Intaneti Archives - Fahamu Hili
Tuesday, October 3Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Intaneti

Tovuti 20 Ambazo Ungetamani Kuzijua Mapema

Tovuti 20 Ambazo Ungetamani Kuzijua Mapema

Tija
Unaweza ukawa unajiuliza tovuti hizo ni zipi? Intaneti imejaa tovuti nyingi sana, za maana na zisizo za maana. Hata hivyo bado tovuti za maana na zenye manufaa zimeweza kujibainisha wazi kati ya zile zisizofaa. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe tovuti 20 ambazo kwa namna moja au nyingine zitakufaa katika maisha yako ya kila siku. 1. Have I Been Pwned? Tovuti: https://haveibeenpwned.com/ Hii ni tovuti nzuri sana kwa ajili ya kukagua kama barua pepe yako imeshavuja kwenye taarifa za siri zilizoibiwa. Hivi leo kuna makampuni na tovuti nyingi zinazodukuliwa na kuibiwa taarifa za watumiaji wake. Hivyo unaweza kuwa ni moja kati ya watu ambao barua pepe zao ziliibiwa. Ikiwa utaambiwa kua barua pepe yako imeonekana kwenye taarifa zilizodukuliwa basi badili neno la siri hara...
Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Fahamu Kuhusu Sehemu ya Mtandao wa Intaneti Iliyofichwa (Deep web na Dark web)

Maarifa, Teknolojia
Hakika ulimwengu huu una  mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu. Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua. Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web. Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web) Deep web ni nini? Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane. ...
Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Mambo 18 ya Kushangaza Kuhusu Intaneti Usiyoyajua

Maarifa, Teknolojia
Hivi leo kuna mambo mengi kuhusu intaneti, lakini hapa nitakuonyesha baadhi ya mambo ambayo naamini yatakuvutia na kukushangaza. Historia ya intaneti inaanzia miaka ya 1950 ikienda sambamba na maendeleo ya kompyuta. Ni wazi kuwa, ulimwengu wa intaneti wa leo ulianzwa na mwanasayansi wa kompyuta wa Uingereza Tim Berners-Lee. Kuundwa kwa intaneti yake ya kwanza, moja kwa moja kulibadili ulimwengu, vyombo vya habari, mahusiano, burudani na mambo mengine mengi. Tunapotazama intaneti leo, ni wazi kuwa tunaona mambo mengi ambayo intaneti imepitia tokea kuanzishwa kwake hadi hivi leo. Karibu ufuatilie makala hii ili ufahamu mambo 18 ya kushangaza kuhusu intaneti usiyoyajua. 1. Tovuti ya kwanza bado ipo Tovuti ya kwanza kutengenezwa bado ipo na inafanya kazi hadi leo. Jambo pekee ni ku...
Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Vitu 11 Unavyotakiwa Kutoviweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Teknolojia
Kuna taarifa nyingi tunazoweka kwenye mtandao; lakini je, sasa ni wakati wa kuweka mipaka juu ya ni lipi la kuweka na kutoweka kwenye mitandao? Ndiyo; huu ni wakati sahihi. Hivyo basi, tambua vitu 11 ambavyo haupaswi kuviweka kwenye mitandao ya kijamii. 1. Tarehe kamili ya kuzaliwa Wakati mwingine unaweza kuvutiwa na namna marafiki zako wanavyoweka taarifa za kuzaliwa kwenye mtandao, au hata misisitizo ya mitandao ya kijamii kama vile Facebook juu ya kukamilisha akaunti yako kwa kuweka tarehe ya kuzaliwa. Kuweka tarehe halisi au kamili ya kuzaliwa kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kutoa mwanya kwa wahalifu kupata taarifa zako muhimu na hata kufungua au kuingilia akaunti zako zinazotumia tarehe yako ya kuzaliwa. Mambo ya kufanya: Ficha au ondoa tarehe yako halisi ya kuzal...
Sababu 7 za Kwanini Uachane na Facebook Sasa Kwa Ajili ya Baadaye Yako

Sababu 7 za Kwanini Uachane na Facebook Sasa Kwa Ajili ya Baadaye Yako

Maendeleo Binafsi, Tija
Miaka kadhaa iliyopita mawasiliano yalikuwa magumu na ya gharama kubwa. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, mawasiliano yamerahisishwa na kuwa ya uhakika zaidi huku ghrama pia ikipungua. Kuwepo wa mtandao wa intaneti pamoja na mitandao ya kijamii kumewafanya watu kukaribiana zaidi. Baada ya kuanzishwa kwa mtandao wa Facebook ambao ulianzia huko Marekani na baadaye kuenea dunia nzima maisha ya watu yamebadilika sana. Facebook ina watumiaji hai zaidi ya bilioni 1.23 na bado Facebook inalenga kuwaongeza zaidi ili kuwafikia watu wote duniani. Pamoja na maendeleo haya makubwa kumeshuhudiwa madhara au changamoto kadha wa kanda zinazotokana na mitandao ya kijamii hasa Facebook. Hivyo basi hapa nitafafanua sababu kadhaa zinazodhihirisha ni kwa namna gani Facebook inakup...
Njia 3 za Kutengeneza Pesa kwa Kutumia YouTube bila Adsense

Njia 3 za Kutengeneza Pesa kwa Kutumia YouTube bila Adsense

Kipato, Tovuti na Blogu
Watengenezaji wengi wa video wanajua jisi ilivyo vigumu kutengeneza pato la uhakika kupitia Youtube kwa kutumia Adsense pekee. Watengenezaji wengi wa video wamekuwa wakifikiri kuwa kupakia video zenye ubora sana kwenye mtandao wa YouTube kutawafanya kupata fedha lakini mambo yamekuwa ndivyo sivyo. Ni vigumu kujua ni kiasi gani unaweza kupata kutokana na Adsense kwenye YouTube, lakini unaweza kukadiria kwa video kutazamwa mara elfu moja utapata takribani dola moja. Kiasi hiki ni kidogo ukilinganisha na kazi utakayokuwa umeifanya ili kukipata. Tazama njia tatu nitakazokueleza zitakazokuwezesha kupata fedha kwenye mtandao wa YouTube bila kutumia Adsense. 1. Mshirika au Wakala Unaweza kupata fedha kwenye YouTube kwa njia ya kuwa mshirika au wakala wa makapuni mbalimbali yanayozalis...