Jobs
  9. “Hakuna siri ya mafanikio, ni matokeo ya maandalizi, kufanya kazi kwa bidii, na kujifunza kutokana na kushindwa.”

    Colin Powell
  10. “Inaonekana mafanikio yameungwa na matendo. Watu waliofanikiwa wanaendelea mbele. Wanafanya makosa lakini hawaachi.”

    Conrad Hilton
  11. “Kama unataka kufanya kitu, utatafuta njia. Kama hutafanya hivyo, utatafuta kisingizio.”

    Jim Rohn
  12. “Siwezi kukupa kanuni ya mafanikio, lakini ninaweza kukupa kanuni ya kushindwa – nayo ni: Jaribu kumridhisha kila mtu.”

    Herbert Bayard Swope
  13. “Mafanikio siyo ufunguo wa furaha. Furaha ni ufunguo wa mafanikio. Kama unapenda unachokifanya, utafanikiwa.”

    Albert Schweitzer
  14. “Mafanikio siyo vitu ulivyokamilisha kwenye maisha yako, bali ni nini ulichowahamasisha wengine kufanya.”

    Hajulikani
  15. “Baadhi ya watu wengine wanaota mafanikio wakati wengine wanaamka na kufanya kazi.”

    Hajulikani
  16. “Mtu mwenye mafanikio ni yule anayeweza kujenga msingi imara kwa kutumia matofali yaliyotupwa na wengine.”

    David Brinkley
  17. “Ili kufanikiwa ni lazima tuamini kuwa tunaweza.”

    Nikos Kazantzakis
  18. “Kushindwa kwingi kwenye maisha ni watu wanaoshindwa kufahamu jinsi walivyo karibu na mafanikio wanapokata tamaa.”

    Thomas Edison
  19. “Mafanikio ni kupata unachotaka, furaha ni kutaka unachopata.”

    Dale Carnegie
  20. “Eneo baya la mafanikio ni kujaribu kutafuta mtu ambaye ana furaha kwa ajili yako.”

    Bette Midler
  21. “Usipoteze muda kupiga ukuta, ukitumaini kuubadili kuwa mlango.”

    Coco Chanel
  22. “Nimefanikiwa leo kwa sababu nilikuwa na rafiki aliyeniamini na sina moyo wa kumwangusha.”

    Abraham Lincoln
  23. “Yote unayohitaji kwenye maisha yako ni ujinga na ujasiri; kisha mafanikio ni hakika.”

    Mark Twain
  24. “Ili kufanikiwa, shauku yako ya mafanikio ni lazima iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.”

    Bill Cosby
  25. “Changamoto kubwa baada ya kufanikiwa ni kunyamaza kuhusu mafanikio hayo.”

    Criss Jami
  26. “Mafanikio hayahusishi kutokufanya kosa bali kutokurudia kosa hilo mara ya pili.”

    George Bernard Shaw
  27. “Mafanikio ni pale ambapo maandalizi na fikra vinakutana.”

    Bobby Unser
  28. “Kila mara kujiamini na bidii kutakupa mafanikio.”

    Virat Kohli
  29. “Mafanikio siyo mwalimu mzuri, kushindwa hukufanya kuwa mnyenyekevu.”

    Shah Rukh Khan
  30. “Kabla ya kitu kingine chochote, maandalizi ni ufunguo wa kufanikiwa.”

    Alexander Graham Bell

Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazo Kuhamasisha Maishani Mwako.

Naamini umehamasika na kupata shauku zaidi ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako ili ufanikiwe. Kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu.

Naamini umebaini wazi kuwa maana ya mafanikio ni pana; pia mafanikio siyo kutokukabiliana na changamoto bali ni kuzikabili.

Je una maoni au maswali? Je umehamasika au kujifunza kitu? Tafadhali tuandikie maoni yako hapo chini. Usisahau kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi. Karibu pia uwashirikishe wengine makala ya nukuu hizi.

4 2 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

0 Maoni
Inline Feedbacks
View all comments
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x