Mambo 6 Usiyoyafahamu Kuhusu Pesa - Fahamu Hili
Friday, March 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Mambo 6 Usiyoyafahamu Kuhusu Pesa

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Dola

Inawezekana unabeba pesa kwenye pochi au mfuko wako au pengine umezitunza benki, lakini ni kwa kiasi gani unafahamu kuhusu pesa? Ni dhahiri kuwa unaweza kuzitumia pesa hadi mwisho wa maisha yako bila hata kujua mambo fulani yanayozihusu. Fuatilia makala hii nikufahamishe mambo 6 usiyoyafahamu kuhusu pesa.

1. Pesa ya noti siyo karatasi

Watu wengi wanafikiri kuwa pesa ya noti imetengenezwa kwa karatasi lakini si kweli. Malighafi zilizotengenezea pesa ya noti, mojawapo ni pamba. Imetengenezwa hivi ili iwe imara zaidi na yenye kukabiliana na mambo kama vile vimiminika na uchafu.

2. Wazo la ATM liliibuka bafuni

Mgunduzi John Shepherd-Barron alipata wazo la kuweka ATM bafuni manamo miaka ya 1960 akiwa bafuni.

ATM

3. Pesa zina virusi vya mafua na cocaine

Utafiti umebaini kuwa kutokana na pesa kupita kwenye mikono na sehemu mbalimbali, nyingi zina virusi vya mafua na chembechembe za madawa ya kulevya (cocaine).

madawa na pesa

4. Wote walio hai sasa walizikuta pesa

Hii ina maana gani? Inaaminika kuwa pesa zilianza kutumika mnamo miaka 5,000 K.B. Ni dhahiri kuwa watu wote walio hai duniani leo walizikuta pesa na kuna uwezekano wakaondoka kabla ya kuja kwa mbadala wa pesa.

5. Asili ya pesa za noti ni China

Inaaminika kuwa pesa za noti zilibuniwa huko China. Mnamo mwaka wa 910 pesa hizi zilimshangaza Marco Polo alipotembelea China katika safari zake.

6. Kutengeneza pesa ni taaluma ngumu

Watu wengi wanafahamu kuwa madaktari na wanasheria wanahitaji miaka mingi (5 – 6) kufuzu taaluma zao. Lakini taaluma ya kutengeneza pesa “engraiving” inahitaji miaka takriban 15 ili kufuzu. Hii pia ndiyo sababu ni vigumu kutengeneza pesa bandia ambazo hazitobainika.

Naamini umepata maarifa fulani ambayo awali haukuwa nayo. Tungependa kupokea maoni, au maswali kutoka kwako, Tafadhali tuandikie hapo chini kisha washirikishe wengine.

2.5 2 votes
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

1 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Stone israel
Stone israel
1 year ago

naitwa stone israel napenda kuuliza kuwa mchina anatumia fedha ya noti ama siliva?

1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x