Blog - Page 20 of 20 - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Blog

Usalama wa Msingi wa Kompyuta: Jinsi ya Kujilinda na Virusi, Wadukuzi na Wezi

Usalama wa Msingi wa Kompyuta: Jinsi ya Kujilinda na Virusi, Wadukuzi na Wezi

Teknolojia
Watu wengi hufikiri kuwa usalama wa kompyuta ni swala gumu lenye changamoto kubwa. Inaweza kuwa hivyo kama hukuchukua hatua sahihi mapema. Katika makala hii utafahamu hatua tano muhimu ambazo zitakuwezesha kujilinda na virusi, wadukuzi na wezi katika kifaa chako cha kielektroniki. 1. Wezesha automatiki sasishi (automatic updates) Programu mbalimbali za kompyuta hutoa masasisho (updates) mara kwa mara ili kuziba mianya mbalimbali hasa ya kiusalama iliyobainika katika matoleo ya awali. Program kama Microsoft Window, Mozilla na Chrome ni baadhi ya programu muhimu zinazohitajika kusasishwa kwa wakati. Hivi leo programu mbalimbali huja na usasishaji wa automatiki lakini watu wengi hupenda kuuzima usasishaji huu bila kuzingatia umuhimu wake wa kiusalama. Hivyo basi, ili kuwa salama zing...
Wanasayansi Wagundua  Rangi inayotumia Jua Kuzalisha Nishati

Wanasayansi Wagundua Rangi inayotumia Jua Kuzalisha Nishati

Habari, Teknolojia
Timu ya wanasayansi nchini Australia imegundua rangi ya sola ambayo inaweza kuzalisha nishati kwa ajili ya matumizi ya majumbani na magari. Timu hiyo iliyoongozwa na Torben Daeneke imesema kuwa inaamini kuwa njia hiyo itatoa nishati nafuu na safi kwa dunia. Nishati kwa ajili ya magari siku za mbeleni Inaweza kufikiriwa kuwa, kuendesha gari kwa nishati itokanayo na rangi ni kichekesho lakini wanayansi hao wamesema inawezekana. Wamesema kwa kuchanganya katalisti yenye rangi nyeupe inayotumika kwenye dawa ya meno, wanasyansi waliweza kutengeneza rangi ambayo ikikutana na jua inabadili maji kuwa hydrojeni ambayo itatumika kuendesha gari. Wamesema changamoto waliyonayo ni namna ya kuhamisha nishati hiyo na kuitumia kwenye gari; pamoja na hili wamesema wameshapata njia kadhaa wanazozifa...
Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Mbinu 10 za Kuanza Biashara na Mtaji Mdogo

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Watu wengi wamekuwa wakitamani kuanza biashara lakini wanafikiri namna ya kuanza kwani mtaji wao ni mdogo sana. Ni ukweli usiopingika kuwa idadi kubwa ya watu walioshindwa kuanzisha biashara wakishindwa katika eno hili la kuanza biashara na mtaji mdogo. Usiogope; kuwa na mtaji mdogo au kutokuwa nao kabisa sio mwisho wako wa kutimiza malengo yako. Zipo mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kukuwezesha kufanya biashara hata kama utakuwa na mtaji mdogo. Tafadhali fuatilia hoja jadiliwa hapo chini kwa ufafanuzi zaidi. 1. Kuwa mbunifu Moja kati ya mambo ambayo yatakusaidia sana kwenye kuanza biashara kwa mtaji mdogo ni ubunifu. Kwa njia ya ubunifu utaweza kushinda biashara na bidhaa zilizoko sokoni kwa urahisi zaidi. Unaweza kufanya haya yafuatayo: Chagua wazo la biashara unalolipenda na ku...
Sifa 10 Zitakazokufanya Kuwa Kiongozi Bora

Sifa 10 Zitakazokufanya Kuwa Kiongozi Bora

Maendeleo Binafsi
Je kiongozi bora ni yule mwenye wafuasi wengi au miaka mingi katika uongozi? La hasha, kiongozi bora hujengwa kwa sifa anuwai. Ni rahisi kufikiri kuwa kiongozi bora hutokea kwa bahati tu au hakuna haja ya kujifunza jinsi ya kuwa kiongozi bora. Wewe kama mtu anayehitaji kusimamia na kuratibu shughuli mbalimbali ni lazima ufahamu sifa zinazomfanya mtu kuwa kiongozi bora ili uwe na mafaniko. Katika makala hii utaweza kufahamu sifa 10 zitakazokufanya kuwa kiongozi bora. 1. Uwazi Uwazi ni sifa muhimu inayomfanya mtu kuwa kiongozi bora. Kiongozi bora ni lazima awe wazi katika utendaji kazi wake. Uwapo kiongozi kuna siri za kazi lakini namna ya utendaji kazi hautakiwi uwe siri au usioeleweka kwa wale unaowaongoza. Kiongozi bora anatakiwa kuwa na mpangilio mzuri na unaoeleweka wa utendaji k...
Tabia 10 zitakazobadili maisha yako

Tabia 10 zitakazobadili maisha yako

Mtindo wa Maisha
Mara nyingi umekuwa ukijiuliza ufanyeje ubadili maisha yako? Je umekuwa ukitamani kuboresha maisha yako kutoka kiwango cha chini kwenda katika kiwango bora zaidi? Kama jibu ni ndiyo basi una mawazo wazuri sana. Unatakiwa kuchukua hatua kadhaa ili basi uweze kuboresha maisha yako kutoka kiwango kimoja kwenda kingine. Katika makala hii nitakujuza tabia kumi ambazo kama utajitahidi kuwa nazo hakika utayabadili maisha yako na kuyafanya kuwa bora zaidi. 1. Epuka marafiki au watu wasiofaa Wahenga walisema “ndege wanaofanana huruka pamoja”. Je kwanini ukae na watu wavivu au wazembe kama wewe huna tabia hizo au zingine zinazofanana na hizo? Jijengee tabia ya kuwaepuka marafiki au watu wasiofaa katika maisha yako kwani hawatakusaidia kufikia malengo yako bali watakudidimiza. Tafuta watu ambao w...