Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 13 of 17
Friday, March 27Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Makosa 8 ya Kuepuka Kabla na Wakati wa Kujenga Nyumba

Makosa 8 ya Kuepuka Kabla na Wakati wa Kujenga Nyumba

Nyumba na Makazi
Nyumba ni hitaji muhimu kwa watu wote. Kila mmoja anatamani na ana ndoto za kununua au kujenga nyumba nzuri na ya kisasa. Ni kweli kuwa ujenzi wa nyumba unahitaji rasilimali nyingi hasa fedha. Pamoja na gharama hizi za ujenzi wa nyumba bado watu wengi wamekuwa wakishindwa kupata nyumba nzuri huku wakiwa tayari wamepoteza kiasi kikubwa cha pesa. Ni wazi kuwa yapo makosa mbalimbali yanayosababisha hali hii yakiwemo yale ya ukosefu wa elimu pamoja na uzembe wa aina mbalimbali. Karibu ufuatilie makala hii ili uweze kufahamu makosa 8 unayoweza kuyaepuka wakati wa kujenga nyumba ili hatimaye uwe na nyumba bora. 1. Kutozingatia kanuni za kununua kiwanja Watu wengi hawafahamu mambo muhimu ya kuzingatia wakati wanaponunua kiwanja. Hivyo hujikuta wakiingia katika matatizo mbalimbali kama vile ku...
Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Kiwanja au Ardhi

Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Kiwanja au Ardhi

Nyumba na Makazi
Ardhi ni rasilimali muhimu ambayo kila mtu anaihitaji kwa namna moja au nyingine. Watu wengi hununua ardhi kwa ajili ya kufanyia shughuli mbalimbali kama vile ujenzi na kilimo. Pamoja na umuhimu huu mkubwa wa ardhi bado watu wengi wanakumbana na changamoto mbalimbali katika maswala yanayohusu kununua na kumiliki ardhi. Wengi hujikuta wakinyang’anywa ardhi zao, kuharibiwa mali, au wakiingia kwenye migogoro mikubwa ya kisheria. Ni wazi kuwa zipo sababu mbalimbali zinazosababisha matatizo haya. Fuatilia makala hii kwa makini ili uweze kufahamu mambo 10 ambayo unapaswa kuyazingatia kabla ya kununua kiwanja au ardhi. 1. Ona kiwanja husika mwenyewe Ni vyema ukafika kwenye eneo la kiwanja husika na kukiona wewe mwenyewe kama kinakuridhisha na kukufaa kwa mahitaji yako. Fahamu mipaka, na ...
Mambo 10 ya Kujifunza Kutoka Kwenye Maisha ya Watoto

Mambo 10 ya Kujifunza Kutoka Kwenye Maisha ya Watoto

Maendeleo Binafsi
Ingawa watu wengine huwachukulia watoto kama watu wasiofaa, watoto ni malaika wa kweli wanaoweza kutufundisha jinsi ya kuishi maisha mazuri. Ingawa wakati mwingine hawatambui wanachokuwa wakikifanya, lakini wanatupa nafasi ya kujifunza vitu vingi ambavyo tunavisahau tunapokuwa watu wazima. Kuna sababu ya kwanini watoto wanaitwa zawadi kutoka kwa Mungu. Wanatufundisha kuboresha maisha yetu, kuona vitu vizuri kwenye maisha pamoja na kujaa tabasamu kila siku. Ni wazi kuwa yapo mambo mengi mazuri na yenye manufaa makubwa ambayo kila mtu anaweza kujifunza kutoka kwa watoto; yafahamu mambo hayo sasa. 1. Kuwa na furaha Maisha ya watoto yamejaa furaha. Mara nyingi utawakuta watoto wakiimba, wakikimbia, wakiruka, wakitaniana kwa furaha bila wasiwasi. Hili limefanya maisha ya utoto kuwa saw...
Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Njia 14 Halali za Kupata Pesa Kupitia Blog

Kipato, Tovuti na Blogu
Je unatafuta njia ya kujipatia pesa kwenye mtandao ambayo siyo ya utapeli? Blog ni njia moja wapo unayoweza kuitumia kujipatia fedha huku ukifanya kile ukipendacho. Katika makala hii nitakushirikisha njia 14 unazoweza kuzitumia kupata pesa kwa kutumia blog yako. Kumbuka! Hizi si njia za kupata pesa za mteremko haraka haraka kwa usiku mmoja. Kamwe usidanganywe na matangazo ya kuwa utafanywa kuwa tajiri mkubwa siku moja. Mambo hayaendi hivyo. Awali ya yote utahitaji kuwa na blog yako; pia utahitajika kuwekeza rasilimali ya muda au pesa kiasi fulani ili kuweza kuona matokeo kutokana na blog yako. 1. Kuwa wakala Unaweza kupata pesa kwenye blog yako kwa njia ya kuwa wakala wa wauzaji wa bidhaa au huduma mbalimbali. Mara mtu anunuapo kitu kwa kukifikia kupitia blog yako basi utapata ...
Mambo 12 ya Kufanya kwa Ajili ya Kesho Yako

Mambo 12 ya Kufanya kwa Ajili ya Kesho Yako

Maendeleo Binafsi
Ni mara ngapi umejiambia kuwa kesho itakuwa siku nzuri na unatamani kuiona na kuiishi? Ni mara chache sana. Hofu na mashaka vimetawala na kuchukua nafasi katika kesho za watu wengi. Jambo zuri kwenye maisha ni kuwa una nafasi ya kutawala mambo mengi yanayotokea katika maisha yako. Kama kesho inafanana na leo hakuna maana; ikiwa leo ulikuwa na huzuni basi angalau kesho iwe na furaha. Hivyo kuna mambo ambayo unaweza kuyafanya leo na kuhakikisha kuwa kesho inakuwa nzuri. Hapa kuna mambo 12 ambayo unayoweza kuyafanya na kuifanya kesho yako kuwa nzuri na yenye tija. 1. Panga kwa ajili ya kesho. George anatukumbusha  kuwa maandalizi bora ya kesho hufanywa leo. Kuwa na mpango wa kesho leo kutakuwezesha kufanya mambo kwa kutegemea mwongozo na mpangilio uliopo badala ya kuamka na kufan...
Vitu 15 Vinavyofanywa na Watu Werevu (Smart)

Vitu 15 Vinavyofanywa na Watu Werevu (Smart)

Tija
Unaweza kujiuliza ni mambo gani yanayomfanya mtu kuwa mwerevu (smart). Je ni wingi wa maarifa anayoyafahamu? Au je ni kiwango cha wastani au cha juu cha kufikiri kwake? Ukweli ni kuwa ni werevu ni uwezo wa kufanya maamuzi yatakayofaa wakati wote; au ni kuweza kuibua kitu kizuri katika kitu kibaya au wakati mbaya. Watu werevu huweza kufanya maamuzi ambayo yanazingatia matokeo ya mbeleni ya maamuzi hayo. Ni dhahiri kuwa watu werevu (smart) ni tofauti na watu wengine kutokana na yale wanayoyafanya au kutofanya. Fahamu mambo 10 ambayo watu werevu hawayafanyi. 1. Hawapuuzi uwekaji akiba Katika maisha ya kiuchumi kuna vipindi viwili; kipindi cha mavuno(shibe) na kipindi cha ukame(njaa). Ni watu wachache sana ndio wanaoweza kuishi katika vipindi hivi viwili bila shida. Watu werevu hawapu...
Mambo 10 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Lionel Messi

Mambo 10 Unayoweza Kujifunza Kutoka kwa Lionel Messi

Hamasa
Lionel Messi alizaliwa tarehe 24 Juni 1987 huko Rosario, Jimbo la Santa Fe huko Argentina. Akiwa na miaka mitano Messi alianza kucheza mpira wa miguu kwenye klabu ya Grandol iliyokuwa ikifundishwa na baba yake. Wakati Messi akiwa mdogo, alibainika kuwa na tatizo au maradhi ya kuwa na upungufu wa seli za ukuaji. Akiwa na umri wa miaka 13 alihamia Uhispania na kujiunga na klabu ya Barcelona ambayo ilikubali kugharamia matibabu yake. Pamoja na changamoto alizokuwa nazo Messi amefanikiwa kupata mafanikio makubwa sana. Messi anachukuliwa kama mchezaji bora zaidi duniani na mmoja kati ya wachezaji bora waliowahi kuwepo. Messi ni mchezaji pekee aliyeshinda tuzo ya FIFA ya Ballon d'Or  mara tano, zikiwemo nne mfulilizo. Pia ni mchezaji pekee aliyeshinda tuzo ya kiatu cha dhahabu (European Gol...
Sababu 9 za Kwanini Umsamehe Aliyekukosea

Sababu 9 za Kwanini Umsamehe Aliyekukosea

Maendeleo Binafsi
Umesikia mara nyingi sana kuwa “Unatakiwa kusamehe na kusahau”. Nini maana halisi ya kusamehe? Kusamehe ni kuamua kutomchukulia mtu hatua na kuondoa kinyongo moyoni mwako kutokana na jambo baya ulilofanyiwa na mtu huyo. Kusamehe kunasema hutakiwi kusikia neno “nisamehe” ndipo uendelee na maisha yako. Kusamehe kumewekwa na ni kwa manufaa zaidi kwa yule aliyekosewa. Ni wazi kuwa katika maisha kuna kukoseana kwa namna mbalimbali. Wapo watu wasiopenda suluhu wala msamaha. Ni dhahiri kuwa ni lazima wewe uliyekosea ufahamu manufaa na sababu za kumsamehe na kumsahau aliyekukosea; manufaa hayo ni haya yafuatayo. 1. Hukuweka huru Kutokusamehe kunakufanya ujisikie vibaya na kuwa kama mfungwa. Jambo baya ni pale utakapomwona yule aliyekukosea anafuraha na anaendelea na maisha yake bila ta...
Mambo 15 ya Kushangaza Kuhusu Afrika

Mambo 15 ya Kushangaza Kuhusu Afrika

Maarifa
Vita, njaa, vifo, maradhi - ni vitu ambavyo wengi wamevisikia na kuvifahamu kuhusu Afrika. Lakini sasa ni wakati wa kubadili mtazamo huu. Afrika ni bara la kushangaza ambalo ni tofauti kabisa na mabara mengine saba. Afrika ina utajiri katika urithi wa utamaduni wa kipekee, utajiri wa rasilimali za asili pamoja na vivutio mbalimbali vya utalii. Nakukaribisha ufuatilie makala hii ili uweze kufahamu mambo 15 ya kushangaza na kusisimua kuhusu Afrika. Mlima Kilimanjaro unapatikana barani Afrika. Mlima huu una urefu wa takriban meta 5,895 kutoka usawa wa bahari. Mlima huu unapatikana kaskazini mwa Tanzania. Zaidi la asilimia 25 ya lugha huzungumzwa Afrika. Inaaminika kuwa kuna takriban lugha 2000 zinazozungumzwa barani Afrika. Lugha zote hizi zinatambuliwa na umoja wa Afrika. Nigeri...
Namna ya Kuwa Mzungumzaji Hamasa (Motivational Speaker)

Namna ya Kuwa Mzungumzaji Hamasa (Motivational Speaker)

Maendeleo Binafsi
Ninapotaja wazungumzaji hamasa (Motivational Speakers) naamini unafahamu kuwa ni watu wanaowasaidia watu kuendeleza na kuwezesha maono au utoto wao wa ndani ili watu husika waweze kufanikiwa. Mzungumzaji hamasa anaweza kuzungumzia mada yoyote ile kulingana na uzoefu wake. Wengi hutamani kuwa wazungumzaji hamasa lakini wameshindwa kujua waanzie wapi. Jambo la msingi katika uzungumzaji hamasa ni shauku yako ya ndani katika mada unayotaka kuizungumzia. Kuwa mzungumzaji hamasa kunahitaji kubaini mada na walengwa wa mada yako bila kusahau kunoa uwezo wako wa kuzungumza mbele ya watu pamoja na kuielewa vyema mada husika. Kama unatamani kuwa mzungumzaji hamasa, fuatilia hoja jadiliwa hapa chini kwa makini ili sasa uweze kuwa mzungumzaji hamasa. 1. Bainisha mada utakayozungumzia Huwezi ku...