Madhara 6 ya Kutazama Televisheni (TV) Unayopaswa Kuyafahamu
Miaka ya nyuma televisheni ilikuwa ni kitu adimu sana. Lakini hivi leo takriban kila familia au mtu ana televisheni nyumbani kwake; inaweza kuwa sebuleni, chumbani au hata kwenye simu yake ya kisasa. Hata wale wasiokuwa na televisheni nyumbani kwao bado wanapata nafasi ya kutazama televisheni kwenye migahawa, mabasi au hata kwenye ofisi za kampuni au taasisi mbalimbali. Televisheni imekuwa ni kifaa muhimu kwa ajili ya habari na burudani; hata hivyo televisheni inaweza kuwa na madhara kadha wa kadha kwako ikiwa haitotawaliwa vyema. Basi karibu ufahamu madhara ya kutazama televisheni (TV)
1. Hupoteza muda
Unapokaa na kuangalia televisheni ni wazi kuwa unatumia muda mwingi na wa muhimu sana. Hii ni kutokana na sababu kuwa watu wengi hutazama televisheni kwa muda mrefu au hata siku...