Nyumba Archives - Fahamu Hili
Friday, September 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Nyumba

Makosa 8 ya Kuepuka Kabla na Wakati wa Kujenga Nyumba

Makosa 8 ya Kuepuka Kabla na Wakati wa Kujenga Nyumba

Nyumba na Makazi
Nyumba ni hitaji muhimu kwa watu wote. Kila mmoja anatamani na ana ndoto za kununua au kujenga nyumba nzuri na ya kisasa. Ni kweli kuwa ujenzi wa nyumba unahitaji rasilimali nyingi hasa fedha. Pamoja na gharama hizi za ujenzi wa nyumba bado watu wengi wamekuwa wakishindwa kupata nyumba nzuri huku wakiwa tayari wamepoteza kiasi kikubwa cha pesa. Ni wazi kuwa yapo makosa mbalimbali yanayosababisha hali hii yakiwemo yale ya ukosefu wa elimu pamoja na uzembe wa aina mbalimbali. Karibu ufuatilie makala hii ili uweze kufahamu makosa 8 unayoweza kuyaepuka wakati wa kujenga nyumba ili hatimaye uwe na nyumba bora. 1. Kutozingatia kanuni za kununua kiwanja Watu wengi hawafahamu mambo muhimu ya kuzingatia wakati wanaponunua kiwanja. Hivyo hujikuta wakiingia katika matatizo mbalimbali kama vile ku...
Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Kiwanja au Ardhi

Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Kiwanja au Ardhi

Nyumba na Makazi
Ardhi ni rasilimali muhimu ambayo kila mtu anaihitaji kwa namna moja au nyingine. Watu wengi hununua ardhi kwa ajili ya kufanyia shughuli mbalimbali kama vile ujenzi na kilimo. Pamoja na umuhimu huu mkubwa wa ardhi bado watu wengi wanakumbana na changamoto mbalimbali katika maswala yanayohusu kununua na kumiliki ardhi. Wengi hujikuta wakinyang’anywa ardhi zao, kuharibiwa mali, au wakiingia kwenye migogoro mikubwa ya kisheria. Ni wazi kuwa zipo sababu mbalimbali zinazosababisha matatizo haya. Fuatilia makala hii kwa makini ili uweze kufahamu mambo 10 ambayo unapaswa kuyazingatia kabla ya kununua kiwanja au ardhi. 1. Ona kiwanja husika mwenyewe Ni vyema ukafika kwenye eneo la kiwanja husika na kukiona wewe mwenyewe kama kinakuridhisha na kukufaa kwa mahitaji yako. Fahamu mipaka, na ...
Njia 8 Rahisi za Kupunguza Matumizi ya Umeme

Njia 8 Rahisi za Kupunguza Matumizi ya Umeme

Nyumba na Makazi
Matumizi hayaepukiki kwenye maisha lakini kubana matumizi inawezekana. Yapo mambo mengi ambayo hugarimu fedha ili kuyamudu yakiwemo huduma kama maji, umeme, gesi na mafuta. Ni dhahiri kuwa ili kupunguza ugumu na changamoto za maisha ni vyema kujifunza namna ya kutumia vitu vyema. Unaweza kuokoa fedha nyingi ambazo zingepotea kwa kulipia gharama zisizo na sababu za matumizi ya umeme. Hivyo fahamu njia 8 rahisi za kupunguza matumizi ya umeme. 1. Zima taa na vifaa visivyokuwa na uhitaji Mara nyingi umeme mwingi hupotea kutokana na kuacha vifaa mbalimbali vikiwa vimewashwa bila sababu. Si jambo la kustajabisha watu kusahau taa za nje ya nyumba hadi saa sita mchana; au hata kuacha vifaa kama vile redio, televisheni au kompyuta vikiwa vimewashwa mchana au usiku kucha bila sababu ya m...
China Kujenga “Mji Msitu” Ambao Utakuwa na Mamilioni ya Mimea na Miti 40,000

China Kujenga “Mji Msitu” Ambao Utakuwa na Mamilioni ya Mimea na Miti 40,000

Teknolojia
China kujenga “mji msitu” ambao utakuwa na mamilioni ya mimea na miti 40,000. Kazi hii inatarajiwa kutekelezwa kwenye Mji Msitu wa Liuzhou ulioko katika milima ya kusini mwa Guangxi kabla ya 2020. Mji huu uliobuniwa na msanifu majengo Stefano Boeri unatekelezwa sasa, ambapo nyumba, ofisi, shule na hosipitali zitafunikwa kabisa na miti na mimea mingine. Mjii huu unatarajiwa kuchukua eneo la hekta 175, na utakapokamilika utaweza kuchukua watu takriban 30,000. Mji huo utakapokamilika utatumia usafiri wa treni ya umeme kutoka Liuzhou. Mji huo pia utatumia nishaji ya joto ardhi (geothemal) kwa matumizi ya ndani nyumba pamoja na umeme jua (solar). Wanaamini kuwa kupanda miti zaidi kutanyonya tani 10,000 za hewa ukaa (C02) na tani 75 za hewa chafuzi nyingine, wakati huo ikizalisha ta...
Wanasayansi Wagundua  Rangi inayotumia Jua Kuzalisha Nishati

Wanasayansi Wagundua Rangi inayotumia Jua Kuzalisha Nishati

Habari, Teknolojia
Timu ya wanasayansi nchini Australia imegundua rangi ya sola ambayo inaweza kuzalisha nishati kwa ajili ya matumizi ya majumbani na magari. Timu hiyo iliyoongozwa na Torben Daeneke imesema kuwa inaamini kuwa njia hiyo itatoa nishati nafuu na safi kwa dunia. Nishati kwa ajili ya magari siku za mbeleni Inaweza kufikiriwa kuwa, kuendesha gari kwa nishati itokanayo na rangi ni kichekesho lakini wanayansi hao wamesema inawezekana. Wamesema kwa kuchanganya katalisti yenye rangi nyeupe inayotumika kwenye dawa ya meno, wanasyansi waliweza kutengeneza rangi ambayo ikikutana na jua inabadili maji kuwa hydrojeni ambayo itatumika kuendesha gari. Wamesema changamoto waliyonayo ni namna ya kuhamisha nishati hiyo na kuitumia kwenye gari; pamoja na hili wamesema wameshapata njia kadhaa wanazozifa...