Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 15 of 17
Monday, February 9Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Hamasa
Kwa mijibu wa jarida la Forbes linaeleza kuwa Reginald Mengi ni miongoni mwa watu maarufu katika tasnia ya habari kupitia kampuni yake ya IPP; ambayo ni moja kati ya kampuni kubwa za habari Afrika. Kampuni yake ya IPP ina magazeti 11 na vituo kadhaa vya televisheni pamoja na vyanzo mabalimbali vya kwenye mtandao. Mengi pia anamiliki kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers, ambayo ni kampuni pekee inayozalisha vinywaji vya jamii ya Coca-Cola kwa kanda ya kaskazini mwa Tanzania. Pia anazalisha maji ya Kilimanjaro yaliyojizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania. Mengi anajihusisha pia na uchimbaji wa madini kupitia kampuni yake ya IPP Resources yenye kampuni tanzu kadhaa. Reginald Mengi pia mekuwa akitoa misaada mbalimbali kusaidia makundi ya watoto, vijana, wanawake, wazee, ...
Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Tija, Usafiri na Safari
Ni wazi kuwa gari linahitaji mafuta ili kusafiri toka sehemu moja hadi nyingine. Lakini swali ni je, unaweza kutawala kiwango cha mafuta kinachotumika? Ndiyo, unawea kutawana kiwango cha mafuta na kupunguza garama za matumizi ya mafuta zisizokuwa na ulazima. Kama unapenda kuokoa kiasi cha mafuta yanayopotea bila sababu ya msingi katika gari lako, basi tumia njia hizi 8 zifuatazo. 1. Kabili upepo Unapoendesha gari upepo hukinzana na gari; hivyo kadri gari linavyokinzana zaidi na upepo ndiyo pia unavyotumia mafuta mengi zaidi. Hivyo basi, usipende kuweka mizigo juu ya gari kwa nje (carrier) au kufungua vioo kwani kutasabisha ukinzani zaidi kati ya gari na upepo. Kwa kukabili upepo vyema utapunguza ukinzani na kuokoa mafuta ambayo yangetumika kukabili ukinzani huo wa upepo. 2. Pu...
Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Teknolojia
Katika ulimwengu wa leo nywila au password si jambo geni. Mara kadhaa umeona au kutumia password katika vitu na maendeo kadhaa kama vile benki, simu, kompyuta n.k. Jambo la kushangaza ni jinsi watu wanavyotumia nywila bila kujali umuhimu wake katika eneo husika. Mtazamo wa ujumla juu ya nywila (password) Nywila ni ufunguo wa kufungua na kufunga sehemu husika; hivyo aliye nao ndiye atakayeweza kufungua na kufunga. Nywila ngumu = usalama zaidi; nywila rahisi = uslama kidogo. Mhalifu anaweza kutumia nywila kufanya uhalifu. Hivyo basi ni muhimu kufahamu namna ya kutengeneza nywila imara na salama kwa ajili ya kifaa au akaunti yako. Fuatilia makala hii ili uweze kujifunza mambo kadhaa ya kufanya ili kutengeneza nywila imara. 1. Epuka namba na maneno rahisi Wengi wetu hatu...
Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Teknolojia
Shughuli nyingi pamoja na kubadilika kwa mtindo wa maisha kumewafanya madereva wengi kusinzia wakati wanaendesha magari. Kusinzia wakati wa kuendesha gari kunaweza kusababisha madhara makubwa. Inashauriwa kuwa unapojisikia kuchoka ni vyema ukapumzika. Panasonic wanaamini kuwa wana utatuzi: kwa kutumia akili bandia (Artificial inteligence) wanaweza kumfanya dereva awe macho wakati wote. Kwa mujibu wa Panasonic kuna aina tano za kusinzia: kutosinzia, kusinzia kidogo, kusinzia halisi, kusinzia sana na kusinzia kulikopitiliza. Kampuni hii ya Kijapani imegundua mfumo wa kwenye magari unaoweza kutambua kusinzia kwa dereva na kupambana nako kabla ya kutokea. Mfumo huu humfwatilia dereva kwa kutumia kamera na vihisi (sensors). Mfumo huu unaweza kutambua mambo kama vile kupepesa macho,...
Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Hivi leo wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika kuwahi na kufanyia kazi fursa mbalimbali. Fursa hizo ni pamoja na uwekezaji katika biashara ndogo na za kati. Ni dhahiri kuwa mama ndiye nayeumia zaidi pale familia inapokuwa na uchumi mbaya. Mama hapendi kuona watoto wanakosa mahitaji yao ya msingi kama vile chakula, mavazi, elimu, matibabu n.k. Hivyo suala la kuboresha kipato cha familia limewafanya wanawake wengi kutafuta njia mbalimbali za kujipatia kipato ikiwemo njia ya kufanya biashara. Hata hivyo pamoja na jitihada hizi zinazofanywa na wanawake, bado biashara zao ngingi hufa kutokana na sababu kadha wa kadha. Fuatana nami katika makala hii ufahamu mambo matano yanayosababisha biashara nyingi za wanawake kufa. 1. Kukosa maarifa na elimu ya biashara Kitu chochote au kazi y...
Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Teknolojia
Kuna taarifa nyingi tunazoweka kwenye mtandao; lakini je, sasa ni wakati wa kuweka mipaka juu ya ni lipi la kuweka na kutoweka kwenye mitandao? Ndiyo; huu ni wakati sahihi. Hivyo basi, tambua vitu 11 ambavyo haupaswi kuviweka kwenye mitandao ya kijamii. 1. Tarehe kamili ya kuzaliwa Wakati mwingine unaweza kuvutiwa na namna marafiki zako wanavyoweka taarifa za kuzaliwa kwenye mtandao, au hata misisitizo ya mitandao ya kijamii kama vile Facebook juu ya kukamilisha akaunti yako kwa kuweka tarehe ya kuzaliwa. Kuweka tarehe halisi au kamili ya kuzaliwa kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kutoa mwanya kwa wahalifu kupata taarifa zako muhimu na hata kufungua au kuingilia akaunti zako zinazotumia tarehe yako ya kuzaliwa. Mambo ya kufanya: Ficha au ondoa tarehe yako halisi ya kuzal...
Dondoo 5 za Kuishi Ndoto Zako

Dondoo 5 za Kuishi Ndoto Zako

Maendeleo Binafsi, Tija
Kila mmoja ana ndoto zake katika maisha yake. Wengine wana ndoto kubwa za kubadilisha ulimwengu huu, huku wengine wakiwa na ndoto za kuishi maisha ya kupata mahitaji yao ya msingi tu. Wote hawa wanahitaji kuzitimiza ndoto zao; lakini kuna vikwazo na mambo mbalimbali ambayo huwazuia watu wasiishi ndoto zao na kuishia kulamu na kulalamika hasa uzeeni. Fuatana nami katika makala hii nikueleze dondoo tano za msingi zitakazokuwezesha kuishi ndoto zako. 1. Tambua kinachokuvuruga Maisha yetu ya kila siku yamejaa vitu na shunguli mbalimbali lakini si zote huturuhusu kuishi katika ndoto zetu. Inawezekana unapenda kitu au tabia fulani kiasi kwamba imetawala au imekuwa ya kwanza kwenye maisha yako. Nitajuaje kitu au tabia imetawala/imekuwa ya kwanza katika maisha? Jibu ni rahisi, kile una...
Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Viwanja Bora Zaidi vya Ndege Duniani

Usafiri na Safari
Je wajua kuwa kuna viwanja vya ndege vinavyopokea ndege zaidi ya 400 kwa siku lakini bado vinamudu kufanya kazi kwa ubora na ufanisi wa juu? AirHelp.com hivi karibuni imetoa orodha ya viwanja bora vya ndege duniani kwa kutegemea vigezo vitatu ambavyo ni: kufanya kazi kwa kuzingatia muda, ubora wa huduma na kuridhika kwa wasafiri. Fuatana nami katika makala hii ili kuona orodha ya viwanja bora zaidi vya ndege duniani. 1. Uwanja wa ndege wa Changi Singapore Uwanja wa ndege wa Changi unakadiriwa kuwa takriban ndege 450 huruka katika uwanja huu kila siku, na kuufanya kuwa uwanja wa ndege wa sita wenye shughuli nyingi Asia na wa 17 duniani. Pamoja na hayo inasemekana kuwa ni aslilimia 12 pekee ya ndege hizo huchelewa kwa zaidi ya dakika 15 - na hili huufanya uwanja huu kuwa bora kabisa...
Hatimaye Ghana Yarusha Satelaiti Yake ya Kwanza Kwenda Anga za Juu

Hatimaye Ghana Yarusha Satelaiti Yake ya Kwanza Kwenda Anga za Juu

Habari, Teknolojia
Satelaiti ijulikanayo kama GhanaSat-1, ambayo iliundwa na wanafunzi kutoka katika Chuo Kikuu cha All Nations cha Koforidua, ilirushwa kwenda kwenye mzingo wa dunia kutoka kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu. Shange na vifijo vya watu takriban 400 wakiwemo wanafunzi na waandisi walikokuwa wakishuhudia tukio hili zilisikika katika mji wa kusini mwa Ghana. Mji huo ndipo lilipofanyika zoezi hilo la urushaji wa satelaiti hiyo. Mawasiliano na chombo hicho yalianza kupokelewa muda mfupi baada ya chombo hicho kurushwa. Maradi huo uligharimu dola za kimarekani 50,000 ulifadhiliwa na shirika la Japan Aerospace Exploration Agency (JAXA). Satelaiti hiyo itatumika katika mambo mabalimbali kama vile kufwatilia ukanda wa pwani wa Ghana, kuchora ramani na kuijengea nchi hiyo uwezo kati...
Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Mambo 5 ya Kufahamu Kabla ya Kulenga Kupata Pesa kupita Kazi za Kwenye Mtandao

Kipato, Tovuti na Blogu
Kila mtu anahitaji kupata pesa ili kumudu mahitaji yake ya kila siku kama vile kununua chakula, nguo, kulipia matibabu, usafiri, ujenzi wa nyumba, n.k. Swali hapa ni kwa njia gani zitapatikana hizo pesa; kwani mara nyingi watu wanajikuta mishahara au kipato chao cha awali hakitoshi. Hivyo basi watu wanatafuta njia mbalimbali za kuwawezesha kuongeza kipato chao. Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamepelekea kukua kwa ajira na biashara katika mtandao; takwimu zinaonyesha kuwa kuna watu wengi wanaoomba na kufanya kazi katika matandao. Fuatana nami katika makala hii ili ufahamu mambo matano ya kuzingatia kabla ya kulenga kupata fedha kupitia kazi za kwenye mtandao. 1. Tovuti za matapeli Hivi leo ni rahisi kuona tovuti zinazojinadi kuwawezesha watu kupa kipato kwa urahisi ndani ...