Mafanikio yana maana mbalimbali kwa kila mtu; kama vile uzuri unavyotofautiana kati ya mtu mmoja hadi mwingine. Ni jukumu lako kubainisha ni nini maana ya mafanikio na ni kwa namna gani utayafikia mafaniko hayo.
Fuatana nami nikushirkishe vitu 10 vinavyozuia mafaniko yako kama unataka kuona na kufikia mafanikio yako.
1. Kutoa visingizio
Acha kulaumu na kulalamikia watu wengine kwa kutokupata kile unachokihitaji. Acha kusingizia serekali na jamii kuwa ndiyo kikwazo cha wewe kufikia mafanikio yako. Watu waliofanikiwa hawalalamiki bali wanafanya kazi kwa bidii kufikia malengo yao.
Kumbuka hakuna mtu aliyefanikiwa sana duniani kwa kusaidiwa na serikali au mtu fulani katika jamii; ukiwepo msaada basi utumie tu kama ngazi.
2. Kutazama tu mapungufu
Umejijengea dhamiri ya kutofanya chochote kwa kuwa wewe unaona tu matatizo. Kwa hakika katika ulimwengu huu kila kitu kina pande mbili; unachotakiwa kufanya ni kuyaona matatizo kwa jicho la mafanikio.
Badili mtazamao wako sasa epuka kuona tu matatizo na mapungufu ili uweze kufanya mambo yenye tija kwa ajili ya mafanikio yako.
3. Kuogopa kushindwa
Mara nyingi napenda kuwashauri watu kuwa ni bora kujaribu ukashindwa kuliko kushindwa hata kujaribu. Umekuwa haufanyi kitu chochote kwa kigezo kuwa unaogopa kushindwa; hakika hotofanikiwa kwani maisha yako yatamalizika wakati hujafanya chochote.
Je ulishwahi kufikiri kila mtu ulimwenguni angewaza kama wewe? Dunia hii isingekuwa na ugunduzi wala maendeleo yoyote.
Mwanasayansi Thomas Edison alijaribu mara 1,000 kutengeneza balbu ya umeme hadi alipofanikiwa. Je kwanini wewe hujajaribu hata mara moja? Anza kufanya leo na utaona matokeo yake.
Soma pia: Mambo 25 Unayoweza Kujifunza Kutokana na Makosa.
4. Kutafuta njia rahisi
Wahenga walisema rahisi ni gharama; pia wakesema rahisi inaumiza. Fahamu kuwa hakuna kitu kizuri kinachopatikana kwa urahisi. Jiulize ni kwa nini madini ya thamani hupatikana chini sana ardhini; baada ya swali hili utagundua kuwa kufikia mafanikio ni kupambana na changamoto.
Fanya kazi kwa bidii, tumia nguvu, juhudi na marifa yako yote ili uweze kufikia malengo yako ya maisha. Acha uvivu tesa mwili na akili yako kwa muda, kwani utaona matokeo mazuri.
5. Kujipiga mwenyewe
Kama hapendi kujipiga au kuumiza mwili wako wa damu na nyama kwanini unaruhusu kupiga au kuumiza akili na fikra zako?
Acha kuwaza mawazo yanayoumiza akili na fikra zako; yaliyopita yamepita, yasahau ujenge maisha mapya. Hakikisha huumizi fikra na akili zako kwani zinahitajika sana katika kufanikiwa kwako.
6. Kutokuwa na shukrani
Jifunze kusukuru na kuridhika kwa vitu na hali uliyonayo. Inawezekana kuna wengine wanatamani hata wawe na uwezo wa kuwa wazima kiafya lakini hawawezi. Ni wazi kuwa, ukiwa na shukurani pia utajifunza kuridhika.
Simaanishi uridhike na matatizo, la hasha, bali ujifunze kutambua unapopata mafanikio fulani; kwani hili litakuhamasisha kusonga mbele zaidi. Nimeshuhudia watu ambao wana mafaniko mengi tu lakini bado wanahangaika na kunung’unika kama vile hawana hitu. Hivyo badili mtazamo wako leo.
7. Ubinafsi na kushughulikia mahitaji yako tu
Inawezekana unawaza sana kuhusu maisha yako na mahitaji yako, tena unafikri kuvipata hivyo ndiko kufanikiwa. Hakia kufanikiwa halisi ni kuweza kuwasaidia na kuwafikia wengine. Pia kutumia mahitaji au matatizo ya wengine kama fursa ni njia bora zaidi ya kuhimiza mafanikio yako.
8. Kuvurugwa
Kuvurungwa? Ndiyo, kuvurugwa kunaweza kukutoa katika njia sahihi ya mafaniko yako. Unataka kuandika kitabu lakini… unataka kusoma lakini… unataka kuanzisha biashara lakini… unajikuta kuna mtu au kitu kinakuingilia.
Usiruhusu mtu au vitu kama vile mitandao ya kijamii kukutoa katika kufanya kile unachotaka kukifanya; jitenge navyo kisha fanyia kazi malengo yako.
Soma pia: Tabia 10 zitakazobadili maisha yako.
9. Kuishi bila malengo
Watu wengi hawana malengo wala hawafahamu maana na umuhimu wa malengo katika maisha yao. Malengo hukuwezesha kuona kituo au fikio fulani la baadaye katika maisha yako. Jiulize leo una malengo?
Je unafanya jitihada kuyafikia? Kama jibu ni hapana, hakika itakuwa ni vigumu sana kwa wewe kufanikiwa. Badili fikra zako sasa, jiwekee malengo na uyafuate
Soma pia: Faida 10 za Kuwa na Malengo Maishani.
10. Kukata tamaa
Ni kweli kuwa changamoto zipo kila siku kwenye maisha yetu, lakini hatutakiwi tuziruhusu zitukatishe tamaa. Inawezekana umekaribia kabisa kufika kwenye mafanikio lakini kutokana na upepo na mawimbi mengi katika njia yako unaamua kuacha na kurudi nyuma.
Nikutie moyo kuwa inuka fanya bidii bila kujali mawimbi na upepo nawe utayaona matunda ya jasho lako ndani ya muda mfupi.
Soma pia: Tabia 10 Unazotakiwa Kijifunza Kutoka kwa Watu Waliofanikiwa.
Mwisho
Nikutie moyo na kukuhamasisha kufanya bidii kadri uwezavyo ili kuyafikia mafanikio. Jitahidi kuziambia fikra zako kuwa unaweza, pia jifunze kwa wale waliofanikiwa. Kila jambo linawezekana chini ya jua, ni wewe tu kuchukua hatua sahihi na kwa wakati sahihi.
Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazo Kuhamasisha Maishani Mwako.
Je una swali au maoni yoyote? Tafadhali tuandikie maoni yako hapo chini, pia karibu uwashirikishe na wengine maarifa haya.
Eston ni mtafiti na mwandishi wa makala mbalimbali zinazohusu tija, maendeleo binafsi pamoja na afya bora. Analenga kuwahamasisha wengine pamoja na kuubadili ulimwengu kwa kupitia maarifa stahiki.
Natamani sana kupata kitabu chenu
Nashukuru sana kwa kutembelea blog yetu ya Fahamuhili; tunashukuru pia kwa maoni yako mazuri. Naahidi kufanyia kazi pendekezo lako.
Nimejifunza na nimebaini nini kikwazo Cha mafanikio yangu
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Kitu kizuri sana hiki na kinatupa mwanga jinsi ya kufanya vizuri zaidi
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Hakika nimejifunza kitu kikubwa
Ila Kama Kuna group lenu mungeniunga0759202142
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Asant sana
Asanten
Mimi kwa Sasa Ni mwanafunzi nasoma chuo Ila nafatilia nakala mbalimbali ili kujua Mambo ya kufanya na kufanikiwa.. Je naweza kufanya biashara nikiwa nasoma?
Bila shaka unaweza kufanya biashara ukiwa unasoma. Tufuatilie tutatoa makala kuhusu hilo. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
APO kweli umetugusa weng ngoja sasa tubadilike
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com