Fahamu Hili Archives - Page 17 of 20 - Fahamu Hili
Wednesday, March 18Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Podcast: Fahamu Hili

Njia 10 za Kujenga Uwezo wa Kuzungumza Mbele ya Watu

Njia 10 za Kujenga Uwezo wa Kuzungumza Mbele ya Watu

Maendeleo Binafsi
Kuzungumza mbele ya watu kunaweza kuwa ni tatizo ikiwa hujiamini au hujajiandaa vyema. Hata hivyo, mazoezi na mtazamo chanya vinaweza kukusaidia kuwa mzungumzaji bora mbele ya watu. Ikiwa unazungumza katika mazingira ya kitaaluma au katika mazingira ya kijamii, tumia njia hizi 10 ili kuboresha uwezo wako vya kuzungumza mbele ya watu. Kumbuka, kuzungumza mbele ya watu kunahusisha kuandaa, kufikiria na kutenda kwa ujasiri, huku ukizingatia sauti yako na lugha ya mwili (body language). 1. Jiandae na fanya mazoezi Watu wengi wamekuwa wakikumbwa na hofu, wasiwasi na hata kutokwa na jasho sana wanapokuwa wanazungumza mbele za watu. Hii inatokana na kuwa na uzoefu mdogo unaoletwa na kutofanya mazoezi ya kutosha ya kuzungumza mbele ya watu. Jitahidi kufanya mazoezi ya kuzungumza mbele za ...
Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Afya
Siyo siri kuwa pombe husababisha matatizo makuwa ya kiafya, yakiwemo magonjwa ya moyo, ini pamoja na majeraha yatokanayo na ajali zitokanazo na ulevi. Ni dhahiri kuwa vinywaji halisi vilivyotengenezwa kwa matunda bila kilevi ni bora zaidi kwa afya yako kuliko vile vyenye kilevi. Licha ya kuwepo kwa kampeni kadha wa kadha zinazopinga matumizi ya pombe, bado watu wengi wameendelea kushikilia kinywaji hiki bila kufahamu athari zake kwenye afya zao. Fuatilia hapa chini athari 12 za pombe kiafya. 1. Matatizo ya moyo Unywaji mkubwa wa pombe husababisha  matatizo mbalimbali ya moyo kama vile cardiomyopathy, ambapo mishipa ya moyo hudhoofika na kushindwa kusukuma damu. Jambo hili huweza kusababisha damu kuganda na kusababisha kiharusi (stroke). Pombe huchangia sana katika kudhoofisha mish...
Faida 9 za Kusikiliza Mziki

Faida 9 za Kusikiliza Mziki

Mtindo wa Maisha
Kama unapenda kusikiliza mziki basi uko kwenye kundi zuri. Watu mbalimbali maarufu wamewahi kutoa maoni yao kuhusu mziki kama vile mwanabayolojia Charles Darwin aliyesema kuwa angepewa nafasi ya kushi tena angetengeneza kanuni ya kusoma mashairi na kusikiliza mziki angalau mara moja kwa wiki. Kwa upande mwingine Albert Einstein alikiri kuwa asingekuwa mwanafizikia basi angekuwa mwanamziki. Tafiti zinabainisha kuwa kusikiliza mziki kuna manufaa mengi kwa ajili ya afya ya mwili na akili. Tafadhali fuatana nami katika makala hii ili nikujuze faida 9 za kusikiliza mziki. 1. Mziki hutufanya tuwe na furaha William James alsisema “Siimbi kwa sababu ninafuraha, bali nafurahi kwa kuwa ninaimba” . Kusikiliza mziki huzalisha kemikali ya dopamane ambayo hutufanya tujisikie vizuri. Hii ndiy...
Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Mambo 5 ya Kujifunza Kutoka kwa Reginald Mengi

Hamasa
Kwa mijibu wa jarida la Forbes linaeleza kuwa Reginald Mengi ni miongoni mwa watu maarufu katika tasnia ya habari kupitia kampuni yake ya IPP; ambayo ni moja kati ya kampuni kubwa za habari Afrika. Kampuni yake ya IPP ina magazeti 11 na vituo kadhaa vya televisheni pamoja na vyanzo mabalimbali vya kwenye mtandao. Mengi pia anamiliki kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers, ambayo ni kampuni pekee inayozalisha vinywaji vya jamii ya Coca-Cola kwa kanda ya kaskazini mwa Tanzania. Pia anazalisha maji ya Kilimanjaro yaliyojizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania. Mengi anajihusisha pia na uchimbaji wa madini kupitia kampuni yake ya IPP Resources yenye kampuni tanzu kadhaa. Reginald Mengi pia mekuwa akitoa misaada mbalimbali kusaidia makundi ya watoto, vijana, wanawake, wazee, ...
Aina 8 za Watu Ambazo ni Sumu za Kuepuka Maishani Mwako

Aina 8 za Watu Ambazo ni Sumu za Kuepuka Maishani Mwako

Tija
Watu wasiofaa wapo kila mahali, kwa hakika wanakwaza na kurudisha maendeleo ya watu nyuma. Ukiwa kama mjasiriamali au mtu mwingine yeyote unatakiwa kufanya bidii kufikia malengo yako bila kuruhusu aina za watu wasiofaa kukuvuruga. Inawezekana unawafahamu watu ambao ni sumu; yawezekana wanafanya kazi na wewe, ni marafiki zako au unaishi nao. Kadri unavyowaepuka katika maisha au kazi yako ndivyo mambo yatakavyozidi kuwa mazuri. Fuatana nami katika makala hii nikushirikishe aina 8 za watu ambazo ni sumu unazotakiwa kuziepuka katika maisha yako. 1. Watu wanaohoji kila kitu Watu wanaohoji kila kitu hutafuta njia ya kupinga na kukosoa kila unachokifanya. Utatumia muda mwingi kuwaelewesha lakini watasikia kwa sikio moja na swala hilo kutokea sikio la pili. Kujaribu kutafuta msaada na ...
Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Njia 8 za Kuokoa Mafuta Unapoendesha Gari

Tija, Usafiri na Safari
Ni wazi kuwa gari linahitaji mafuta ili kusafiri toka sehemu moja hadi nyingine. Lakini swali ni je, unaweza kutawala kiwango cha mafuta kinachotumika? Ndiyo, unawea kutawana kiwango cha mafuta na kupunguza garama za matumizi ya mafuta zisizokuwa na ulazima. Kama unapenda kuokoa kiasi cha mafuta yanayopotea bila sababu ya msingi katika gari lako, basi tumia njia hizi 8 zifuatazo. 1. Kabili upepo Unapoendesha gari upepo hukinzana na gari; hivyo kadri gari linavyokinzana zaidi na upepo ndiyo pia unavyotumia mafuta mengi zaidi. Hivyo basi, usipende kuweka mizigo juu ya gari kwa nje (carrier) au kufungua vioo kwani kutasabisha ukinzani zaidi kati ya gari na upepo. Kwa kukabili upepo vyema utapunguza ukinzani na kuokoa mafuta ambayo yangetumika kukabili ukinzani huo wa upepo. 2. Pu...
Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Teknolojia
Katika ulimwengu wa leo nywila au password si jambo geni. Mara kadhaa umeona au kutumia password katika vitu na maendeo kadhaa kama vile benki, simu, kompyuta n.k. Jambo la kushangaza ni jinsi watu wanavyotumia nywila bila kujali umuhimu wake katika eneo husika. Mtazamo wa ujumla juu ya nywila (password) Nywila ni ufunguo wa kufungua na kufunga sehemu husika; hivyo aliye nao ndiye atakayeweza kufungua na kufunga. Nywila ngumu = usalama zaidi; nywila rahisi = uslama kidogo. Mhalifu anaweza kutumia nywila kufanya uhalifu. Hivyo basi ni muhimu kufahamu namna ya kutengeneza nywila imara na salama kwa ajili ya kifaa au akaunti yako. Fuatilia makala hii ili uweze kujifunza mambo kadhaa ya kufanya ili kutengeneza nywila imara. 1. Epuka namba na maneno rahisi Wengi wetu hatu...
Faida 7 za Kula Mayai Wakati wa Kifungua Kinywa

Faida 7 za Kula Mayai Wakati wa Kifungua Kinywa

Mtindo wa Maisha
Mayai ni kitu kilichozoeleka na kinachopatikana kwa gharama nafuu. Kutokana na kuzoeleka huku watu wengi wamekuwa wakipuuza umuhimu au nafasi ya mayai katika afya zao. Pengine kupuuza huku kunatokana na mazoea au ukosefu wa elimu juu ya faida zinazopatikana kutokana na ulaji wa mayai. Fuatana nami katika makala hii ili nikueleze faida 7 za kula mayai wakati wa kifungua kinywa. 1. Hutunza shibe Protini zilizoko ndani ya mayai hukufanya kutohisi njaa mapema. Ina maana kuwa ukila mayai unaweza kukaa muda marefu zaidi bila kula ikilinganishwa na mikate au vyakula vingine vya ngano. 2. Husaidia kupunguza uzito Ulaji wa mayai husadia kupunguza uzito wa mwili. Utafiti uliofanyika umeonyesha kuwa watu wanaokula mayai wamefanikiwa kupunguza uzito wa miili yao kwa kiasi kikubwa ikilingani...
Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Panasonic Waja na Teknolojia ya Kumzuia Dereva Kusinzia

Teknolojia
Shughuli nyingi pamoja na kubadilika kwa mtindo wa maisha kumewafanya madereva wengi kusinzia wakati wanaendesha magari. Kusinzia wakati wa kuendesha gari kunaweza kusababisha madhara makubwa. Inashauriwa kuwa unapojisikia kuchoka ni vyema ukapumzika. Panasonic wanaamini kuwa wana utatuzi: kwa kutumia akili bandia (Artificial inteligence) wanaweza kumfanya dereva awe macho wakati wote. Kwa mujibu wa Panasonic kuna aina tano za kusinzia: kutosinzia, kusinzia kidogo, kusinzia halisi, kusinzia sana na kusinzia kulikopitiliza. Kampuni hii ya Kijapani imegundua mfumo wa kwenye magari unaoweza kutambua kusinzia kwa dereva na kupambana nako kabla ya kutokea. Mfumo huu humfwatilia dereva kwa kutumia kamera na vihisi (sensors). Mfumo huu unaweza kutambua mambo kama vile kupepesa macho,...
Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Mambo 5 Yanayosababisha Biashara za Wanawake Kufa

Biashara na Uchumi, Ujasiriamali
Hivi leo wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika kuwahi na kufanyia kazi fursa mbalimbali. Fursa hizo ni pamoja na uwekezaji katika biashara ndogo na za kati. Ni dhahiri kuwa mama ndiye nayeumia zaidi pale familia inapokuwa na uchumi mbaya. Mama hapendi kuona watoto wanakosa mahitaji yao ya msingi kama vile chakula, mavazi, elimu, matibabu n.k. Hivyo suala la kuboresha kipato cha familia limewafanya wanawake wengi kutafuta njia mbalimbali za kujipatia kipato ikiwemo njia ya kufanya biashara. Hata hivyo pamoja na jitihada hizi zinazofanywa na wanawake, bado biashara zao ngingi hufa kutokana na sababu kadha wa kadha. Fuatana nami katika makala hii ufahamu mambo matano yanayosababisha biashara nyingi za wanawake kufa. 1. Kukosa maarifa na elimu ya biashara Kitu chochote au kazi y...