Kuzungumza mbele ya watu kunaweza kuwa ni tatizo ikiwa hujiamini au hujajiandaa vyema. Hata hivyo, mazoezi na mtazamo chanya vinaweza kukusaidia kuwa mzungumzaji bora mbele ya watu. Ikiwa unazungumza katika mazingira ya kitaaluma au katika mazingira ya kijamii, tumia njia hizi 10 ili kuboresha uwezo wako vya kuzungumza mbele ya watu. Kumbuka, kuzungumza mbele ya watu kunahusisha kuandaa, kufikiria na kutenda kwa ujasiri, huku ukizingatia sauti yako na lugha ya mwili (body language).
1. Jiandae na fanya mazoezi
Watu wengi wamekuwa wakikumbwa na hofu, wasiwasi na hata kutokwa na jasho sana wanapokuwa wanazungumza mbele za watu. Hii inatokana na kuwa na uzoefu mdogo unaoletwa na kutofanya mazoezi ya kutosha ya kuzungumza mbele ya watu.
Jitahidi kufanya mazoezi ya kuzungumza mbele za watu kwa kutumia njia zifuatazo:
- Zungumza mbele ya familia au marafi zako mara kwa mara kwa ujasiri.
- Unaweza kusimama mbele ya kioo chumbani na kufanya mazoezi ya kuzungumzia jambo fulani.
- Toa michango katika warsha, mikutano na makongamano mbalimbali.
- Sikiliza na tazama wazungumzaji waliobobea.
Ni dhahiri kuwa ukizingatia haya ndani ya muda mfupi utaweza kuboresha kiwango chako cha kuzungumza mbele ya watu.
2. Elewa hadhira yako
Kuelewa hadhira yako ni jambo muhimu litakalokuwezesha kufahamu mambo mbalimbali kama vile lugha, mahitaji, mifano na hata maudhui yatakayowasilishwa.
Mambo ya kuzingatia:
- Jinsia
- Umri
- Elimu
- Imani
- Hali ya uchumi n.k.
Mambo haya ni muhimu kwani yatakuwezesha kutengeneza hotuba au mazungumzo yanayowalenga wahusika zaidi. Kwa mfano unapozungumza na wanawake ni vyema ukagusa zaidi mambo yanayowahusu. Pia unapozungumza na watu wa imani au mtazamo fulani ni vyema ukazungumza kwa namna ambayo haitaathiri imani au msimamo wao. Hiyo, ni muhimu sana kuifahamu hadhira yako vyema.
3. Pangilia utakachozungumza
Ufanisi katika kuzungumza mbele za watu unahitaji kujiandaa na kupangailia vyema vile utakayoyazungumza. Epuka fikra za mimi nimezoea kazi hii au nalifahamu sana swala hili. Jizoeze kutengeneza mpangilio mzuri wa hotuba au mada utakayoizungumzia. Pia kumbuka kuandaa mada yako kwa njia ambayo inavutia wasikilizaji na unayoweza kuifuata.
4. Pokea mrejesho na uufanyie kazi
Kipimo cha ubora wako kipo na kinatokana na wasikilizaji au watazamaji wako. Hivyo ni muhimu kupokea mrejesho kutoka kwa hadhira yako na kuufanyia kazi. Ikiwa wasikilizaji au watazamaji wako watatoa mrejesho kama vile kusema unazungumza haraka sana au kwa sauti ya chini sana, basi jitahidi kuyafanyia kazi. Kwa kufanya hivi utarekebisha mapungufu yaliyojitokeza na wakati mwingine hayatatokea tena; hivyo utakuwa bora zaidi.
5. Kuwa mcheshi, tumia simulizi na lugha vyema
Ni vyema kama mtu unayezungumza mbele ya watu utajifunza kuwa mcheshi, kutumia simulizi na lugha vyema. Epeka kuwachosha wasikilizaji; wafanye wacheke na kufurahi; wasimulie jambo linaloendana na mada japo kwa ufupi ili wasichoshwe na mada yako na kuacha kukusikiliza. Pia zingatia lugha unayoitumia; hakikisha lugha unayoitumia inakupa uhuru wewe na wasililizaji wako; pia hakikisha unaimudu vyema lugha husika.
6. Usisome pekee
Watu wengine husoma tu badala ya kuzungumza mbele za watu. Haimaanishi kuwa ikiwa umeandika mada yako basi ndiyo ukaisome kama gazeti mbele ya watu. Jitahidi kuzungumza zaidi, tena ukitazama hadhira yako; tumia kile ulichoandika kama mwongozo pekee. Kumbuka, ukisoma badala ya kuzungumza utawafanya wasikilizaji kuchoshwa na kile unachokiwasilisha mbele yao.
7. Tumia sauti na mikono yako vyema
Kutokana na kukosa uzoefu pamoja na maandalizi duni watu wengi hujikuta wakipoteza sauti au kushindwa kutumia viungo vya mwili vyema kama vile mikono na mikao ya uso (Facial impresions). Kuzungumza mbele ya watu kunahitaji matumizi mazuri ya sauti pamoja na viungo kama vile mikono, kwani si jambo jema kusimama au kukaa kama roboti bila hata kujigusa wakati unazungumza mbele ya watu. Hivyo ni muhimu kuzingatia mambo haya ili uweze kujenga uwezo wa kuzungumza mbele ya watu.
8. Teka usikivu mwanzoni
Kuna usema usemi usemao “Nyota njema huonekana asubuhi”; ni dhahiri kuwa ukianza kuzungumza mbele ya watu vibaya ndivyo itakavyokuwa kwa mchakato mzima. Jitahidi kuteka usikivu wa hadhira yako mwanzoni ili wavutiwe kukuzikiliza na kukutazama muda wote unapozungumza.
9. Tumia vifaa sauti na picha vyema
Kuna wakati mwingine utahitajika kutumia vifaa kama vile vipazasauti au vifaa onyeshi kama vile projekta. Hakikisha unavimudu na umeviandaa vyema kabla ya kuvitumia katika kuzungumza kwako.
Mambo ya kukumbuka:
- Tazama kama kuna uhitaji wa kifaa husika na je, unaweza kukitumia kwa uhuru? Kwa mfano hakuna haja ya kutumia kipazasauti wakati una sauti ya kutosha na unazungumza na watu wachache tu kama vile 20.
- Hakikisha kifaa kinafanya kazi vyema na kinafaa kwa hadhira yako.
- Zingatia watu wenye mahitaji maalumu kama vile viziwi; vipofu, n.k
Kwa kufanya hivi utaweza kujenga uwezo wako wa kimaandalizi katika swala zima la kuzungumza mbele ya watu.
10. Shirikisha hadhira
Haimaanishi kuwa, kwa kuwa watu wamekaa ili kukusikiliza basi haihitajiki kuwashirikisha au kusikiliza hoja na mawazo yao. Hii ni njia bora itakayokuwezesha kuifahamu na kuimudu vyema hadhira yako.
Njia za kushirikisha hadhira:
- Uliza maswali pia ruhusu kuulizwa maswali
- Washirikishe katika majadiliano
- Pokea mapendekezo na maoni yao
Kwa kufanya hivi utavutia zaidi hadhira yako; pia utaweza kupata mambo kadha wa kadha kutoka kwa hadhira yako ambayo yatakuwezesha kuboresha uwezo wako zaidi.
Hitimisho
Zilizoelezewa hapa ni njia au mambo ambayo yatakuwezesha kuwa mzungumzaji mzuri au kukuongezea uwezo wa kuzungumza mbele ya watu. Tumeona kuwa maadhalizi na mazoezi ni mambo makuu muhimu katika kujenga uwezo wa kuzungumza mbele za watu. Jiamini, jiandae na fanya mazoezi nawe utaweza kuwa mazungumzaji bora kabisa mbele ya watu.
Je ungependa kuwa mzungumzaji bora mbele ya watu? Je uwezo wako umejengeka kutokana na njia hizi? Tuandikie maoni yako hapo chini kisha washirikishe wengine.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Ndio napenda kuwa mzungmzaj bora mbele ya watu nitazfata njia hiz
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
mimi ni mwalimu,public speaker na mjasiriamal changamoto yangu kubwa ni kukosa seminar, au makongamano ya kuongea unaweza kutazama kazi zangu youtube kwa jina la david john 27
Hongera sana. Anza na wale wanaokuzunguka kwanza, marafiki, ndugu, majirani, marafiki zako wa kwenye mitandao n.k. taratibu utafahamika na kuitwa kwingine. Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com
shukran sana bro nimependa san hili somo maana napenda sana kuwa mzungumzaji mzuri san kwahyo nataka kuzifanyia kazi hizi points zote ili niweze kuboresha uzungumzaji wangu mbele ya watu.asante san🙏
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
mimi naitwa Nick Charlz ni mtu nayependa kujifunza mambo mbalimbali na hasa kuzungumza mbele ya umati na kuiteka hadhira hivyo kutokana na njia 10 ulizoziainisha hapo juu , kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa elimu uliyoitoa kwani jambo hili kwangu limekuwa ni changamoto na kuanzia leo nitazifuata nakuahidi kukupa majibu ya nitakachokuwa nimekifanyia kazi
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com
Infact kuorganize stement mbele za wa watu….u can be very confident lakini ukafer kwenye kupangilia maneno