Fahamu Hili Archives - Page 11 of 20 - Fahamu Hili
Wednesday, March 18Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Podcast: Fahamu Hili

Njia 7 Bora za Kushinda au Kukabiliana na Hofu

Njia 7 Bora za Kushinda au Kukabiliana na Hofu

Maendeleo Binafsi
Watu wengi wanakabiliwa na kuathiriwa na hofu katika maisha yao kwa namna moja au nyingine. Hofu hizi zinaweza kusababishwa na mazingira, mtu, kitu au hata sababu za kisaikolojia. Hofu isiposhughulikiwa kwenye maisha inaweza kuwa ni kikwazo kikubwa cha mafanikio ya mtu husika. Wengi wanatamani kukabiliana na hofu lakini bado hawajui namna ya kukabili hofu zinazowakumba. Soma pia: Aina 70 za Hofu (Phobia) Unazotakiwa Kuzifahamu. Je uko tayari kushinda hofu sasa? Karibu nikushirikishe njia 7 ambazo unaweza kuzitumia kukabiliana na hofu maishani mwako. 1. Punguza au ondoa mawazo na imani potofu Wakati mwingine watu wanapata hofu kutokana na imani au fikra potofu pekee. Kwa mfano unaogopa kinyonga kwa sababu umesikia kuwa kikikugusa utatokwa na ngozi au kufa; je una uhakika juu ...
Mambo 10 Usiyojua Kama Unaweza Kuyafanya kwa Kutumia Google

Mambo 10 Usiyojua Kama Unaweza Kuyafanya kwa Kutumia Google

Tija
Google ni rafiki wa karibu katika maisha yetu. Kupitia injini pekuzi ya Google tunaweza kupata majibu ya maswali mbalimbali. Ni ukweli usiopingika kuwa katika matumizi yetu ya teknolojia hatuwezi kuepuka kutumia Google. Kupitia Google unaweza kupata majibu ya maswali mbalimbali, kazi, marafiki, bidhaa, huduma, elimu n.k. Pamoja na nafasi hii kubwa ya Google kwenye maisha na kazi zetu, bado watu wengi hawafahamu vyema matumizi mbalimbali ya Google. Karibu nikufahamishe mambo 10 usiyojua kama unaweza kuyafanya kwa kutumia Google. 1. Kikokotozi (calculator) Ikiwa unataka kufanya mahesabu kadhaa, huhitaji kikokotozi au simu yenye kikokotozi kama uko karibu na Google.  Kwa kuandika neno calculator kwenye ukurasa wa Google mara moja utapata kikokotozi kwa ajili ya kufanyia hesabu....
Mambo 25 Unayoweza Kujifunza Kutokana na Makosa

Mambo 25 Unayoweza Kujifunza Kutokana na Makosa

Maendeleo Binafsi
Je wewe unapenda kufanya makosa? Mimi binafsi sipendi kufanya makosa. Ingawa watu wengi wamekuwa wakijaribu kujitahidi kuepuka makosa; bado wamejikuta wakiendelea kufanya makosa. Ni wazi kuwa makosa hayaepukiki kwenye maisha ya kila siku ya binadamu. Kutokana na sababu za kibinadamu, maamuzi na matendo tunayoyafanya yana mapungufu mbalimbali; hivyo haiwezekani kuepuka makosa. Kama haiwezekani  kuepuka makosa sasa tunafanyaje? Jibu ni wazi kabisa kuwa tunajifunza kutokana na makosa hayo ili tuyaepuke au tuboreshe mambo mbalimbali mbeleni. Karibu nikufahamishe mambo 25 ambayo unaweza kujifunza kutokana na makosa mbalimbali unayoyafanya kila mara maishani mwako. 1. Hutuonyesha vitu na mambo tusiyoyafahamu Ni wazi kuwa makosa mengine hutokea kwa kufanya vitu au maamuzi tu...
Faida 10 za Kupumzika

Faida 10 za Kupumzika

Mtindo wa Maisha
Kutokana na mabadiliko ya mtindo wa maisha, watu wengi hawapati muda wa kutosha wa kupumzika. Mara nyingi mtu anapozidiwa hupunguza zaidi muda wa kupumzika ili akamilishe majukumu yake. Ni wazi kuwa watu wengi hawafahamu umuhimu wa kupumzika, ndiyo maana hawatengi muda wa kutosha wa kupumzika. Ni ukweli usiopingika kuwa kupumzika kuna manufaa makubwa sana kwenye miili na utendaji wetu wa kazi kila siku. Ikiwa unataka kuboresha utendaji wako wa kazi pamoja na afya yako, fahamu faida 10 za kupumzika. 1. Huongeza uwezo wa kumbukumbu Ubongo wa mwanadamu unahitaji kupumzika ili uweze kujijenga na kufanya kazi vyema. Ikiwa mtu hatapata muda wa kutosha wa kupumzika, uwezo wake wa kutunza kumbukumbu utapungua. Pia utafiti uliofanyika umebaini kuwa kutokupumzika huongeza kiasi fulani...
Mambo 15 ya Kufanya ili Kuwa Bora Zaidi

Mambo 15 ya Kufanya ili Kuwa Bora Zaidi

Maendeleo Binafsi
Kama mtu mwenye shauku kubwa ya maendeleo binafsi, kila siku huwa nachunguza njia bora za kunifanya niwe bora zaidi. Naamini wewe pia unapenda kuwa bora zaidi ili uongeze tija na ufanisi wako. Karibu nikufahamishe mambo 15 ambayo unaweza kuyafanya kuanzia sasa ili uweze kuwa bora zaidi. 1. Soma vitabu Vitabu ni chanzo kikubwa cha hekima; Kadri unavyosoma vitabu ndivyo unavyozidi kupata hekima hii. Kupitia vitabu unaweza kujifunza mambo mbali mbali kama vile: Njia za kukabiliana na matatizo mbalimbali. Njia za kufanya mambo mbalimbali kwa ufanisi. Jinsi ya kuboresha maisha yako. Hamasa kutoka kwa waliofanikiwa n.k. Maarifa mapya usiyoyajua. Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo unaweza kujifunza au kuyapata kutoka kwenye vitabu. Hivyo ikiwa unataka kuwa bora zaid...
Faida 5 za Kusema “Hapana”

Faida 5 za Kusema “Hapana”

Tija
Ni muhimu kukumbuka kuwa “Hapana” ni jibu rahisi pia dogo sana lakini lina nguvu kubwa. Ni vyema kufahamu nguvu iliyoko kwenye jibu la “Hapana” ili tuweze kuboresha maisha yetu. Kila siku kwenye maisha yetu tunatakiwa kufanya maamuzi fulani ya kukataa au kukubaliana na mipango au jambo fulani. Ni wazi kuwa maamuzi tunayoyafanya kuhusu mambo na mipango hii, ndiyo huamua na kuatawala hali za maisha yetu ya sasa na baadaye. Karibu nikushirikishe faida 5 za kusema hapana katika mipango na mambo mbalimbali kwenye maisha yako. 1. Hukutenga na mipango mibaya Siyo kila mpango unafaa kwenye maisha yako. Mipango mingine inaweza kuangamiza ndoto na malengo yako. Kwa mfano mtu akakushawishi uingie kwenye biashara ya dawa za kulevya, je unafikiri utaweza kweli kupata manufaa ya uh...
Makosa 25 ya Kuepuka Unapotengeneza Tovuti (website) au Blog

Makosa 25 ya Kuepuka Unapotengeneza Tovuti (website) au Blog

Tovuti na Blogu
Kuna tovuti na blog nyingi zinazotengenezwa kila siku, lakini siyo zote zinakidhi viwango vya ubora. Hili linasababishwa na tovuti nyingi kutengenezwa bila kuzingatia kanuni muhimu za utengenezaji wa tovuti au blog. Zipo athari nyingi za kutengeneza tovuti zenye ubora mdogo kama vile kupoteza wasomaji au watembeleaji pamoja na kupata nafasi ndogo kwenye injini pekuzi. Ni muhimu ukafahamu kuwa  tovuti (website) au blog ni sura yako au ya biashara yako kwenye ulimwengu. Hivyo ikiwa hutozingatia utengenezaji bora wa tovuti au blog yako, basi utaharibu picha yako au ya biashara yako. Ikiwa unataka kutengeneza tovuti (website) au blog bora, basi fahamu makosa 25 yakuepuka wakati wa kutengeneza tovuti au blog. 1. Muundo mbaya wa tovuti au blog Kosa la muundo mbaya wa tovuti hufany...
Tabia 10 Unazotakiwa Kijifunza Kutoka kwa Watu Waliofanikiwa

Tabia 10 Unazotakiwa Kijifunza Kutoka kwa Watu Waliofanikiwa

Maendeleo Binafsi
Ikiwa wewe ni mjasiriamali unayeanza au umeajiriwa sehemu fulani, kuna tabia ambazo unatakiwa kuzifahamu na kuzifanya ili uwe na mafanikio. Watu wengi hufikiri kuwa mafanikio ni jambo linalotokea kwa bahati tu; lakini mafanikio ni matokeo ya tabia au mikakati inayofanywa mara kwa mara. Hivi leo kuna watu tunaowachukulia kuwa wamefanikiwa; watu hawa wana tabia fulani za msingi zinazofanana. Karibu nikufahamishe tabia 10 za watu waliofanikiwa ambazo unaweza kujifunza ili uweze kufanikiwa. 1. Wana mipango Watu waliofanikiwa hawafanyi kazi bila mipango madhubuti. Watu hawa hupanga mipango mbalimbali wanayotakiwa kuitekeleza; mwishoni hukagua kama mipango yao wameitekeleza jinsi ipasavyo. Ni muhimu kujifunza tabia hii ya kujiwekea mipango na kufanya mambo kulingana na mipango husika bi...
Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha

Nukuu (Quotes) 30 za Mafanikio Zitakazokuhamasisha

Hamasa
Kila mtu ana maana yake ya mafanikio. Ni wazi kuwa mafanikio ni kuweza kukabiliana na changamoto au kushindwa bila kukata tamaa au kuacha. Mara nyingi huwa napenda kusoma nukuu (Quotes) mbalimbali kwani huwa zinanipa hamasa kubwa ya kuzidi kufanyia kazi ndoto zangu. Naamini hata wewe unaweza kuhamasika na kupata ari zaidi kwa kusoma nukuu hizi 30 za mafanikio. Soma pia: Nukuu (Quotes) 50 Zitakazo Kuhamasisha Maishani Mwako. Naamini umehamasika na kupata shauku zaidi ya kufanyia kazi malengo na ndoto zako ili ufanikiwe. Kila kitu kinaanza kwenye fikra zetu. Naamini umebaini wazi kuwa maana ya mafanikio ni pana; pia mafanikio siyo kutokukabiliana na cha...
Faida 10 za Kuwa na Malengo Maishani

Faida 10 za Kuwa na Malengo Maishani

Maendeleo Binafsi
Kabla hujakamilisha chochote maishani, ni lazima ufahamu unahitaji nini. Ni lazima ukae chini utafakari kama kile unachokifanya kina thamani kwako; ikiwa hakina thamani, basi tenga muda ujiwekee malengo yenye maana kwako. Kujiwekea malengo maishani kuna umuhimu mkubwa kwani hutufanya tujikite sawasawa kwenye kila tunachokifanya. Je uko tayari kuweka malengo? Karibu nikufahamishe faida 10 utakazozipata ikiwa utajiwekea malengo maishani mwako. 1. Hukupa mwongozo Awali ya yote, malengo hukupa mwongozo na mwelekeo maishani mwako. Malengo hukuwezesha kubaini kitu unachokilenga, na hukufanya uelekeze nguvu zako kwenye kitu husika. Badala ya kushika hiki na kile au kuwa huyu na yule, malengo yatakuwezesha kufahamu unatakiwa kufanya nini au kuwa nani. 2. Hukuwezesha kufanya...