Fahamu Hili Archives - Page 13 of 20 - Fahamu Hili
Wednesday, March 18Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Podcast: Fahamu Hili

Fahamu Njia 6 za Kulinda Akaunti Zako za Mitandao ya Kijamii

Fahamu Njia 6 za Kulinda Akaunti Zako za Mitandao ya Kijamii

Teknolojia, Tija
Mitandao ya kijamii ni kitu muhimu sana kwenye maisha binafsi na shughuli za kiuchumi kama vile biashara. Kutokana na umuhimu huu, kuna haja ya kuhakikisha akaunti zako za mitandao ya kijamii zinakuwa salama. Je ulishawahi kufikiri nini kitatokea ikiwa mtu mbaya atapata nafasi ya kuingia kwenye akaunti zako? Ni wazi kuwa mambo kama haya hapa chini yanaweza kutokea: Kuiba wafuasi wako utakaokuwa umewakusanya muda mrefu. Kutapeli watu mbalimbali wanaokufahamu katika mitandao ya kijamii kwa kutumia akaunti yako. Kuchafua taswira yako; kumbuka mtu mbaya anaweza kuweka maudhui mabaya yatakayoshusha hadhi yako. Kuiba ama kutumia vibaya taarifa zako binafsi zilizoko kwenye akaunti yako. Ni wazi kuwa ipo sababu ya kuhakikisha akaunti zako za mitandao ya kijamii zinakuwa sal...
Mpiga Ngoma Maarufu wa Mtaani Anayetengeneza Midundo kwa Kutumia Ndoo

Mpiga Ngoma Maarufu wa Mtaani Anayetengeneza Midundo kwa Kutumia Ndoo

Hamasa
Nani anahitaji ngoma wakati anaweza kutumia ndoo kutengeneza sauti na midundo ya pekee? Mpiga ngoma wa mtaani kule Australia aitwaye Gordo, ambaye awali alisoma nchini Japan, anafahamu kuwa inawezekana kutengeneza muziki kutoka kwenye kila kitu bila tatizo lolote. Akiwa mwenye nguvu, nia na shauku, Gordo anaonekana akitumia ndoo, vijiti vya kupigia ngoma na miguu yake kutengeneza midundo mizuri ya ngoma. Ikiwa hana shughuli na wasanii wengine, mwaliko kwenye tukio au sherehe basi utamkuta Gordo akiwa kwenye mitaa ya Sydney akidhihirisha kipaji chake katika jamii. Watu wengi huvutiwa na kipaji chake na hata kumzawadia pesa na vitu vingine; naamini hata wewe utakapotazama video zake hapa chini, hakika atakuvutia na kukuhamasisha sana. Karibu! https://www.youtube.com/watch?v=s...
Kanuni 15 za Ujasiriamali Ambazo ni Lazima Uzifahamu

Kanuni 15 za Ujasiriamali Ambazo ni Lazima Uzifahamu

Ujasiriamali
Ikizingatiwa kuwa upatikanaji wa ajira umekuwa wa shida sana, watu wengi hujikuta wakiwa na chaguo la kuwa wajasiriamali pekee kwenye maisha yao. Wengi hutamani au hata kujiingiza kwenye ujasiriamali, lakini siyo wote wanaofanikiwa kutokana na kutokufahamu kanuni muhimu za ujasiriamali. Ni wazi kuwa ili uanzishe kitu chochote chenye mafanikio, ni lazima ufahamu kanuni za kukifanya kitu hicho jinsi ipasavyo. Ikiwa wewe ni mjasiriamali, au unataka kuwa mjasiriamali, basi fuatilia makala hii ili nikufahamishe kanuni 15 za ujasiriamali. 1. Kuwa mtatuzi wa matatizo Ujasiriamali ni zaidi ya kupata pesa, ni lazima kwanza utatue changamoto ya mtu ndipo utaweza kupata pesa kutoka kwa mtu husika. Ni muhimu ukafahamu kanuni hii kama mjasiriamali kwani hutojikita kutafuta pesa bali utajiki...
Mambo 20 ya Kukushangaza Kuhusu Dhahabu

Mambo 20 ya Kukushangaza Kuhusu Dhahabu

Maarifa
Dhahabu ni moja kati ya madini ya thamani duniani. Dhahabu huchimbwa katika sehemu mbalimbali duniani na kisha kutumiwa kutengeneza vitu mbalimbali kama vile fedha, medali, vito vya thamani n.k Nchi nyingi zimejizolea utajiri mkubwa kutokana na madini haya; pamoja na utajiri huu pia nchi nyingi zimesababishiwa uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na uchimbaji wa dhahabu. Naamini umewahi kusikia mengi kuhusu dhahabu, lakini sasa fuatilia makala hii nikufahamishe mambo 20 yakushangaza kuhusu dhahabu. Katika tani moja ya simu za mkononi unaweza kupata dhahabu nyingi zaidi kuliko ambayo ungeipata kutoka kwenye gwangala la dhahabu (gold ore). Ikiwa utafanikiwa kukusanya dhahabu yote iliyoko baharini, basi kila mtu duniani anaweza kupata dhahabu takriban kilo 4. Inakadiriwa k...
Mambo 20 Usiyoyajua Kuhusu Jengo Refu Zaidi Duniani la Burj Khalifa

Mambo 20 Usiyoyajua Kuhusu Jengo Refu Zaidi Duniani la Burj Khalifa

Maarifa
Je unalifahamu jengo la Burj Khalifa lililoko Dubai? Burj Khalifa ni jengo refu zaidi duniani linalodhihirisha uwezo mkubwa wa wahandisi majengo wa karne ya 21. Unapozungumzia urefu wake au kutazama muundo wake, kwa hakika jengo hili litakushangaza; jengo hili liligharimu takriban dola bilioni 1.5 za Kimarekani kulijenga. Pamoja na kuwa ni jengo refu zaidi duniani, jengo hili limevunja rekodi nyingine kadha wa kadha zilizokuwa zimewekwa na majengo mengine. Naamini unapenda kulifahamu zaidi ili kuongeza maarifa yako. Karibu ufuatilie makala hii ili nikujulishe mambo 20 usiyoyajua kuhusu jengo hili la Burj Khalifa. Burj Khalifa ni jengo refu zaidi lililotengenezwa na binadamu duniani, lina urefu wa futi 2,723 au mita 829.8 kutoka kwenye kilele chake hadi ardhini. Hivyo kulifanya ...
Tovuti 20 Ambazo Ungetamani Kuzijua Mapema

Tovuti 20 Ambazo Ungetamani Kuzijua Mapema

Tija
Unaweza ukawa unajiuliza tovuti hizo ni zipi? Intaneti imejaa tovuti nyingi sana, za maana na zisizo za maana. Hata hivyo bado tovuti za maana na zenye manufaa zimeweza kujibainisha wazi kati ya zile zisizofaa. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe tovuti 20 ambazo kwa namna moja au nyingine zitakufaa katika maisha yako ya kila siku. 1. Have I Been Pwned? Tovuti: https://haveibeenpwned.com/ Hii ni tovuti nzuri sana kwa ajili ya kukagua kama barua pepe yako imeshavuja kwenye taarifa za siri zilizoibiwa. Hivi leo kuna makampuni na tovuti nyingi zinazodukuliwa na kuibiwa taarifa za watumiaji wake. Hivyo unaweza kuwa ni moja kati ya watu ambao barua pepe zao ziliibiwa. Ikiwa utaambiwa kua barua pepe yako imeonekana kwenye taarifa zilizodukuliwa basi badili neno la siri hara...
Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Kazi za Ujenzi Zilizoheshimu Mazingira ya Asili

Maarifa
Kila siku binadamu anafanya shughuli mbalimbali katika kuandaa au kutengeneza mazingira bora kwa ajili yake kuishi. Kazi hii zinahusisha ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji, makazi, viwanda, ofisi n.k. Hata hivyo, shughuli hizi za binadamu hupelekea uharibifu mkubwa wa mazingira ya asili ikiwemo misitu, mito, milima, wanyama, maziwa, hewa n.k Wapo watu waliolitambua hili na kuamua kufanya kazi zao kwa kuzingatia kulinda na kuheshimu mazingira ya asili. Karibu utazame picha kadha wa kadha zinazonyesha kazi hizo. 1. Nyumba ya duara iliyojengewa kwenye mti huko Tokyo, Japan 2. Mgahawa wa kahawa huko Shanghai, China 3. Mti katikati ya nyumba huko Almaty, Kazakhstan 4. Mti kwenye hoteli huko Izmir Uturuki 5. Nyumba ya makazi huko West Virginia 6. Nyumba iliyojengwa katik...
Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Maarifa, Teknolojia
Hakika ulimwengu huu una  mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu. Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua. Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web) Deep web ni nini? Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane. ...
Mambo 25 Yakushangaza Kuhusu Mwili wa Binadamu

Mambo 25 Yakushangaza Kuhusu Mwili wa Binadamu

Maarifa
Inawezekana unatazama mwili wako kwa juu juu pekee bila kufahamu mambo mengi yaliyojificha kwenye mwili wako. Ni hakika kuwa mwili umeumbwa kwa namna ya pekee sana inayouwezesha kufanya kazi pamoja na kuonekana jinsi ulivyo. Naamini unapenda kupata maarifa kwa kuufahamu mwili wako vyema. Karibu ufuatilie makala hii ili nikujuze mambo 25 yakukushangaza kuhusu mwili wa binadamu. 1. Ubongo unatumia asilimia 20 ya oksijeni pamoja na kalori Ni wazi kuwa utendaji kazi wa ubongo unahitaji oksijeni asilimia 20 pamoja na kalori kutoka kwenye mwili ili kufanya kazi jinsi ipasavyo. 2. Kila mtu ana harufu yake Mbali na mapacha wa kufanana, kila mtu ana harufu yake ya pekee inayomtofautisha kati yake na mtu mwingine. 3. Uwezo mkubwa wa kufikiri unahusiana na kiasi cha ndoto mtu anazoota In...
Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Mtindo wa Maisha
Pombe ni kinywaji kinachotumiwa na watu wengi pasipo hata kufahamu athari zake. Pombe ina athari mbalimbali kiafya na kisaikolojia. Wengi baada ya kuathiriwa na pombe hutamani kuacha matumizi ya pombe lakini ni wachache tu ndiyo hufanikiwa katika hili. Ikiwa unataka kuacha au kumsaidia mtu mwingine kuacha pombe, basi fuatilia njia 12 za uhakika za kuacha pombe. 1. Epuka watu watakaokushawishi kunywa pombe Mara nyingi kama wewe unapenda kunywa pombe utakuwa na marafiki wanaokunywa pombe pia. Ni wazi kuwa marafiki wanaokunywa pombe watakuhimiza kunywa hata kwa kukununulia au hata pengine kukukebehi na kukubeza juu ya uamuzi wako wa kuacha pombe. Hivyo ikiwa unataka kuacha kunywa pombe ni lazima uepuke marafiki au watu wanaoweza kukushawishi kunywa pombe. Unaweza kutafuta ma...