Mbinu 10 za Uhakika za Kufahamu Kiingereza/English kwa Muda Mfupi - Fahamu Hili
Friday, June 2Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Mbinu 10 za Uhakika za Kufahamu Kiingereza/English kwa Muda Mfupi

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Kufahamu Kiingereza

Kujifunza lugha mpya kunaweza kuwa ni kugumu, lakini inawezekana. Je unatamani kufahamu na kumudu lugha ya Kiingereza kwa muda mfupi? Kumudu Kiingereza inawezekana lakini kuna mambo kadhaa unatakiwa kuyafahamu na kuyafanya kwa uhakika.

Ikiwa unapenda kuwa wa kimataifa, basi fuatilia mbinu 10 za uhakika zitakazo kuwezesha kufahamu Kiingereza/English kwa muda mfupi.

1. Penda na furahia Kiingereza

Ili uweze kufanya au kujifunza kitu chochote ni lazima kwanza ukipende. Ikiwa unataka kufahamu Kiingereza kwa muda mfupi ni lazima ukipende kwani ndipo utaweza kujifunza kila mara bila kuchoka wala kukata tamaa. Kila mara jihamasishe kwa kutafakari manufaa utakayoyapata baada ya kufahamu Kiingereza vizuri.

2. Jifunze Kiingereza kila siku

Huwezi kufahamu Kiingereza kama hutojifunza kila siku. Hakikisha unaongeza misamiati, unajifunza matamshi pamoja na kanuni mbalimbali za lugha.

Mambo ya kukumbuka hapa:

  • Nunua kamusi ya Kiswahili na Kiingereza.
  • Soma vitabu na machapisho mbalimbali yaliyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.
  • Tumia tovuti za kujifunza lugha kama vile Duolingo, Babbel, BBC Learning English n.k. kujifunza Kiingereza.
  • Kama inawezekana, tafuta mwalimu au chuo cha kujifunza Kiingereza.

3. Zungumza Kiingereza

Huwezi kumudu kuzungumza Kiingereza kama hutozungumza. Jitahidi katika kutumia Kiingereza katika mazungumzo yako hata kama utakosea.

Jifunze maneno uliyoyazoea kuyatumia mara kwa mara na uyafahamu kwa Kiingereza ili uyatumie katika mazungumzo.

Jambo la kuzingatia ni kuangalia tu mtu unaye ongea naye; ikiwa mtu hajui Kiingereza basi usitumie Kiingereza kwani anaweza kuona unamdharau.

Hata kama huna mtu wa kuzungumza nae, unaweza kuzungumza mwenyewe tu kwa sauti ndogo bila shida; kwani ni mambo mangapi unayokuwa unanayawaza na kuyajadili akilini mwako peke yako? Anza kuzungumza sasa.

4. Andika Kiingereza

Kuandika kwa Kiingereza kutakusaidia sana kuboresha uwezo wako wa Kiingereza cha kuandika. Ikiwa unaandika ujumbe, machapisho (posts) kwenye mitandao ya kijamii, kadi, au hata shajara (diary); basi tumia lugha ya Kiingereza.

5. Usiogope kukosea

Ni rahisi mtu kushindwa kujifunza Kiingereza kwa kigezo tu cha kuogopa kufanya makosa. Makosa ni hatua muhimu katika kujifunza kitu chochote.

Unapofanya makosa na kuyabaini, ni wazi kuwa mbeleni hutoyarudia tena. Hivyo, tumia Kiingereza katika kila eneo bila kuogopa kufanya makosa.

6. Sikiliza na tazama vitu au vipindi vya Kiingereza

Najua wengi ni wafuasi wa miziki na filamu; miziki na filamu za Kiingereza zinaweza kukusaidia kwa kiasi kikubwa kujifunza lugha. Usipende kutazama filamu zilizotafsiriwa; jitahidi kujifunza maana za maneno unayosikia kwenye filamu na miziki kwa kutumia kamusi niliyoitaja kwenye hoja namba moja.

Jitahidi pia kutazama vipindi au hotuba mbalimbali zilizoandaliwa kwa lugha ya Kiingereza kupitia televisheni au mtandao wa YouTube. Jifunze jinsi watu wanavyotamka maneno pamoja na kuchunguza maana zake.

7. Waza kwa Kiingereza

Kuwaza kwa Kiingereza? Ndiyo, kuwaza kwa Kiingereza kutaongeza uwezo wako wa lugha kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano badala ya kuwaza “Nitakwenda mjini kesho…” unaweza kuwaza “I will go to town tomorrow…” n.k. Kwa kufanya hivi kutakujengea uwezo wa kutumia na kufahamu Kiingereza zaidi.

8. Elewa na usikariri kanuni

Kila lugha ina kanuni zake. Usipoteze nguvu kubwa kukariri kanuni, bali elewa matumizi ya kanuni zinazotawala mpangilio wa maneno na matumizi yake.

Kwa mfano sentensi nyingi za Kiingereza huwa na (Mtenda-Tendo-Mtendwa au Kitendwa) yaani (Subject-Verb-Object)

Mf. Mary killed the dog.

John is cooking the food.

Kufahamu kanuni kama hii na nyinginezo, kutakuwezesha kuelewa kwanini mtenda huanza kisha kufuatiwa na tendo pamoja na mtendwa au kitendwa katika sentensi za Kiingereza.

9. Tafuta rafiki au mshirika

Ikiwa kuna mtu ambaye mnaweza kujifunza kwa pamoja, basi mshirikishe ili mjifunze kwa pamoja. Au ikiwa kuna mtu anamudu vyema Kiingereza, unaweza kumwomba akusaidie katika mchakato wako wa kujifunza.

Kwa kufanya hivi utaweza kuuliza maswali au hata kuzungumza moja kwa moja na mshirika wako. Kama wewe ni mtumiaji mzuri wa mtandao, unaweza kupata mshirika kwenye mtandao pia.

10. Kuwa na subira na usikate tamaa

Ni wazi kuwa zipo chngamoto katika kujifunza lugha mpya hasa Kiingereza. Lakini ni muhimu ukafahamu kuwa ni swala la muda, uvumilivu, mazoezi na nia tu ndivyo vitakavyokuwezesha kufahamu Kiingereza vyema. Hakuna kitu kizuri kinachotokea kwa usiku mmoja, fanya bididi usikatishwe tamaa na changamoto; nawe kwa hakika utafikia lengo.

Soma pia: Hatua 7 za Maumivu Zisizoepukika Kabla ya Kufanikiwa.

Hitimisho

Ni ukweli usiopingika kuwa kufahamu Kiingereza siyo lazima uwe umezaliwa kwenye nchi ya watu wanaozungumza Kiingereza, bali ni kuzingatia mbinu tajwa hapo juu pekee. Naamini ukizingatia mbinu zilizojadiliwa hapo juu kwa bidii utaona matokeo mazuri katika uwezo wako wa lugha ndani ya muda mfupi.

Je bado umekwama kwenye kujifunza Kiingereza? Je una swali au maoni? Tafadhali tuandikie hapo chini; pia usisahau kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook pamoja na kuwashirikisha wengine makala hii.

3.6 17 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
guest

36 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Shukuru mohamed shabani
Shukuru mohamed shabani
4 years ago

Na shukuru sana kwa muongozo

Kornelio Maanga
Reply to  Shukuru mohamed shabani
4 years ago

Nashukuru sana kwa kutembelea blog yetu ya Fahamuhili; tunashukuru pia kwa maoni yako mazuri.

Hemedy ally
Hemedy ally
Reply to  Kornelio Maanga
2 years ago

Dah nashukuru sana kuingia humu kwenye blog yenu

Kornelio Maanga
Reply to  Hemedy ally
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Mussa Mc
Mussa Mc
3 years ago

Vizuri sana na je vipi kama mtu huna hata mtu mmoja mshiriki inawezekana kujifunza kiingereza?

Kornelio Maanga
Reply to  Mussa Mc
3 years ago

Ndiyo, unaweza kujifunza kwa kutumia mbinu nyingine tajwa; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Titus setembo
Titus setembo
Reply to  Kornelio Maanga
2 years ago

Ningependa kuzijua mbinu zingine kama hyo moja uliyoitaja hapo juu kuhusu kwenye sentensi kuanza na Mtenda, tendo afu mtendwa, hii nimeielewa, nahitaji kufahamu zingine

Kornelio Maanga
Reply to  Titus setembo
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Simon daniel
Simon daniel
3 years ago

Nimependezewa na maarifa mbalimbali mnayotoa

Kornelio Maanga
Reply to  Simon daniel
3 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

lilian danie
lilian danie
Reply to  Kornelio Maanga
3 years ago

asante sana kwa ushauri mzuri wa namna ya kujifunza kingereza

Kornelio Maanga
Reply to  lilian danie
3 years ago

Asante sana; karibu sana Fahamuhili.com

sam ckiper
sam ckiper
3 years ago

kwanza kabisa nianze kwa kuwashukuru kwa kazi ya kuelimisha jamii pia namimi ni mmoja kati ya wanao jifunza kiingereza kwa bidii sana ila nilikuwa naomba msaada zaidi

Kornelio Maanga
Reply to  sam ckiper
3 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com tukupe ushauri.

Shabani
Shabani
3 years ago

Nashukuru mungu kwa elim mlio nipatia hakika tufkie malengo bi~ithin Allah

Kornelio Maanga
Reply to  Shabani
3 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

AISHA ABDULLA
AISHA ABDULLA
2 years ago

Asante sana kwa kuelimisha jamii njia nzuri ya kutumia kwa kujifunza lugha

Kornelio Maanga
Reply to  AISHA ABDULLA
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani kwetu; karibu sana Fahamuhili.com

Hemedy ally
Hemedy ally
2 years ago

Sasa samahani ivi ikitokea labda sina mtu wa kuzungunza naye lakini napenda lugha ya kingereza naweza kufanyaje ili kuepukana na shida hii ya kutokujua kingereza?

Kornelio Maanga
Reply to  Hemedy ally
2 years ago

Zipo njia nyingi za kujifunza ndugu; pia wapo watu na mazingira ambayo kiingereza kinapata nafasi zaidi, jitahidi kuyatafuta hayo; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Felix
Felix
2 years ago

Napenda nijue mapema sana kaka yani nimeona huu ujumbe naimani nitafanikiwa tu asnte Mungu akuzidishie Upeo mkubwa sana

Kornelio Maanga
Reply to  Felix
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Meshack
Meshack
2 years ago

Nahitaj lafik to teach me english

Kornelio Maanga
Reply to  Meshack
2 years ago

Wapo tele mtandaoni ndugu; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Nick
Nick
2 years ago

Kwanza nashukuru saan kwa ushauri wenu ila mimi kila nikijifunza nakata tamaa na naham ya kujua kiundani zaid

Kornelio Maanga
Reply to  Nick
2 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

Annir
Annir
2 years ago

Mimi Nina tatizo la masikio limeanza nipo darasa la 3 sasa hadi sasa hv nipo chuo kikuu kutamka maneno ya kiingereza no shida japo kuandika na maana za maneno najua he nifanyeje

Kornelio Maanga
Reply to  Annir
2 years ago

Pole sana kwa tatizo hilo je umewaona wataalamu wa afya ya masikio?

Stamili nungu
Stamili nungu
Reply to  Kornelio Maanga
10 months ago

Natamani balaa na sijui kitu du

Kornelio Maanga
Reply to  Stamili nungu
9 months ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; jifunze kila mara utafahamu kiingereza bila shida. Karibu sana Fahamuhili.com

Omar philimon
Omar philimon
1 year ago

Nahitaji kujifunza English unanisaidiaje

Kornelio Maanga
Reply to  Omar philimon
9 months ago

Tafadhali zingataia makala yetu. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com

Rashidi
Rashidi
1 year ago

Nawashkr sna wenye blog hii kwa kuweze kutujuza vitu mbali mbali kuhusu kujifunza luga ya kingreza Asanten sn

Kornelio Maanga
Reply to  Rashidi
9 months ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com

Seseph
Seseph
10 months ago

Good

Kornelio Maanga
Reply to  Seseph
9 months ago

You are welcome! Fahamuhili Maarifa bila kikomo.

36
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x