Vinywaji Archives - Fahamu Hili
Tuesday, October 3Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Vinywaji

Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Njia 12 za Uhakika za Kuacha Pombe

Mtindo wa Maisha
Pombe ni kinywaji kinachotumiwa na watu wengi pasipo hata kufahamu athari zake. Pombe ina athari mbalimbali kiafya na kisaikolojia. Wengi baada ya kuathiriwa na pombe hutamani kuacha matumizi ya pombe lakini ni wachache tu ndiyo hufanikiwa katika hili. Ikiwa unataka kuacha au kumsaidia mtu mwingine kuacha pombe, basi fuatilia njia 12 za uhakika za kuacha pombe. 1. Epuka watu watakaokushawishi kunywa pombe Mara nyingi kama wewe unapenda kunywa pombe utakuwa na marafiki wanaokunywa pombe pia. Ni wazi kuwa marafiki wanaokunywa pombe watakuhimiza kunywa hata kwa kukununulia au hata pengine kukukebehi na kukubeza juu ya uamuzi wako wa kuacha pombe. Hivyo ikiwa unataka kuacha kunywa pombe ni lazima uepuke marafiki au watu wanaoweza kukushawishi kunywa pombe. Unaweza kutafuta ma...
Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Madhara 12 ya Pombe Kiafya

Afya
Siyo siri kuwa pombe husababisha matatizo makuwa ya kiafya, yakiwemo magonjwa ya moyo, ini pamoja na majeraha yatokanayo na ajali zitokanazo na ulevi. Ni dhahiri kuwa vinywaji halisi vilivyotengenezwa kwa matunda bila kilevi ni bora zaidi kwa afya yako kuliko vile vyenye kilevi. Licha ya kuwepo kwa kampeni kadha wa kadha zinazopinga matumizi ya pombe, bado watu wengi wameendelea kushikilia kinywaji hiki bila kufahamu athari zake kwenye afya zao. Fuatilia hapa chini athari 12 za pombe kiafya. 1. Matatizo ya moyo Unywaji mkubwa wa pombe husababisha  matatizo mbalimbali ya moyo kama vile cardiomyopathy, ambapo mishipa ya moyo hudhoofika na kushindwa kusukuma damu. Jambo hili huweza kusababisha damu kuganda na kusababisha kiharusi (stroke). Pombe huchangia sana katika kudhoofisha mish...
Faida 10 za Kunywa Maziwa Usizozifahamu

Faida 10 za Kunywa Maziwa Usizozifahamu

Mtindo wa Maisha
Maziwa hufanya mambo mengi mazuri kwa ajili ya afya yako. Wataalamu wa afya na wauzaji wa maziwa wamekuwa wakieleza faida kadha wa kadha za kunywa maziwa. Je umewahi kujiuliza hasa ni faida gani hizo zitokanazo na unywaji wa maziwa? Ni wakati wako sasa wa kujiuliza kwa kina juu ya faida zitokanazo na unywaji wa maziwa. Fuatana nami katika makala hii nikueleze faida 10 zitokanazo na unywaji wa maziwa. 1. Hujenga na kulainisha ngozi Je unamfahamu Cleopatra? Cleopatra alikuwa ni malikia wa Misri anaesadikiwa kuwa mzuri sana. Inaaminikia uzuri wa Cleopatra ulitokana na tabia yake ya kuogea maziwa mara kwa mara. Hivyo basi, ni wazi kuwa, vitamini na virutubisho vilivyoko katika maziwa ni muhimu kwa ajili ya ngozi bora. Ni vyema kunywa angalau bilauri moja ya maziwa kila siku. 2. Hu...