Kornelio Maanga, Author at Fahamu Hili - Page 6 of 17
Friday, March 27Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Author: Kornelio Maanga

Kornelio ni mjasiriamali, mfuasi mkubwa wa masuala ya kompyuta na msanifu mtandao toka mwaka 2008. Amekuwa akifanya kazi mbalimbali zinazohusiana na Teknolojia ya Habari Mawasiliano (TEHAMA), bila kusahau uandishi wa makala kadha wa kadha katika tovuti na blog mbalimbali. Anapenda kujifunza na kuwafundisha watu wengine mambo mbalimbali pamoja na mbinu za kuboresha maisha ya kila siku.
Mambo 9 ya Kuzingatia Wakati Wa Kuchagua Kampuni ya Matangazo Kwenye Blog

Mambo 9 ya Kuzingatia Wakati Wa Kuchagua Kampuni ya Matangazo Kwenye Blog

Tovuti na Blogu
Kuweka matangazo kwenye blog ni njia mojawapo ya kupata pesa kupitia blog ambayo inafahamika kwa watu wengi. Kuna baadhi ya blog au tovuti ambazo zimefanikiwa kutengeneza pesa nyingi sana wakati nyingine zikiwa hazipati pesa za maana au hazipati kabisa kupitia njia hii ya matangazo. Kwa hakika watu wengi huchagua njia ya kuweka matangazo ya kampuni mbalimbali kwenye blog zao ili kujipatia kipato kutokana na kutokufahamu njia nyingine za kupata pesa au kutokana na kuona blog nyingine zikitumia njia hiyo. Ikiwa basi wewe ni mmojawapo wa watu wanaotaka kutumia njia ya kuweka matangazo kwenye blog ili kupata pesa, basi fahamu mambo 9 ya kuzingatia wakati wa kuchagua kampuni ya matangazo kwenye blog au tovuti yako. 1. Wakati sahihi Kuna wakati sahihi wa kujiunga na kampuni ya matang...
Njia 12 za Kupunguza Gharama za Uendeshaji wa Kampuni

Njia 12 za Kupunguza Gharama za Uendeshaji wa Kampuni

Biashara na Uchumi
Mbinu mojawapo ya kuongeza faida katika kampuni au biashara yako ni kwa kupunguza matumizi ya kampuni yako. Suala la kupunguza matumizi ya pesa ni muhimu zaidi hasa pale ambapo kampuni inakuwa inakabiliwa na changamoto za kifedha. Kwa hakika kupunguza matumizi ya uendeshaji wa kampuni ni jambo linalowezekana ikiwa mikakati na hatua stahiki zitachukuliwa. Ikiwa unapenda kufahamu jinsi ya kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni, basi fahamu njia 12 unazoweza kuzitumia kufanikisha lengo hili. 1. Tathimini upya matumizi Kuna matumizi mbalimbali kwenye kila kampuni lakini siyo yote ni ya muhimu. Matumizi mengine ni ya lazima lakini yamepewa kipaumbele kuliko umuhimu wake. Kwa kupunguza matumizi ya vitu kama vile simu, umeme, maji, mafuta au hata intaneti, kutaokoa kiasi kikubw...
Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla na Wakati wa Kuendesha Gari Umbali Mrefu

Mambo 10 ya Kuzingatia Kabla na Wakati wa Kuendesha Gari Umbali Mrefu

Usafiri na Safari
Kuendesha gari ni suala linalohitaji umakini na utulivu mkubwa, hasa pale unapoendesha gari umbali mrefu. Mara kwa mara kumeshuhudiwa ajali mbalimbali ambazo kimsingi zinatokana na madereva kutokuzingatia kanuni muhimu katika utumiaji wa vyombo vya usafiri. Ili kuhakikisha usalama wako pamoja na watumiaji wengine wa barabara, yapo mambo kadhaa unayopaswa kuyazingatia kabla na wakati wa kuendesha gari umbali mrefu. 1. Kagua na andaa gari Kabla ya safari yoyote gari linahitaji kukaguliwa na kuandaliwa, hasa kabla ya safari ndefu. Kuna mambo kadhaa unayohitaji kuyakagua kwenye gari lako: Kagua hali na ubora wa magurudumu. Hakikisha magurudumu yamejaa vizuri na hayajazeeka. Kagua mafuta lainishi (oil). Hakikisha gari yako ina mafuta lainishi ya kutosha tena ya ubora unaotakiwa...
Kikombe cha Kisasa Kinachozuia Vitu Kumwagika

Kikombe cha Kisasa Kinachozuia Vitu Kumwagika

Teknolojia
Lengo kubwa la teknolojia ni kurahisisha maisha pamoja na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi. Kila siku kumekuwa kukibuniwa teknolojia mbalimbali hasa kwa lengo la kutatua matatizo mbalimbali yanayomkabili mwanadamu. Inawezekana umewahi kupoteza nyaraka zako muhimu au hata kuharibu vifaa vyako vya thamani kama vile simu au kompyuta kutokana na kumwagikiwa vimiminika kama vile maji, kahawa au chai. Teknolojia kutoka MightyMug inakuja na kikombe maalumu ambacho huzuia kinywaji kilichoko ndani yake kumwagika. Inawezekana una mtoto mkorofi au unafanya kazi kwenye eneo lenye mitikisiko mingi; sasa kwa kutumia kikombe kutoka MightyMug utaepusha vitu vyako vya thamani kumwagikiwa vimiminika. Sifa  za kikombe cha MightyMug Kikombe cha MightyMug kina uwezo wa kujishikiza kw...
Tofauti 10 Kati ya Mwajiriwa na Mjasiriamali

Tofauti 10 Kati ya Mwajiriwa na Mjasiriamali

Ujasiriamali
Kwa hakika kuna tofauti kubwa kati ya mwajiriwa na mjasriamali; tofauti hii inahusisha tabia, fikra, maamuzi au hata matendo. Kuna baadhi ya watu ni wajasiriamali kwa mwonekano lakini kitabia ni waajiriwa; wapo pia wengine ni waajiriwa kimwonekano lakini ni wajasiriamali kitabia. Ikiwa basi unataka kuwa mjasiriamali, ni muhimu ufahamu tofauti 10 za msingi zilizopo kati ya mwajiriwa na mjasiriamali. 1. Mwajiriwa hupumzika kwenye likizo lakini mjasiriamali hutumia likizo kufanya kazi zaidi Kwa kawaida waajiriwa hufurahia muda wa likizo kwa sababu ndipo hupata muda wa kupumzika. Hali ni tofauti kwa mjasiriamali kwani hana likizo, na ikiwa ni mjasiriamali aliyeajiriwa, basi atatumia likizo yake kuendeleza mradi au biashara yake. 2. Mwajiriwa hulenga kupanda cheo lakini mjasiriamal...
Madaraja 15 Makubwa au Marefu Zaidi Duniani

Madaraja 15 Makubwa au Marefu Zaidi Duniani

Maarifa
Kwa siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa maendeleo makubwa katika shughuli mbalimbali za binadamu. Sekta ya ujenzi na usafiri ni moja kati ya sekta ambazo binadamu amepiga hatua kubwa. Kila siku kumekuwa kukibuniwa na kufanyika maboresho mbalimbali katika miundombinu ya usafirishaji. Kumeshuhudiwa ujenzi wa barabara za kisasa, reli, viwanja vya ndege au hata kubuniwa kwa baadhi ya aina mpya za usafiri. Kutokana na hili, yapo madaraja mbalimbali yaliyojengwa sehemu mbalimbali duniani ili kuboresha usafiri wa barabara na reli. Karibu uongeze maarifa yako kwa kufahamu madaraja 15 makubwa au marefu zaidi duniani kwa sasa. 1. Daraja la Danyang–Kunshan Daraja la Danyang–Kunshan ndilo daraja refu kuliko yote duniani, lina urefu wa kilometa 164.8. Daraja hili linapatikana huko China kat...
Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Benki

Mambo 10 Muhimu ya Kuzingatia Wakati wa Kuchagua Benki

Kipato
Benki ni taasisi muhimu ambayo siyo rahisi mtu kukwepa kuitumia kwa njia moja au nyingine. Kuhifadhi au kusafirisha pesa kwa njia za zamani kumepitwa na wakati; sasa ni wakati wa kutumia mifumo salama na ya kisasa. Kwa kuwa benki ni taasisi muhimu, huna budi kuchukua hatua kadhaa ili kupata benki nzuri kwa ajili ya shughuli zako za kifedha. Ikiwa unataka kupata benki nzuri, basi fahamu mambo 10 unayopaswa kuzingatia wakati wa kuchagua benki kwa ajili ya matumizi yako. 1. Usalama wa pesa zako Kwa kawaida kila benki husimamiwa na benki kuu ya nchi ili kuhakikisha usalama wa fedha za wateja. Hata hivyo kuna baadhi ya benki huanzishwa na kuendeshwa kinyemela bila kuwa chini ya benki kuu. Ni muhimu kuhakikisha benki unayotaka kuitumia imesajiliwa na inajiendesha kwa kuzingatia sh...
Vitu 10 Vinavyoharibu Maadili ya Watoto

Vitu 10 Vinavyoharibu Maadili ya Watoto

Mahusiano na Familia
Kwa miaka ya hivi karibuni kumeshuhudiwa kuporomoka kwa maadili ya watoto kwa kiwango kikubwa. Hili limepelekea kuibuka kwa maswali mengi juu ya ni nini hasa chanzo cha tatizo hili. Hivi leo watoto wengi hawaheshimu wazazi wala waliowazidi umri, wanatumia pombe na madawa, wanaiba, wana kiburi, wavivu, n.k. Kwa hakika vipo vitu vinavyochangia katika kuporomoka kwa maadili ya watoto. Karibu nikushirikishe vitu 10 vinavyoharibu maadili ya watoto. 1. Wazazi kuwa mfano mbaya Wazazi wa karne hii wengi wanawalaumu watoto kuwa wana maadili mabaya, lakini chanzo cha tatizo hili ni wao wenyewe. Wazazi wamekuwa wakilewa, kutukanana, kupigana au hata kufanya mambo mengine machafu kama vile uzinzi mbele ya watoto. Kwa hakika tabia hizi zinapofanywa mbele ya watoto nao huziiga na kuzifany...
Sababu 11 za Kwanini Watu Hawakupendi

Sababu 11 za Kwanini Watu Hawakupendi

Maendeleo Binafsi
Kuna baadhi ya watu wanapendwa sana kwenye jamii au mazingira yanayowazunguka, kwa ujumla tunaweza kusema wanapendwa takriban na watu wote. Lakini wapo wengine wasiopendwa kabisa, na hata kama wanapendwa, basi wanapendwa na watu wachache sana. Kuishi katika jamii inayokupenda kunakufanya kuwa mwenye furaha na ufanisi katika yale unayoyafanya. Wapo baadhi ya watu wanatambua kuwa hawapendwi, lakini hawajui sababu za tatizo hilo wala njia ya kulitatua. Ikiwa unataka kufahamu kwanini baadhi ya watu hawakupendi, basi fahamu sababu 11 zinazosababisha watu wasikupende. 1. Siyo msikivu Kama unavyopenda kusikilizwa, ndivyo na watu wengine wanavyopenda kusikilizwa. Ikiwa huna muda wa kusikiliza mawazo au matatizo ya watu wengine, nao pia hawatakuwa na muda wa kupenda kukusikiliza. Epuka tabia z...
Faida 15 za Kufunga Kula Unazotakiwa Kuzifahamu

Faida 15 za Kufunga Kula Unazotakiwa Kuzifahamu

Mtindo wa Maisha
Watu wengi wanafahamu kuwa kufunga kula ni swala linalohusiana na imani zaidi. Wengi hawafahamu kuwa kufunga kula kuna manufaa ya kiafya pia. Kufunga kula ni tendo lenye historia ndefu sana ambayo kimsingi chimbuko lake ni sababu za kiimani. Hata hivyo shuhuda na tafiti mbalimbali zimedhihirisha kuwa kuna manufaa mengine kemkem ya kufunga kula mbali na yale ya kiimani. Ikiwa basi unapenda kuongeza maarifa pamoja na kuboresha afya yako, fahamu faida 15 za kufunga kula. 1. Huboresha metaboli Metaboli ni mchakato ambao mwili hutumia virutubisho kutoka kwenye vyakula ili kujipa nguvu. Unapofunga kwanza unapumzisha mfumo wako wa umeng’enyaji, pili unaufanya mchakato wa metaboli kwenda vizuri kwani mwili utatumia vyema virutubisho vilivyoko mwilini tayari. 2. Huboresha mzunguko w...