
Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi
Kwa mijibu wa jarida la Forbes linaeleza kuwa Reginald Mengi ni miongoni mwa watu maarufu katika tasnia ya habari kupitia kampuni yake ya IPP; ambayo ni moja kati ya kampuni kubwa za habari Afrika. Kampuni yake ya IPP ina magazeti 11 na vituo kadhaa vya televisheni pamoja na vyanzo mabalimbali vya kwenye mtandao. Mengi pia anamiliki kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers, ambayo ni kampuni pekee inayozalisha vinywaji vya jamii ya Coca-Cola kwa kanda ya kaskazini mwa Tanzania. Pia anazalisha maji ya Kilimanjaro yaliyojizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania. Mengi anajihusisha pia na uchimbaji wa madini kupitia kampuni yake ya IPP Resources yenye kampuni tanzu kadhaa. Reginald Mengi pia mekuwa akitoa misaada mbalimbali kusaidia makundi ya watoto, vijana, wanawake, wazee, ...










