Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 9 of 17
Friday, March 27Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Makosa 15 ya Kuepuka Katika Malezi ya Watoto

Makosa 15 ya Kuepuka Katika Malezi ya Watoto

Mahusiano na Familia
Swala la malezi ya watoto ni swala nyeti, pana, gumu, na lenye changamoto nyingi; hivyo linahitaji umakini mkubwa na maarifa stahiki. Kutokana na umuhimu huu basi, ni wazi kuwa changamoto au matatizo mengi ya kimalezi yanayotokea kwenye maisha ya watoto yanatokana na makosa yanayofanywa na wazazi katika malezi. Pamoja na kwamba hakuna kanuni ya malezi, lakini yapo makosa ambayo wazazi wanapaswa kuyaepuka katika swala la malezi ili kuhakikisha watoto wao wanakuwa katika maadili na misingi sahihi. Karibu nikufahamishe makosa 15 ambayo kila mzazi au mlezi anatakiwa kuyaepuka katika malezi ya kilasiku ya watoto. 1. Kumfurahisha mtoto Kumfurahisha mtoto ni muhimu kufanywa na kila mzazi au mlezi, lakini ni lazima kuwe na kiasi. Wazazi wengi wamekuwa wakifanya kosa la kutaka kuwafa...
Njia 10 za Kukufanya Kuwa na Furaha

Njia 10 za Kukufanya Kuwa na Furaha

Tija
Kutokana na changamoto za kimazingira, kiuchumi na kijamii, watu wengi wamejikuta wakikosa furaha. Ni wazi kuwa kukosa furaha kuna madhara makubwa kwenye afya ya mwili, akili na hata katika utendaji wako wa kazi. Watu wengi hutamani kuwa na furaha lakini bado hawapati furaha; wengi hudhani kuwa na vitu kama vile pesa ndiyo chanzo cha furaha, lakini mambo hayawi kama walivyotarajia pindi wapatapo vitu hivyo. Je unahitaji kuwa na furaha ili uboreshe afya na ufanisi wa utendaji kazi wako? Karibu nikushirikishe njia 10 za kukufanya kuwa na furaha. 1. Samehe Watu wengi hukosa furaha kutokana na kubeba uchungu na maumivu yaliyotokana na watu waliowakosea. Ikiwa unataka kuwa na furaha ni muhimu kumsamehe aliyekukosea hata kama hajaomba msamaha. Kumsamehe aliyekukosea kuna manufaa k...
Athari 5 za Kutumia Vyombo vya Chakula vya Plastiki

Athari 5 za Kutumia Vyombo vya Chakula vya Plastiki

Afya
Plastiki ina nafasi kubwa kwenye jamii ya leo; hutumika kwenye magari, vyombo vya nyumbani, vifaa vya watoto vya kuchezea, simu, kompyuta n.k. Kwa hakika siyo rahisi mtu kumaliza siku nzima bila kutumia kifaa chochote cha plastiki. Pamoja na nafasi hii kubwa ya matumizi ya plastiki, plastiki imekuwa na athari mbalimbali kwenye afya ya binadamu pamoja na mazingira. Karibu nikufahamishe madhara au athari 5 zitokanazo na matumizi ya vifaa au vyombo vya chakula vilivyotengenezwa kwa plastiki. 1. Sumu zilizoko kwenye plastiki zinaweza kukufanya uugue Tafiti mbalimbali zimebainisha kuwa sumu zilizoko kwenye vifaa vya plastiki zinaweza kusababisha maradhi kama vile saratani, maradhi ya kupoteza kumbukumbu, maradhi ya moyo pamoja na kupoteza uwezo wa kuona. Wataalamu mbalimbali wali...
Faida 10 za Kuogea Maji ya Baridi

Faida 10 za Kuogea Maji ya Baridi

Mtindo wa Maisha
Watu wengi hupenda kuogea maji ya moto, hii ni kutokana na kuogopa baridi au sababu za kimazoea tu. Ingawa mara nyingi umekuwa ukisisitiziwa kuwa maji moto yana manufaa mengi, lakini hata maji ya baridi nayo yana manufaa yake. Je uko tayari kuongeza maarifa au hata kubadili mtazamo wako? Karibu nikushirikishe faida 10 za kuogea maji ya baridi. 1. Huongeza utayari Maji ya baridi hukufanya uchangamke, hili ni tofauti na maji ya moto. Mara nyingi mtu anapoogea maji ya baridi hasa baada ya kuamka humfanya awe katika hali nzuri ya kuwa tayari kuendelea na majukumu yake. Kumbuka hata wakati wa kuogea maji baridi kasi ya upumuaji hubadilika na kukufanya kuongeza kiasi cha oksijeni kinachoingia mwilini. 2. Hulainisha ngozi na nywele Maji moto huchubua ngozi na nywele, hasa kwa kuondo...
Sababu 10 za Kwanini Baadhi ya Watu Kamwe Hawatafanikiwa

Sababu 10 za Kwanini Baadhi ya Watu Kamwe Hawatafanikiwa

Maendeleo Binafsi
Kila mtu anatamani kufanikiwa, lakini siyo wote wanatimiza lengo hili. Ni wazi kuwa hakuna njia ya mkato ya kufika kwenye kitu kizuri. Ukiwachunguza sana watu waliofanikiwa, utagundua kuwa kuna tabia au mambo kadhaa yanayoshabihiana kati yao. Pia ukiwachunguza watu walioshindwa au ambao hawajafanikiwa, utabaini pia kuna tabia au mambo kadhaa yanayofanana kati yao. Je unatamani kufanikiwa? Basi fahamu sababu 10 zinazowafanya baadhi ya watu kamwe wasifanikiwe kwenye maisha yao. 1. Kutokujali muda Mafanikio yamefugwa kwenye muda. Ili mtu aweze kufanikiwa ni lazima ajifunze kutumia muda wake vyema. Watu wasiofanikiwa hawana mipaka; huchelewa kila mahali, pia hawathamini muda wa wengine. Hawana vipaumbele wala muda wa kuweka malengo na vipaumbele kwenye maisha yao; wao huishi tu ...
Njia 5 za Kuongeza Kasi na Usahihi wa Kuandika (Typing) kwa Kutumia Kompyuta

Njia 5 za Kuongeza Kasi na Usahihi wa Kuandika (Typing) kwa Kutumia Kompyuta

Tija
Kuandika kwa kasi na kwa usahihi kwa kutumia kompyuta kuna manufaa mengi kama vile kuweza kufanya kazi kubwa kwa muda mfupi, kuweza kuandika mambo mbalimbali kwa kutumia kompyuta na hata sifa ya kukuwezesha kupata kazi mbalimbali. Hivyo, najua unatamani kuandika kwa kasi kubwa na kwa usahihi kwa kutumia kompyuta; lakini tatizo bado hujaweza kuacha kasi ya kudonoa na kuweza kuandika kwa kasi kubwa na kwa usahihi. Karibu ufahamu njia 5 ambazo unaweza kuzitumia ili kuboresha uwezo wako wa kuandika kwa kutumia kompyuta. 1. Elewa na tumia baobonye (keyboard) vyema Ili uweze kuongeza kasi yako ya kuandika pamoja na usahihi ni lazima uelewe baobonye vyema na kuitumia vyema. Zingatia haya yafuatayo: Elewa mpangilio wa vitufe kwenye baobonye. Panga vidole kulingana na vitufe sta...
Virusi 10 vya Kompyuta Hatari Zaidi Kuwahi Kutokea

Virusi 10 vya Kompyuta Hatari Zaidi Kuwahi Kutokea

Maarifa
Virusi vya kompyuta ni tatizo la muda mrefu ambalo limeathiri watu wengi kwa namna moja au nyingine. Inawezekana wewe ni mmojawapo kati ya wale waliowahi kuathiriwa na virusi vya kompyuta; inawezekana pia hujawahi kuathiriwa au hata kusikia swala hili kabisa. Katika muda ambao Mungu amenijalia kutumia kompyuta (2002 - hadi sasa), nimeshuhudia mengi na kukabiliana na mengi kuhusu virusi vya kompyuta. Nimewahi kuona watu wakilia kwa kupoteza taarifa muhimu, wengine wakitoa fedha nyingi kutengeneza kompyuta zao zilizoathirika. Mimi mwenyewe nimewahi kuathiriwa mara kadhaa na virusi hivi. Hivyo basi, hebu leo tutazame virusi 10 vya kompyuta vilivyowahi kutokea ambavyo ni hatari zaidi. 1. Code Red Kirusi cha Code Red kiliibuka mnamo mwaka 2001 na kubainiwa na wafanyakazi wawi...
Njia 7 Bora za Kushinda au Kukabiliana na Hofu

Njia 7 Bora za Kushinda au Kukabiliana na Hofu

Maendeleo Binafsi
Watu wengi wanakabiliwa na kuathiriwa na hofu katika maisha yao kwa namna moja au nyingine. Hofu hizi zinaweza kusababishwa na mazingira, mtu, kitu au hata sababu za kisaikolojia. Hofu isiposhughulikiwa kwenye maisha inaweza kuwa ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya mtu husika. Wengi wanatamani kukabiliana na hofu lakini bado hawajui namna ya kukabili hofu zinazowakumba. Soma pia: Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu. Je uko tayari kushinda hofu sasa? Karibu nikushirikishe njia 7 ambazo unaweza kuzitumia kukabiliana na hofu maishani mwako. 1. Punguza au ondoa mawazo na imani potofu Wakati mwingine watu wanapata hofu kutokana na imani au fikra potofu pekee. Kwa mfano unaogopa kinyonga kwa sababu umesikia kuwa kikikugusa utatokwa na ngozi au kufa; je una uhakika juu ...
Mambo 10 Usiyojua Kama Unaweza Kuyafanya kwa Kutumia Google

Mambo 10 Usiyojua Kama Unaweza Kuyafanya kwa Kutumia Google

Tija
Google ni rafiki wa karibu katika maisha yetu. Kupitia injini pekuzi ya Google tunaweza kupata majibu ya maswali mbalimbali. Ni ukweli usiopingika kuwa katika matumizi yetu ya teknolojia hatuwezi kuepuka kutumia Google. Kupitia Google unaweza kupata majibu ya maswali mbalimbali, kazi, marafiki, bidhaa, huduma, elimu n.k. Pamoja na nafasi hii kubwa ya Google kwenye maisha na kazi zetu, bado watu wengi hawafahamu vyema matumizi mbalimbali ya Google. Karibu nikufahamishe mambo 10 usiyojua kama unaweza kuyafanya kwa kutumia Google. 1. Kikokotozi (calculator) Ikiwa unataka kufanya mahesabu kadhaa, huhitaji kikokotozi au simu yenye kikokotozi kama uko karibu na Google.  Kwa kuandika neno calculator kwenye ukurasa wa Google mara moja utapata kikokotozi kwa ajili ya kufanyia hesabu....
Mambo 25 Unayoweza Kujifunza Kutokana na Makosa

Mambo 25 Unayoweza Kujifunza Kutokana na Makosa

Maendeleo Binafsi
Je wewe unapenda kufanya makosa? Mimi binafsi sipendi kufanya makosa. Ingawa watu wengi wamekuwa wakijaribu kujitahidi kuepuka makosa; bado wamejikuta wakiendelea kufanya makosa. Ni wazi kuwa makosa hayaepukiki kwenye maisha ya kila siku ya binadamu. Kutokana na sababu za kibinadamu, maamuzi na matendo tunayoyafanya yana mapungufu mbalimbali; hivyo haiwezekani kuepuka makosa. Kama haiwezekani  kuepuka makosa sasa tunafanyaje? Jibu ni wazi kabisa kuwa tunajifunza kutokana na makosa hayo ili tuyaepuke au tuboreshe mambo mbalimbali mbeleni. Karibu nikufahamishe mambo 25 ambayo unaweza kujifunza kutokana na makosa mbalimbali unayoyafanya kila mara maishani mwako. 1. Hutuonyesha vitu na mambo tusiyoyafahamu Ni wazi kuwa makosa mengine hutokea kwa kufanya vitu au maamuzi tu...