Ni muhimu kukumbuka kuwa “Hapana” ni jibu rahisi pia dogo sana lakini lina nguvu kubwa. Ni vyema kufahamu nguvu iliyoko kwenye jibu la “Hapana” ili tuweze kuboresha maisha yetu.
“’Hapana’ ni sentensi kamili. Haihitaji maelezo ya ziada. Kwa hakika unaweza kujibu ombi la mtu kwa jibu rahisi la ‘Hapana’.”
Kila siku kwenye maisha yetu tunatakiwa kufanya maamuzi fulani ya kukataa au kukubaliana na mipango au jambo fulani.
Ni wazi kuwa maamuzi tunayoyafanya kuhusu mambo na mipango hii, ndiyo huamua na kuatawala hali za maisha yetu ya sasa na baadaye.
Karibu nikushirikishe faida 5 za kusema hapana katika mipango na mambo mbalimbali kwenye maisha yako.
1. Hukutenga na mipango mibaya
Siyo kila mpango unafaa kwenye maisha yako. Mipango mingine inaweza kuangamiza ndoto na malengo yako.
Kwa mfano mtu akakushawishi uingie kwenye biashara ya dawa za kulevya, je unafikiri utaweza kweli kupata manufaa ya uhakika? Unaweza kukamatwa na maisha yako yakaishia gerezani.
Huu ni mfano wa mipango mibaya ambayo watu wanapaswa kutokusita kusema hapa; kumbuka hakuna mkato kwenye mafanikio.
“Jifunze kusema ‘hapana’ kwa mazuri ili uweze kusema ‘ndiyo’ kwa bora.”
Soma pia: Tabia 10 Unazotakiwa Kijifunza Kutoka kwa Watu Waliofanikiwa.
2. Hukufanya kuonekana mtu mwenye msimamo
Tutatambua vipi msimamo wako ikiwa wewe unakubali kila kitu? Ni muhimu kusema hapana ili watu watambue kuwa una masimamo fulani ambao hauwezi kuuacha.
Ikiwa kuna jambo au kitu ambacho hukipendi, basi tumia buasara kusema hapa ili watu waheshimu msimamo wako.
Kwa mfano ikiwa wewe hutumii pombe au sigara, basi sema wazi hapa kwa vitu hivi hata kama hutamfurahisha unayempa jibu hilo.
3. Hufanya mawazo yako yaheshimike
Watu wataheshimu mawazo yako kama unayabainisha na kuyatetea wazi. Kusema hapana ni njia ya kuonyesha aina ya mawazo uliyonayo.
Tumia hekima na busara kupinga mawazo yale ambayo wewe huyataki; moja kwa moja wale unaowaeleza wataweza kutambua wazi mawazo yako na kuyaheshimu.
4. Hukuokolea fedha na muda
“Kama kweli unataka kuwa mtumiaji mzuri wa muda, unatakiwa kujifunza kusema hapana kwa watu wengine na kufanya hivyo mara kwa mara.”
Unaposema hapana utaepuka mambo na tabia mbalimbali ambazo zinaweza kukupotezea muda na pesa nyingi.
Ni muhimu kusema hapana kwa maswala kama vile pombe, uzinzi, matumizi mabaya mitandao ya kijamii, uzururaji, n.k.
Soma pia: Kanuni 9 za Kufanikiwa katika Matumizi ya Muda.
5. Hukuwezesha kufikia ndoto na maono yako
Ili tuweze kufikia ndoto zetu tunahitaji kuepuka mambo mbalimbali yasiyoendana na ndoto au maono yetu.
Ka njia ya kusema hapana unaweza kuondoa mambo yote ambayo kwa namna moja au nyingine hayakuwezeshi kutimiza ndoto au maono yako.
Inaweza kuwa ni mtu, kazi, tabia n.k. ambavyo haviendani na ndoto zako; hivo ni muhimu kusema hapana.
Soma pia: Faida 10 za Kuwa na Malengo Maishani.
Neno la Mwisho:
Naamini umeona jinsi jibu dogo la “Hapana” lilivyo na nguvu kubwa katika maisha yako.
Ni muhimu kufahamu kuwa mtu mwenye malengo ni lazima aweze kusema hapana kwa vitu, watu, tabia au kazi ambazo hazimuwezeshi kutimiza malengo yake. Je wewe huwa unasema hapana?
Tafadhali tuandikie maoni yako hapo chini. Usisahau pia kuwashirikisha wengine makala hii pamoja na kufuatilia ukurasa wetu wa Facebook ili kufahamu mengi zaidi.
Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Nimeipenda hii blog kwakweli muandishi mungu amjaalie
Tunashukuru sana kwa kuwa msomaji wetu; pia tunashukuru kwa maoni yako ya thamani; tunakutakia kila la heri katika kutimiza malengo yako…karibu sana Fahamuhili.
Nahitaji kujiunga
Asante, karibu Fahamuhili.com.
Kabisa ni vyema tukazifahamu njia zinazoweza kutusaidia kutunza pesa vizuri
Asante sana kwa maoni yako ya thamani; na kwa kuwa msomaji wetu. Karibu sana Fahamuhili.com