Kwanini ni muhimu kunywa maji?
Miili yetu inaundwa na asilimia 70 ya maji, hivyo ni muhimu kunywa maji ya kutosha ili kuufanya mwili kufanya kazi vyema. Iwapo mwili wako haupati maji ya kutosha, hali hii inaweza kusababisha madhara mbalimbali ya muda mfupi na muda mrefu kama vile magonjwa ya shinikizo la damu, saratani pamoja na magonjwa ya figo.
Ninawezaje kutumia maji kama tiba?
Unaweza kutumia maji kama tiba ya matatizo mbalimbali kwa kufanya haya yafuatayo:
- Kunywa takriban Mililita 160 za maji kabla ya kuswaki au kula chochote mara tu unapoamka.
- Kunywa maji angalau dakika 30 kabla ya kula, lakini si ndani ya dakika 45 baada ya kifungua kinywa, chakula cha mchana au chakula cha jioni.
- Kama huwezi kunywa angalau bilauri 4 za maji basi anza na moja kisha ongeza taratibu kadri mwili wako unavyomudu.
Karibu ufahamu faida 8 za msingi za kunywa maji kabla ya kula chochote unapoamka.
1. Huondoa sumu mwilini
Unywaji wa maji mengi husaidia kuondoa sumu mwilini kwani huwezesha viungo kama vile figo kufanya kazi yake vyema. Unapokunywa maji kabla ya kula chochote asubuhi utauwezesha mwili wako pia kujenga misuli na kuzalisha seli mpya za damu.
Soma pia: Njia 12 za Kuondoa Sumu Mwilini.
2. Huboresha metaboli
Metaboli ni mchakato ambao mwilli hutumia vyakula (wanga, protini na mafuta) ili kupata nguvu na kujijenga. Hivyo basi, unywaji wa maji huwezesha mchakato huu kwenda vyema na kuufanya mwili kuwa na afya njema.
Kunywa maji kabla ya kula chochote unapoamka huufanya utumbo kuwa tayari kufyonza virutubisho. Kumbuka, maji ni muhimu kwa ajili ya watoto na watu wazima pia.
3. Husaidia kupunguza uzito
Wapo watu wanaopenda kupunguza uzito wa miili yao kwani uzito mkubwa si jambo zuri kiafya. Yakupasa kukumbuka kuwa unapoamka na kuanza kutumia vinywaji kama vile soda na juisi (sharubati) vitachangia sana kuongeza uzito wako wa mwili.
Utafiti unaonyesha kuwa soda ina sukari gramu 35 na gramu 140 za kalori ikilinganisha na maji ambayo vyote ni sifuri. Hivyo basi, ni vyema ukapendelea kunywa maji zaidi kuliko vinywaji vingine.
4. Huondoa kiungulia na matatizo ya umeng’enyaji wa chakula
Kunywa maji kutakusaidia kuzimua asidi inayopatikana tumboni ambayo ndiyo hupelekea tatizo la kiungulia. Sanjari na hayo unywaji wa maji utarahisisha na kuhimiza mchakato mzima wa umeng’enywaji wa chakula.
Hivyo basi, kama unakabiliwa na matatizo haya ni vyema kuzingatia unywaji wa maji kabla ya kutumia dawa mbalimbali.
5. Huboresha na kuimarisha ngozi
Utafiti unaonyesha kuwa kunywa maji takriban mililita 500 kunarahisisha mzunguko mzuri wa damu katika ngozi. Hivyo basi, hili hupelekea kuondoa sumu mbalimbali katika ngozi na kuiacha ngozi yako katika hali nzuri kiafya.
Soma pia: Faida 10 za Kunywa Maziwa Usizozifahamu.
6. Huhamasisha ukuaji wa nywele bora zenye afya
Upungufu wa maji mwilini una madhara makubwa sana kwa afya yako. Utafiti unaonyesha kuwa ÂĽ ya uzito wa nywele zako ni maji. Hivyo kutokunywa maji yakutosha kutakufanya kuwa na ukuaji duni wa nywele; pia kutafanya nywele zako kuwa dhaifu.
Kwa ajili ya afya na mwonekano bora wa nywele zako jidahidi kunywa maji yakutosha hasa unapoamka asubuhi.
7. Huzuia mawe kwenye figo
Unywaji wa maji huzimua asidi inayosababisha mawe kwenye figo ambayo hupatikana tumboni. Unywaji wa maji ya kutosha kutakuepusha kwa kiasi kikubwa na matatizo ya figo. Ili kurahisisha utendaji kazi wa figo zako pamoja na afya yake, zingatia kunywa maji ya kutosha hasa asubuhi.
Soma pia: Rangi 11 za Mkojo na Maana Zake Kwenye Mwili wako.
8. Huongeza kinga ya mwili
Kujijenga kwa kinga mwili hutegemea sana maji katika mwili wako. Hivyo ni vyema kuhakikisha unaongeza kinga ya wili wako kwa kunywa maji ya kutosha hasa kabla ya kula kitu chochote.
Neno la mwisho
Ninakuhimiza kujenga utamaduni wa kujali na kulinda afya yako ili uweze kuwa mtu mwenye mafanikio zaidi. Tumeona swala la unywaji wa maji lilivyo na umuhimu; swala hili ni wewe kuamua tu kulifanyia kazi kwani halina gharama yoyote.
Je wewe huwa unakunywa maji? Kiasi gani na saa ngapi? Tupe maoni yako kisha washirikishe wengine makala hii. Karibu pia ulike ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.
Eston ni mtafiti na mwandishi wa makala mbalimbali zinazohusu tija, maendeleo binafsi pamoja na afya bora. Analenga kuwahamasisha wengine pamoja na kuubadili ulimwengu kwa kupitia maarifa stahiki.
Thanks so much indeed I have learned alot
Asante sana; karibu tena Fahamuhili.com
Nimependa makala zenu ni nzuri na zinaelimisha iwapo mtu ataamua kuzifatilia kwa umakini mzuri Asanteni sana kwa elimu nzuri
Swali Kunywa maji wakati wa asubuhi ni lazima uwe ujasukutua tu
Au hata ukiwa umeishasukutua nayo ni nzuri? naomba jibu
Nashukuru sana kwa kutembelea blog yetu ya Fahamuhili; tunashukuru pia kwa maoni yako mazuri. Jambo muhimu ni kuzingatia kunywa maji ya kutosha asubuhi: haijalishi ni baada ya kusukutua au la. Karibu sana Fahamuhili.com
Asante san kwa nakala nzuri cha kuongezea ni kuwa tunashauliwa kabla ya kulala tupige mswaki kisha asubuh kabla ya kupiga mswaki tunywe maji kwani bacteria wanaokuw kinywani muda uo wanafaida mwilini na kusaidia kutibu maradhi kama malaria nk shukran
asanteni sana kwa kutuelimisha
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Maji ni muhimu sana ndomana Mungu amesema katika Kitibu chake kitakatifu Qur an. Amejaalia kutojana na maji uhai.
Nashukuru sana
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Nimeelewa sana unywaji wa maji ingawa watu hulipuuza
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Samahani nauliza hayo ya kunywa Asb je yanatakiwa yawe uvuguvugu au ya kawaida
Tofauti yake ni ndogo kimatokeo; bali nafasi ya maji ni ile ile ndugu; kunywa aina ile ambayo unaona inakupendeza zaidi. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Naitaj kujua maji hayo ambayo tunatakiwa kunywa ni ya moto au baridi
Yale ambayo unaona unapendezwa nayo, nafasi ya maji mwilini ni ile ile. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
tupemegine mengi utusaidie
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Makala nimeipenda kwa kweli
Asante sana kwa maoni yako ya thamani kwetu; karibu sana Fahamuhili.com
Asante sana kwa uponyaji!
Utukufu kwa Mungu; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
mi huwa nakunywa maji takribani lita moja na nusu kwa siku
Hongera sana; Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Mimi nakunywa maji asubuhi nikisha swali kabla ya kula kitu, nakua nakunywa glasi 2 tu.
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Asante nilikuwa na hofu Kwa sababu Mimi nanywa maji.mingi
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Samahani nataka kuuliza unaweza kunywa maji asubuhi ukachanganya na limao? Je, kuna madhara yoyote kiafya na pia kuna faida gani kiafya.
Asante sana kwa kutupatia mambo muhimu kama hayo
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
Takribani nina siku4 nimeanza kunywa maji, ila siku zote nilikua nakunywa nusu lita ila leo ndio nimekunywa lita moja
Nikaona vyema niingie mtandaoni kujua zaidi faida za kunywa maji
Kifupi mko vizuli na maeleweka na mungu awabariki sana
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Hallow nina swali hapa, nini kinacho sababisha joto kali sana baada ya kunywa pombe kali kesho yake asubuhi na kuendelea.