Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 5 of 17
Friday, March 27Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Mambo 9 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Web Host

Mambo 9 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Web Host

Tovuti na Blogu
Kuna mahali ambapo kila tovuti au blog hutunzwa, mahali hapo ndipo hufahamika kama web host. Web host bora ni muhimu sana kwa ajili ya tovuti au blog yako. Watu wengi wamekuwa wakifanya makosa wakati wa kuchagua web host kutokana na uelewa mdogo juu ya umuhimu wa web host bora pamoja na njia za kubaini web host bora. Madhara ya web host duni ni: Kasi ndogo ya tovuti yako au blog. Athari ya kudukuliwa kutokana na miundombinu duni ya usalama. Kukosa huduma bora na muhimu. Kutokupatikana kwa tovuti yako kila wakati. Ikiwa unataka kuchagua web host bora kwa ajili ya tovuti au blog yako, basi fahamu mambo 9 muhimu ya kuzingatia wakati wa kuchagua web host. 1. Bainisha mahitaji yako Kabla ya kuchagua web host ni muhimu ubainishe mahitaji yako kwanza. Je tovuti au blo...
Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kutafuta Mpenzi Kwenye Mtandao wa Intaneti

Sababu 7 za Kwa nini Hutakiwi Kutafuta Mpenzi Kwenye Mtandao wa Intaneti

Mahusiano na Familia
Maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia hasa katika sekta ya mawasiliano yamebadili mambo mengi. Hili ni tofauti na hapo awali ambapo watu walitegemea njia duni za mawasiliano kama vile posta. Kutokana na maendeleo haya katika teknolojia ya mawasiliano, suala la mahusiano pia limebadilika kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanaweza kutafuta wapenzi kwenye mtandao wa intaneti bila kizuizi chochote. Kwa hakika bila shaka kila jambo lina uzuri na ubaya  wake; hivyo suala la kutafuta wapenzi kwenye mtandao linatakiwa kutazamwa kwa jicho la pili. Ikiwa umejiunga au unataka kujiunga na mitandao ya kutafuta wapenzi, basi fahamu sababu 7 za kwanini hutakiwi kutafuta mpenzi kwenye mtandao wa intaneti. 1. Watu wanaigiza uhalisia Katika eneo ambalo watu wanaigiza uhalisia wa maisha kw...
Mambo Matano ya Kuzingatia Kabla ya Kuajiri Mtu Kupitia Mtandao wa Intaneti

Mambo Matano ya Kuzingatia Kabla ya Kuajiri Mtu Kupitia Mtandao wa Intaneti

Biashara na Uchumi
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili maisha ya mwanadamu kwa kiasi kikubwa. Sekta ya ajira nayo imepokea mabadiliko mengi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hivi leo ni rahisi mtu kuishi Afrika akafanya kazi Marekani au mtu akaishi India akaajiriwa Tanzania. Haya yote ni kutokana na teknolojia kuwezesha watu kuajiri au kuajiriwa kwa kupitia njia ya mtandao wa intaneti. Kwa kutambua kuwa kuajiri kwa njia ya mtandao ni njia nzuri ya kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni pamoja na kupata mtu mwenye sifa stahiki kwa kazi husika, basi fahamu mambo matano ya kuzingatia kabla ya kuajiri mtu kupitia mtandao. 1. Maarifa sahihi Kuna wafanyakazi wengi kwenye mtandao wa intaneti, lakini siyo wote ni bora au wana maarifa stahiki. Ni muhimu sana kufanya utafiti wa ...
Mambo 10 ya Kufanya Ili Kuepuka Ajali Unapoendesha Pikipiki

Mambo 10 ya Kufanya Ili Kuepuka Ajali Unapoendesha Pikipiki

Usafiri na Safari
Pikipiki au kwa jina maarufu bodaboda, zinatumiwa na watu wengi sana kwa usafiri. Licha ya pikipiki kutumiwa kama usafiri, wengine huzitumia kama chanzo cha kipato chao cha kila siku. Hata hivyo kila mmoja amewahi kusikia au kushudia juu ya changamoto kubwa ya ajali inayokabili usafiri wa pikipiki au bodaboda. Wengine wamepata majeraha, kupoteza maisha, kupoteza mali au hata kupata ulemavu wa kudumu. Pasipo shaka sasa ni wakati wa kutazama ni nini hasa chanzo cha ongezeko kubwa la ajali za pikipiki ili kikabiliwe. Ikiwa unaendesha pikipiki au unataka kuongeza maarifa yako, basi fahamu mambo 10 ya kufanya ili kuepuka ajali unapoendesha pikipiki au bodaboda. 1. Pata elimu sahihi ya kuendesha pikipiki Pikipiki ni chombo cha kitaalamu kinachohitaji maarifa sahihi ya kukitumia. A...
Sifa 10 Ambazo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuwa Nazo

Sifa 10 Ambazo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuwa Nazo

Ujasiriamali
Kwa hakika ujasiriamali ni chaguo muhimu sana kwenye karne hii ya sasa ili kujipatia kipato. Hivi leo kuna wajasiriamali wengi waliofanikiwa na wengine hawajafanikiwa. Kwa hakika wajasiriamali waliofanikiwa wanafahamu na wanaziishi sifa za wajasiriamali bora. Ni wazi kuwa huwezi kuwa mjasiriamali bora wakati una sifa za mwajiriwa. Ili kuwa mjasiriamali ni lazima kuzifahamu na kuziishi sifa za mjasiriamali. Karibu nikufahamishe sifa 10 za mjasiriamali. 1. Mwenye malengo Malengo ni mwongozo wa kukuwezesha kufanikisha jambo lolote. Kuwa na malengo ni sifa muhimu ambayo kila mjasiriamali anapaswa kuwa nayo. Je umeamua kuwa mjasiriamali kwenye nini? Kwa ajili ya nini? Malengo yatakuongoza ufanye nini, wapi lini na kwa ajili ya nini. Bila malengo utafanya mambo bila mwongozo wowot...
Sababu 6 za Kwanini Mara Nyingi Wanawake Huishi Zaidi ya Wanaume

Sababu 6 za Kwanini Mara Nyingi Wanawake Huishi Zaidi ya Wanaume

Afya
  Mara nyingi tumeshuhudia katika familia nyingi mwanaume akitangulia kufa kabla ya mwanamke. Simaanishi kuwa wanaume wote wanakufa mapema, lakini mara nyingi wanawake huishi zaidi kuliko wanaume. Swala hili limepelekea kuibua shauku ya kufanya utafiti zaidi juu ya sababu za wanaume wengi kufa mapema kuliko wanawake. Kwa kuwa lengo la Fahamuhili.com ni kukupa maarifa, basi karibu ufahamu kwanini mara nyingi wanawake huishi miaka mingi zaidi ya wanaume. 1. Wanawake hujali afya zao zaidi Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya zilibaini kuwa wanawake hujali afya zao zaidi. Tafiti hizo zinaeleza kuwa wanawake wengi wanapojihisi kuumwa huenda hosipitalini ili kupata ushauri wa kitaalamu. Hali ni tofauti kwa wanaume, kwani wao huvumilia maumizu au hata kutumia...
Mambo 6 Muhimu ya Kufanya Kabla ya Kustaafu

Mambo 6 Muhimu ya Kufanya Kabla ya Kustaafu

Kipato
Kustaafu ni msimu mpya ambao kila mwajiriwa anapaswa kuufahamu na kujiandaa kwa msimu huo vyema. Kumeshuhudiwa watu wakiishi maisha ya taabu na mahangaiko makubwa baada ya kustaafu. Hili linatokana na kutokujiandaa vyema kabla ya kustaafu. Kwa kufahamu umuhimu wa kujiandaa vyema kabla ya kustaafu; karibu ufahamu mambo 6 muhimu ya kufanya kabla ya kustaafu. 1. Jiandae kisaikolojia Kustaafu ni kipindi tofauti sana na kipindi ulichokuwa kwenye ajira. Kipindi hiki utakutana na mtindo mpya wamaisha tofauti na ule uliouzoea. Ni muhimu kujiandaa kisaikolojia kwa maswala kama vile kukaa bila kupata mshahara, ofisi, gari la kampuni au taasisi, nyumba ya taasisi au kampuni pamoja na manufaa mengine ya wafanyakazi. Andaa fikra zako kutambua kuwa wakati wa kufaidi mambo mbalimbali ku...
Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Nyumba

Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla ya Kununua Nyumba

Nyumba na Makazi
Kila binadamu anahitaji nyumba kwa ajili ya makazi. Kutokana na umuhimu wa nyumba, baadhi ya watu wamekuwa wakiamua kujenga nyumba zao wenyewe au kununua nyumba zilizojengwa tayari. Hata hivyo, bado watu hawapati nyumba bora zinazokidhi mahitaji yao kutokana na sababu mbalimbali. Ni wazi kuwa ili upate nyumba bora kuna mambo ambayo unatakiwa kuyafahamu na kuyazingatia. Ikiwa unataka kununua nyumba kwa ajili ya matumizi yako, basi fahamu mambo 10 ya kuzingatia kabla ya kununua nyumba. 1. Tambua mahitaji yako Mara nyingi nyumba hujengwa kwa kutegemea mahitaji ya mmiliki. Hivyo kabla hujanunua nyumba bainisha mahitaji yako kwa nyumba husika. Ikiwa unataka kuitumia kuishi basi hakikisha inakufaa, ikiwa pia unataka kuitumia kwa matumizi ya kibiashara, hakikisha inakidhi mahitaji ...
Tabia 10 za Watu Waliojipanga

Tabia 10 za Watu Waliojipanga

Maendeleo Binafsi
Kuna watu ukitazama utendaji wao wa kazi au maisha yao yanavutia. Ukitazama jinsi wanavyotekeleza mambo yao unaweza kufikiri kuna mfumo fulani unawaendesha au kuwaongoza kwa siri. Mara nyingi watu hawa huwa na mfuatano au mpangilio mzuri na unaoeleweka wa kazi au maamuzi yao. Kwa kifupi watu hawa hufanikiwa sana na ndiyo huitwa watu waliojipanga. Inawezekana nawe unahitaji kufahamu sifa za watu waliojipanga ili ujifunze jambo. Basi karibu nikushirikishe tabia 10 za watu waliojipanga. 1. Wanaandika kila kitu Kuandika vitu ni njia mojawapo ya kutekeleza mambo kwa mpangilio. Watu waliojipanga huandika mambo yote wanayotakiwa kufanya ili wasiyasahau na wanyafanye kwa wakati. Watu waliojipanga hukagua pale walipoandika mara kwa mara ili kuona wamekamilisha lipi na lipi bado hawaj...
Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kuhifadhi Nyaraka Muhimu Salama

Mambo 7 ya Kuzingatia ili Kuhifadhi Nyaraka Muhimu Salama

Tija
Katika maisha yetu ya kila siku hatuwezi kuepuka kuwa na nyaraka mbalimbali. Baadhi ya nyaraka ni za muhimu sana kwetu kiasi cha kutoweza kuzipata tena iwapo zitaharibika au kupotea. Ni ukweli usiopingika kuwa nyaraka kama vile vyeti ya taaluma, bima, hati za kusafiria, leseni, wosia, vyeti vya ndoa, talaka, mikataba, hati za nyumba na viwanja ni baadhi ya nyaraka zinazotakiwa kutunzwa sana. Kutokana na watu wengi kutofahamu umuhimu wa nyaraka mbalimbali au kutokuzihifadhi vyema, wengi wamejikuta kwenye matatizo makubwa baada ya nyaraka zao muhimu kuharibika au kupotea. Ikiwa basi unataka kuweka nyaraka zako salama, karibu nikushirikishe mambo 7 ya kuzingatia ili kuhifadhi nyaraka muhimu salama. 1. Tumia kabati au sanduku maalumu ya kuhifadhi nyaraka Zipo kabati na masan...