Mafuta ya Nazi Hatari kwa Afya - Fahamu Hili
Friday, September 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Mafuta ya Nazi Hatari kwa Afya

Washirikishe Wengine Makala Hii:

Nazi

Watafiti wa afya nchini Marekani wamesema matumizi ya mafuta ya nazi si salama kwa afya kama ilivyo kwa nyama ya ng’ombe na siagi.

Shirika la Moyo la Marekani (AHA), limeeleza kuwa mafuta yaliyoko kwenye nazi yanaweza kuongeza lehemu (cholesterol) mbaya katika mwili wa binadamu.

Kwa mujibu wa AHA, wanadai kuwa kuna mafuta 82% katika nazi. Kuna zaidi ya 63% kwenye siagi, 50% kwenye nyama ya ng’ombe na 39% kwenye nyama ya nguruwe. Wataalamu hao wameongeza kuwa mafuta hayo yanaweza kusababisha lehemu (cholesterol) mbaya katika mwili wa binadamu.

Baadhi ya watu hudai kuwa ulaji wa mafuta ya nazi una manufaa kwa afya ya mlaji lakini AHA wamesema madai hayo hayajadhibitishwa.

Wamependekeza kuwa, watu wajitahidi kupunguza kiasi cha mafuta yenye lehemu wanayoyatumia kila siku katika maisha yao.

Katika hatua nyingine huko Uingereza mamlaka ya afya ya uma imeshauri wanaume kula gramu 30 za mafuta pekee huku wanawake wakishauriwa kutumia gramu 20 pekee za mafuta yanayochangia lehemu katika mwili.

Habari hii inakuja kwa mshangao baada ya miaka mingi ya kusikika uzuri wa vitu vingi vitokanavyo na nazi kuwa vyenye msaada kiafya. Kwa hakika sasa unaweza kupata mafuta ya nazi katika kila kitu kuanzia dawa za nywele hadi dawa za meno.

Wataalamu wa lishe wanasema kuwa mafuta ya nazi yanaweza kuwa mazuri kutumika juu ya mwili wako tu, na sio ndani ya mwili wako.

Je una maoni gani juu ya utafiti huu? Wakazi wa pwani ambao ni watumiaji wakubwa wa nazi wanakubaliana na utafiti huu? Tafadhali, tupe maoni yako pia washirikishe wengine.

1 1 vote
Pendekeza Ubora wa Makala Hii
Washirikishe Wengine Makala Hii:
Subscribe
Notify of
guest

2 Maoni
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
EZRONI SAMWEL
EZRONI SAMWEL
4 years ago

duh!!!
Baada ya hilo kuthibitishwa jamii ipewe tahadhari maana matumizi ya mafuta ya nazi ni makubwa sana Tanzania haswa kwa wakazi wa pwani na zanzibari.
Mamlaka husika hazina budi kutimiza wajibu wake.

Kornelio Maanga
Reply to  EZRONI SAMWEL
4 years ago

Asante sana kwa maoni yako ya thamani; karibu sana Fahamuhili.com

2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x