Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 12 of 17
Friday, March 27Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Maarifa
Kila siku binadamu anafanya shughuli mbalimbali katika kuandaa au kutengeneza mazingira bora kwa ajili yake kuishi. Kazi hii zinahusisha ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji, makazi, viwanda, ofisi n.k. Hata hivyo, shughuli hizi za binadamu hupelekea uharibifu mkubwa wa mazingira ya asili ikiwemo misitu, mito, milima, wanyama, maziwa, hewa n.k Wapo watu waliolitambua hili na kuamua kufanya kazi zao kwa kuzingatia kulinda na kuheshimu mazingira ya asili. Karibu utazame picha kadha wa kadha zinazonyesha kazi hizo. 1. Nyumba ya duara iliyojengewa kwenye mti huko Tokyo, Japan 2. Mgahawa wa kahawa huko Shanghai, China 3. Mti katikati ya nyumba huko Almaty, Kazakhstan 4. Mti kwenye hoteli huko Izmir Uturuki 5. Nyumba ya makazi huko West Virginia 6. Nyumba iliyojengwa katik...
Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Maarifa, Teknolojia
Hakika ulimwengu huu una  mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu. Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua. Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web) Deep web ni nini? Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane. ...
Mambo 25 Yakushangaza Kuhusu Mwili wa Binadamu

Mambo 25 Yakushangaza Kuhusu Mwili wa Binadamu

Maarifa
Inawezekana unatazama mwili wako kwa juu juu pekee bila kufahamu mambo mengi yaliyojificha kwenye mwili wako. Ni hakika kuwa mwili umeumbwa kwa namna ya pekee sana inayouwezesha kufanya kazi pamoja na kuonekana jinsi ulivyo. Naamini unapenda kupata maarifa kwa kuufahamu mwili wako vyema. Karibu ufuatilie makala hii ili nikujuze mambo 25 yakukushangaza kuhusu mwili wa binadamu. 1. Ubongo unatumia asilimia 20 ya oksijeni pamoja na kalori Ni wazi kuwa utendaji kazi wa ubongo unahitaji oksijeni asilimia 20 pamoja na kalori kutoka kwenye mwili ili kufanya kazi jinsi ipasavyo. 2. Kila mtu ana harufu yake Mbali na mapacha wa kufanana, kila mtu ana harufu yake ya pekee inayomtofautisha kati yake na mtu mwingine. 3. Uwezo mkubwa wa kufikiri unahusiana na kiasi cha ndoto mtu anazoota In...
Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Mtindo wa Maisha
Pombe ni kinywaji kinachotumiwa na watu wengi pasipo hata kufahamu athari zake. Pombe ina athari mbalimbali kiafya na kisaikolojia. Wengi baada ya kuathiriwa na pombe hutamani kuacha matumizi ya pombe lakini ni wachache tu ndiyo hufanikiwa katika hili. Ikiwa unataka kuacha au kumsaidia mtu mwingine kuacha pombe, basi fuatilia njia 12 za uhakika za kuacha pombe. 1. Epuka watu watakaokushawishi kunywa pombe Mara nyingi kama wewe unapenda kunywa pombe utakuwa na marafiki wanaokunywa pombe pia. Ni wazi kuwa marafiki wanaokunywa pombe watakuhimiza kunywa hata kwa kukununulia au hata pengine kukukebehi na kukubeza juu ya uamuzi wako wa kuacha pombe. Hivyo ikiwa unataka kuacha kunywa pombe ni lazima uepuke marafiki au watu wanaoweza kukushawishi kunywa pombe. Unaweza kutafuta ma...
Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Maarifa, Teknolojia
Hivi leo kuna mambo mengi kuhusu intaneti, lakini hapa nitakuonyesha baadhi ya mambo ambayo naamini yatakuvutia na kukushangaza. Historia ya intaneti inaanzia miaka ya 1950 ikienda sambamba na maendeleo ya kompyuta. Ni wazi kuwa, ulimwengu wa intaneti wa leo ulianzwa na mwanasayansi wa kompyuta wa Uingereza Tim Berners-Lee. Kuundwa kwa intaneti yake ya kwanza, moja kwa moja kulibadili ulimwengu, vyombo vya habari, mahusiano, burudani na mambo mengine mengi. Tunapotazama intaneti leo, ni wazi kuwa tunaona mambo mengi ambayo intaneti imepitia tokea kuanzishwa kwake hadi hivi leo. Karibu ufuatilie makala hii ili ufahamu mambo 18 ya kushangaza kuhusu intaneti usiyoyajua. 1. Tovuti ya kwanza bado ipo Tovuti ya kwanza kutengenezwa bado ipo na inafanya kazi hadi leo. Jambo pekee ni ku...
Makosa 8 ya Kuepuka Unapofanya Biashara Kwenye Mtandao

Makosa 8 ya Kuepuka Unapofanya Biashara Kwenye Mtandao

Biashara na Uchumi
Kufanya biashara kwenye mtandao ni jambo lenye faida na changamoto zake. Unaweza ukawa na bidhaa nzuri sana, lakini ukumbuke kuwa kila siku kunaanzishwa tovuti za kuuza bidhaa mtandaoni. Haijalishi kuwa wewe ni muuzaji wa bidhaa wa siku nyingi au wa karibuni, ni wazi kuwa utakutana na changamoto kadha wa kadha. Sasa utafanyaje? Hakuna jibu rahisi, bali ni wazi kuwa makosa unayofanya wakati wa kuendesha biashara kwenye mtandao, ndiyo yanayokugharimu wewe na mapato yako. Yafuatayo ni makosa 8 ambayo unatakiwa kufanya juu chini ili kuhakikisha unayaepuka unapofanya biashara kwenye mtandao. 1. Kukosa kitengo cha huduma kwa wateja Ni rahisi mtu kukaa dukani kwake siku nzima ili kuwahudumia wateja; lakini unaona hakuna umuhimu wa kukaa karibu na wateja wake wa kwenye mtandao. Kumbuka ha...
Mambo 20 Yakushukuru Kwa Ajili Yake Kwenye Maisha

Mambo 20 Yakushukuru Kwa Ajili Yake Kwenye Maisha

Hamasa
Wakati mwingine tunatazama tu mambo ambayo hatuna kwenye maisha, kuliko yale tuliyo nayo. Mara nyingi huwa hatutambui umuhimu wa kitu hadi pale tunapokikosa. Niwazi kuwa wapo watu wanaotafuta vile tunavyoviona ni vidogo lakini hawavipati. Ni muhimu kutenga muda wa kukumbuka yale mambo yote ambayo tunapaswa kushukuru kwa ajili yake. Kama una chochote kati ya hivi basi yakupasa kushukuru. Afya njema Mara nyingi hatutambui kuwa na afya njema pekee ni jambo muhimu na kubwa sana. Kuna wengi wanaotamani kuwa na afya kama ya kwako lakini hawana; hivyo yakupasa kushukuru kwa afya njema. Pesa ulizonazo Unaweza kufikiri kiasi cha pesa ulizonazo ni kidogo sana hivyo hauhitaji kushukuru. Kuna mahali pengine wewe ni tajiri mkubwa sana. Wapo wasiokuwa na pesa wala chochote kile wanachow...
Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Teknolojia
Kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari mawasiliano (TEHAMA), mfumo wa biashara pia umebadilika. Hivi leo ni rahisi kutuma na kupokea pesa, kuuza au hata kununua bidhaa kwa njia ya mtandao. Watu wengi hupenda kufanya manunuzi na mauzo ya bidhaa kwenye mtandao kutokana na urahisi wa upatikanaji wa bidhaa na huduma kupitia mtandao. Pamoja na nafasi hii kubwa ya mtandao katika maswala yanayohusu fedha, zipo changamoto mbalimbali zinazoandamana na miamala na manunuzi ya kwenye mtandao. Fahamu jinsi unavyoweza kujilinda unapofanya miamala au manunuzi mbalimbali kupitia mtandao. 1. Tumia kinga-virusi (antivirus) bora Mtandao wa intanet ni chanzo kikubwa cha virusi na wadukuzi. Hivyo ni vyema ukatumia programu madhubuti kwa ajili ya kukukinga na virusi na wadukuzi mara unapofanya manu...
Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Sababu 13 za Kwa Nini Biashara Nyingi Hufa

Biashara na Uchumi
Hakuna mtu anayeanzisha biashara akitegemea ife, lakini wakati mwingine hili hutokea. Utafiti umebaini kuwa biashara na kampuni nyingi hufa ndani ya kipindi cha miaka miwili hadi mitano tangu kuanzishwa kwake. Kufa kwa biashara siyo jambo zuri, ni wazi kuwa kila mtu nayefanya biashara atatamani kufanya juu chini ili ainusuru biashara yake isife. Zipo sababu mbalimbali zinazosababisha biashara mbalimbali kufa. Fahamu sababu 13 zinazosababisha biashara nyingi kufa pamoja na jinsi ya kuziepuka. 1. Mipango duni Ili ufanikiwe katika biashara unahitaji mpango mzuri wa biashara. Biashara nyingi zinazoanzishwa Afrika hazina mipango madhubuti ya kibiashara inayoonyesha maswala kama vile muundo wa utawala, mtaji, mikakati au mipango ya mauzo, n.k Biashara nyingi pia hukosa lengo; jambo a...
Njia 8 za Kutambua Bidhaa Feki au Bandia

Njia 8 za Kutambua Bidhaa Feki au Bandia

Tija
Mara nyingi tunanunua vitu na bidhaa mbalimbali bila kuzifahamu au kuzichunguza vyema. Hili limepelekea watu wengi kununua bidhaa zisizofaa kwao au zenye madhara kwenye afya zao. Kutokana na ukosefu wa elimu pamoja na kuishi kwa mazoea, watu wengi hawajui wala hawachunguzi vyema bidhaa wanazozinunua ili kuhakikisha ubora wake. Madhara ya kutumia bidhaa feki au bandia: Matatizo ya kiafya kama vile saratani na ulemavu. Upotevu wa fedha. Ajali (Milipuko, shoti ya umeme, n.k). Huathiri uchumi. Ni wazi kuwa yapo madhara mengi yatokanayo na matumizi ya bidhaa feki. Hivyo ni vyema ukafahamu njia za kubaini bidhaa hizi. 1. Ofa na matangazo yasiyo ya kawaida Wahenga walisema “Chema chajiuza kibaya chajitembeza”; ni vyema ukawa makini na bidhaa zenye punguzo kubwa la bei ku...