Fahamu Hili Archives - Page 12 of 20 - Fahamu Hili
Wednesday, March 18Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Podcast: Fahamu Hili

Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu

Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu

Maarifa
Hofu ni hisia ambazo zinatulinda na vitisho vinavyotuzunguka. Kila mtu ana hofu, lakini viwango na aina ya hofu hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Wapo watu ambao huhofu juu ya vitu na mambo mbalimbali hadi kushindwa kuendelea na majukumu au maisha yao ya kawaida. Ikiwa unapenda kufahamu aina za hofu (phobia) ili pia uchunguze kama una aina hizo basi fuatilia makala hii nikufahamishe aina 70 za hofu. Pogonophobia – Pogonophobia ni hofu ya kuogopa ndevu au kukaa karibu na mtu mwenye ndevu. Hofu hii huwapata zaidi wanawake. Astraphobia – Hofu hii pia inajulikana kama astrapophobia, brontophobia, keraunophobia, au tonitrophobia; hii ni hofu ya kuogopa radi. Photophobia – Hii ni hofu ya kuogopa mwanga; mara nyingi husababishwa na matatizo ya kiafya ya macho. So...
Njia 10 za Kuamka Mapema Asubuhi

Njia 10 za Kuamka Mapema Asubuhi

Tija
Kuamka mapema asubuhi kuna manufaa mengi sana. Unapoamka mapema asubuhi unaongeza ufanisi na tija katika utendaji wako wa kazi. Kumbuka pia muda wa asubuhi ndipo mtu anapokuwa na afya njema kiakili na kimwili; hivyo kuamka mapema kutakuwezesha kuutumia muda huu vyema. Pamoja na umuhimu huu wa kuamka mapema, siyo watu wengi wanaoweza kutimiza lengo lao la kuamka mapema. Zipo sababu mbalimbali zinazosababisha tatizo hili kama vile matatizo ya kiafya, kisaikolojia na hata kimazingira. Ikiwa basi wewe ni mmoja wapo wa watu wanaotamani kuamka mapema, basi fahamu njia 10 za kukuwezesha kuamka mapema asububi. 1. Lala muda sahihi Muda wa kulala ni muhimu sana katika kukuwezesha kuamka mapema asubuhi. Hakikisha unalala mapema na unapata muda wa kutosha wa kulala. Kwa kawaida bina...
Faida 11 za Push Up Kiafya Unazotakiwa Kuzijua

Faida 11 za Push Up Kiafya Unazotakiwa Kuzijua

Mtindo wa Maisha
Mazoezi ni njia moja wapo ya kutufanya tuwe vizuri na wenye afya njema. Kama unahitaji zoezi ambalo litanufaisha sehemu mbalimbali za mwili wako, push ups ni zoezi moja wapo. Push up ni zoezi ambalo linaweza kufanywa na wanaume na wanawake bila gharama yoyote; na faida zake ni zaidi ya kunyoosha tu misuli. Naamini unapenda afya njema pamoja na maarifa; fuatilia makala hii nikufahamishe faida 11 za zoezi la push up kiafya ikiwa utalifanya mara kwa mara. 1. Huboresha mkao na mwonekano wako Push up ni njia bora ya kuufanya mgongo wako unyooke. Push up huimarisha na kuweka sehemu mbalimbali za mwili wako kukaa jinsi ipasavyo; kwa njiaa hii huufanya mwili wako uwe na mwonekano mzuri. 2. Huimarisha misuli Unapopiga push up unahusisha misuli mbalimbali kwenye mwili wako; misuli hii ni ...
Application/Programu 10 Muhimu za Kuwa Nazo Kwenye Simu (2017)

Application/Programu 10 Muhimu za Kuwa Nazo Kwenye Simu (2017)

Teknolojia
Ni wazi kuwa sasa kuna ongezeko kubwa sana la matumizi ya simu za mkononi hasa simu za kisasa (smartphone). Ni ukweli usiopingika kuwa yapo matumizi mengi ya simu za mkononi pamoja na programu zake (applications) ambayo bado hayajafahamika vyema kwa watumiaji wake. Fuatilia makala hi ufahamu programu 10 muhimu kuwa nazo kwenye simu yako ili uwe mwenye tija zaidi. 1. Google Drive Google drive ni zaidi ya hazina ya mafaili. Google Drive inakuwezesha kutengeneza ofisi yako ndogo yenye uwezo mzuri wa kuunda, kupanga, kuhariri na hata kusambaza mafaili mbalimbali kadri upendavyo. 2. Android Device Manager Ukizingatia kwamba simu ni muhimu sana kwenye maisha yetu, tunahitaji kitu cha kutusaidia ikiwa jambo litakwenda vibaya. Android Device Manager itakuwezesha kufanya mambo kama vile ...
Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako

Nukuu (Quotes) 50 Zitakazokuhamasisha Maishani Mwako

Hamasa
Yale tunayoyawaza na kuyatafakari kwenye fikra zetu yana nafasi kubwa sana kwenye maisha yetu. Ikiwa tunataka kufanikiwa basi ni lazima tufikiri na kutafakari juu ya kufanikiwa. Vivyo hivyo ikiwa tunahitaji kuhamasika kufanya mambo mbalimbali maishani, ni lazima tusome, tusikilize, tutazame na hata tutafakari vitu vitakavyotuhamasisha. Karibu nikufahamishe nukuu 50 (quotes) ambazo zitakuhamasisha katika maswala mbalimbali unayoyafanya maishani mwako. Naamini umehamasika na kufurahia nukuu hizi za hamasa. Ni wazi kuwa kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu - tunavyowaza ndivyo ...
Mbinu 7 za Uandishi Bora wa Vitabu

Mbinu 7 za Uandishi Bora wa Vitabu

Tija
Hivi leo vitabu ni moja kati ya vyanzo vikuu vya maarifa; ingawa bado watu wengi hawafahamu tunu inayopatikana katika vitabu. Mara nyingi umekuwa ukisoma vitabu kadha wa kadha ambavyo vimekuburudisha au hata kukufundisha mambo mengi. Lakini pia inawezekana wewe una mambo ambayo ungependa kuyaweka katika vitabu. Ni wazi kuwa kuna mbinu mbalimbali unazoweza kuzitumia kuandika kitabu ili kiweze kufikisha ujumbe au kutimiza lengo lililokusudiwa. Karibu ufahamu mbinu 7 zitakazokuwezesha katika uandishi wa vitabu. 1. Chagua wazo bora Hatua ya kwanza kabisa katika uandishi wa kitabu ni kuchagua mada au wazo bora. Hakikisha unachagua wazo au mada kwa makini ambayo itakuwezesha kukamilisha lengo lako. Unaweza kuzingatia haya: Chagua mada ambayo unaipenda na unaielewa vyema. Chag...
Fahamu Vitu Vilivyotengenezwa Upya (recycled) na Kuzalisha Vitu Vingine vya Kuvutia

Fahamu Vitu Vilivyotengenezwa Upya (recycled) na Kuzalisha Vitu Vingine vya Kuvutia

Maarifa
Hivi leo wabunifu mbalimbali wametokea duniani. Wabunifu wengine wamejikita kwenye kutumia ubunifu wao kukabiliana na changamoto mbalimbali hasa za uharibifu wa mazingira. Wapo watu na wabunifu mbalimbali walioona umuhimu wakutengeneza (recycle) tena vitu mbalimbali ambavyo matumizi yake yamekwisha, ili vifae tena kwa matumizi mengine. Mara nyingi tumeshuhudia magurudumu, chupa, mapipa, na hata vifaa vya mitambo mbalimbali vikitupwa hovyo baada ya kumalizika kwa matumizi yake. Lakini sasa ungana nami nikushirikishe vitu kadhaa vilivyotengenezwa upya (recycled) na kuzalisha vitu vya kuvutia na vyenye tija kubwa. 1. Mapipa ya kemikali na mafuta 2. Matairi yaliyozeeka 3. Injini ya gari na sehemu nyingine za gari 4. Sehemu za baisikeli 5. Chupa za plastiki Picha hizi...
Mbinu 10 za Uhakika  za Kufahamu Kiingereza/English kwa Muda Mfupi

Mbinu 10 za Uhakika za Kufahamu Kiingereza/English kwa Muda Mfupi

Tija
Kujifunza lugha mpya kunaweza kuwa ni kugumu, lakini inawezekana. Je unatamani kufahamu na kumudu lugha ya Kiingereza kwa muda mfupi? Kumudu Kiingereza inawezekana lakini kuna mambo kadhaa unatakiwa kuyafahamu na kuyafanya kwa uhakika. Ikiwa unapenda kuwa wa kimataifa, basi fuatilia mbinu 10 za uhakika zitakazo kuwezesha kufahamu Kiingereza/English kwa muda mfupi. 1. Penda na furahia Kiingereza Ili uweze kufanya au kujifunza kitu chochote ni lazima kwanza ukipende. Ikiwa unataka kufahamu Kiingereza kwa muda mfupi ni lazima ukipende kwani ndipo utaweza kujifunza kila mara bila kuchoka wala kukata tamaa. Kila mara jihamasishe kwa kutafakari manufaa utakayoyapata baada ya kufahamu Kiingereza vizuri. 2. Jifunze Kiingereza kila siku Huwezi kufahamu Kiingereza kama hutojifunza kila si...
Makosa 10 ya Kuepuka Unapotengeneza Logo au Nembo

Makosa 10 ya Kuepuka Unapotengeneza Logo au Nembo

Biashara na Uchumi
Nembo au logo ni jiwe la msingi la bidhaa na kampuni yako. Utambulisho wa biashara, kampuni yako au bidhaa unaonyeshwa kupitia nembo yako, ambayo ni pamoja na jina la kampuni yako. Hivyo, nembo ni moja kati ya mambo makuu ambayo yanafanya biashara yako kukumbukwa na kutambulika. Kwa kutambua umuhimu huu, kampuni na watu mbalimbali wamekuwa wakiwekeza fedha nyingi ili kupata nembo bora. Pamoja na kuwekeza pesa nyingi, bado kampuni na watu wengi hawapati nembo bora. Kwa mfano kampuni ya Pepsi iliwekeza dola milioni 1 lakini wakaishia kupata nembo iliyokumbana na ukosoaji mkubwa. Ni wazi kuwa kuna mambo unayotakiwa kuyazingatia kabla ya kuamua kulipia au kutengeneza nembo yako. Fahamu makosa 10 ambayo kama utayaepuka wakati wa kutengeneza au kuchagua nembo, basi utaweza kuwa na n...
Rangi 11 za Mkojo na Maana Zake Kwenye Mwili wako

Rangi 11 za Mkojo na Maana Zake Kwenye Mwili wako

Afya
Ni watu wachache sana ndiyo hupenda kuchunguza rangi za mikojo yao. Lakini kiuhalisia rangi hizi zinaeleza mambo mengi kuhusu afya yako; Ikiwa hunywi maji ya kutosha au una maradhi fulani, basi utafahamu kupitia rangi hizi. Hapa chini kuna mchoro-taarifa (infographic) unaoonyesha kinachomaanishwa na rangi 11 za mkojo na nini unachotakiwa ufanye. Naamini sasa umepata maarifa; pia naamini sasa hutopuuzia tena kuchunguza mkojo wako. Je una swali au maoni yoyote? Tafadhali tuandikie hapo chini kisha washirikishe wengine makala hii. Usisahau pia kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.