Fahamu Hili Archives - Page 8 of 20 - Fahamu Hili
Wednesday, March 18Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Podcast: Fahamu Hili

Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Mambo Matano ya Kufanya ili Kuharakisha Kupona Majeraha

Afya
Hakuna mtu anayependa kupata majeraha au kuchelewa kupona majeraha. Kwa kuwa uhai na uzima wetu haupo mikononi mwetu, ni vyema tukafahamu kuwa kuna wakati tunaweza kuumia. Kwa kutambua hili karibu nikufahamishe mambo matano unayoweza kuyafanya ili kuharakisha kupona majeraha. 1. Kula vizuri Lishe bora ni muhimu wakati wote, lakini ni muhimu zaidi mara unapokuwa na majeraha. Ili uweze kupona majeraha mapema unahitaji ule matunda na vyakula vyenye protini, vitamini C, B12 pamoja na madini ya chuma kwa wingi. Vyakula na matunda hayo ni kama vile machungwa, mapapai, mayai, maziwa, samaki, maharage, n.k. Kwa kula vyakula hivi mwili utaweza kutibu majeraha kwa haraka zaidi. 2. Pumzika vya kutosha Kupumzika ni njia ya kuupa mwili nafasi ya kujijenga na kujitibu wakati wa majeraha. K...
Mambo 10 ya Kuzingatia Unapomtafutia Mtoto Shule

Mambo 10 ya Kuzingatia Unapomtafutia Mtoto Shule

Mahusiano na Familia
Hivi leo kuna shule nyingi, lakini siyo shule zote ni bora au zinafaa kwa ajili ya mtoto wako. Hii ni kutokana na shule nyingi kuanzishwa na kuendeshwa kwa misingi ya kibiashara kuliko huduma. Swala la kuhakikisha mtoto wako anapata elimu bora ni swala la msingi. Hii ni kutokana na nafasi na umuhimu wa elimu kwa maisha ya sasa na ya baadaye ya mtoto. Ikiwa unataka kupata shule nzuri kwa ajili ya mtoto wako, karibu nikufahamishe mambo 10 ya kuzingatia unapomtafutia au kumchagulia mtoto wako shule. 1. Kiwango cha ufaulu Hakuna mzazi au mlezi ambaye anapenda mtoto wake asifanikiwe kwenye masomo. Kufanikiwa kwa mtoto kwa kiasi kikubwa kunategemea kiwango cha ufaulu cha shule. Ni wazi kuwa shule inayofaulisha vyema itakuwa inafundisha vyema pia. Hivyo kagua kwanza matokeo ya miti...
Changamoto 12 za Ujasiriamali na Jinsi ya Kuzikabili

Changamoto 12 za Ujasiriamali na Jinsi ya Kuzikabili

Ujasiriamali
Kila jambo lina changamoto zake, ujasiriamali nao unachangamoto zake nyingi. Ni wazi kuwa wajasiriamali wakubwa na wadogo, wote hukutana na changamoto; tofauti yao ni chanzo cha changamoto hizo na njia wanazozitumia kuzikabili. Wajasiriamali wadogo ndiyo wamekuwa wakikabiliwa zaidi na changamoto hizo na hata kupelekea kupoteza biashara au miradi yao. Inawezekana wewe ni mmoja wapo wa wajasiriamali wanaokabiliana na changamoto. Karibu nikushirikishe changamoto 12 za ujasiriamali na jinsi ya kuzikabili. 1. Mtaji Kila biashara inahitaji mtaji ili iweze kujiendesha na kujipanua. Wajasiriamali wengi wanashindwa kuanzisha biashara au kupanua biashara zao kutokana na kukosa mtaji. Suluhisho: Kumbuka! Siyo lazima upate mtaji wote unaouhitaji, unaweza kuanza na mtaji kidogo sana n...
Yafahamu Majengo 10 Marefu Zaidi Duniani

Yafahamu Majengo 10 Marefu Zaidi Duniani

Maarifa
Dunia imeendelea kushuhudia uhaba mkubwa wa rasilimali mbalimbali kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu. Moja ya rasilimali ambazo zimekua adimu sana duniani kwa wakati huu ni ardhi, uhaba wa ardhi umefanya wahandisi kote duniani kuumiza vichwa vyao kufikiri namna ambavyo ardhi iliyopo itatumika vyema na kwa manufaa zaidi kwa wengi. Pamoja na sababu nyingine lukuki, ufinyu wa ardhi umechangia kwa kiasi kikubwa kujengwa kwa majengo marefu na ya kushangaza katika maeneo mbalimbali duniani. Yafuatayo ni majengo kumi marefu zaidi duniani maarufu kama sky scrapers kwa lugha ya kimombo. 10. International Commerce Centre Jengo hili linashika nafasi ya kumi kwa majengo marefu zaidi duniani. Lina urefu wa mita 484 pamoja na ghorofa 108; lilijengwa mwaka 2010. 09. Shanghai worl...
Mbinu 9 za Kuacha Tabia Mbaya

Mbinu 9 za Kuacha Tabia Mbaya

Maendeleo Binafsi
  Tabia mbaya zimekuwa zikiwakabili na kuwatesa watu wengi. Haipingiki kuwa tabia mbaya huwazuia watu wengi kufikia malengo yao kwenye maisha. Tabia kama vile uvivu, ulevi, madawa ya kulevya, uzinzi, matumizi mabaya ya pesa, ugomvi, kupoteza muda, n.k. ni baadhi tu ya tabia ambazo zimekuwa zikiwaathiri watu wengi. Hata hivyo, waathiriwa wa tabia hizi wengi hutamani kuziacha, lakini wanashindwa kufahamu waanzie wapi na watumie njia gani ili kuacha tabia hizo. Ikiwa basi unataka kuboresha maisha yako, karibu nikufahamishe mbinu 9 unazoweza kuzitumia ili kuacha tabia mbaya. 1. Jikumbushe na tafakari madhara ya tabia hiyo Ili kupata motisha wa kuacha tabia mbaya, kila mara jikumbushe na tafakari madhara unayoyapata kutokana na tabia hiyo. Kwa mfano ikiwa ni tabia ya u...
Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Faida 25 za Kutembea kwa Miguu

Mtindo wa Maisha
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo. Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii. Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida 25 za kutembea kwa miguu. Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu. Huimarisha mifupa. Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi. Husaidia kupunguza uzito. Huzuia saratani ya utumbo mpana. Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua. Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance). Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya...
Maswali 10 Muhimu ya Kujiuliza Kabla ya Kuacha Kazi

Maswali 10 Muhimu ya Kujiuliza Kabla ya Kuacha Kazi

Kipato
Wakati wengine wakitafuta kazi usiku na mchana, wengine wanatamani kuacha kazi mara moja. Kutokana na sababu mbalimbali, swala la kuacha kazi linawakabili watu wengi. Mazingira mabaya ya kazi, matatizo ya kifamilia au kiafya yamekuwa chanzo kikubwa cha watu kutamani au kutaka kuacha kazi. Swala la kuacha kazi ni swala nyeti ambalo linahitaji utulivu na maamuzi yenye kuhusisha utafiti na busara kubwa. Wengi huacha kazi kutokana na misukosuko midogo na kujikuta wakiingia kwenye matatizo makubwa zaidi. Ikiwa unataka kuacha kazi unayoifanya ili utafute nyingine au ujiajiri mwenyewe, basi jiulize maswali haya 10 kabla ya kumpungia mwajiri wako mkono. 1. Je unaacha kwa sababu sahihi? Inawezekana umekaripiwa na mwajiri wako kutokana na kosa ulilolifanya, swala hili limekukasirisha ...
Mambo 12 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Bill Gates

Mambo 12 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Bill Gates

Hamasa
Kwa mujibu wa Forbes 2017, Bill Gates ndiye mtu tajiri zaidi duniani akiwa na utajiri unaokadiriwa kuwa dola za Marekani bilioni 86. Bill Gates ndiye mwanzilishi na mmiliki wa kampuni ya Microsoft. Microsoft ni kampuni iliyotengeneza programu endeshi (operating system) maarufu na mashuhuri sana duniani ya Window. Kampuni hii pia inazalisha bidhaa nyingine kama vile vifaa vya michezo ya kielektroniki, pogramu mbalimbali pamoja na vifaa vingine vya kiteknolojia. Kwa hakika Bill Gates ni mtu aliyefanikiwa sana ambaye kila mtu anayetaka kufanikiwa anaweza kujifunza mambo kadhaa kutoka kwake. Kwa kutambua umuhimu wa kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa, karibu nikushirikishe mambo 12 unayoweza kujifunza kutoka kwa Bill Gates. 1. Anza mapema kadri iwezekanavyo Bill Gates alianza kuj...
Vitu Vinne Vinavyokufanya Usikamilishe Kazi Zako

Vitu Vinne Vinavyokufanya Usikamilishe Kazi Zako

Tija
Hakuna mtu anayependa kushindwa kukamilisha kazi au kitu alichokianza. Hata hivyo mara nyingi kutokukamilisha kazi hutokea kwa watu wengi. Ni ukweli usiopingika kuwa zipo sababu kadha wa kadha zinazosababisha tatizo hili. Karibu nikufahamishe vitu vinne vinavyokufanya usikamilishe kazi zako. 1. Usingizi Kuna usemi usemao “usingizi ni mlango wa umaskini”; kwa hakika kulala kupita kiasi ni jambo ambalo litakupotezea muda mwingi pamoja na ufanisi. Unapolala sana unakosa muda wa kutosha kutimiza majukumu yako. Pia kulala muda mrefu hukufanya uamke ukiwa umechoka na kukufanya ukose ari na motisha wa kufanya kazi. Soma pia: Njia 10 za Kuamka Mapema Asubuhi. 2. Intaneti na simu Maendeleo yana manufaa yake na hasara zake. Kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, watu wengi...
Sifa 17 za Kuzingatia Kwa Mtu Unayetaka Kuoa au Kuolewa Naye

Sifa 17 za Kuzingatia Kwa Mtu Unayetaka Kuoa au Kuolewa Naye

Mahusiano na Familia
Swala la mtu wa kuoa au kuolewa naye ni swala nyeti linalohitaji maamuzi yanayohusisha hekima, utulivu, kumwomba Mungu pamoja na uchunguzi wa kutosha. Maisha ya watu wengi yamekuwa na matatizo makubwa kutokana na kufanya makosa katika kuchagua mtu wa kuoa au kuolewa naye. Kwa hakika hakuna mtu au mwenzi mkamilifu, lakini kuna sifa za msingi ambazo kila mtu unayetarajia kuoa au kuolewa anapaswa kuzizingatia na kuzitilia maanani. Naamini unapenda kuoa au kuolewa na mtu sahihi. Karibu nikushirikishe sifa 17 za kuzingatia kwa mtu unayetaka kuoa au kuolewa naye. 1. Ana malengo na maono Hakikisha mtu unayetaka kuoana naye ni mtu mwenye malengo katika maisha yake. Mtu mwenye malengo hujishughulisha kila mara kuhakikisha anaandaa baadaye yake. Mtu asiyekuwa na malengo huwaza matumiz...